Kwingineko
Vita ya kiatu cha dhahabu imeanza mapema mno

MBIO za kuwania Kiatu cha Dhahabu katika Kombe la Dunia 2026 zimeanza kwa kasi ambayo haijawahi kuonekana kwa miaka mingi.
Baada ya michezo miwili pekee ya hatua ya makundi, Lionel Messi tayari amefunga mabao matano, huku Erling Haaland na Kylian Mbappé wakifunga mabao manne kila mmoja.
Kinachofanya takwimu hizi kuvutia zaidi ni kwamba katika Kombe la Dunia 2014 na 2018, mshindi wa Kiatu cha Dhahabu alimaliza mashindano akiwa na mabao sita pekee.
Sasa, kabla hata hatua ya makundi haijamalizika, Messi amebakiwa bao moja tu kufikia idadi hiyo, wakati Haaland na Mbappé wako mabao mawili nyuma.
Messi, Mbappé na Haaland wote walifunga mabao mawili katika michezo yao ya jana usiku na kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mechi.
Kwa sasa ni mapema kutabiri nani atashinda Kiatu cha Dhahabu, lakini jambo moja ni wazi: mbio za mwaka 2026 zinaonekana kuwa kali zaidi kuliko ilivyokuwa katika Kombe la Dunia kadhaa zilizopita.




