Africa

Simba Queens kutinga nusu fainali?

TIMU ya soka ya wanawake Simba Queens inashuka uwanjani leo dhidi ya Green Buffaloes katika mchezo wa mwisho wa kundi A michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa wanawake inayoendelea Morocco.

Simba Queens inahitaji ushindi katika mchezo huo katika uwanja wa Grand De Marrakech ili kufuzu.

Timu hizo zina pointi pointi 3 kila moja ingawa Buffaloes ni ya pili na Simba Queens ya tatu hivyo klabu yoyote itakayoshinda itafuzu nusu fainali.

FAR Rabat Women inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 6.

Related Articles

Back to top button