World Cup

Kivumbi kukamilisha makundi kombe la dunia

MICHEZO ya kukamilisha mechi za makundi katika michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea Qatar inaanza leo.

Katika Kundi A wawakilishi wa Afrika Senegal itakamilisha mechi za makundi kwa kupambana na Ecuador wakati wenyeji wa michuano hiyo ambayo tayari imeondolewa Qatar itapambana na Uholanzi.

Kundi B litashuhudia Iran ikipambana na Marekani wakati England itavaana na Wales.

Brazil, Ufaransa na Ureno tayari zimefuzu hatua ya 16 bora.

 

Related Articles

Back to top button