Africa

Kocha wa Misri azimia kisa ugomvi wa wake zake

CAIRO: Kocha wa timu ya taifa ya Misri, Hossam Hassan, ameripotiwa kuwa katikati ya tukio la ugomvi kati ya wake zake wawili, tukio ambalo linadaiwa kumfanya aanguke na kupoteza fahamu wakati akijaribu kuwatenganisha.

Kwa mujibu wa taarifa ya talkSPORT, tukio hilo lilitokea katika mgahawa wa Porto Marina, ambapo mzozo kati ya mke wa kwanza wa Hassan, Howaida El-Gharbawy, na mke wake wa pili, Dina Mostafa, uligeuka kuwa mapambano makali ya kimwili.

Ripoti hiyo inasema walinzi wa hoteli walilazimika kuingilia kati ili kuwatenganisha wanawake hao wawili, ambao wote walidaiwa kupata majeraha madogo na michubuko.

Hassan, ambaye alishuhudia tukio hilo, alidaiwa kujaribu kuingilia kati na kuwatenganisha, lakini baadaye akaanguka.

Baada ya tukio hilo, Hassan aliripotiwa kuamua kuachana na mke wake wa kwanza, Howaida El-Gharbawy.

Talaka hiyo ilithibitishwa na Mohamed Shams, wakili anayemwakilisha mke wa pili wa Hassan.

Tukio hilo limezua mjadala mkubwa kutokana na nafasi ya Hassan kama kocha wa timu ya taifa ya Misri.

Related Articles

Back to top button