Habari MpyaKwingineko

Rais uefa awatolea uvivu Saudi Arabia.

RAIS wa shirikisho  la soka barani Ulaya Aleksander Ceferin ametema nyongo kwa taifa la Saudi Arabia kwa kitendo chao cha kuendelea kuwasajili wachezaji wenye majina  makubwa kutoka Ulaya.

Cerefin amesema  usajili wanaofanya Saudi Arabia ni makosa makubwa kwenye soka lao kwani walipaswa kuwekeza kwenye soka la vijana kuliko kutumia fedha nyingi kuwasajili wachezaji ambao wanakaribia kumaliza soka lao.

“kununua wachezaji wanaomalizia soka lao sio mfumo wa kuendeleza soka, kosa kama hilo walilifanya China”,amesema Cerefin.

Timu mbalimbali kutoka Saudi Arabia zimetenga fungu la maana  kwa ajili ya kufanya usajili ambapo tayari nyota kadhaa wamenasa kwenye mtego wa pesa kutoka Uarabuni akiwemo Cristiano Ronaldo aliyenaswa na  Al-Nassr pamoja na  Karim Benzema aliyejiunga na Al- Ittihad.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button