Ligi KuuNyumbani

Mtibwa Sugar kuiduwaza Simba leo?

LIGI Kuu Tanzania Bara inaendelea leo kwa mchezo mmoja kupigwa Dar es Salaam.

Katika mchezo huo Simba itaikaribisha Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Azam Complex uliopo eneo la Chamazi.

Simba inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 47 baada ya michezo 22 wakati Mtibwa ipo nafasi 16 mwisho wa msimo ikiwa na pointi 17 baada ya michezo 23.

Kwa mara ya mwisho Simba na Mtibwa zilikutana katika mchezo wa ligi Agosti 17, 2023, Simba ikishinda kwa mabao 4-2 kwenye uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.

Related Articles

Back to top button