Filamu

The Rock kutoka upya na ‘The Smashing Machine ’

NEW YORK: MWANA MIELEKA wa WWE, Dwayne Johnson maarufu The Rock anayefanya vizuri katika filamu za Hollywood anatarajiwa kuonekana katika tamthila ya MMA ‘The Smashing Machine’ amba oni mradi mpya kwake utakao muingizia fedha nyingi.

Kama ilivyoripotiwa kuwa Johnson ataonekana katika tamthilia hiyo iliyoandikwa na mwandishi anafanya vizuri katika uandishi wa tamthilia Zeke Goodman.

Tamthilia hiyo itafanyika Kusini mwa California ikionyesha mwanzoni mwa milenia ambapo kijana aliyetengwa anajikuta akishawishiwa na gwiji wa kutoa motisha kwa watu ambaye ndiye The Rock.

The Rock anatumia jina la Guru akionekana kama mrembo, lakini anatumia nafasi hiyo kujificha huku akifanya mambo yake nyuma ya pazia.

A24 ndiyo inayoandaa tamthilia hiyo na kuifadhili ikishirikiana na Shiny Penny Productions ya Stacey Sher, na Seven Bucks Productions ya Johnson mwenyewe.

Mwandishi Goodman alipata umaarufu katika filamu za Amazon ‘I Know What You Did Last Summer’ na ‘Cruel Intentions’.

Ingawa ‘The Smashing Machine’ na ‘Breakthrough’ zinaashiria kuondoka kwa Johnson, lakini awali alikiri akitamka demi-god Maui katika mfululizo wa filamu ya ‘Moana’ ya Disney huku akidai ilikuwa ni kubadilisha maisha tu.

Alipoulizwa Maui anamaanisha nini kwake, aliiambia HELLO ya Uingereza! Kucheza kwa Maui kumebadilisha maisha yake.

“Uzoefu wa filamu hizi mbili unaenda zaidi kuliko uhusika mwingine wowote ambao nimecheza, Huu ni utamaduni wangu. Yeye ni sehemu yangu,

“Tabia ya Maui imechochewa na babu, ambaye alikuwa Chifu Mkuu Peter Maivia. Ina maana kubwa kwangu.”

“Ninashukuru kuwa sehemu ya miradi mikubwa kwa miaka mingi, lakini naweza kusema ukweli kwamba, zaidi ya ‘Jumanji’, zaidi ya ‘Rampage’ au ‘Jungle Cruise’, yoyote kati ya hizo, jambo moja ambalo linasumbua akili za watu ni kwamba mimi ndiye mtu anayeimba katika filamu hizo.

The Rock pia atacheza Maui katika urejeshaji wa moja kwa moja wa ‘Moana’ na “amefurahishwa” sana na filamu hiyo.
Alisema: “Nimefurahishwa sana. Hadithi ya ‘Moana’ sisi sote tunaipenda, lakini ni ya moja kwa moja wakati huu.

“Siwezi kusema mengi, lakini tuna uongozaji mzuri wa Tommy Kail na ni muziki wa Lin-Manuel Miranda.
“Ni sherehe maalum sana ya hadithi ya kushangaza ambayo inasikika kwa kila mtu ulimwenguni,” alieleza The Rock.

Related Articles

Back to top button