AFCONAfrica

Kivumbi kufuzu AFCON leo

MECHI tatu za kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika(AFCON) zinapigwa leo kwenye viwanja tofauti.

Miamba ya Afrika, Misri itakuwa ugenini kuivaa Guinea ukiwa mchezo wa kundi D kwenye uwanja wa Grand Marrakech uliopo Morocco.

Sudan Kusini ipo uwanjani hivi sasa kuikabili Gambia kwenye uwanja wa Suez Canal uliopo Ismailia, Misri katika mchezo wa kundi G ambapo ni dakika ya 23 na timu hizo zipo sare ya  bao 1-1.

Katika kipute kingine Guinea-Bissau itakuwa nyumbani kuivaa Sao Tome na Principe kwenye uwanja wa September 24 katika jiji la Bissau.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button