Filamu

‘One Battle After Another’ ya Thomas Anderson kuwania tuzo za National Board of Review

LOS ANGELES: “One Battle After Another” imetajwa movie bora ya mwaka 2025 na National Board Review Awards ambayo pia mwanzo imeweza kupokea tuzo chini ya Director Paul Thomas Anderson.

Ni tuzo baada ya tuzo kwa filamu mpya alioigiza Leonardo DiCaprio, ambayo imeng’ara katika tangazo la tuzo za kifahari za National Board of Review (NBR) lililotolewa Jumatano huko Los Angeles.

Baada ya ushindi muhimu wa hivi karibuni katika tuzo za Gotham na New York Film Critics Circle, kasi ya filamu hiyo kutoka kwa mwandishi na mtayarishaji wa “Boogie Nights,” Anderson, iko juu zaidi kuliko wakati mwingine wowote, na wachambuzi wengi wakitabiri kuwa filamu hiyo inaweza pia kushinda tuzo kuu kwenye Oscars mwezi Machi.

Filamu imepata mafanikio makubwa kwa watazamaji na wakosoaji, ikipata asilimia 94 ya “fresh” kwenye tovuti ya Rotten Tomatoes, pamoja na sifa tele kwa uigizaji wa DiCaprio, Penn, Infiniti, Del Toro, Teyana Taylor na Regina Hall. “One Battle After Another” iliongoza katika kilele cha sanduku la mauzo (box office) ilipoingia kwenye majumba ya sinema Septemba, na hadi sasa imekusanya zaidi ya dola milioni 200 duniani kote.

Mbali na “One Battle After Another,” NBR iliorodhesha filamu 10 nyingine bora zaidi za mwaka: “Avatar: Fire and Ash,” “F1,” “Frankenstein,” “Jay Kelly,” “Marty Supreme,” “Rental Family,” “Sinners,” “Train Dreams,” “Wake Up Dead Man: A Knives Out Mystery,” na “Wicked: For Good.”

Washindi wa National Board of Review watasherehekewa rasmi katika sherehe itakayofanyika Januari 13 mjini New York, iliyoandaliwa na Willie Geist wa NBC News, siku mbili tu baada ya Golden Globes zitakazofanyika Los Angeles Januari 11.

Related Articles

Back to top button