Barcelona wapeleka Pauni milioni 60 kwa Rodri

BARCELONA: KLABU ya Barcelona bado ipo ‘bize’ kuhakikisha inamnasa kiungo wa Manchester City, Rodri baada ya kuwasilisha ofa mpya ya Pauni milioni 60.
Baada ya wiki iliyopita ofa yao ya Pauni milioni 45 kupigwa chini, sasa wamerejea na ofa hiyo inayotajwa angalau italeta ushawishi.
City wenyewe wanataka Pauni milioni 80 kwa nahodha huyo wa Uhispania na mshindi wa Kombe la Dunia 2026.
Imeelezwa Mkurugenzi wa Michezo wa Barca, Deco yuko mbioni kuhakikisha anakamilisha dili hilo mapema ili amgeukie Julian Alvarez wa Atletico Madrid.
Barca ambayo inapambana kuweka sawa takwimu za mahesabu yake ya usajili pia inatajwa kuwa mawindoni kusaka beki wa kati baada ya Ronald Araujo kutimkia Liverpool.
Hata hivyo, bado mashabiki wa Barca wanasubiri mpaka mwisho juu ya hilo ili kupata uhakika kwani hivi karibuni nyota lukuki walihusishwa kuhamia kwao lakini mambo yalikwama hewani.
Real Madrid ambao wanatajwa pia kuhitaji huduma ya Rodri, ingawa kwa sasa ni kama imejiweka pembeni, yenyewe imekamilisha usajili wa winga Muivorycoast, Yan Diomande kutoka RB Leipzig.




