Ligi Daraja La Kwanza
Hispania, Japan zatangulia robo fainali Kombe la Dunia Wanawake
HISPANIA na Japan leo zimetinga robo fainali ya michuano ya soka Kombe la Dunia kwa wanawake inayoendelea New Zealand na Australia baada ya kushinda mechi zao za hatua ya 16 bora.
Kuingia hatua hiyo Hispania imeikanda Uswisi kwa mabo 5-1 wakati Japan imeipa kichapo Norway cha mabao 3-1.
Katika timu tatu za Afrika zilifuzu 16 bora, Afrika Kusini itakipiga dhidi ya Uholanzi Agosti 6, Nigeria ikiikabili England Agosti 7 na Morocco kupepetena na Ufaransa Agosti 8.