Kwingineko

Vijana wa Azam FC wakabidhiwa picha ya Alexander Isak

VIJANA wanne kutoka timu ya vijana ya Azam FC, baada ya kuwasili nchini Sweden kwenye kliniki ya siku 40 kwa ajili ya kuendelezwa vipaji vyao wamekabidhiwa picha ya mchezaji wa Newcastle United Alexander Isak.
Alexander Isak ni mchezaji bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu ya Uingereza ambaye alilelewa na klabu ya Aik FC ya Sweden.
Vijana hao wako nchini humo ikiwa ni matokeo ya mkataba wa ushirikiano kati ya klabu ya Azam FC na AIK FC.
Vijana hao beki wa kati Pius Severine, beki wa kushoto Ismail Omar, kiungo mshambuliaji Adinani Rashid na Mohammed Shilla.
Azam FC imekuwa na utamaduni mzuri wa kuwapa fursa ya kwenda nje kujaribu bahati zao. Ilishafanya kwa wachezaji kadhaa kama Farid Musa na Shaban Chilunda ambao walipata nafasi ya kwenda Tenerife, Hispania miaka ya nyuma na wengine Canada.

Related Articles

Back to top button