Filamu

Muigizaji David Hekili wa Lilo & Stitch, amefariki dunia

NEW YORK:MUIGIZAJI David Hekili Kenui Bell, anayejulikana katika Lilo & Stitch ya kampuni ya utengenezaji filamu ya Disney, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 57, dada yake, Jalene Kanani Bell, amethibitisha habari hizo kupitia ukurasa wake wa Facebook.

David Hekili ni muigizaji chipukizi aliyeibukia katika filamu hiyo dada yake amemkumbuka kwa maneno; “Ni kwa moyo mzito ninashiriki kwamba kaka yangu mkarimu, mwenye talanta, mcheshi, mwenye kipaji David H. K. Bell atatumia leo katika kampuni ya Baba yetu wa Mbinguni.”

“Nilikutana na kaka yangu nikiwa na miaka 18 bna sikuwa na baba yeye alinipa upendo usio na masharti ambao ningeweza kuuliza na ninaamini kwamba familia yake yote na marafiki walipokea vivyo hivyo kutoka kwake.”

Wiki mbili tu zilizopita, David alikuwa na familia yake usiku wa uzinduzi wa filamu ya Lilo & Stitch huko Kapolei, wakati aliposherehekea maoneesho yake ya kwanza kwenye skrini kubwa.

Kando ya uigizaji, David alifanya kazi kama msimamizi msaidizi wa uwanja wa ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ellison Onizuka Kona huko Keahole.

Mwezi uliopita David aliingia kwenye Instagram baada ya waigizaji wa Lilo & Stitch na wahudumu, akaandika: “Sasa, Mahalo kwa kila mtu aliyefanya kazi kwenye filamu hii! Nilijua itakuwa maalum kuhudhuria oneesho la Waigizaji na washiriki wengine na haikukatisha tamaa! Ilipendeza sana kuona nyota wengi huko Hawaii.”

Related Articles

Back to top button