Ligi Ya WanawakeNyumbani

Yanga Princess dimbani SLWPL leo

LIGI Kuu ya soka ya wanawake Tanzania Bara(SLWPL) inaendelea leo kwa mchezo mmoja mkoani Dar es Salaam.

Katika mchezo huo Yanga Princess ni wenyeji wa The Tiger Queens kwenye uwanja wa Uhuru.

Yanga inashika nafasi ya 4 katika msimamo wa SLWPL ikiwa na pointi 14 baada ya michezo 7 wakati The Tiger Queens ipo nafasi ya 8 ikiwa na pointi 4 baada ya michezo 6.

JKT Queens ndio inayoongoza ligi hiyo yenye timu 10 ikiwa na pointi 17 baada ya michezo 7 wakati Mkwawa Queens ipo nafasi ya mwisho ikiwa na pointi 1 baada ya michezo 7.

Related Articles

Back to top button