Serie A

Napoli wamsajili Hojlund kwa mkataba wa kudumu

NAPLES:MABINGWA wa Italia, Napoli, wamemsajili mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund kwa mkataba wa kudumu kutoka Manchester United baada ya kuwa na msimu mzuri wa mkopo nchini Italia.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na klabu zote mbili, Napoli imelipa euro milioni 50 (takribani dola milioni 58) kukamilisha uhamisho wa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23.

Hojlund alifunga mabao 16 katika mechi 44 za mashindano yote msimu uliopita, akichangia Napoli kutwaa taji la Supercoppa Italiana na kumaliza katika nafasi ya pili kwenye ligi ya Serie A.

Mshambuliaji huyo alijiunga na Manchester United mwaka 2023 akitokea Atalanta na kufunga mabao 26 katika mechi 95 alizoichezea timu hiyo ya England.

Uhamisho huo unampa Napoli uhakika wa kuendelea kuwa na mshambuliaji aliyethibitisha uwezo wake katika soka la Italia, huku klabu hiyo ikitarajia kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu mpya wa mashindano ya ndani na kimataifa.

Related Articles

Back to top button