Africa

Azam ugenini shirikisho Afrika

KLABU ya Azam leo itakuwa ugenini Libya kuikabili Al Akhdar katika mchezo wa raundi ya pili Kombe la Shirikisho Afrika katika uwanja wa Benina Martyrs ulipo mji wa Benghazi.

Mchezo huo ni miongoni mwa mechi 9 za michuano hiyo zinazopigwa leo.

Awali akizungumza na Spotileo Mtendaji Mkuu wa Azam Abdulkarim Amin ‘Popat’ amesema klabu hiyo imejipanga vyema kuhakikisha inapata ushindi dhidi ya Al Akhadar.

Popat amesema malengo ni kufika mbali kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika angalau hatua ya makundi hivyo wamezungumza na wachezaji na wanaamini watapata matokeo mazuri.

“Tumefika salama na tunawashukuru wenzetu Al Akhdar wametupa mapokezi mazuri na wachezaji wetu wanaonekana wana ari kubwa ni imani ya kila mmoja wetu kwamba tutapata matokeo mazuri kesho,” amesema Popat.

Amesema wachezaji wapo katika hali nzuri kwa ajili ya mechi hiyo.

Michezo mingine inayopigwa leo ni kama ifuatavyo:

St Michel United           vs     Motema Pembe
AS Kigali                     vs      Al-Nasr
Ferroviario da Beira      vs     Diables Noirs
Kipanga                      vs     Club Africain
Saint-Eloi Lupopo         vs     Sagrada Esperance
Sporting Gagnoa          vs     JS Saoura
Al Hilal Wau                 vs     Pyramids
AS Real Bamako          vs      Hearts of Oak

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button