Africa

Yanga kutinga makundi CAFCL?

KLABU ya Yanga leo inashuka dimbani katika mchezo wa marudiano kuwania kufuzu makundi Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al-Merrikh ya Sudan.

Mchezo huo utafanyika uwanja wa Azam Complex, Dar es salaam.

Katika mchezo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Kigali Pele, Rwanda Septemba 16, Yanga ilishinda kwa mabao 2-0.

Matokeo ya suluhu, sare ya mabao ya idadi yoyote au kufungwa bao lisizozidi moja katika mchezo wa leo yataipeleka moja kwa moja Yanga makundi ya michuano hiyo.

Related Articles

Back to top button