DAR ES SALAAM; Msanii wa filamu nchini Jacquline Wolper amesema anaweza kufanya utani wa mambo mengine, lakini si kuhusu ndoa yake.
Amesema yapo mambo akitaniwa hawezi kujali, lakini sio kuhusu ndoa yake na familia kwa ujumla.
“Niseme tu kabisa mjuwe leteni utani kwenye mambo yote nitapuuzia, lakini sio familia, ndoa wala baba watoto wangu, sitawafumbia macho kabisa,”amesema Wolper.