Mastaa

Rehema Simfukwe ataja siri aliyoificha kwa miaka

DAR ES SALAAM:MWANAMUZIKI maarufu katika Muziki wa Injili nchini Rehema Simfukwe amevunja ukimya kwa mara ya kwanza kwa kuamua kutoa sababu za kutunga wimbo wa Chanzo ambao umekuwa ukipendwa na kuvuta hisia za watu wengi kutokana na mashairi yaliyoandikwa katika wimbo huo.

Nyota huyo tangu alipotoa wimbo huo miaka minne iliyopita hakuwahi kutoa sababu za kutunga na kuimba wimbo huo lakini ameona sasa ni wakati muafuaka kuwaambia Watanzania.

Akizungumza Dar es Salaam katika hafla ya kushereheke kumbukizi ya kuzaliwa kwa mtoto wake wa kwanza Dorcas ambaye ametimiza miaka sita, Simfukwe alisema mtoto huyo ndiye aliyesababisha kuimba wimbo huo ni mtoto ambaye alimzaa akiwa na changamoto ya kupooza kwa ubongo au mtindio wa ubongo.

“Mungu amenijaalia watoto watatu lakini duniani huku watu wengi wanajua nina watoto wawili. Mtoto wangu wa kwanza anaitwa Dorcas ambaye alizaliwa na changamoto ya kupooza ubongo au mtindio wa ubongo kwa hiyo alikuwa na changamoto sana katika maisha yake,

“Changamoto hiyo kwa Dorcas ilisababisha tangu alipozaliwa tukawa na maisha ya hosipitali siku hadi siku. Nimekuwa nikiimba nyimbo za injili, nafanya mahojiano na vyombo vya habari kuhusu wimbo wa Chanzo lakini sijawahi kueleza upande wa pili kuhusu wimbo huu,” amesema.

Amesema amekuwa kimya muda wote kwasababu alikuwa anasubiri apate kibali kutoka kwa Mungu kuzungumzia wimbo huo na hiyo ndio sababu ya kutunga na kuimba wimbo huo ambao unazungumzia maisha halisi ya Mtoto Dorcas.

“Ukiusikiliza wimbo huu utaona ndani yake kuna ujumbe uliobeba maumivu ya Dorcas na ndio sababu ya kuimba wimbo huo, nafahamu tangu ulipotoka watu wameuopokea, na wamekuwa wakiuimba na kuufurahia na nimekuwa nikiulizwa sababu za kuimba wimbo huu.

“ Nilimuahidi Mungu kuwa sitasema hili mpaka pale atakaponiruhusu na nimekaa na hii siri kwa miaka kadhaa na ninaamini Mungu amenipa mtoto Dorcas ili niwe mfano kwa wengine, ili nisaidie wengine wenye watoto wenye changamoto kama za Dorcas.

Hata hivyo, wakati wakisherehekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa mtoto Dorcas ametangaza kufungua kituo cha kuelea watoto ambao wanachangamoto ya mtindio wa ubongo. Kituo hicho kitafahamika kwa jina la Dorcas Home Care Initiative kilichopo Madale jijini Dar es Salaam.

“Kwa wale ambao wataguswa basi wanaweza kutuchangia kupitia akaunti ya NBC 074172000439TZS na 074173000101 wakati namba ya benki ya CRDB ni 015C0005PQW00 TZS na namba ya M-pesa ni 0768571613(Dorcas Home Care, “amesema mwanamuziki Rehema Simfukwe,”alisema.

Mwisho

Related Articles

Back to top button