
KLABU ya Mashujaa ya Kigoma imepanda daraja kucheza Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara msimu wa 2023/2024.
Mashujaa imefanikiwa kupanda daraja baada ya kuitoa Mbeya City kwa jumla ya magoli 4-1 katika michezo miwili ya mtoani ikishinda nyumba uwanja wa Lake Tanganyika 3-1 na leo kuifunga Mbeya City ugenini uwanja wa Sokoine goli 1-0.
Kwa matokeo hayo Mbeya City imeshuka daraja hivyo kucheza Ligi ya Championship msimu ujao.