Ligi KuuNyumbani

Prisons vs Azam mechi ya kibabe

NYASI za uwanja wa Sokoine jijini Mbeya leo zitawaka moto wakati Tanzania Prisons itakapoikaribisha Azam katika mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara.

Azam ipo nafasi ya 5 katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 8 baada ya michezo 4 wakati Prisons inashika nafasi ya 11 ikiwa na pointi 4 baada ya michezo 4 pia.

Mara ya mwisho timu hizo kukutana katika mchezo wa ligi kuu Juni 22, 2022 Azam iliifunga Prisons bao 1-0.

Azam na Tanzania Prisons zimekutana mara 13 huku Prisons ikiambulia ushindi mara 1 wakati Azam imeshinda mara 9 na michezo 3 zimetoka sare.

Katika mfululizo wa ligi hiyo Septemba 29 Ruvu Shooting ilitumia vizuri uwanja wa nyumbani baada ya kuichapa Coastal Union mabao 2-1 katika uwanja wa Uhuru.

Nayo Dodoma Jiji ikapata ushindi wa kwanza katika ligi baada ya kutoka kufua mbele dhidi ya Geita Gold kwa bao 1-0 katika uwanja wa Liti mjini Singida.

Related Articles

Back to top button