EPL

Tottenham “Ni Janga”’

LONDON: MSHAMBULIAJI wa kulia wa Tottenham Hotspur, Pedro Porro, ameeleza kuwa msimu wa klabu hiyo katika Ligi Kuu ya England ni “janga” huku akiweka lawama kwa majeraha na ukosefu wa wachezaji wa akiba.

Tottenham, ambayo kwa sasa haina wachezaji 10 kutokana na majeraha, haijashinda mechi ya ligi katika michezo 10 iliyopita na ipo nafasi ya 16 katika msimamo wa ligi.

Akizungumza kabla ya mechi ya nyumbani dhidi ya Crystal Palace Porro, 26, alisema : “Tuko na pointi moja tu juu ya kikomo cha kushuka daraja na siwezi hata kuelewa kinachoendelea. Hali yetu katika Ligi Kuu ni janga, na huo ndio ukweli. Ni hali ngumu. Wakati huna kikosi cha kushindana katika mashindano manne, ni vigumu.”

Porro alikosa mechi nne za ligi kutokana na jeraha la misuli kabla ya kurudi kucheza kwenye kipigo cha 2-1 cha Tottenham dhidi ya Fulham Jumapili iliyopita.

“Unapopitia wachezaji wote waliokuwa na majeraha na kuona wanaweza kucheza mechi za Ligi Kuu, unagundua tatizo,” Porro amesema.

“Ukiangalia kikosi cha awali (starting XI) unasema ‘wow!’ … Naona hapo ndipo tatizo lilipo.”

Tottenham ilitolewa katika raundi ya nne ya League Cup na Newcastle kabla ya kushindwa na Aston Villa katika raundi ya tatu ya FA Cup mwanzoni mwa mwaka huu.

“Ninaamini lazima uunde mradi wa kudumu ili kushindana kwa kila kitu,” Porro alisema. “Hali ile ile tulikuwa nayo msimu uliopita. Tulifanya vizuri katika Europa League na kuishinda, lakini katika Ligi Kuu, ilikuwa hadithi ile ile Tottenham walimaliza wa 17 msimu uliopita,.”

Related Articles

Back to top button