
KLABU ya Yanga imetangaza kuachana na winga wake Dickson Ambundo
Ambundo alijiunga na Yanga mwaka 2021 akitokea Dodoma Jiji na sasa mabingwa hao wa kandanda la Tanzania wameamua kuachana na mchezaji huyo.
Kwenye taarifa iliyotolewa na Yanga kupitia ukurasa wao wa Instagram Usiku wa Juni 20 Yanga wamemshukuru nyota huyo.
” Tunamshukuru kwa mchango wake kipindi chote alichokuwa na yanga, tunamtakia kila lenye kheri katika maisha yake nje ya Yanga