Tetesi
United hawatanii kwa Mount

MANCHESTER United wapo tayari kutoa pauni milioni 55 kupata saini ya kiungo Mason Mount kutoka Chelsea.
Arsenal na Liverpool pia zinaiwinda saini ya Muingereza huyo.
Kwa mujibu wa mtandao wa ’90 Minutes’ Chelsea itafanya majadiliano ya mustakabali wa mchezaji huyo wiki ijayo.
Mtandao wa Mail Online wa nchini Uingereza umeripoti kuwa kocha wa United, Eric Ten Hag anatamani uhamisho huo ukamilike haraka majira ya kiangazi.