
LIGI Kuu ya Tanzania Bara inaendelea leo kwa mchezo mmoja mkoani Tanga.
Coastal Union itakuwa mwenyeji wa Yanga kwenye uwanja wa Mkwakwani.
Yanga itaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kuwakanda watani wa jadi Simba mabao 5-1 Novemba 5 kwenye uwanja Benjamin Mkapa, Dar es Salaam wakati Coastal Union ilitoka suluhu dhidi ya Namungo Novemba Mosi kwenye uwanja wake wa nyumbani.