Nyumbani
Tanzania, Morocco kushirikiana michezo

Tanzania na Morocco zitaendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta ya michezo.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro amesema hayo Dar es Salaam leo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Morocco hapa nchini Zakaria El Goumiri.
Kwa upande wake Balozi Zakaria El Goumiri amesema nchi yake itaiunga mkono Tanzania katika ujenzi wa miondombinu ya michezo ili kuendelea kukuza vipaji vya wanamichezo ambao watakuwa ni hazina kwa mataifa hayo kwenye timu za taifa.