Ligi KuuNyumbani

Prisons kuisweka gerezani Coastal leo?

LIGI Kuu ya soka Tanzania Bara inaendelea leo kwa mchezo mmoja jijini Mbeya.

Tanzania Prisons inaikaribisha Coastal Union katika uwanja wa Sokoine jijini humo.

Prisons inashika nafasi ya 8 ikiwa na pointi 14 baada ya michezo 10 wakati Coastal ipo nafasi 13 ikiwa na pointi 8 baada ya michezo 7.

Novemba 9 kulifanyika michezo miwili ya ligi hiyo ambapo Simba imetoka sare ya bao 1-1 na Singida Big Stars katika uwanja wa LITI mjini Singida huku Azam ikishinda mabao 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji katika uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Related Articles

Back to top button