Filamu

Egbuson: Maisha yana siri nyingi sana

NIGERIA: MUIGIZAJI maarufu wa Nollywood Timini Egbuson amefichua kuwa aliwahi kukaribia kuiwakilisha Nigeria kwenye Big Brother Africa, lakini alitemwa.

Ameeleza kuwa kurudi nyuma kuligeuka kuwa baraka, kwani alioneshwa kipindi maarufu cha TV cha MTV Shuga Naija mwaka huo huo.

Akiongea katika kipindi cha hivi karibuni cha podcast ya Ligi ya Utamaduni, Egbuson alibainisha kuwa ingawa fursa zinazotokana na vikwazo, wakati mwingine zinaweza kutumika kama chachu ya mafanikio makubwa zaidi.

Amesema, “Nimejifunza kwamba wakati mwingine, fursa zilizopotea zinaweza kuwa baraka. Nina wafanyakazi wenzangu wengi ambao wamepata fursa ambazo watu walitaka pia.

“Lakini ninapotazama historia ya maisha yangu, baadhi ya mambo ambayo ningeweza kuyapata yangeniondoa kabisa hapa nilipo, na ninaamini kwamba nilipo leo ndipo nilipopangwa na Mungu.

“Ilitakiwa niwe kwenye Big Brother Africa miaka ya nyuma tulikuwa watano hivi tumefanya mambo yote muhimu wakatuomba tupaki virago tusubiri kuitwa ili nijiunge na kipindi, hata niliajiri mtu wa kusimamia mitandao yangu ya kijamii lakini hawakunichagua, nafikiri Tayo alienda, sina uhakika na nani alienda mwaka huo, lakini huo ndio mwaka ambao nilifanya kazi yangu ya MTV Shuga na MTV ndio nimezindua leo.

“Kama ningeendelea na Big Brother, kelele zingekuwa zimepungua kwa sasa au ningekuwa sijafanikiwa katika tasnia ya burudani. Kwa hivyo, wakati mwingine, unapopoteza fursa, lazima uhesabu kuwa ni baraka, kung’uta vumbi kwenye miguu yako na uendelee kusonga mbele.

Related Articles

Back to top button