Africa
Yanga yaondoka na pointi 1 Ghana
KLABU ya Yanga imetoka sare ya bao 1-1 na Medeama ya Ghana katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi kwenye uwanja wa Baba Yara uliopo mji wa Kumasi, Ghana.
Mchezo mwingine wa kundi D umezikutanisha Al Ahly iliyoikaribisha CR Belouizdad ambapo zimetoka suluhu.
Yanga itarudiana na Medeama Desemba 20 Dar es Salaam huku CR Belouizdad ikiikaribisha Al Ahly huko Algeria.
Msimamo wa kundi D ni kama ifuatavyo:
| # | TIMU | P | W | D | L | F | A | GD | PTS |
| 1 | Al Ahly | 3 | 1 | 2 | 0 | 4 | 1 | 3 | 5 |
| 2 | Medeama SC | 3 | 1 | 1 | 1 | 3 | 5 | -2 | 4 |
| 3 | CR Belouizdad | 3 | 1 | 1 | 1 | 4 | 2 | 2 | 4 |
| 4 | Yanga | 3 | 0 | 2 | 1 | 2 | 5 | -3 | 2 |




