Generated by All in One SEO v4.9.5.1, this is an llms.txt file, used by LLMs to index the site. # SpotiLEO Tanzania Standard Newspapers ## Sitemaps - [XML Sitemap](https://spotileo.co.tz/sitemap.xml): Contains all public & indexable URLs for this website. ## Posts - [Paula: Wiki nzima ni ya kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa](https://spotileo.co.tz/paula-wiki-nzima-ni-ya-kusherehekea-siku-yangu-ya-kuzaliwa/) - DAR ES SALAAM: Paul Kajala amesema wiki hii yote ni maalumu kwa ajili ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, huku akieleza kuwa anaadhimisha hatua mpya ya maisha yake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Paula aliandika: "This birthday week, I'm celebrating the woman I'm becoming," akimaanisha kuwa anasherehekea mwanamke anayezidi kuwa kadri siku zinavyosonga. Sambamba na - [Diamond, Zuchu, Abby Chams Wang'ara Tuzo za AFRIMMA 2026](https://spotileo.co.tz/diamond-zuchu-abby-chams-wangara-tuzo-za-afrimma-2026/) - DAR ES SALAAM: WASANII wa muziki kutoka Tanzania wameendelea kuonesha ushindani katika jukwaa la kimataifa baada ya jumla ya wasanii 11 kutajwa kuwania tuzo za African Muzik Magazine Awards (AFRIMMA) 2026, zitakazofanyika Septemba 12, 2026, jijini Dallas, Texas, Marekani. Kwa mujibu wa waandaaji wa tuzo hizo, Tanzania imepata uwakilishi mkubwa katika vipengele mbalimbali, ikiwemo vya - [Irene Uwoya: Sina shida na mtu,](https://spotileo.co.tz/irene-uwoya-sina-shida-na-mtu/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva na mwigizaji Irene Uwoya amesema kuwa hana tabia ya kuwa na migogoro na watu, akisisitiza kuwa yeye ni mtu wa upendo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Irene aliandika kuwa iwapo mtu ataonekana kuwa na shida naye, basi huenda ametumia muda na nguvu nyingi kutengeneza mgogoro huo. "Mimi sina - [BASATA yajadili kutangaza sanaa za Tanzania kupitia Miss World 2026](https://spotileo.co.tz/basata-yajadili-kutangaza-sanaa-za-tanzania-kupitia-miss-world-2026/) - DAR ES SALAAM: BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limeanza maandalizi ya kuitangaza Tanzania kupitia sanaa na ubunifu katika mashindano ya Miss World 2026, yatakayofanyika nchini Vietnam. Hatua hiyo imejiri baada ya Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Sanaa za Ufundi wa BASATA, Bona Masenge, kufanya mazungumzo na Miss World Tanzania 2026, Latricia Ian, pamoja na waratibu - [Praise: Utukufu wote ni wa Mungu, sitapunguza kasi baada ya ushindi wa BSS](https://spotileo.co.tz/praise-utukufu-wote-ni-wa-mungu-sitapunguza-kasi-baada-ya-ushindi-wa-bss/) - DAR ES SALAAM: MSHINDI wa shindano la Bongo Star Search 2026, Praise Wisdom, amesema ushindi alioupata ni matokeo ya neema ya Mungu na sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wake, huku akiahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii katika safari yake ya muziki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Praise amesema bado haamini ndoto yake ya kushinda shindano - [Hamad Furahisha atamba kumchapa Patrick](https://spotileo.co.tz/hamad-furahisha-atamba-kumchapa-patrick/) - DAR ES SALAAM: Bondia Hamad Furahisha, maarufu kwa jina la Mfupa wa Sokwe, ametamba kuwa atamfunza adabu mpinzani wake John Patrick katika pambano la Dar Boxing Derby litakalofanyika Julai 24, 2026, Ubungo jijini Dar es Salaam. Akizungumza wakati akiendelea na maandalizi ya pambano hilo nyumbani kwake Yombo Dovya, Temeke, Furahisha amesema wapinzani wake wamefanya makosa - [Wiki ya Simba kuzinduliwa Kreta ya Ngorongoro](https://spotileo.co.tz/wiki-ya-simba-kuzinduliwa-kreta-ya-ngorongoro/) - ARUSHA: Klabu ya Simba imechagua eneo la kipekee la Kreta ya Ngorongoro kuzindulia rasmi maadhimisho ya Wiki ya Simba mwaka huu, huku viongozi wakieleza kuwa tukio hilo linalenga kuunganisha michezo na utalii. Akizungumzia kuhusu maandalizi hayo, Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ally amesema uzinduzi utafanyika Julai 25 katika eneo la Hippo Pool (Ngoriktoktok) - [Judo yatakiwa kuleta dhahabu Jumuiya ya Madola](https://spotileo.co.tz/judo-yatakiwa-kuletea-dhahabu-jumuiya-ya-madola/) - DAR ES SALAAM: Serikali imewataka wachezaji wa timu ya taifa ya judo kupambana kwa nguvu zote katika Michezo ya Jumuiya ya Madola ili kuiletea Tanzania medali, ikisisitiza kuwa taifa lina matarajio makubwa kwao. Akizungumza wakati wa kutembelea kambi ya timu hiyo, Ofisa Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Oscar Zabron, amesema Serikali imewekeza - [Ulinzi waimarishwa mechi ya England na Argentina](https://spotileo.co.tz/ulinzi-waimarishwa-mechi-ya-england-na-argentina/) - ATLANTA: Mamlaka za usalama jijini Atlanta, Marekani, zimetangaza kuimarisha ulinzi kuelekea mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Dunia kati ya England na Argentina utakaochezwa Jumatano. Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na ukubwa wa mchezo huo na historia ndefu ya ushindani kati ya mataifa hayo mawili, ambayo pia yaliwahi kupigana Vita vya Falkland mwaka 1982. Polisi - [Norway yapokelewa kwa shwange na vifijo](https://spotileo.co.tz/norway-yapokelewa-kwa-shwange-na-vifijo/) - OSLO: Licha ya kutolewa kwenye robo fainali ya Kombe la Dunia 2026, timu ya taifa ya Norway imepokelewa kwa shangwe kubwa nyumbani, huku zaidi ya mashabiki 100,000 wakifurika mitaa ya jiji la Oslo kuwapongeza wachezaji kwa safari yao ya kihistoria. Norway iliondolewa na England kwa kufungwa mabao 2-1 baada ya muda wa nyongeza, lakini hilo - [Mbappe, Lamine Yamal uso kwa uso leo](https://spotileo.co.tz/mbappe-lamine-yamal-uso-kwa-uso-leo/) - DALLAS: Nyota wawili wanaotikisa soka duniani kwa sasa, Kylian Mbappe wa Ufaransa na Lamine Yamal wa Hispania, wanatarajiwa kukutana uso kwa uso katika pambano la nusu fainali ya Kombe la Dunia, huku kila mmoja akisaka kuiongoza timu yake kutinga fainali. Mbappe ameonesha makali makubwa mbele ya lango katika mashindano hayo, akifunga mabao nane kutokana na - [Azam yapigwa faini ya Sh. milioni 50](https://spotileo.co.tz/azam-yapigwa-faini-ya-sh-milioni-50/) - DAR ES SALAAM: KAMATI ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeitoza Azam FC faini ya Sh milioni 50 baada ya klabu hiyo kukataa kushiriki kwenye sherehe za kukabidhiwa tuzo na zawadi kufuatia fainali ya Kombe la Shirikisho la Benki ya CRDB iliyochezwa Julai 4, 2026, Uwanja wa Gombani, Pemba. Katika mchezo - [Her Initiative kujengea ujuzi wanawake 50](https://spotileo.co.tz/her-initiative-kujengea-ujuzi-wanawake-50/) - DAR ES SALAAM: Shirika la Her Initiative limechagua wanawake vijana 50 kujiunga na programu ya Panda Academy inayolenga kuwajengea uwezo wa kubadili bidhaa na vipaji vyao kuwa biashara zenye chapa imara, ushindani na uwezo wa kukua katika soko. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Her Initiative, Lydia Charles Moyo, - [Kingo: Tasnia ya filamu, tamthilia yahitaji kuungwa mkono](https://spotileo.co.tz/kingo-tasnia-ya-filamu-tamthilia-yahitaji-kuungwa-mkono/) - DARE ES SALAAM: Mchora katuni maarufu na muigizaji wa tamthilia mbalimbali nchini, Abdul Kingo, amesema tasnia ya filamu na tamthilia nchini inaendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo, lakini inahitaji kuungwa mkono na wadau mbalimbali ili kufikia malengo ya kukuza ubora, ajira na ushindani katika soko la ndani na kimataifa. Abdul Kingo alitoa kauli hiyo alipotembelea - [Bambo aipongeza Simba, Mangungu kutwaa Kombe la Shirikisho FA](https://spotileo.co.tz/bambo-aipongeza-simba-mangungu-kutwaa-kombe-la-shirikisho-fa/) - DAR ES SALAAM: Muigizaji wa vichekesho na shabiki wa klabu ya Simba, Dickson Makwaya maarufu Bambo, ameipongeza timu hiyo kwa kutwaa Kombe la Shirikisho FA. Bambo amesema ushindi huo ni ishara ya kurejea kwa timu katika ushindani na unapaswa kuwa chachu ya mafanikio makubwa zaidi kwa mwakani. Bambo, ambaye alionekana akiwa pamoja na Mwenyekiti wa - [Picha za Zari, Shakib zazua minong’ono mtandaoni](https://spotileo.co.tz/picha-za-zari-shakib-zazua-minongono-mtandaoni/) - KAMPALA: Baada ya kutangaza kuachana mwezi uliopita kutokana na kile walichokiita tofauti zisizoweza kusuluhishwa, mastaa wa Afrika Mashariki Zari Hassan maarufu kama Zari The Boss Lady na mumewe Shakib Cham wamezua gumzo jipya kufuatia kusambaa kwa picha mpya zinazowaonesha wakiwa pamoja kwa ukaribu nchini Uganda. Picha hizo, ambazo zimesambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, - [Aly Mayai ashangazwa Samatta kustaafu timu ya Taifa](https://spotileo.co.tz/aly-mayai-ashangazwa-samatta-kustaafu-timu-ya-taifa/) - DAR ES SALAAM: Mchambuzi wa masuala ya soka, Aly Mayai, amesema ameshtushwa na uamuzi wa nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta, kutangaza kustaafu kuitumikia timu ya taifa, akieleza kuwa bado alikuwa na uwezo mkubwa wa kuendelea kuisaidia Tanzania katika mashindano ya kimataifa. Akizungumza kuhusu uamuzi huo, Aly Mayai alisema Samatta ni mmoja wa wachezaji walioiletea - [Uhuru Seleman aomba kukutana na Waziri Makonda](https://spotileo.co.tz/uhuru-seleman-aomba-kukutana-na-waziri-makonda/) - DAR ES SALAAM: Mchezaji wa zamani wa Simba na kocha wa viungo wa Klabu ya KMC, Uhuru Seleman, amesema anatamani kupata nafasi ya kukutana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Paul Makonda, akiamini anaweza kumsaidia kupata suluhisho la tatizo la goti ambalo limekuwa likimsumbua kwa muda mrefu. Uhuru alisema anaamini mazungumzo ya ana - [Manqoba: Nimekuja kuifanya Yanga itawale Afrika](https://spotileo.co.tz/manqoba-nimekuja-kuifanya-yanga-itawale-afrika/) - DAR ES SALAAM: Kocha mpya wa Yanga, Manqoba Mngqithi, amesema amekuja ndani ya klabu hiyo kutimiza ndoto ya kuifanya itawale soka la Afrika, akieleza kuwa lengo lake kuu ni kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League). Kupitia mtandao wake, amesema ameifuatilia Yanga kwa muda mrefu na anatambua ukubwa wa klabu hiyo, jambo - [Msuva atua Newroz FC baada ya kung'ara Al Talaba](https://spotileo.co.tz/msuva-atua-newroz-fc-baada-ya-kungara-al-talaba/) - BAGHDAD: Mchezaji wa Taifa Stars, Simon Msuva, ameanza ukurasa mpya wa maisha yake ya soka baada ya kujiunga na klabu ya Newroz FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Iraq, akitokea Al Talaba FC ya nchini humo. Uhamisho huo umekamilika kuelekea msimu mpya wa mashindano. Mshambuliaji huyo wa Tanzania anajiunga na Newroz akiwa na rekodi nzuri kutoka - [Kiungo wa Afrika Kusini Jayden Adams afariki dunia](https://spotileo.co.tz/kiungo-wa-afrika-kusini-jayden-adams-afariki-dunia/) - JOHANNESBURG: Soka la Afrika Kusini limegubikwa na majonzi kufuatia kifo cha kiungo wa klabu ya Mamelodi Sundowns na timu ya taifa ya Afrika Kusini (Bafana Bafana), Jayden Adams, aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 25. Adams amefariki siku chache baada ya kuisaidia Afrika Kusini katika fainali za Kombe la Dunia 2026, ambapo alicheza mechi - [Hamisa Mobetto: Bima iliokoa gari langu baada ya ajali](https://spotileo.co.tz/hamisa-mobetto-bima-iliokoa-gari-langu-baada-ya-ajali/) - DAR ES SALAAM: Mwanamitindo, Hamisa Mobetto, amesema huduma ya bima ilimsaidia kuepuka hasara baada ya gari lake kupata ajali. Hamisa ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kutangazwa rasmi kuwa balozi wa kampeni ya "Upo Salama". Amesema kama asingekuwa na bima, angelazimika kutumia fedha nyingi kutengeneza gari lake. "Nilipata ajali iliyosababishwa - [Mbappe ang'ara, Deschamps akoshwa](https://spotileo.co.tz/mbappe-angara-deschamps-akoshwa/) - FOX BOROUGH: Nahodha wa Ufaransa, Kylian Mbappe, alifidia kukosa mkwaju wa penalti kwa kufunga bao la kuvutia lililoiongoza timu yake kuichapa Morocco mabao 2-0 na kutinga nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026. Katika mchezo wa robo fainali uliochezwa usiku wa Julai 9 mjini Foxborough, Massachusetts, Marekani, Mbappe aliifungia Ufaransa bao la kwanza dakika ya - [Hispania, Ubelgiji kukiwasha leo kusaka nusu fainali Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/hispania-ubelgiji-kukiwasha-leo-kusaka-nusu-fainali-kombe-la-dunia/) - LOS ANGELES: Mabingwa wa Ulaya, Hispania, watashuka dimbani leo kuikabili Ubelgiji katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Dunia 2026 wakisaka tiketi ya kutinga nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu walipotwaa taji hilo mwaka 2010. Mchezo huo utakaopigwa katika Uwanja wa Los Angeles nchini Marekani unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku mshindi akikutana - [Chapo aahidi kumaliza pambano mapema](https://spotileo.co.tz/chapo-aahidi-kumaliza-pambano-mapema/) - DAR ES SALAAM: Bondia Mohamed Chapo wa Masaki amemjibu mpinzani wake Bakari Kibiki maarufu kama Simba wa Kigamboni, akiahidi kumaliza pambano lao kabla halijafika mwisho katika tamasha la Dar Boxing Derby litakalofanyika Julai 24, 2026 Dar es Salaam. Akizungumza wakati akiendelea na maandalizi yake, Chapo amesema amesikia maneno na tambo za mpinzani wake, lakini anaamini - [Ahoua, Belouizdad wapeana mkono wa kwaheri](https://spotileo.co.tz/ahoua-belouizdad-wapeana-mkono-wa-kwaheri/) - ALGIERS: RASMI klabu ya CR Belouizdad ya Algeria imethibitisha kuachana na kiungo mshambuliaji wa Ivory Coast, Jean Charles Ahoua. Belouizdad imetangaza kuachana na Ahoua kupitia majukwaa yake ya mitandao ya kijamii baada ya pande hizo mbili kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba. Taarifa zaidi zinafafanua kuwa Ahoua ameondoka baada ya kutoridhishwa na mazingira ya timu hiyo - [Klopp: Tulizunguka na Mbappe kwenye ndege, kisha akaenda PSG](https://spotileo.co.tz/klopp-tulizunguka-na-mbappe-kwenye-ndege-kisha-akaenda-psg/) - BOSTON: BAADA ya mechi ya usiku wa kuamkia leo ambayo Ufaransa iliikunyuga Morocco mabao 2-0, Kylian Mbappe alikuwa na kocha Jurgen Klopp wakionesha kidole jukwaani na kucheka. Kicheko hicho nyuma yake kina stori kubwa kwani walikuwa wakionyeshana mama yake Mbappe, Fayza na kukumbuka mwaka 2017 Liverpool ilipotaka kumsajili nahodha huyo wa Ufaransa na kugonga mwamba. - [Jua Kali aahidi makubwa miaka 30 ya Bongo fleva](https://spotileo.co.tz/jua-kali-aahidi-makubwa-miaka-30-ya-bongo-fleva/) - MSANII wa muziki kutoka Kenya, Paul Nunda maarufu kwa jina la Jua Kali, amewasili jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya maandalizi ya kushiriki Tamasha la Miaka 30 ya Bongo Fleva litakalofanyika kesho, Julai 10, 2026, katika Ukumbi wa Mlimani City. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokelewa, Jua Kali ali amesema - [Ray C: Msiite msanii wa zamani, mlichelewa kuja mjini](https://spotileo.co.tz/ray-c-msiite-msanii-wa-zamani-mlichelewa-kuja-mjini/) - MSABNII wa muziki wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, amesema hataki kuitwa msanii wa zamani au mkongwe, akieleza kuwa matumizi ya kauli hiyo hayampi heshima anayostahili na mara nyingi hutumiwa na watu walioingia kwenye tasnia ya muziki baadaye. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Ray C alisema anapinga tabia ya baadhi - [Collina: Hakuna anayeweza kuhoji uadilifu wa waamuzi Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/collina-hakuna-anayeweza-kuhoji-uadilifu-wa-waamuzi-kombe-la-dunia/) - GEORGIA: Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ya FIFA, Pierluigi Collina, ametoka hadharani na kufafanua sababu za kukataliwa kwa bao la Misri dhidi ya Argentina baada ya mapitio ya VAR kwenye mchezo wa Kombe la Dunia 2026. Collina ameeleza hayo baada ya Shirikisho la Soka Misri (EFA), kumlaumu mwamuzi wa mechi hiyo ya hatua ya 16 - [Balozi Yakubu, TFB na Ufaransa waweka mikakati kukuza sekta ya filamu](https://spotileo.co.tz/balozi-yakubu-tfb-na-ufaransa-waweka-mikakati-kukuza-sekta-ya-filamu/) - DAR ES SALAAM: BALOZI wa Tanzania nchini Ufaransa, Saidi Othman Yakubu, na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (TFB), Dk. Gervas Kasiga, wameweka mikakati ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ufaransa kwa lengo la kukuza sekta ya filamu na kuitangaza Tanzania kimataifa. Katika kikao kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania mjini Paris, viongozi hao - [Nsangazelu: Serengeti Boys wanaimarika](https://spotileo.co.tz/nsangazelu-serengeti-boys-wanaimarika/) - CHINA: Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Elieneza Nsangazelu, amesema ameridhishwa na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake katika ushindi dhidi ya China, akieleza kuwa timu ilitekeleza vyema mpango wa mchezo licha ya ushindani mkubwa. Katika mechi hiyo Jana, Serengeti iliibuka na ushindi wa mabao 2-0. Akizungumza baada ya mchezo huo, Nsangazelu amesema Serengeti Boys ilitawala umiliki - [Nsajigwa ana matumaini Prisons kubaki Ligi Kuu](https://spotileo.co.tz/nsajigwa-ana-matumaini-prisons-kubaki-ligi-kuu/) - MBEYA: KOCHA Mkuu wa Tanzania Prisons, Shadrack Nsajigwa, amesema bado ana matumaini timu yake kubaki katika Ligi Kuu licha ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Mbeya City katika mchezo wa mtoano wa kuwania nafasi ya kubaki ligi hiyo. Matokeo hayo yameihakikishia Mbeya City kuendelea kushiriki Ligi Kuu msimu ujao. Ni baada ya awali kushinda - [Serikali Morocco yakana uvumi wa kuikataa Afrika](https://spotileo.co.tz/serikali-morocco-yakana-uvumi-wa-kuikataa-afrika/) - RABAT: Serikali ya Morocco imekanusha taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa Waziri wa Michezo, Mohamed Berrada alisema taifa hilo haliiwakilishi Afrika katika Michuano ya Kombe la Dunia na haihitaji uungwaji mkono wa mataifa mengine ya bara hilo. Katika ufafanuzi uliotolewa na wizara hiyo, Berrada amesema hajawahi kutoa kauli yoyote kwa chombo chochote cha - [Ufaransa, Morocco mechi ya kibabe Leo](https://spotileo.co.tz/ufaransa-morocco-mechi-ya-kibabe-leo/) - BOSTON: Ufaransa na Morocco zinakutana leo katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Dunia 2026 utakaopigwa kwenye Uwanja wa Boston Stadium, Foxborough, Marekani, huku kila timu ikisaka tiketi ya kufuzu nusu fainali. Ufaransa ni miongoni mwa timu zinazopewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa, imekuwa katika kiwango bora baada ya kushinda michezo yake yote mitano - [Raga yajivunia hatua ya kihistoria Burundi](https://spotileo.co.tz/raga-yajivunia-hatua-ya-kihistoria-burundi/) - DAR ES SALAAM: LICHA ya timu ya taifa ya Rugby (raga) kutofanya vizuri kimataifa, Chama cha Rugby Tanzania (TRU) kimesema timu za taifa za wanaume na wanawake katika mashindano ya Burundi Cross-Border Rugby 7s zimeweka historia muhimu katika maendeleo ya mchezo huo nchini. Mashindano hayo yaliyofanyika jijini Bujumbura yalizikutanisha timu za taifa kutoka Burundi, Uganda, - [Moallin: Changamoto zimetumarisha](https://spotileo.co.tz/moallin-changamoto-zimetumarisha/) - DAR ES SALAAM: Kocha wa Yanga, Abdi Hamid Moallin, amesema msimu wa 2025/26 ulikuwa mrefu na wenye changamoto nyingi, lakini changamoto hizo zimeifanya timu kuwa imara zaidi na hatimaye kufanikiwa kutwaa ubingwa wa tano mfululizo. Akizungumza Dar es Salaam Moallin amesmea kwa sasa anaelekea mapumzikoni baada ya msimu kumalizika, huku uongozi wa klabu ukiendelea na - [Samatta aaga, wadau wamsihi asubiri Afcon](https://spotileo.co.tz/samatta-aaga-wadau-wamsihi-asubiri-afcon/) - DAR ES SALAAM: UAMUZI wa nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta kutangaza kustaafu kuitumikia timu ya taifa umeibua hisia na maoni mbalimbali kutoka kwa viongozi wa Serikali, wadau wa soka na wachezaji, wengi wao wakimtaka afikirie upya kabla ya kufanya uamuzi wa mwisho. Miongoni mwa waliotoa maoni yao ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa - [Hossam akerwa na waamuzi](https://spotileo.co.tz/hossam-akerwa-na-waamuzi/) - ATLANTA: Kocha wa Misri Hossam Hassan amesema hatafuatilia tena mechi zilizobaki za Kombe la Dunia 2026 baada ya timu yake kuondolewa kwa maumivu katika hatua ya 16 bora. Misri ilikuwa njiani kuandika historia baada ya kuongoza mabao 2-0 hadi dakika za mwisho, lakini ilishuhudia Argentina ikigeuza mchezo na kushinda kwa mabao 3-2 yaliyofungwa katika dakika - [Baba ake Neymar amkingia kifua mwanae](https://spotileo.co.tz/baba-ake-neymar-amkingia-kifua-mwanae/) - Baba wa nyota wa Brazil, Neymar Jr., Neymar Santos Sr. amemtaka mwanawe asiache kucheza soka licha ya Brazil kutolewa na Norway katika hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia 2026. Neymar Jr aliingia kipindi cha pili akitokea benchi na kufunga bao la kufutia machozi kwa mkwaju wa penalti, lakini halikutosha kuizuia Brazil kupoteza kwa - [Hossam: FIFA inamlinda Messi](https://spotileo.co.tz/hossam-fifa-inamlinda-messi/) - ATLANTA: Kocha Mkuu wa Misri, Hossam Hassan, amelishutumu Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kwa kile alichodai kuwa linalinda maslahi yake kwa kuhakikisha nahodha wa Argentina, Lionel Messi, anaendelea kubaki kwenye Kombe la Dunia la 2026. Hossam alitoa kauli hiyo kwa hasira baada ya Misri kuondolewa katika hatua ya 16 bora kufuatia kupoteza kwa mabao 3-2 - [Dayna Nyange ajivunia binti yake, akumbushia maumivu](https://spotileo.co.tz/dayna-nyange-ajivunia-binti-yake-akumbushia-maumivu/) - MOROGORO: Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Dayna Nyange, ameonesha furaha na shukrani baada ya binti yake, Rahma, kufaulu mtihani wa Kidato cha Sita kwa Daraja la Kwanza katika tahasusi ya Fizikia, Kemia na Baiolojia (PCB). Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Dayna amesema mafanikio hayo ni zawadi kubwa kutoka kwa Mungu na - [TSA yatangaza kikosi Mashindano ya kuogelea Kanda ya tatu](https://spotileo.co.tz/tsa-yatangaza-kikosi-mashindano-ya-kuogelea-kanda-ya-tatu/) - DAR ES SALAAM: Shirikisho la Kuogelea Tanzania (TSA) limetangaza kikosi kitakachoiwakilisha nchi katika Mashindano ya Kuogelea Kanda ya tatu Afrika, yatakayowakutanisha waogeleaji bora kutoka mataifa mbalimbali ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuregenzi wa Elimu na Maendeleo wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA) Jeremiah Keema, msafara wa Tanzania - [Ronaldo amaliza safari ya Kombe la Dunia kwa machozi, Hispania yatinga robo fainali](https://spotileo.co.tz/ronaldo-amaliza-safari-ya-kombe-la-dunia-kwa-machozi-hispania-yatinga-robo-fainali/) - DALLAS: Safari ya nguli wa soka duniani, , katika Kombe la Dunia imefikia tamati kwa huzuni baada ya Ureno kuchapwa bao 1-0 na Hispania katika hatua ya 16 Bora. Bao la dakika za nyongeza lililofungwa na Mikel Merino liliihakikishia Hispania nafasi ya robo fainali, huku Ronaldo akionekana akitokwa na machozi baada ya filimbi ya mwisho, - [Marekani yatolewa kwa aibu, Ubelgiji yatinga robo fainali](https://spotileo.co.tz/marekani-yatolewa-kwa-aibu-ubelgiji-yatinga-robo-fainali/) - SEATTLE: Ndoto ya Marekani ya kutwaa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza imefikia tamati baada ya kuchapwa mabao 4-1 na Belgium katika hatua ya 16 Bora, matokeo yaliyoipeleka Ubelgiji robo fainali kukutana na Hispania. Marekani, ambao walikuwa wakicheza mbele ya mashabiki wao, walionekana kupoteza mwelekeo tangu dakika za mwanzo, huku Ubelgiji ikitumia makosa ya - [BMT yatafuta fursa Paris za ushirikiano](https://spotileo.co.tz/bmt-yatafuta-fursa-paris-za-ushirikiano/) - PARIS: KATIBU Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha, ametembelea Taasisi ya Taifa ya Utaalamu na Uendelezaji Bora wa Michezo ya Ufaransa (INSEP) kwa lengo la kutafuta fursa za ushirikiano zitakazowezesha kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya michezo pamoja na kuboresha matokeo ya wanamichezo wa Tanzania. INSEP ni taasisi yenye mchango mkubwa - [Lemah: Tuzo hii ni chachu kuendelea kumtumikia Mungu](https://spotileo.co.tz/lemah-tuzo-hii-ni-chachu-kuendelea-kumtumikia-mungu/) - BAGAMOYO: Mshindi wa tuzo ya Muimbaji bora wa Kiume katika tuzo za TASUBA Awards 2026, Erick Lemah amesema hatua hiyo ni neema ya Mungu na chachu ya kuendelea kumtumikia kupitia muziki wa Injili. Akizungumza na Spoti Leo, Erick amesema anajivunia ushindi huo huku akimpa Mungu utukufu kwa mafanikio aliyoyapata. "Kwa unyenyekevu mkubwa namshukuru Mungu kwa - [Rais Samia amjulia hali Pacome Aga Khan, ampa pole](https://spotileo.co.tz/rais-samia-amjulia-hali-pacome-hospitali-ampa-pole/) - DAR ES SALAAM: Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amemtembelea na kumpa pole kiungo wa Yanga, Pacome Zouzoua, ambaye anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, kufuatia majeraha aliyoyapata katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya JKT Tanzania. Rais Samia alipata fursa ya kumjulia hali Pacome alipokuwa hospitalini hapo kumtembelea Sheikh Rashid - [Ronaldo kuibeba Ureno leo?](https://spotileo.co.tz/ronaldo-kuibeba-ureno-leo/) - ARLINGTON: Macho ya dunia leo yataelekezwa kwenye Uwanja wa Dallas, Arlington, Marekani, ambako Ureno na Hispania zitamenyana katika hatua ya 16 Bora ya Kombe la Dunia 2026 kwenye pambano linalotarajiwa kuwa kali kutokana na ushindani wa muda mrefu kati ya mataifa hayo jirani. Mchezo huo utaweka uso kwa uso nyota mkongwe Cristiano Ronaldo wa Ureno - [Waamuzi wa Kuogelea Kukutana Dar kuboresha Ufanisi](https://spotileo.co.tz/waamuzi-wa-kuogelea-kukutana-dar-kuboresha-ufanisi/) - DAR ES SALAAM: SHIRIKISHO la Michezo ya Maji Afrika kwa kushirikiana na Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA) limeandaa kliniki maalumu ya mafunzo kwa waamuzi na maofisa wa kiufundi wa mchezo wa kuogelea yenye lengo la kuongeza ujuzi na kuboresha viwango vya usimamizi wa mashindano barani Afrika. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TSA, mafunzo hayo - [Tonny Rashid kumvaa Juma Choki Dar Boxing Debi](https://spotileo.co.tz/tonny-rashid-kumvaa-juma-choki-dar-boxing-debi/) - DAR ES SALAAM: BONDIA Tonny Rashid amerejea nchini akitokea Afrika Kusini baada ya kukamilisha kambi ya maandalizi kuelekea pambano lake dhidi ya Juma Choki litakalofanyika Julai 24, 2026 katika tamasha la Dar Boxing Debi jijini Dar es Salaam. Akizungumza mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Rashid amesema - [Wadau wa soka wapinga uamuzi wa FIFA](https://spotileo.co.tz/wadau-wa-soka-wapinga-uamuzi-wa-fifa/) - SHIRIKISHO la Soka Duniani (FIFA) limekumbwa na wimbi la ukosoaji kutoka kwa viongozi wa soka na wadau mbalimbali baada ya kusitisha adhabu ya kufungiwa mechi moja kwa mshambuliaji wa Marekani, Folarin Balogun, hatua iliyomruhusu kucheza dhidi ya Belgium katika hatua ya 16 Bora ya Kombe la Dunia. Uamuzi huo ulifanyika baada ya taarifa kwamba Rais - [Wakati ni ukuta, kwa heri Neymar](https://spotileo.co.tz/wakati-ni-ukuta-kwa-heri-neymar/) - NEW JERSEY: Huenda isiwe simulizi tamu kwa masikio ya wapenda soka duniani kote, lakini huo ndio ukweli. Nyota aliyebebeshwa matumaini makubwa tangu ujana wake, Neymar da Silva Santos Júnior, ameucheza mchezo wake wa mwisho katika historia ya michuano ya Kombe la Dunia. Kutoka kwa kijana aliyeushangaza ulimwengu kwa kipaji chake cha kipekee, hadi kuwa mfungaji - [Dar City yaendeleza ubabe ligi ya mkoa](https://spotileo.co.tz/dar-city-yaendeleza-ubabe-ligi-ya-mkoa/) - DAR ES SALAAM: Timu ya mpira wa kikapu ya Dar City imeendelea kuonesha ubabe katika Ligi ya Mkoa wa Dar es Salaam baada ya kuifunga Pazi vikapu 66-51 katika mchezo uliopigwa jana. Mchezo huo ulikuwa wa ushindani mkubwa, huku kila timu ikipambana kusaka ushindi tangu mwanzo hadi mwisho. Hata hivyo, Dar City ilitumia ubora wake - [Prince Dube aiaga Yanga kwa hisia: Nitawabeba moyoni milele](https://spotileo.co.tz/prince-dube-aiaga-yanga-kwa-hisia-nitawabeba-moyoni-milele/) - DAR ES SALAAM: MSHAMBULIAJI wa Zimbabwe, Prince Dube, amewaaga mashabiki wa Yanga, maarufu kama Wananchi, baada ya kutambulishwa rasmi na klabu yake mpya ya Hardrock FC ya Zimbabwe. Dube amesema ameshindwa hata kupata maneno sahihi ya kuelezea namna anavyoihisi Yanga, akieleza kuwa klabu hiyo imekuwa zaidi ya timu ya mpira wa miguu kwake, bali ni - [Yanga yapigwa faini ya Sh milioni 100, Hersi apelekwa Kamati ya Maadili](https://spotileo.co.tz/yanga-yapigwa-faini-ya-sh-milioni-100-hersi-apelekwa-kamati-ya-maadili/) - DAR ES SALAAM:BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeitoza Yanga faini ya Sh milioni 100 na kuwapeleka Rais wa klabu hiyo, Hersi Said, pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu, Andre Mtine, katika Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kufuatia ukiukaji wa kanuni za matumizi ya vyumba vya kubadilishia nguo. Uamuzi huo - [Riyad Mahrez atangaza kustaafu kuichezea Algeria](https://spotileo.co.tz/riyad-mahrez-atangaza-kustaafu-kuichezea-algeria/) - BAADA ya safari ya Algeria kumalizika kwenye Kombe la Dunia, nahodha wa timu hiyo, Riyad Mahrez, ametangaza rasmi kustaafu kuichezea timu ya taifa. Mahrez alitoa taarifa hiyo mara baada ya Algeria kuondolewa kwenye mashindano hayo, akithibitisha kuwa mechi hiyo ndiyo ilikuwa ya mwisho kwake akiwa na jezi ya taifa lake. "Hii ilikuwa mechi yangu ya - [Simeone: Julián Álvarez ndiye mchezaji bora tuliyenaye Atlético](https://spotileo.co.tz/simeone-julian-alvarez-ndiye-mchezaji-bora-tuliyenaye-atletico/) - MADRID:KOCHA wa Atlético Madrid, Diego Simeone, amezungumzia kwa mara ya kwanza mustakabali wa Julián Álvarez tangu mshambuliaji huyo aombe kuondoka katika klabu hiyo majira haya ya joto. Akizungumza na ESPN, Simeone alimwaga sifa kwa nyota huyo wa Argentina na kueleza kuwa ni mchezaji muhimu sana ndani ya kikosi chake. "Julián ni mchezaji wa ajabu. Kwangu, - [Ronaldo amuenzi Jota baada ya ushindi dhidi ya Croatia](https://spotileo.co.tz/ronaldo-amuenzi-jota-baada-ya-ushindi-dhidi-ya-croatia/) - TORONTO:BAADA ya kuiongoza Ureno kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Croatia na kutinga hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia, Cristiano Ronaldo alitoa heshima maalumu kwa aliyekuwa mchezaji mwenzake, Diogo Jota. Mara baada ya mchezo kumalizika, Ronaldo alivaa jezi ya timu ya taifa ya Ureno yenye namba 21, namba aliyokuwa akiitumia Diogo Jota. - [Ibenge: Simba ni timu imara, lakini tupo tayari kutwaa ubingwa](https://spotileo.co.tz/ibenge-simba-ni-timu-imara-lakini-tupo-tayari-kutwaa-ubingwa/) - ZANZIBAR:KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema kikosi chake kipo tayari kwa pambano la fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB dhidi ya Simba, akisisitiza kuwa wanaiheshimu timu hiyo lakini wanaingia uwanjani kwa lengo la kutwaa ubingwa. Ibenge amesema Simba ni moja ya timu bora nchini, hivyo mchezo huo utahitaji maandalizi makubwa ya kiufundi - [Bao la Ronaldo dhidi ya Croatia laandika historia mpya Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/bao-la-ronaldo-dhidi-ya-croatia-laandika-historia-mpya-kombe-la-dunia/) - TORONTO:BAO alilofunga Cristiano Ronaldo kwenye ushindi wa mabao 2-1 wa Ureno dhidi ya Croatia limeandika historia mpya katika Kombe la Dunia 2026. Hilo lilikuwa bao la kwanza kabisa kwa Ronaldo kufunga katika hatua za mtoano za Kombe la Dunia tangu aanze kushiriki mashindano hayo, rekodi ambayo alikuwa hajawahi kuifikia katika michuano yake yote iliyopita. Bao - [Modrić aondoka akiwa ameandika historia kubwa ya Croatia](https://spotileo.co.tz/modric-aondoka-akiwa-ameandika-historia-kubwa-ya-croatia/) - TORONTO:KIUNGO wa Croatia, Luka Modrić, ameaga rasmi Kombe la Dunia baada ya safari yake ya miaka mingi kufikia mwisho. Akiwa na umri wa miaka 40, Modrić ameondoka akiwa mmoja wa wachezaji walioandika historia kubwa zaidi kwenye mashindano hayo, baada ya kushiriki Kombe la Dunia mara tano akiwa na timu ya taifa ya Croatia. Mafanikio yake - [Mshindi wa BSS msimu 16 kujulikana Julai 11](https://spotileo.co.tz/mshindi-wa-bss-msimu-16-kujulikana-julai-11/) - DAR ES SALAAM: Mshindi wa fainali ya Mashindano ya Bongo Star Search (BSS) Msimu wa 16 atajinyakulia zawadi ya Sh milioni 50 katika fainali itakayofanyika Julai 11, 2026, kwenye Ukumbi wa Haddypro, Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam. Akizungumza na Spoti LEO, Mkurugenzi wa Benchmark Productions, Ritha Paulsen, amesema maandalizi ya fainali hiyo yamefikia hatua - [Hersi, Arafat wapeta mchujo Yanga](https://spotileo.co.tz/hersi-arafat-wapeta-mchujo-yanga/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga imetangaza orodha ya wagombea waliopita katika mchujo wa awali wa uchaguzi wa viongozi wa klabu hiyo, huku Rais wa sasa, Hersi Said, akipitishwa kuwania tena nafasi ya urais. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Malangwe Mchungahela, mgombea Arafat Haji naye amepitishwa kuwania - [Pulisic: Tulionyesha Uimara Hata Baada ya Kubaki Wachezaji 10](https://spotileo.co.tz/pulisic-tulionyesha-uimara-hata-baada-ya-kubaki-wachezaji-10/) - CALIFORNIA: Nahodha wa Marekani, Christian Pulisic amesema ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Bosnia-Herzegovina umeonesha uimara wa kikosi chao baada ya kumaliza sehemu kubwa ya mchezo wakiwa pungufu kufuatia kadi nyekundu aliyopewa mshambuliaji Folarin Balogun. "Tulilazimika kupambana kwa nguvu ili kupata ushindi huu. Mambo hayakwenda kama tulivyopanga baada ya kadi nyekundu, lakini hiyo inaonyesha jinsi - [Jeshi Stars: Tutatetea ubingwa msimu ujao](https://spotileo.co.tz/jeshi-stars-tutatetea-ubingwa-msimu-ujao/) - DAR ES SALAAM: KAIMU Meneja wa Jeshi Stars, Charles Malima, amesema timu hiyo haitaridhika na ubingwa ilioutwaa msimu huu, badala yake imeanza maandalizi ya kuhakikisha inautetea katika msimu ujao. Malima amesema ubingwa huo umetokana na kazi kubwa, nidhamu na kujituma kwa wachezaji waliopambana katika msimu uliokuwa na ushindani mkali. Ameeleza kuwa mafanikio hayo yamechangiwa pia - [Tiger wa Tabata, Black watambiana Dar Boxing Derby](https://spotileo.co.tz/tiger-wa-tabata-black-watambiana-dar-boxing-derby/) - DAR ES SALAAM: BONDIA Ibrahim Paul, maarufu kama Tiger wa Tabata, amejibu tambo na vitisho vya mpinzani wake Abdullazack Hamis, anayefahamika kwa jina la Black Cobra wa Kimara, kuelekea pambano la Dar Boxing Derby litakalopigwa Julai 24, 2026, Dar es Salaam. Akizungumza akiwa kambini Tabata Kimanga wakati akiendelea na maandalizi ya pambano hilo, Tiger amesema - [Kane: Najivunia imani iliyooneshwa na wachezaji wenzangu](https://spotileo.co.tz/kane-najivunia-imani-iliyooneshwa-na-wachezaji-wenzangu/) - GEORGIA: Nahodha wa England, Harry Kane amesema anajivunia imani na moyo wa kupambana uliooneshwa na wachezaji wenzake baada ya kuiongoza timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya DR Congo na kutinga hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia. Kane aliibuka shujaa wa England kwa kufunga mabao mawili ndani ya dakika 11, - [Serikali kugharamia matibabu ya Mkubwa Fella](https://spotileo.co.tz/serikali-kugharamia-matibabu-ya-mkubwa-fella/) - DAR ES SAALAAM: WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Serikali itaanza kugharamia matibabu ya mdau wa muziki, Saidi Fella maarufu kama Mkubwa Fella, ambaye ana changamoto ya kiafya kwa muda mrefu. Makonda alitoa tamko hilo alipokutana na wasanii wa Bongo Fleva wanaojiandaa na tamasha la maadhimisho ya miaka 30 ya muziki - [Makonda: Njoeni tuenzi miaka 30 ya Bongo Fleva](https://spotileo.co.tz/makonda-njoeni-tuenzi-miaka-30-ya-bongo-fleva/) - DAR ES SALAAM: Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, ametoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha la kuadhimisha miaka 30 ya muziki wa Bongo Fleva litakalofanyika Julai 10 Mlimani City, akisema tukio hilo si la burudani pekee, bali ni fursa ya kutafakari historia na mchango wa muziki katika maendeleo ya - [Dk. Yonazi “Tutumie AFCON kama fursa ya kujitangaza kimataifa”](https://spotileo.co.tz/dk-yonazi-tutumie-afcon-kama-fursa-ya-kujitangaza-kimataifa/) - DAR ES SALAAM: Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Makatibu Wakuu ya Maandalizi ya Michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2027), Dk. Jim Yonazi, amesema michuano ya AFCON ni fursa adhimu ya kuitangaza Tanzania Kimataifa kupitia sekta mbalimbali ikiwemo - [Mexico yaweka rekodi mpya tangu Italia 1990](https://spotileo.co.tz/mexico-yaweka-rekodi-mpya-tangu-italia-1990/) - MEXICO:TIMU ya taifa ya Mexico inaendelea kuwa gumzo kubwa kwenye Kombe la Dunia 2026 kutokana na rekodi na kiwango kikubwa ilichokionesha tangu kuanza kwa mashindano hayo. Mexico sasa imefikisha mechi 10 za Kombe la Dunia katika Uwanja wa Azteca bila kupoteza hata moja, jambo linaloendelea kuifanya Azteca kuwa moja ya ngome ngumu zaidi katika historia - [olise aikaribia rekodi ya Pelé kombe la dunia](https://spotileo.co.tz/olise-aikaribia-rekodi-ya-pele-kombe-la-dunia/) - Michael Olise anaendelea kuwa mmoja wa wachezaji wanaovutia zaidi katika Kombe la Dunia 2026 kutokana na uwezo wake mkubwa wa kutengeneza mabao. Kiungo huyo wa Ufaransa tayari ametoa pasi nne za mabao ndani ya mechi nne za Kombe la Dunia, jambo lililomfanya kuwa kinara wa orodha ya watoa pasi za mabao kwenye mashindano hayo hadi - [Hakuna aliyewahi kufanya hivi kwenye Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/hakuna-aliyewahi-kufanya-hivi-kwenye-kombe-la-dunia/) - KYLIAN Mbappé ameendelea kuonesha kwa nini anatajwa kuwa mmoja wa wachezaji bora duniani baada ya kuweka rekodi mpya katika historia ya Kombe la Dunia. Mshambuliaji huyo wa Ufaransa sasa ndiye mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika hatua za mtoano za Kombe la Dunia, akiwa na mabao 9, rekodi iliyomfanya kuwazidi magwiji wa Brazil, Ronaldo Nazário - [Makonda: Tuhubiri amani na kumtanguliza Mungu kwenye saluni zetu](https://spotileo.co.tz/makonda-tuhubiri-amani-na-kumtanguliza-mungu-kwenye-saluni-zetu/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewataka wamiliki na wafanyakazi wa saluni nchini kumtanguliza Mungu katika shughuli zao za kila siku, akisisitiza kuwa mafanikio ya kweli yanatokana na kipaji alichowapa Mungu na si ushirikina. Makonda amesema kuwa tangu amelipopewa dhamana ya uwaziri ameendelea kumtanguliza Mungu, akieleza kuwa kufanya hivyo kumemfungulia - [Nduwumwe kinara wa mabao Ligi kuu](https://spotileo.co.tz/nduwumwe-kinara-wa-mabao-ligi-kuu/) - DAR ES SALAAM: PAZIA la msimu wa 2025/26 wa Ligi Kuu Tanzania Bara limefungwa huku mshambuliaji wa Singida Black Stars, Mossi Nduwumwe, akimaliza msimu akiwa kinara baada ya kufunga mabao 17. Kiungo wa Azam FC, Feisal Salum, amehitimisha msimu akiwa nafasi ya pili kwa mabao 15 na asisti tisa, huku Allan Okello wa Yanga SC - [JKT Tanzania yaomba radhi jeraha ya Pacome](https://spotileo.co.tz/jkt-tanzania-yaomba-radhi-jeraha-ya-pacome/) - DAR ES SALAAM: UONGOZI wa Klabu ya JKT Tanzania umeomba radhi kufuatia kuumia kwa kiungo wa Yanga SC, Pacome Zouzoua, katika mchezo wa kuhitimisha msimu wa 2025/26 wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa Juni 30, 2026 kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam. Pacome alipata jeraha baada ya kugongana na mchezaji wa JKT - [Yanga yatwaa ubingwa kwa rekodi, Mtibwa yashuka daraja](https://spotileo.co.tz/yanga-yatwaa-ubingwa-kwa-rekodi-mtibwa-yashuka-daraja/) - DAR ES SALAAM:YANGA imehitimisha msimu wa Ligi Kuu Bara kwa kishindo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa mwisho uliochezwa Uwanja wa Jenerali Isamuhyo, na kutwaa ubingwa kwa mara ya tano mfululizo huku ikiweka rekodi ya kufikisha pointi 75, idadi ambayo haijafikiwa na timu yoyote msimu huu. - [Makonda awataka wasusi na vinyozi kujiendeleza kielimu kukuza biashara zao](https://spotileo.co.tz/makonda-awataka-wasusi-na-vinyozi-kujiendeleza-kielimu-kukuza-biashara-zao/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewataka wasusi na vinyozi nchini kujiendeleza kielimu ili kuongeza ujuzi na kukuza biashara zao kwa kutoa huduma zenye viwango vya juu. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chama cha Salonist Tanzania, Makonda amesema taaluma ya ususi na unyoaji ina nafasi kubwa ya kuchangia uchumi, - [Mzee Yusuph: "Nikisoma mashairi yangu, hata mimi nashangaa nilivyoandika"](https://spotileo.co.tz/mzee-yusuph-nikisoma-mashairi-yangu-hata-mimi-nashangaa-nilivyoandika/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa muziki wa Taarab, Mzee Yusuph, amesema kwa sasa maisha yake yamebadilika na hafuati tena mambo aliyokuwa akiyapitia zamani. Akizungumza na Spoti leo kwa hisia, amesema kuwa kila anaposoma mashairi aliyowahi kuyaandika, hujikuta akijiuliza kama kweli ni yeye aliyeyaandika kutokana na uzito wa ujumbe uliomo. "Nikila ninapepewa na mwili na suguliwa, lakini - [Pazia la Ligi Kuu kuhitimishwa leo](https://spotileo.co.tz/pazia-la-ligi-kuu-kuhitimishwa-leo/) - DAR ES SALAAM: LIGI Kuu Bara inatarajiwa kutamatika leo Juni 30, 2026 ambapo Yanga itakuwa ugenini ikimechuana dhidi ya JKT Tanzania huku Simba ikiikaribisha KMC. Macho yote yatakuwa kwenye Uwanja wa Jenerali Isamuhyo kutazamia mchezo huo ambao utaamua hatma ya Yanga. Yanga inahitaji ushindi au sare tu kutangaza ubingwa wa tano mfululizo kwa maana hiyo - [Prisons, Best Six, Tai mabingwa wavu Dar](https://spotileo.co.tz/prisons-best-six-tai-mabingwa-wavu-dar/) - DAR ES SALAAM: TIMU za Jeshi Stars, Tanzania Prisons, Best Six na Tai zimetawazwa mabingwa wa Ligi ya Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam (DAREVA) kwa msimu wa 2026 katika makundi ya Seria A na Seria B. Katika Seria A, Jeshi Stars ilitwaa ubingwa wa wanaume huku Tanzania Prisons ikitwaa ubingwa wa wanawake. - [TPC yamteua Dk Janeth Mlay kwenye ufundi](https://spotileo.co.tz/tpc-yamteua-dk-janeth-mlay-kwenye-ufundi/) - DAR ES SALAAM: KAMATI ya Paralimpiki Tanzania (TPC) imefanya maboresho makubwa ya kiutawala na kiufundi kwa kumteua Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Janeth Mlay, kuwa Mkurugenzi wa Ufundi. Hii ni mara ya kwanza imeanzisha kamati ya ufundi itakayosimamia maandalizi ya wanamichezo kuelekea Michezo ya Paralimpiki ya Los Angeles 2028 (LA28). - [Serikali kutumia bilioni 15 kuondoa changamoto za matamasha Zanzibar](https://spotileo.co.tz/serikali-kutumia-bilioni-15-kuondoa-changamoto-za-matamasha-zanzibar/) - ZANZIBAR:SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema itatumia sh. bilioni 15 kujenga Kijiji cha Utamaduni kitakachoweka pamoja matamasha mbalimbali yanayofanyika visiwani humo, hatua inayolenga kumaliza changamoto ya ukosefu wa eneo la kudumu kwa ajili ya shughuli za sanaa na utamaduni. Akizungumza katika hafla ya kufunga Tamasha la 29 la Kimataifa la Filamu la Nchi za - [Namna Wahdzabe walivyofurahia chakula, muziki Zanzibar](https://spotileo.co.tz/namna-wahdzabe-walivyofurahia-chakula-muziki-zanzibar/) - ZANZIBAR:JAMII ya Wahadzabe kutoka mkoani Arusha ilikuwa miongoni mwa vivutio vya Tamasha la 29 la Kimataifa la Filamu la Nchi za Jahazi (ZIFF) 2026, ambapo walipata fursa ya kufurahia chakula na burudani ya muziki pamoja na washiriki wengine wa tamasha hilo. Wahadzabe walihudhuria tamasha hilo sambamba na maonesho ya filamu ya We Are Hadza, inayoangazia - [Comnet Zanzibar ndiyo mabingwa resi za Ngalawa 2026](https://spotileo.co.tz/comnet-zanzibar-ndiyo-mabingwa-resi-za-ngalawa-2026/) - ZANZIBAR:KAMPUNI ya Comnet Zanzibar imeibuka mabingwa wa mashindano ya resi za ngalawa yaliyofanyika katika ufukwe wa Serena, Unguja, Juni 28, 2026, ikiwa ni sehemu ya shughuli za kuhitimisha Tamasha la 29 la Kimataifa la Filamu la Nchi za Jahazi (ZIFF). Mashindano hayo yalishirikisha ngalawa 11 kutoka taasisi na kampuni mbalimbali, ambapo Comnet iliongoza mbio hizo - [Tamthilia ya Noma, Sultan Tamba zang’ara Tuzo za ZIFF 2026](https://spotileo.co.tz/tamthilia-ya-noma-sultan-tamba-zangara-tuzo-za-ziff-2026/) - ZANZIBAR:WASANII wa Tanzania, Uganda na Kenya wameibuka vinara katika Tuzo za Tamasha la Kimataifa la Filamu la Nchi za Jahazi (ZIFF) 2026 zilizohitimishwa usiku wa Juni 28, huku ushindi ukionesha ukuaji wa tasnia ya filamu Afrika na ushindani mkubwa kati ya kazi za kitaifa, Afrika Mashariki na bara zima. Miongoni mwa matukio makubwa ya tamasha - [Filamu ya Nigeria yashinda tuzo ya jumla ZIFF 2026](https://spotileo.co.tz/filamu-ya-nigeria-yashinda-tuzo-ya-jumla-ziff-2026/) - ZANZIBAR:FILAMU ya ‘A Land Apart’ kutoka Nigeria imeibuka mshindi wa tuzo ya juu zaidi katika Tamasha la 29 la Kimataifa la Filamu la Nchi za Jahazi (ZIFF) 2026 baada ya kutangazwa kuwa Filamu Bora ya Mwaka (Best Film) kwenye hafla ya utoaji wa tuzo iliyofanyika Juni 28 mjini Zanzibar. Filamu hiyo iliyoongozwa na Bem Pever - [Tamasha la ZIFF 2026 lazinduliwa kiaina](https://spotileo.co.tz/tamasha-la-ziff-2026-lazinduliwa-kiaina/) - ZANZIBAR:MSIMU wa 29 wa Tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar (ZIFF 2026) umezinduliwa kwa shamrashamra kubwa na maonesho ya kipekee ya utamaduni katika Ukumbi wa Wangazija wa Wakfu, huku ukiwakutanisha wasanii, watayarishaji wa filamu, wanadiplomasia na wadau wa sanaa kutoka mataifa mbalimbali duniani. Uzinduzi huo uliopambwa na burudani za asili za Kizanzibari, gwaride la - [Isarito: Wasanii tutumie Kiswahili kuitangaza Tanzania kimataifa](https://spotileo.co.tz/isarito-wasanii-tutumie-kiswahili-kuitangaza-tanzania-kimataifa/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa filamu za Bongo Movie, Isarito Mwakalindile, amewataka wasanii nchini kuendelea kutumia lugha ya Kiswahili katika kazi zao za sanaa ili kuitangaza lugha hiyo pamoja na kuitangaza Tanzania katika majukwaa ya kimataifa. Akizungumza na SpotiLeo, Isarito amesema Kiswahili ni moja ya alama muhimu za utambulisho wa Tanzania, hivyo matumizi yake katika - [Mzee Yusuph Mwinyi:Amani ianze ngazi ya familia](https://spotileo.co.tz/mzee-yusuph-mwinyiamani-ianze-ngazi-ya-familia/) - DAR ES SALAAM:MZEE Yusuph Mwinyi amesema kuwa matumizi ya maneno mabaya dhidi ya wengine ni uvunjifu wa amani unaoweza kusababisha hofu na wasiwasi katika jamii. Akizungumza na SpotiLeo, Mzee Yusuph amesema kuwa amani inapaswa kuanzia ndani ya familia kabla ya kuenea katika jamii na taifa kwa ujumla. Ameeleza kuwa hata kumfokea mke au mwanafamilia bila - [Kliniki ya raga kwa wanawake kuanza kesho](https://spotileo.co.tz/kliniki-ya-raga-kwa-wanawake-kuanza-kesho/) - DAR ES SALAAM: CHAMA cha Raga Tanzania (TRU), kupitia Idara ya Raga ya Wanawake, kinatarajia kuanza kliniki ya Raga ya Wanawake ya siku mbili yenye lengo la kukuza uwezo wa wachezaji na makocha wa raga nchini Tanzania. Kliniki hiyo itaendeshwa na Philadelphia Orlando, nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya wanawake ya Kenya (Kenya - [Wahadzabe Wanogesha Tamasha la ZIFF 2026](https://spotileo.co.tz/wahadzabe-wanogesha-tamasha-la-ziff-2026/) - ZANZIBAR:WASHIRIKI kutoka kabila la Wahadzabe wamekuwa kivutio kikubwa katika Tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar (ZIFF 2026), baada ya kuonesha utamaduni wao wa kipekee uliovutia mamia ya wageni waliohudhuria tamasha hilo visiwani Zanzibar. Wahadzabe hao, waliowasili kutoka Mkoa wa Arusha, walipata fursa ya kuonesha baadhi ya mila, desturi na mbinu zao za maisha ya - [Mwalimu aawapa zawadi marafiki zake](https://spotileo.co.tz/mwalimu-aawapa-zawadi-marafiki-zake/) - MOROGORO: MSHAMBULIAJI wa Simba, Seleman Mwalimu, amesema bao alilofunga katika mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar jana amelitoa kama zawadi maalumu kwa rafiki zake wa karibu Wilson Nangu pamoja na Montero ambao walimpa hamasa kubwa kabla ya mchezo. Seleman alisema Nangu ni mmoja wa watu wake wa karibu ambaye pia ni shabiki mkubwa wa Simba na - [Serikali kuipatia ZIFF eneo la kudumu](https://spotileo.co.tz/serikali-kuipatia-ziff-eneo-la-kudumu/) - ZANZIBAR:SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imepongeza mwendelezo wa matamasha makubwa ya sanaa yanayofanyika visiwani humo, ikieleza kuwa yamekuwa chachu ya ukuaji wa sekta ya utalii kwa kuvutia maelfu ya wageni kutoka ndani na nje ya nchi na hivyo kuongeza mchango wa utalii katika uchumi wa taifa. Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa msimu wa 29 - [Ibenge: Uchovu ulituathiri dhidi ya Yanga](https://spotileo.co.tz/ibenge-uchovu-ulituathiri-dhidi-ya-yanga/) - ZANZIBAR: KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema uchovu uliowakumba wachezaji wake kutokana na ratiba ya mechi kubana hatua iliyochangia kupoteza mchezo wao dhidi ya Yanga uliomalizika kwa kipigo cha mabao 3-0 jana kwenye Uwanja wa New Amaan Zanzibar. Akizungumza baada ya mchezo huo jana Ibenge amesema timu yake haikuanza vizuri mchezo huo na - [Tamasha la ZIFF 2026 lawaombea nguli wa filamu waliofariki dunia](https://spotileo.co.tz/tamasha-la-ziff-2026-lawaombea-nguli-wa-filamu-waliofariki-dunia/) - ZANZIBAR:KABLA ya kuwakaribisha watazamaji kushuhudia filamu ya kufungulia tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar (ZIFF 2026) Juni 24,2026 , Mkurugenzi wa Tamasha la ZIFF, Hatibu Madudu, aliusimamisha ukumbi uliokuwa na zaidi ya watu 300 kwa dakika moja ya ukimya ili kuwakumbuka na kuwaombea wasanii watatu nguli wa tasnia ya filamu Afrika mashariki waliofriki dunia - [Asikwambie mtu, kuaga kunaumiza bwana!](https://spotileo.co.tz/asikwambie-mtu-kuaga-kunaumiza-bwana/) - MEXICO CITY:SAFARI ya kipekee ya Guillermo Ochoa katika soka la kimataifa imekaribia kufikia mwisho baada ya golikipa huyo kuonekana kwa mara ya mwisho katika Kombe la Dunia akiwa na timu ya taifa ya Mexico. Ochoa mwenye umri wa miaka 40 aliingia uwanjani katika Kombe lake la Dunia la sita, hatua inayomuweka miongoni mwa wachezaji wachache - [Unashaanga hachezi vizuri kumbe kawekwa kwenye kibuyu](https://spotileo.co.tz/unashaanga-hachezi-vizuri-kumbe-kawekwa-kwenye-kibuyu/) - MGANGA wa jadi kutoka Ghana, Nana Kwaku Bonsam, amedai kuwa alitumia nguvu za kiroho kumzuia mshambuliaji wa England, Harry Kane, kufanya vizuri katika mchezo wa Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Ghana. Akizungumza baada ya mchezo huo, Bonsam alieleza kuwa alikuwa akifanya “kazi ya kiroho” kabla ya mechi hiyo kwa lengo la kumdhibiti Kane na - [Hii timu inagawa dozi bila kuangalia usoni](https://spotileo.co.tz/hii-timu-inagawa-dozi-bila-kuangalia-usoni/) - TIMU ya taifa ya Mexico imeonesha kuwa ni moja ya timu zinazopaswa kuogopwa katika Kombe la Dunia 2026 baada ya kutawala Kundi A na kumaliza hatua ya makundi kwa ushindi wa mechi zote tatu. Ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya timu ya taifa ya Czechia uliihakikishia Mexico kumaliza kileleni mwa kundi hilo, huku ikikusanya alama - [Chaba wa Wahdzabe alalamikia watu wanaomtumia mitandaoni bila ridhaa yake](https://spotileo.co.tz/chaba-wa-wahdzabe-alalamikia-watu-wanaomtumia-mitandaoni-bila-ridhaa-yake/) - ZANZIBAR:MWMBAJI maarufu kutoka jamii ya Wahadzabe, Chaba, ameeleza masikitiko yake kuhusu baadhi ya watu wanaotumia jina, picha na video zake kwenye mitandao ya kijamii bila kumhusisha wala kumpatia manufaa yoyote. Akizungumza wakati wa Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar, ZIFF 2026, Chaba alisema amekuwa akiona maudhui mengi yanayosambazwa mtandaoni yakimhusisha yeye na maisha ya jamii - [Charles M’Mombwa atua Zabbar St. Patrick](https://spotileo.co.tz/charles-mmombwa-atua-zabbar-st-patrick/) - VALLETA: KIUNGO wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Charles M’Mombwa amekamilisha usajili wake wa kujiunga na klabu ya Zabbar St. Patrick FC ya Malta. Kupitia taarifa rasmi ya klabu hiyo, Zabbar St. Patrick imeeleza kufurahishwa na ujio wa M’Mombwa mwenye umri wa miaka 28, ambaye anajiunga na timu hiyo baada ya kuwa na - [Jeraha la Koné Lamgharimu Madibo Mechi Tano](https://spotileo.co.tz/jeraha-la-kone-lamgharimu-madibo-mechi-tano/) - FIFA imemfungia mechi tano kiungo wa timu ya taifa ya Qatar, Assim Madibo, kufuatia tukio lililosababisha majeraha makubwa kwa kiungo wa Canada, Ismaël Koné, katika Kombe la Dunia 2026. Adhabu hiyo imekuja baada ya Koné kupata majeraha yatakayomuweka nje ya uwanja kwa takribani miezi mitano, jambo ambalo limekuwa pigo kubwa kwa Canada katika kipindi hiki - [Barnaba aingia rasmi kwenye Filamu,](https://spotileo.co.tz/barnaba-aingia-rasmi-kwenye-filamu/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Elias Barnaba, ametangaza rasmi kuingia katika tasnia ya filamu baada ya kuzindua tamthilia yake mpya ya Kikulacho Season 1 kupitia kampuni yake ya High Table Film. Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo, Barnaba amesema wengi hawafahamu kuwa safari yake ya sanaa ilianzia kwenye - [Isarito awakaribisha wageni kutembelea vivutio vya utalii Tanzania](https://spotileo.co.tz/isarito-awakaribisha-wageni-kutembelea-vivutio-vya-utalii-tanzania/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa filamu nchini, Isarito Mwakalindile, amewakaribisha wageni kutoka mataifa mbalimbali kutembelea Tanzania, akieleza kuwa nchi ina amani, vivutio vya kipekee vya utalii na mazingira rafiki yanayowawezesha wageni kufurahia uzuri wa maliasili, utamaduni na ukarimu wa Watanzania. Akizungumza na SpotiLeo, Isarito amesema Tanzania ni miongoni mwa mataifa yenye amani na utulivu mkubwa - [Lyanga: Tunahitaji ushindi kujiweka nafasi nzuri](https://spotileo.co.tz/lyanga-tunahitaji-ushindi-kujiweka-nafasi-nzuri/) - SINGIDA: MSHAMBULIAJI wa Singida Black Stars, Ayoub Lyanga, amesema kikosi chao kimejiandaa vizuri kuelekea mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Tanzania Prisons, huku akisisitiza kuwa wachezaji wote wana morali kubwa ya kuhakikisha wanapata ushindi. Lyanga amesema wanafahamu ugumu wa mchezo huo kutokana na Tanzania Prisons kupambana kuboresha nafasi yao kwenye msimamo wa ligi, lakini Singida - [TRA United na Coastal Union zapania pointi tatu Arusha](https://spotileo.co.tz/tra-united-na-coastal-union-zapania-pointi-tatu-arusha/) - ARUSHA: TRA United itakuwa nyumbani kesho Juni 24, 2026 kuikaribisha Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu, huku kila timu ikiingia uwanjani ikiwa na dhamira ya kuondoka na pointi tatu muhimu. Kocha wa TRA United, Etienne Ndayiragije, amesema maandalizi ya timu yake yamekamilika na kikosi kipo tayari kwa mchezo huo. Amesema kurejea kwa baadhi ya - [TPC yazindua mashindano ya Taifa ya Paralimpiki](https://spotileo.co.tz/tpc-yazindua-mashindano-ya-taifa-ya-paralimpiki/) - DAR ES SALAAM: KAMATI ya Paralimpiki Tanzania (TPC) imezindua rasmi mashindano ya Taifa ya watu wenye Ulemavu, yatakayokuwa msingi wa kuibua vipaji na kuandaa timu ya taifa kwa ajili ya Michezo ya Paralimpiki ya Los Angeles 2028 nchini Marekani. Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa TPC, Ramadhan Namkoveka, uamuzi huo wa kihistoria umeidhinishwa - [Yanga, Azam zatambiana, mechi ya presha, kisasi](https://spotileo.co.tz/yanga-azam-zatambiana-mechi-ya-presha-kisasi/) - ZANZIBAR: YANGA na Azam zinakutana tena kesho katika mchezo wa Ligi Kuu utakaochezwa kwenye Uwanja wa New Amaan Zanzibar. Timu hizo zimetoka kukutana katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho juzi ambapo Yanga ilipoteza mabao 3-2 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza. Kocha Mkuu wa Yanga, Abdihamid Moallin, amesema kikosi chake kiko tayari - [Huyu mwandishi wa habari hatakuja kusahau hii siku](https://spotileo.co.tz/21242-2/) - TEXAS:USHINDI wa Argentina dhidi ya Austria katika Kombe la Dunia 2026 ulileta furaha kubwa kwa mashabiki wa Albiceleste, lakini pia ulimzawadia mwandishi mmoja wa habari kumbukumbu ambayo huenda akaisimulia maisha yake yote. Mwandishi wa TyC Sports, Joaquín Bruno, alijikuta katikati ya tukio la kipekee baada ya Lionel Messi kufunga bao la pili lililoihakikishia Argentina ushindi - [Hakuna mashabiki wanaowazidi hawa kwa sasa](https://spotileo.co.tz/21235-2/) - NEW JERSEY:BAADA ya kusubiri kwa miaka 24 kurejea Kombe la Dunia, timu ya taifa ya Norway imehakikisha nafasi yake katika hatua ya mtoano na kuendelea kuwa moja ya timu zinazovutia mashindanoni humo. Mbali na ushindi wao uwanjani, mashabiki wa Norway wamevutia macho ya dunia kwa shangwe maarufu ya "Viking Row", ambayo imekuwa moja ya sherehe - [Doku arejea kambini baada ya kushuhudia kuzaliwa kwa mtoto wake](https://spotileo.co.tz/doku-arejea-kambini-baada-ya-kushuhudia-kuzaliwa-kwa-mtoto-wake/) - WINGA wa timu ya taifa ya Ubelgiji, Jérémy Doku, anatarajiwa kuungana tena na wenzake kambini baada ya kusafiri kwenda London kushuhudia kuzaliwa kwa mtoto wake wa kwanza wa kiume aliyepewa jina la Praise. Doku alipata ruhusa ya kuondoka kwa muda katika kambi ya Ubelgiji ili kuwa pamoja na familia yake katika tukio hilo muhimu. Hata - [Hii italeta shida ila ukweli ndio huo](https://spotileo.co.tz/hii-italeta-shida-ila-ukweli-ndio-huo/) - NAHODHA wa timu ya taifa ya Argentina, Lionel Messi, ameongeza tena sababu za kutajwa miongoni mwa wachezaji wakubwa zaidi katika historia ya soka baada ya kufikia takwimu ya kipekee katika Kombe la Dunia. Messi sasa ana mabao 12 aliyofunga katika Kombe la Dunia tangu alipofikisha umri wa miaka 35, idadi ambayo imezidi mabao yote aliyowahi - [Vita ya kiatu cha dhahabu imeanza mapema mno](https://spotileo.co.tz/vita-ya-kiatu-cha-dhahabu-imeanza-mapema-mno/) - MBIO za kuwania Kiatu cha Dhahabu katika Kombe la Dunia 2026 zimeanza kwa kasi ambayo haijawahi kuonekana kwa miaka mingi. Baada ya michezo miwili pekee ya hatua ya makundi, Lionel Messi tayari amefunga mabao matano, huku Erling Haaland na Kylian Mbappé wakifunga mabao manne kila mmoja. Kinachofanya takwimu hizi kuvutia zaidi ni kwamba katika Kombe - [‘Simba tunautaka ubingwa wa shirikisho’ Ahmed](https://spotileo.co.tz/simba-tunautaka-ubingwa-wa-shirikisho-ahmed/) - ARUSHA: WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamesema wanautaka ubingwa wa Kombe la Shirikisho. Kauli hiyo imetolewa na Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, mkoani Arusha ambapo Simba tayari imetua huko kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali wa kombe la shirikisho dhidi ya Coastal Union unaotarajiwa kuchezwa kesho. Akizungumza na wanachama na mashabiki wa - [Abuya: Tutaendelea kupambana kutimiza malengo yetu](https://spotileo.co.tz/abuya-tutaendelea-kupambana-kutimiza-malengo-yetu/) - ARUSHA: MCHEZAJI wa Yanga, Duke Abuya, amesema ushindi na tuzo ya mchezaji bora aliyopata katika mchezo dhidi ya Fountain Gate ni matokeo ya ushirikiano wa timu nzima na sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki. Akizungumza baada ya kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mechi katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Fountain Gate kwenye Sheikh Amri - [Bunge bonanza kutimua vumbi Juni 20](https://spotileo.co.tz/bunge-bonanza-kutimua-vumbi-juni-20/) - DAR ES SALAAM: BENKI ya CRDB imekabidhi vifaa vya michezo na zawadi zitakazotolewa kwa washindi wa CRDB Bank Bunge Grand Bonanza litakalofanyika Juni 20, 2026 katika Uwanja wa Jamhuri, mkoani Dodoma, huku Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, akitarajiwa kuwa mgeni rasmi. Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo leo, Mkurugenzi - [Shamsa Ford: "Naomba talaka zote](https://spotileo.co.tz/shamsa-ford-naomba-talaka-zote/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa filamu za Bongo, Shamsa Ford, amefunguka hadharani kuhusu ndoa yake na kumuomba mume wake kumpa talaka zote, akisisitiza kuwa hana nia ya kurejea kwenye uhusiano huo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shamsa alichapisha video inayomuonyesha akilia huku akieleza kwa hisia kuwa anataka kupewa talaka kamili na si talaka moja, akidai - [Waamuzi watatu wasimamishwa mizunguko mitano](https://spotileo.co.tz/waamuzi-watatu-wasimamishwa-mizunguko-mitano/) - DAR ES SALAAM:WAAMUZI watatu wa Ligi Kuu wameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kwa mizunguko mitano kutokana na mapungufu ya kiuchezeshaji yaliyojitokeza katika michezo tofauti ya ligi. Waamuzi hao ni Liston Hiari wa Dar es Salaam aliyechezesha mchezo kati ya Mbeya City FC na Mtibwa Sugar, pamoja na Hance Mabena wa Tanga na mwamuzi msaidizi Frank - [Simba, Mtibwa Sugar zatozwa milioni 15, ushirikina](https://spotileo.co.tz/simba-mtibwa-sugar-zatozwa-milioni-15-ushirikina/) - DAR ES SALAAM :KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imezitoza faini Simba SC na Mtibwa Sugar jumla sh milioni 15 kutokana na makosa tofauti yaliyobainika katika michezo ya Ligi Kuu. Mtibwa Sugar imetozwa faini ya Sh milioni tano baada ya wachezaji wake pamoja na baadhi ya viongozi - [Messi bado gumzo duniani, Hat-trick yake yazua mjadala](https://spotileo.co.tz/messi-bado-gumzo-duniani-hat-trick-yake-yazua-mjadala/) - NAHODHA wa Argentina, Lionel Messi, ameendelea kutawala vichwa vya habari katika Kombe la Dunia 2026 baada ya kuonesha kiwango cha hali ya juu kwa kufunga mabao matatu (hat-trick) hatua iliyomfikisha kwenye rekodi ya mabao 16 katika historia ya mashindano hayo. Messi, ambaye tayari anatajwa kuwa mmoja wa wachezaji bora kuwahi kucheza soka duniani, ameendelea kuthibitisha - [Matokeo Kombe la dunia 2026 yazidi kuishangaza dunia](https://spotileo.co.tz/matokeo-kombe-la-dunia-2026-yazidi-kuishangaza-dunia/) - MASHINDANO ya Kombe la Dunia 2026 yameendelea kuwa gumzo kubwa duniani baada ya mechi kadhaa za hatua ya makundi kutoa matokeo ya kusisimua na ya kushangaza, huku mataifa makubwa yakianza kampeni zao kwa presha kubwa. Miongoni mwa matokeo yaliyozua mjadala mkubwa ni sare ya mabao 1-1 kati ya Portugal National Football Team na DR Congo - [Kaseba amtaka Mwabaka kutetea mabondia](https://spotileo.co.tz/kaseba-amtaka-mwabaka-kutetea-mabondia/) - DAR ES SALAAM: MWENYEKITI anayemaliza muda wake wa Chama cha Mabondia wa Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBA), Japheth Kaseba, amemtaka mwenyekiti mpya wa chama hicho, Kisua Mwabaka, kuwa tayari kukabiliana na lawama na upinzani katika kutetea maslahi ya mabondia nchini. Kauli hiyo imekuja baada ya Mwabaka kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TPBA katika uchaguzi uliofanyika jana - [Ruto aialika Arsenal kutembelea Kenya](https://spotileo.co.tz/ruto-aialika-arsenal-kutembelea-kenya/) - NAIROBI, Kenya: RAIS wa Kenya na shabiki mkubwa wa timu ya soka ya Arsenal , William Ruto, ameialika klabu hiyo kutembelea nchini Kenya mwakani kufuatia ushindi wake wa kihistoria wa ubingwa wa Ligi Kuu England uliomaliza ukame wa miaka 22 bila taji hilo. Ruto alitoa kauli hiyo Juni 18 katika mahojiano maalumu, akieleza kushangazwa na - [Hat-trick YA Messi ilivyomtoa machozi KOCHA SCALONI](https://spotileo.co.tz/hat-trick-ya-messi-ilivyomtoa-machozi-kocha-scaloni/) - MISSOURI:KOCHA wa Argentina Lionel Scaloni alishindwa kuficha hisia zake baada ya Lionel Messi kufunga hat-trick na kuiongoza Argentina kupata ushindi muhimu katika Kombe la Dunia. Kocha huyo alionekana akiwa na machozi baada ya mechi, picha iliyogusa mashabiki wengi wa soka duniani na kuonesha uhusiano mkubwa uliopo kati yake na nahodha huyo wa Argentina. Safari ya - [AI kumrejesha Val Kilmer kwenye filamu Hollywood](https://spotileo.co.tz/ai-kumrejesha-val-kilmer-kwenye-filamu-hollywood/) - LOS ANGELES, Marekani: Tasnia ya filamu Hollywood imejikuta katikati ya mjadala mkubwa kufuatia taarifa kwamba teknolojia ya akili bandia (AI) inatarajiwa kutumika kumrejesha marehemu mwigizaji maarufu Val Kilmer katika filamu mpya, hatua ambayo imeibua maswali kuhusu maadili, haki za wasanii na mustakabali wa sekta ya burudani duniani. Taarifa hizo zimezua hisia tofauti miongoni mwa watayarishaji - [Michezo ni sekta inayopewa kipaumbele na serikali](https://spotileo.co.tz/michezo-ni-sekta-inayopewa-kipaumbele-na-serikali/) - IRINGA: SERIKALI imeahidi kuendelea kuipa kipaumbele sekta ya michezo nchini kutokana na mchango wake mkubwa katika maendeleo ya vijana, uchumi wa taifa na kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia mashindano mbalimbali. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma, wakati akifunga mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Tanzania kwa Shule - [Kapombe ataja siri waliyotumia kwa Mbeya City](https://spotileo.co.tz/kapombe-ataja-siri-waliyotumia-kwa-mbeya-city/) - DAR ES SALAAM: NAHODHA wa Simba SC, Shomari Kapombe, amesema kilichowapa ushindi kwa Mbeya City ni umakini na tahadhari. Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu hiyo inayotetea nafasi ya kujinusuru isishuke daraja, mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya jana. Akizungumza baada ya mchezo huo, Kapombe, amesema timu yake ilicheza - [Serengeti Girls yajipanga kwa nusu fainali Cecafa](https://spotileo.co.tz/serengeti-girls-yajipanga-kwa-nusu-fainali-cecafa/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Msaidizi wa Serengeti Girls, Esther Chabruma, amesema kikosi chake kitarejea mazoezini kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Kenya kabla ya mchezo ujao wa nusu fainali. Katika mchezo wa hatua ya makundi wa michuano ya Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), - [Ally: Dar City tulikuwa bora kuliko JKT](https://spotileo.co.tz/ally-dar-city-tulikuwa-bora-kuliko-jkt/) - DAR ES SALAAM: MCHEZAJI wa Dar City, Ally Abdallah, amesema wanafurahia ushindi wa pointi 62-33 walioupata dhidi ya JKT kwa kuwa wapinzani wao ni miongoni mwa timu zinazowapa ushindani mkubwa kila wanapokutana katika Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam. Akizungumza baada ya mchezo huo uliochezwa jana usiku kwenye Uwanja wa Don Bosco, Oysterbay, - [Brooklyn Beckham afichua siri ya mgogoro wa wazazi wake](https://spotileo.co.tz/broklyn-beckham-afichua-siri-ya-mgogoro-wa-wazazi-wake/) - LONDON: BROOKLYN Beckham, mtoto mkubwa wa nyota wa zamani wa soka David Beckham na mbunifu wa mitindo Victoria Beckham, amezua gumzo kubwa duniani baada ya kuzungumza kwa mara ya kwanza taarifa za kuwepo kwa mgogoro ndani ya familia yake. Brooklyn, ambaye kwa muda mrefu amekuwa akihusishwa na taarifa za kutofautiana na baadhi ya wanafamilia wake, - [Uchunguzi Kifo cha muigizaji India waendelea](https://spotileo.co.tz/uchunguzi-kifo-cha-muigizaji-india-waendelea/) - MUMBAI, INDIA : Tasnia ya filamu na televisheni nchini India imegubikwa na majonzi kufuatia kifo cha ghafla cha mwigizaji chipukizi Sanchita Ugale, aliyefahamika zaidi kupitia tamthilia maarufu ya ‘Kumkum Bhagya’. Kifo chake kimetikisa mashabiki, waigizaji wenzake na wadau wa burudani nchini humo ambapo inadaiwa Sanchita alifariki dunia katika makazi yake yaliyopo Nalasopara, jimbo la Maharashtra - [Selena Gomez ala dodo la uongozaji filamu Hollywood](https://spotileo.co.tz/selena-gomez-ala-dodo-la-uongozaji-filamu-hollywood/) - LOS ANGELES, Marekani: Msanii maarufu wa muziki na filamu, Selena Gomez, ameendelea kupiga hatua kubwa katika tasnia ya burudani ya Hollywood baada ya kupata nafasi muhimu zaidi katika kazi yake ya uigizaji na utayarishaji wa filamu. Taarifa zilizotolewa na kampuni ya Disney zinaeleza kuwa Gomez atafanya kwa mara ya kwanza kazi ya uongozaji wa filamu - [Wasanii wanaotaka kutumbuiza Sauti za Busara 2027 dirisha limefunguliwa](https://spotileo.co.tz/wasanii-wanaotaka-kutumbuiza-sauti-za-busara-2027-dirisha-limefunguliwa/) - ZANZIBAR : WAANDAAJI WA Tamasha la Kimataifa la Muziki la Sauti za Busara linalofanyika kila mwaka visiwani Zanzibar wamesema zimebaki wiki mbili pekee kabla ya kufungwa kwa dirisha la maombi ya wasanii wanaotaka kushiriki katika Tamasha hilo kwa mwaka 2027. Pia waandaaji hao wamewataka wasanii wa ndani ya Afrika na na wale wa kutoka nje - [Mendy: Kukosa umakini kuliigharimu Senegal dhidi ya Ufaransa](https://spotileo.co.tz/mendy-kukosa-umakini-kuliigharimu-senegal-dhidi-ya-ufaransa/) - EAST RUTHERFORD, Marekani: Kipa wa timu ya taifa ya Senegal, Edouard Mendy, amesema kukosa umakini katika nyakati muhimu za mchezo ndiko kulikochangia timu yake kupoteza kwa mabao 3-1 dhidi ya Ufaransa katika mchezo wao wa kwanza wa Kombe la Dunia uliochezwa Jumanne. Senegal ilianza mchezo huo kwa kiwango kizuri na kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga - [Mshambuliaji wa Iran apata Visa ya Marekani, aleta utulivu kambini](https://spotileo.co.tz/mshambuliaji-wa-iran-apata-visa-ya-marekani-aleta-utulivu-kambini/) - SEATTLE, Marekani : Timu ya taifa ya Iran imepata afueni kubwa katika kampeni yake ya Kombe la Dunia baada ya mshambuliaji wake Mehdi Torabi kupewa visa mpya ya kuingia Marekani, hatua itakayomruhusu kuendelea kuichezea nchi yake katika mechi zilizobaki za mashindano hayo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisa mmoja wa timu hiyo Jumanne, Torabi - [Deschamps amsifu Mbappe kwa rekodi mpya kombe la dunia](https://spotileo.co.tz/deschamps-amsifu-mbappe-kwa-rekodi-mpya-kombe-la-dunia/) - EAST RUTHERFORD, Marekani: Kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps, amempongeza nahodha wake Kylian Mbappe baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Senegal kwenye mchezo wa ufunguzi wa Kundi I wa Kombe la Dunia 2026. Mbappe aliiongoza Ufaransa kupata ushindi huo muhimu baada ya kufungua ukurasa wa mabao - [Messi alingana na rekodi ya Klose baada ya kuizamisha Algeria](https://spotileo.co.tz/messi-alingana-na-rekodi-ya-klose-baada-ya-kuizamisha-algeria/) - KANSAS CITY: NAHODHA wa Argentina, Lionel Messi, ameandika historia nyingine katika Kombe la Dunia baada ya kufunga hat-trick na kuifikisha timu yake kwenye ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Algeria katika mchezo wa Kundi J uliochezwa Kansas City, Marekani. Hat-trick hiyo imemwezesha Messi kufikisha mabao 16 katika historia ya Kombe la Dunia na kulingana na - [Haaland ang'ara Norway ikiichapa Iraq 4-1](https://spotileo.co.tz/haaland-angara-norway-ikiichapa-iraq-4-1/) - FOXBOROUGH: NAHODHA na mshambuliaji hatari wa Norway, Erling Haaland, ameanza vyema kampeni yake ya kwanza ya Kombe la Dunia baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Iraq kwenye mchezo wa Kundi I uliochezwa usiku wa kuamkia leo. Haaland, mwenye umri wa miaka 25, alikuwa kivutio kikubwa kabla ya mchezo huo na - [Bandari, Rhino Rangers vita ya ubingwa wa First Ligi](https://spotileo.co.tz/bandari-rhino-rangers-vita-ya-ubingwa-wa-first-ligi/) - DAR ES SALAAM: HATIMAYE bingwa wa Ligi Daraja la pili (First League) atafahamika leo wakati Bandari Tanzania ikishuka dimbani kuivaa Rhino Rangers katika mchezo wa fainali utakaopigwa saa 1:00 jioni kwenye Uwanja wa Azam Complex. Timu zote mbili zinaingia kwenye mchezo huo zikiwa na morali kubwa baada ya kufanya vizuri msimu mzima na kufanikiwa kutimiza - [Matumaini ya Wachina Kombe la Dunia yapo kwa refa wao](https://spotileo.co.tz/matumaini-ya-wachina-kombe-la-dunia-yapo-kwa-refa-wao/) - BEIJING: WAKATI timu ya taifa ya China ikiendelea kukosa nafasi katika Kombe la Dunia kwa miaka mingi, macho ya mamilioni ya mashabiki wa nchi hiyo sasa yameelekezwa kwa mtu ambaye si mchezaji wala kocha, bali mwamuzi maarufu wa soka, Ma Ning. Ma Ning, anayejulikana kwa jina la utani la ‘Card Master’ kutokana na tabia yake - [Kifaa kinachosaidia moyo wa Eriksen](https://spotileo.co.tz/kifaa-kinachosaidia-moyo-wa-eriksen/) - DENMARK:WIKIENDI iliyopita, Christian Eriksen aliwapa hofu mashabiki wa soka duniani baada ya kuanguka uwanjani katika dakika ya 65 ya mchezo dhidi ya Ukraine, tukio ambalo liliwakumbusha wengi yaliyotokea wakati wa Euro 2020. Baada ya Eriksen kuanguka, wachezaji wa timu zote mbili walikusanyika kumzunguka huku madaktari wakikimbilia kutoa huduma ya haraka. Kwa muda mfupi, hali hiyo - [Wakati mwingine mpira unatukumbusha mengi](https://spotileo.co.tz/21046-2/) - MEXICO:KWA wengi ilikuwa ni bao la kawaida katika Kombe la Dunia. Lakini kwa Raúl Jiménez, lilikuwa moja ya nyakati kubwa zaidi katika maisha yake. Miaka sita iliyopita, Jiménez alikuwa karibu kupoteza kila kitu baada ya kupata jeraha baya la kichwa katika mchezo wa Ligi Kuu England kati ya Arsenal na Wolverhampton Wanderers. Katika tukio hilo, - [Zion Suzuki:Kipa wa Japan mwenye asili ya Ghana](https://spotileo.co.tz/21075-2/) - MONTERREY:MIAKA michache iliyopita, wengi walikuwa wanajiuliza kama Zion Suzuki angeweza kufikia kiwango cha juu katika soka la kimataifa. Leo, kipa huyo ni mmoja wa nyota wanaovutia zaidi katika Kombe la Dunia 2026. Zion Suzuki alikulia nchini Japan akiwa na baba mwenye asili ya Ghana na mama raia wa Japan. Kutokana na mchanganyiko huo wa asili, - [Stori ya mjini ni kuhusu huyu baba mwenye miaka 40](https://spotileo.co.tz/21082-2/) - ATLANTA:USIKU wa kihistoria wa golikipa Vozinha dhidi ya Hispania haukuishia kwenye 'saves' zake pekee, bali pia ulimshuhudia akiondoka na tuzo ya Mchezaji Bora wa Mechi baada ya kuiongoza Cape Verde kupata sare ya bila kufungana. Vozinha alikuwa shujaa mkubwa wa Cape Verde katika mchezo huo wa Kombe la Dunia 2026, akifanya saves kadhaa muhimu zilizowazuia - [Michuano ya kanda ya Karate kufanyika Iringa](https://spotileo.co.tz/michuano-ya-kanda-ya-karate-kufanyika-iringa/) - DAR ES SALAAM: SHIRIKISHO la Karate Tanzania limeandaa mashindano ya Taifa ya kanda yatakayofanyika Juni 28-29 katika kumbi za Chuo Kikuu RUCU mkoani Iringa. Kwa mujibu wa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Karate Tanzania, Sensei Said Kiswabi mikoa zaidi ya 10 inatarajia kuoneshana kazi. Kiswabi amesema mashindano hayo yatashirikisha wachezaji zaidi ya - [Mkakati kwa wageni wa Afcon 2027 wawasilishwa](https://spotileo.co.tz/mkakati-kwa-wageni-wa-afcon-2027-wawasilishwa/) - DAR ES SALAAM:MWENYEKITI wa Kamati Tendaji ya Huduma kwa Wageni wa AFCON 2027, Danford Emmanuel, amewasilisha rasmi Mkakati wa Taifa wa utoaji wa huduma kwa wageni watakaowasili nchini kushiriki na kuhudhuria mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027. Wasilisho hilo limefanyika Juni 16, 2026, katika ukumbi wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es - [Barker: Hatuwadharau Mbeya City](https://spotileo.co.tz/barker-hatuwadharau-mbeya-city/) - MBEYA:KOCHA Mkuu wa Simba, Steven Barker, amesema kikosi chake hakitawadharau Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, akieleza kuwa mechi za mwisho wa msimu huwa ngumu kutokana na kila timu kupambana kutimiza malengo yake. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Mbeya kuelekea mchezo wa kesho utakaochezwa saa nane mchana, Barker amesema Mbeya - [nthony Joshua awa kivutio kwa wanawake](https://spotileo.co.tz/nthony-joshua-awa-kivutio-kwa-wanawake/) - BONDIA maarufu wa uzani wa juu duniani, Anthony Joshua, ameibua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kushiriki video na picha zinazoonesha upande wake wa kawaida na wa upole akicheza na mbuzi. Nyota huyo mwenye asili ya Nigeria lakini anayeiwakilisha Uingereza aliweka chapisho kwenye Instagram lililoambatana na maneno ‘Village boy’, jambo ambalo liliwavutia maelfu - [Shakira, Madonna, BTS watajwa fainali Kombe la Duinia 2026](https://spotileo.co.tz/shakira-madonna-bts-watajwa-fainali-kombe-la-duinia-2026/) - NEW YORK: SHIRIKISHO la Soka Duniani, FIFA, limeibua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki wa soka na muziki baada ya kuthibitisha kuwa mastaa wa kimataifa Shakira, Madonna na BTS watakuwa sehemu ya burudani ya fainali ya Kombe la Dunia 2026. Tangazo hilo limepokelewa kwa furaha kubwa duniani kote, huku mashabiki wakitarajia kushuhudia moja ya maonesho makubwa - [Stevo Simple Boy ataka wazichape na X-wake](https://spotileo.co.tz/stevo-simple-boy-ataka-wazichape-na-x-wake/) - NAIROBI: MWANAMUZIKI maarufu wa Kenya, Stevo Simple Boy, ameibua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kutoa pendekezo lisilotarajiwa la kutaka kuzipiga na mpenzi wake wa zamani, Pritty Vishy, ili wamalize tofauti na migogoro ambayo imekuwa ikiendelea kati yao kwa muda mrefu. Kauli hiyo ilitolewa wakati wa mahojiano yaliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, ambapo msanii huyo alimtaka - [Aliyeacha kazi benki na kutimiza ndoto ya Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/aliyeacha-kazi-benki-na-kutimiza-ndoto-ya-kombe-la-dunia/) - ATLANTA:WAKATI timu ya taifa ya Cape Verde ikiwa imeshacheza mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia 2026, mmoja wa wachezaji waliovutia wengi ni beki Roberto Carlos Lopes, ambaye safari yake ya soka imejaa maamuzi makubwa na ya kishujaa. Roberto Carlos Lopes, aliyezaliwa na kukulia nchini Ireland, aliwahi kuwa mfanyakazi wa benki akiwa na umri - [Mitaa ya Cape Verde yaendeleza furaha, Golikipa Vozinha atajwa kila kona](https://spotileo.co.tz/mitaa-ya-cape-verde-yaendeleza-furaha-golikipa-vozinha-atajwa-kila-kona/) - CAPE VERDE: KATIKA Jiji la Praia na maeneo mengine nchini Cape Verde, wananchi walisherehekea matokeo ya sare ya 0-0 dhidi ya mabingwa wa zamani wa Kombe la Dunia Hispania, wenye magari walipiga honi, wengine walipeperusha bendera za taifa na kuimba nyimbo za kuisifu timu yao. Pia mitandao ya kijamii nchini humo ilifurika jumbe za pongezi - [Polisi yatwaa ubingwa, Chaneta yatamba kuibua vipaji](https://spotileo.co.tz/polisi-yatwaa-ubingwa-chaneta-yatamba-kuibua-vipaji/) - DODOMA:TIMU ya Polisi imeibuka bingwa wa Ligi ya Netiboli Daraja la Kwanza 2026 baada ya kuifunga Uhamiaji Queens mabao 43-36 katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Ushindi huo umehitimisha kampeni nzuri ya Polisi iliyodhihirisha ubora, nidhamu na mshikamano katika mashindano hayo yaliyoshirikisha timu mbalimbali kutoka nchini kote. Wakati ligi hiyo - [Rosemary, Nyamhanga watamba baada ya kutwaa tuzo](https://spotileo.co.tz/rosemary-nyamhanga-watamba-baada-ya-kutwaa-tuzo/) - DAR ES SALAAM:WASHINDI wa tuzo za wachezaji bora wa mwezi Mei katika mashindano ya mpira wa wavu nchini, Rosemary Lazier wa Bandari na Fabian Nyamhanga wa TPDC, wamesema kutwaa tuzo hizo kumewaongezea hamasa ya kufanya vizuri zaidi na kuendelea kupambania mafanikio makubwa katika timu zao. Rosemary amesema amepokea tuzo hiyo kwa furaha kubwa kwani ilikuwa - [Yanga macho yote kwa Fountain Gate](https://spotileo.co.tz/yanga-macho-yote-kwa-fountain-gate/) - DAR ES SALAAM:VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga, leo wameondoka kuelekea mkoani Arusha kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Fountain Gate utakaochezwa Juni 18 katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Yanga inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na morali kubwa baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mashujaa katika mchezo uliochezwa - [TPC yaanza Mbio za Los Angeles](https://spotileo.co.tz/tpc-yaanza-mbio-za-los-angeles/) - DAR ES SALAAM: KAMATI ya Paralympic Tanzania (TPC) imekamilisha rasmi safu yake ya uongozi baada ya kufanya uchaguzi mdogo uliojazwa nafasi zilizoachwa wazi, huku viongozi wapya wakitakiwa kuanza kazi mara moja kwa lengo la kuongeza ushiriki wa Tanzania katika Michezo ya Paralympic ya Los Angeles 2028. Katika uchaguzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa - [Bodi ya filamu yazindua filamu “Kifurushi” kuelimisha jamii dhidi ya dawa za kulevya](https://spotileo.co.tz/bodi-ya-filamu-yazindua-filamu-kifurushi-kuelimisha-jamii-dhidi-ya-dawa-za-kulevya/) - DAR ES SALAAM:BODI ya Filamu Tanzania imezindua filamu ya "Kifurushi" inayolenga kuelimisha jamii kuhusu athari za usafirishaji wa dawa za kulevya na umuhimu wa kuzingatia taratibu sahihi za usafirishaji wa mizigo. Uzinduzi huo, uliofanyika katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli, Mbezi Mwisho jijini Dar es Salaam, ukiongozwa na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti - [Bielsa:Sikuangalia kamera kwa sababu mimi siyo model](https://spotileo.co.tz/bielsasikuangalia-kamera-kwa-sababu-mimi-siyo-model/) - FLORIDA:KOCHA wa timu ya taifa ya Uruguay, Marcelo Bielsa, ametoa majibu makali baada ya kuulizwa kuhusu picha yake rasmi ambayo imekuwa ikizungumziwa na mashabiki katika siku za karibuni. Bielsa alionekana kutotazama moja kwa moja kamera wakati wa upigaji picha rasmi wa mashindano, jambo ambalo lilizua maswali kutoka kwa baadhi ya mashabiki na vyombo vya habari. - [Ni Mo Salah au De Bruyne leo?](https://spotileo.co.tz/ni-mo-salah-au-de-bruyne-leo/) - SEATTLE:KATIKA mchezo wa leo unaowakutanisha miamba wawili wa soka kutoka Afrika na Ulaya, kila mmoja akitamba katika anga zake,wakati Ubelgiji ikiwa ni taifa bora barani Ulaya na Misri ikiwa dume la soka Afrika,ndani yao zipo stori zinazofanana kutoka kwa wanaume wawili wakubwa wa soka la dunia. Mohamed Salah na Kevin De Bruyne, wote wakiwa na - [UEFA yatupa kete UEFA 2029](https://spotileo.co.tz/uefa-yatupa-kete-uefa-2029/) - BARCELONA:DIMBA la Camp Nou limeingia rasmi kwenye kinyang’anyiro cha kuandaa fainali ya UEFA Champions League ya mwaka 2029, baada ya zoezi la maombi kufikia hatua ya mwisho. Kwa sasa viwanja viwili tu ndivyo vimebaki, na mshindi atajulikana Septemba 15 huko Thessaloniki, Ugiriki. Wamiliki wa uwanja huo, FC Barcelona, wanapiga hesabu za kumaliza maboresho makubwa kabla - [Ahmed Ally: Simba tupo tayari kwa Pamba Jiji](https://spotileo.co.tz/ahmed-ally-simba-tupo-tayari-kwa-pamba-jiji/) - DAR ES SALAAM: MENEJA Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema kikosi cha timu hiyo kimekamilika kuelekea mchezo wa Jumapili dhidi ya Pamba Jiji baada ya nyota wote kurejea na kuwa katika hali nzuri. Akizungumza kupitia mtandao wa Simba Ahmed amesema kurejea kwa wachezaji wote kunatoa faraja kwa benchi la ufundi na kuongeza ushindani - [Yanga yatoa siku 13 matawi yafanye uchaguzi](https://spotileo.co.tz/yanga-yatoa-siku-13-matawi-yafanye-uchaguzi/) - DAR ES SALAAM: MWENYEKITI wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Wakili Malangwe Mchungahela, ametangaza rasmi kuanza kwa mchakato wa uchaguzi wa klabu hiyo kwa kuyaagiza matawi yote yenye sifa kufanya uchaguzi wa viongozi na wajumbe kuanzia Juni 13 hadi Juni 26, 2026. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mchungahela amesema hatua - [Moallin: Kila mechi ni fainali katika mbio za ubingwa](https://spotileo.co.tz/moallin-kila-mechi-ni-fainali-katika-mbio-za-ubingwa/) - KIGOMA: KOCHA Mkuu wa Yanga, Abdihamid Moallin, amesema kikosi chake kipo tayari kwa mchezo wa kesho dhidi ya Mashujaa FC utakaochezwa Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma, akisisitiza kuwa kila mechi iliyosalia ni fainali katika harakati za kutwaa ubingwa wa tano mfululizo. Moallin amesema maandalizi ya timu yamekwenda vizuri wakati wa dirisha la mapumziko ya - [Shime:Tunataka Kombe la CECAFA nyumbani](https://spotileo.co.tz/shimetunataka-kombe-la-cecafa-nyumbani/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Timu ya Taifa ya Wanawake chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Girls), Bakari Shime amesema kikosi chake kipo tayari kwa changamoto ya michuano ya CECAFA itakayoanza kesho, akisisitiza dhamira yao ni kutetea heshima ya nyumbani kwa kubakisha taji hilo. Shime amesema mashindano hayo hayatakuwa mepesi kutokana na kushirikisha - [Mchungahela ateuliwa kuongoza kamati ya uchaguzi Yanga](https://spotileo.co.tz/mchungahela-ateuliwa-kuongoza-kamati-ya-uchaguzi-yanga/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga imetangaza uteuzi wa wajumbe watano watakaounda Kamati ya Uchaguzi baada ya kupitishwa na Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo huku wakili Malangwe Mchungahela akiteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Juni 12, 2026 na Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga, wajumbe walioteuliwa ni - [Serikali yalenga Kudhibiti kamari Mpya wa Asilimia 5](https://spotileo.co.tz/serikali-yalenga-kudhibiti-kamari-mpya-wa-asilimia-5/) - DODOMA:WAZIRI wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema Serikali inapendekeza kuanzishwa kwa ushuru wa bidhaa wa asilimia 5 kwenye thamani ya dau la kamari zinazochezwa kupitia michezo ya kubashiri ya ardhini na mtandaoni, kasino za ardhini na mtandaoni, mashine za sloti pamoja na michezo ya vikaragosi (virtual games). Akiwasilisha bungeni mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio - [Serikali kupunguza ada za Leseni za maudhui mtandaoni](https://spotileo.co.tz/serikali-kupunguza-ada-za-leseni-za-maudhui-mtandaoni/) - DODOMA:WAZIRI wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema Serikali inapendekeza kupunguza kwa kiwango kikubwa ada mbalimbali za leseni za maudhui mtandaoni zinazotumiwa zaidi na vijana, hatua inayolenga kuboresha mazingira ya biashara na kuharakisha ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini. Akiwasilisha Bungeni mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, - [Bidhaa za urembo kuongezewa Ushuru hadi Asilimia 15](https://spotileo.co.tz/bidhaa-za-urembo-kuongezewa-ushuru-hadi-asilimia-15/) - DODOMA: WAZIRI wa Fedha, Khamis Mussa Omar, amesema Serikali imependekeza kutoza ushuru wa bidhaa wa asilimia 10 kwa mashine za kukaushia rangi za kucha za UV/LED zinazoingizwa nchini na kutambulika kwa HS Code 8516.79.00. Akiwasilisha bungeni mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Waziri Khamis amesema hatua hiyo - [Serikali kupandisha kodi mirabaha taasisi za michezo](https://spotileo.co.tz/serikali-kupandisha-kodi-mirabaha-taasisi-za-michezo/) - DODOMA:SERIKALI imependekeza kuongeza kiwango cha kodi ya zuio kwenye mrabaha kwa taasisi za michezo na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutoka asilimia tano hadi asilimia 10 kuanzia mwaka wa fedha 2026/27. Hatua hiyo imetangazwa na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar, wakati akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/27 Bungeni jijini Dodoma. - [Okello, Barker watwaa tuzo za Mei Ligi Kuu](https://spotileo.co.tz/okello-barker-watwaa-tuzo-za-mei-ligi-kuu/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO mshambuliaji wa Yanga Allan Okello, ameendelea kuthibitisha ubora wake baada ya kutangazwa Mchezaji Bora wa Mwezi Mei wa Ligi Kuu msimu wa 2025/26. Okello ametwaa tuzo hiyo baada ya kuonesha kiwango cha juu mwezi huo kwa kufunga mabao tisa na kutoa pasi moja ya bao katika dakika 509 za michezo sita - [Wachezaji Ujerumani kujichanga nauli za mashabiki wao](https://spotileo.co.tz/wachezaji-ujerumani-kujichanga-nauli-za-mashabiki-wao/) - MAREKANI:WACHEZAJI wa timu ya taifa ya Ujerumai watatoa sehemu ya posho zao kulipia gharama za usafiri kwa mashabiki 600 watakaosafiri kwa basi mpaka uwanja MetLife katika mji wa New Jersey ambako timu hiyo itacheza mechi yake ya mwisho ya Kundi E dhidi ya Ecuador Juni 25, mwaka huu . Ujerumani wanafanya hivyo kuwapunguzia mzigo mashabiki - [Singida: Ubora wetu unatupa imani dhidi ya JKT](https://spotileo.co.tz/singida-ubora-wetu-unatupa-imani-dhidi-ya-jkt/) - DAR ES SALAAM:OFISA Habari na Mawasiliano wa Singida Black Stars, Hussein Massanza, amesema maandalizi ya timu hiyo kuelekea mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya JKT Tanzania yanaendelea vizuri huku kikosi kikiwa na morali ya juu ya kupata matokeo chanya. Akizungumza na waandishi wa habari leo, Massanza amesema wanaifahamu na kuiheshimu JKT Tanzania, lakini wanaamini ubora - [JKT Queens yakumbana na adhabu nzito](https://spotileo.co.tz/jkt-queens-yakumbana-na-adhabu-nzito/) - DAR ES SALAAM: KAMATI ya Soka la Wanawake imeitoa adhabu mbalimbali kwa viongozi, wachezaji na waamuzi kufuatia matukio yaliyojitokeza katika michezo ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania (TWPL), huku JKT Queens ikiwa miongoni mwa timu zilizoathirika zaidi. Katika kikao kilichofanyika Dar es Salaam, kamati hiyo ilipitia taarifa za mchezo namba 95 kati ya Mashujaa Queens - [Galatasaray: Osimhen hauzwi](https://spotileo.co.tz/galatasaray-osimhen-hauzwi/) - UTURUKI: RAIS wa Galatasaray, Dursun Özbek, amesema klabu hiyo haina mpango wowote wa kumuuza mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen licha ya kuendelea kuvutia vilabu vikubwa vya Ulaya. Özbek amesema ni jambo la kawaida kwa mchezaji mwenye kiwango kikubwa kama Osimhen kuingia kwenye rada za klabu kubwa, lakini akasisitiza kuwa maslahi ya Galatasaray ndiyo kipaumbele cha - [John Terry: Kukosekana kwa Nigeria kombe la Dunia ni pengo kubwa](https://spotileo.co.tz/john-terry-kukosekana-kwa-nigeria-kombe-la-dunia-ni-pengo-kubwa/) - NGULI wa zamani wa England na Chelsea, John Terry, amesema kutokuwepo kwa Nigeria kwenye Kombe la Dunia 2026 ni pigo kubwa kwa mashindano hayo, akisisitiza kuwa taifa hilo lina historia kubwa ya soka na lingeongeza ushindani mkubwa. Nigeria ilikosa nafasi ya kufuzu baada ya kumaliza nyuma ya Afrika Kusini katika hatua ya makundi ya kufuzu - [Mbeya City yapanga kuzima moto wa kushuka daraja](https://spotileo.co.tz/mbeya-city-yapanga-kuzima-moto-wa-kushuka-daraja/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Mbeya City, Salum Mayanga, amesema kikosi chake kimefanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye michezo iliyopita kwa lengo la kuongeza ushindani katika mechi zilizosalia za Ligi Kuu. Mayanga amesema tangu kumalizika kwa mchezo wao wa mwisho kabla ya mapumziko ya Kalenda ya FIFA, benchi la ufundi limeelekeza nguvu katika kuboresha eneo - [Thierry Henry, Pele wapewa mitaa Marekani](https://spotileo.co.tz/thierry-henry-pele-wapewa-mitaa-marekani/) - NEW YORK: JIJI la New York limezindua heshima maalum kwa mastaa wawili wakubwa wa soka duniani kwa kubadilisha kwa muda majina ya baadhi ya mitaa na kuyapa majina ya Thierry Henry na Pele kuelekea kuanza rasmi kwa Kombe la Dunia 2026. Hatua hiyo imekuja wakati dunia ikisubiri mashindano hayo makubwa yanayoandaliwa kwa pamoja na Marekani, - [Mwakinyo aomba radhi baada ya kupoteza pambano](https://spotileo.co.tz/mwakinyo-aomba-radhi-baada-ya-kupoteza-pambano/) - ABIDJAN: BONDIA nyota wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameomba radhi kwa mashabiki wake baada ya kupoteza pambano dhidi ya bondia wa Ufaransa, Michel Soro, katika pambano lililofanyika jijini Abidjan, Ivory Coast. Kupitia ujumbe wake baada ya pambano hilo, Mwakinyo amesema anafahamu maumivu na masikitiko waliyonayo mashabiki wake kutokana na matokeo hayo, huku akisisitiza kuwa hatetei kushindwa - [FIFA yatetea Visa, bei za Tiketi kuelekea Kombe la Dunia 2026](https://spotileo.co.tz/fifa-yatetea-visa-bei-za-tiketi-kuelekea-kombe-la-dunia-2026/) - MEXICO: SHIRIKISHO la Soka Duniani (FIFA) limetetea uamuzi wake kuhusu bei za tiketi na namna masuala ya visa yanavyoshughulikiwa kuelekea kuanza rasmi kwa Kombe la Dunia 2026, huku mashindano hayo yakianza leo kwa mchezo wa ufunguzi kati ya Mexico na Afrika Kusini. Mashindano ya mwaka huu yanayoandaliwa kwa pamoja na Marekani, Mexico na Canada yanaingia - [Estadio Azteca na rekodi za kibabe](https://spotileo.co.tz/estadio-azteca-na-rekodi-za-kibabe/) - MEXICO:ESTADIO Azteca, linaweza kuwa jina geni kwa wapenzi wa kandanda wa kizazi cha sasa ila haibadilishi chochote katika uhalisia wa kuwa moja ya viwanja vinavyobeba historia kubwa kupita vyote duniani. Huu ni uwanja wa taifa wa nchi ya Mexico. Ni uwanja wenye uwezo wa kubeba mashabiki 87,523, idadi inayoufanya kuwa uwanja mkubwa katika ukanda wa Latin - [Maajabu ya Kombe la Dunia 2026 haya hapa](https://spotileo.co.tz/maajabu-ya-kombe-la-dunia-2026-haya-hapa/) - MACHO ya dunia leo yanaelekezwa kwenye kuanza rasmi kwa Kombe la Dunia 2026 ambalo linaingia kwenye historia kama toleo kubwa zaidi kuwahi kuandaliwa tangu mashindano hayo yaanze. Kwa mara ya kwanza, mashindano hayo yanafanyika kwa mfumo mpya wenye timu 48 badala ya timu 32 zilizokuwa zikishiriki miaka iliyopita. Mbali na ongezeko la timu, Kombe la - [Mzee Onyango afariki dunia](https://spotileo.co.tz/mzee-onyango-afariki-dunia/) - DAR ES SALAAM:TASNIA ya filamu nchini imepata pigo kufuatia kifo cha mwigizaji mkongwe, Issa Joseph maarufu kama Mzee Onyango, ambaye amefariki dunia usiku wa kuamkia leo, Juni 11, 2026. Mzee Onyango amefariki katika Hospitali ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda. Akizungumza na waandishi wa habari, mtoto - [BASATA yawahamasisha wasanii kuandaa kazi za AFCON 2027 kuitangaza Tanzania](https://spotileo.co.tz/basata-yawahamasisha-wasanii-kuandaa-kazi-za-afcon-2027-kuitangaza-tanzania/) - DAR ES SALAAM:KAIMU Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Bwana Edward Buganga, amewataka wasanii nchini kutumia fursa ya mashindano ya AFCON 2027 kwa kuandaa kazi mbalimbali za sanaa zitakazosaidia kuitangaza Tanzania na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Buganga ametoa wito huo alipokutana na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Foby, katika - [Watengeneza filamu Nigeria wakimbilia YouTube](https://spotileo.co.tz/watengeneza-filamu-nigeria-wakimbilia-youtube/) - LAGOS: SEKTA ya filamu nchini Nigeria (Nollywood) inaendelea kushuhudia mabadiliko makubwa huku watengenezaji wengi wa filamu wakichagua kuachana na sinema na majukwaa ya kulipia kama Netflix na Amazon Prime, na kuelekeza kazi zao moja kwa moja kwenye YouTube. Hatua hiyo imefungua fursa mpya kwa kizazi kipya cha watayarishaji wa filamu wanaotafuta uhuru wa ubunifu na - [Tatjana Maria adai amekossewa heshima na waandaaji](https://spotileo.co.tz/tatjana-maria-adai-amekossewa-heshima-na-waandaaji/) - LONDON:BINGWA mtetezi wa mashindano ya Queen’s Club, Tatjana Maria wa Ujerumani, amesikitishwa na uamuzi wa waandaaji wa mashindano hayo kutompa mwaliko wa moja kwa moja (wildcard), hali iliyomlazimu kucheza mechi za mchujo ili kufuzu hatua kuu. Maria, ambaye mwaka jana aliandika historia kwa kutwaa ubingwa wa wanawake katika klabu hiyo baada ya miaka 52 tangu - [Iran yalalamikia kunyanganywa tiketi za mashabiki kombe la dunia](https://spotileo.co.tz/iran-yalalamikia-kunyanganywa-tiketi-za-mashabiki-kombe-la-dunia/) - NEW YORK: SHIRIKISHO la Soka la Iran (FFIRI) limelaani hatua ya kuondolewa kwa mgawo wa tiketi za mashabiki wake kuelekea Kombe la Dunia, siku chache kabla ya kuanza kwa mashindano hayo. Kwa mujibu wa FFIRI, kanuni za Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) zinatoa asilimia nane ya tiketi za kila mchezo kwa nchi shiriki ili zigawiwe - [Timu ya Taifa ya Kenya yaibugiza Lesotho mabao 6-0](https://spotileo.co.tz/timu-ya-taifa-ya-kenya-yaibugiza-lesotho-mabao-6-0/) - LUSAKA: TIMU ya Taifa ya Wanawake ya Kenya, Harambee Starlets, imeonesha ubora mkubwa baada ya kuichapa Lesotho mabao 6-0 katika mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON). Nyota wa mchezo huo alikuwa Eglay Mukhwana aliyefunga mabao mawili huku Violet Nanjala, Terry Engesha, Fasila Adhiambo na Catherine - [Muongoza filamu wa Marekani adai viumbe wa angani wameshafika duniani](https://spotileo.co.tz/muongoza-filamu-wa-marekani-adai-viumbe-wa-angani-wameshafika-duniani/) - LOS ANGELES: MTAYARISHAJI na mwongozaji maarufu wa filamu aliyeshinda tuzo za Oscar, Steven Spielberg, amesema anaamini viumbe kutoka sayari nyingine wamewahi kufika katika sayari ya dunia na huenda baadhi yao wapo hadi sasa. Spielberg alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha CBS Sunday Morning wakati akitangaza filamu yake mpya ya kisayansi inayojulikana kama ‘Disclosure - [Ariana Grande arejea jukwaani baada ya miaka saba](https://spotileo.co.tz/ariana-grande-arejea-jukwaani-baada-ya-miaka-saba/) - CALIFORNIA: MWIMBAJI, mtunzi wa nyimbo na mwigizaji wa Marekani, Ariana Grande, amerejea rasmi kwenye ziara za muziki baada ya kukaa mbali na jukwaa kwa takribani miaka saba. Ziara yake mpya ya ‘Eternal Sunshine Tour’ kwa tamasha hilo imefanyika katika ukumbi wa Oakland Arena, California nchini Marekani. Tamasha hilo lilivutia maelfu ya mashabiki waliojitokeza kushuhudia kurejea - [Julio: Mashujaa hatutafungwa na Yanga kirahisi](https://spotileo.co.tz/julio-mashujaa-hatutafungwa-na-yanga-kirahisi/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Mashujaa FC, Jamhuri Kihwelu 'Julio', amesema hana hofu ya kuikabili Yanga akieleza kuwa ana uzoefu mkubwa dhidi ya mabingwa hao na anaamini si kazi rahisi kwake kufungwa na timu hiyo. Akizungumza kuelekea mchezo wa Ligi Kuu utakaowakutanisha Mashujaa na Yanga Jumamosi, Julio amesema amewahi kupata ushindi dhidi ya Yanga - [Barker: Simba yaanza kutafuta wachezaji wapya](https://spotileo.co.tz/barker-simba-yaanza-kutafuta-wachezaji-wapya/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Simba, Steve Barker, amesema benchi la ufundi tayari limeanza kazi ya kutafuta wachezaji wa kuongeza nguvu kikosini kuelekea msimu ujao licha ya kuridhishwa na ubora wa kikosi cha sasa. Barker amesema mchakato huo ni sehemu ya mipango ya kuhakikisha timu inaendelea kuwa na ushindani mkubwa katika mashindano ya ndani - [Yanga wameshatua Kigoma](https://spotileo.co.tz/yanga-wameshatua-kigoma/) - DAR ES SALAAM:KIKOSI cha Yanga kimewasili mkoani Kigoma leo Juni 11 kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mashujaa utakaochezwa Jumamosi. Mabingwa hao wa Tanzania Bara walikuwa wakiendelea na maandalizi ya mchezo huo kwa kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa KMC kabla ya kuondoka mapema hii leo, wakilenga kujiweka katika hali nzuri ya ushindani - [Isha Mashauzi arejea kuadhimisha miaka 20 ya muziki](https://spotileo.co.tz/isha-mashauzi-arejea-kuadhimisha-miaka-20-ya-muziki/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa taarabu nchini, Isha Ramadhan maarufu kama Isha Mashauzi, ametangaza kurejea rasmi kwenye anga la muziki baada ya ukimya wa muda, huku akipanga kufanya tamasha maalum mwezi Agosti mwaka huu kuadhimisha miaka 20 tangu aanze safari yake ya muziki. Akizungumza na waandishi wa Habari Dar es Salaam jana Juni - [Ushindi wa Perez kumrejesha Mourinho Real Madrid](https://spotileo.co.tz/ushindi-wa-perez-kumrejesha-mourinho-real-madrid/) - MADRID:KLABU ya Real Madrid inatarajiwa kumtangaza rasmi Jose Mourinho kama kocha mkuu mpya baada ya rais wa klabu hiyo, Florentino Perez, kushinda uchaguzi wa urais na kuendelea kuiongoza miamba hiyo ya soka la Hispania. Mourinho, mwenye umri wa miaka 63, alisaini mkataba wa miaka mitatu mwezi uliopita, lakini utekelezaji wake ulikuwa unategemea matokeo ya uchaguzi - [TSA yafurahishwa na mashindano ya vijana, waogeleaji wapata nafasi timu ya taifa](https://spotileo.co.tz/tsa-yafurahishwa-na-mashindano-ya-vijana-waogeleaji-wapata-nafasi-timu-ya-taifa/) - DAR ES SALAAM:UONGOZI wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA) umeeleza kufurahishwa na mafanikio ya Mashindano ya Klabu za Vijana wenye umri wa miaka sita hadi 12, yaliyowezesha baadhi ya waogeleaji kuchaguliwa kujiunga na timu ya taifa ya vijana. Mashindano hayo yalimalizika katika bwawa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya IST, Masaki, jijini Dar es - [Rayvanny aula Kombe la Dunia 2026 Canada](https://spotileo.co.tz/rayvanny-aula-kombe-la-dunia-2026-canada/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Raymond Mwakyusa ‘Rayvanny’, ameendelea kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa baada ya kutangaza kuwa atakuwa miongoni mwa wasanii watakaotumbuiza katika shughuli za 2026 FIFA World Cup huko Toronto, Canada. Rayvanny amethibitisha taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo alishiriki ujumbe ulioonesha - [Yanga Veterani yalalamikia utata wa umri](https://spotileo.co.tz/yanga-veterani-yalalamikia-utata-wa-umri/) - DAR ES SALAAM: KOCHA wa Yanga Veterani, Ken Mkapa, ameibua mjadala kuhusu suala la umri katika mashindano ya maveterani akidai baadhi ya timu zinatumia wachezaji wanaoonekana kuwa na umri mdogo kuliko uliotarajiwa katika mashindano hayo. Mkapa, ambaye ni beki wa zamani wa kushoto wa Yanga, amesema tofauti ya umri ilionekana wazi katika mechi yao ya - [Barka Seif afungua ukurasa mpya kuelekea La Masia](https://spotileo.co.tz/barka-seif-afungua-ukurasa-mpya-kuelekea-la-masia/) - BARCELONA: KIPAJI chipukizi cha soka nchini, Barka Seif, kimeandika historia baada ya kupata fursa ya kujiunga na programu ya vijana ya klabu maarufu duniani ya FC Barcelona, La Masia, hatua inayotajwa kuwa mafanikio makubwa kwa maendeleo ya soka la vijana Tanzania. Barka, ambaye amekulia na kuendelezwa katika programu ya ukuzaji vipaji ya Magnet, amepata nafasi - [Azam FC kuwafuata Fountain Gate kwa tahadhari](https://spotileo.co.tz/azam-fc-kuwafuata-fountain-gate-kwa-tahadhari/) - DAR ES SALAAM: TIMU YA Azam FC imesema inatarajia kupata upinzani mkali kutoka kwa Fountain Gate katika mchezo ujao wa Ligi Kuu baada ya kuonesha kubadilika hivi karibuni chini ya Kocha Fred Minziro. Akizungumza na Spotileo Ofisa Habari na Mawasiliano wa Azam FC Thabit Zakaria ‘Zakazakazi’ amesema kwa kutambua na umuhimu wa mchezo huo wachezaji - [Mwamuzi wa Somalia azuiwa kuingia Marekani, afukuzwa Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/mwamuzi-wa-somalia-azuiwa-kuingia-marekani-afukuzwa-kombe-la-dunia/) - MAREKANI: NDOTO ya mwamuzi wa soka kutoka Somalia, Omar Abdulkadir Artan, ya kuchezesha mechi za Kombe la Dunia 2026 imefikia tamati ghafla baada ya kunyimwa ruhusa ya kuingia nchini Marekani, hatua iliyomfanya kuondolewa rasmi kwenye orodha ya waamuzi wa mashindano hayo. Artan, ambaye alikuwa ameandika historia kwa kuwa Mwamuzi wa kwanza kutoka Somalia kuteuliwa na - [Eriksen aamua kupumzika baada ya kutoka hospitali](https://spotileo.co.tz/eriksen-aamua-kupumzika-baada-ya-kutoka-hospitali/) - DENMARK: KIUNGO nyota wa Denmark, Christian Eriksen, ameondoa hofu kwa mashabiki wa soka duniani baada ya kuthibitisha kuwa anaendelea vizuri akiwa nyumbani pamoja na familia yake kufuatia kuanguka ghafla wakati wa mechi ya kirafiki kati ya Denmark na Ukraine wiki iliyopita. Eriksen, mwenye umri wa miaka 34, alisema tukio hilo lilikuwa tofauti na lile la - [Pinela Justine afunguka Komenti iliyomuumiza zaidi mtandaoni](https://spotileo.co.tz/pinela-justine-afunguka-komenti-iliyomuumiza-zaidi-mtandaoni/) - DAR ES SALAAM: MSANII, Mwanamitindo na mtumishi wa Mungu kutoka Tanzania, Pinela Justine, amesema kuwa moja ya komenti zilizowahi kumuumiza zaidi kwenye mitandao ya kijamii ni madai ya baadhi ya watu kwamba anatumia bangi. Pinela amesema mara nyingi watu huandika maoni kwenye mitandao bila kutambua kuwa maneno yao yanaweza kuwaumiza wengine kihisia na kuwavunja moyo. - [Colman Domingo afunguka urafiki wake na Chadwick Boseman](https://spotileo.co.tz/colman-domingo-afunguka-urafiki-wake-na-chadwick-boseman/) - NEW YORK: MUIGIZAJI maarufu wa Hollywood, Colman Domingo, amefunguka kuhusu uhusiano wake wa karibu na marehemu Chadwick Boseman, akieleza jinsi nyota huyo wa filamu ya Black Panther alivyokuwa chanzo kikubwa cha hamasa na mwongozo katika maisha yake ya kisanii. Domingo, ambaye alicheza pamoja na Boseman katika filamu ya ‘Ma Rainey's Black Bottom’ ya mwaka 2020, - [Tuchel: Bellingham apigania nafasi ya kwanza](https://spotileo.co.tz/tuchel-bellingham-apigania-nafasi-ya-kwanza/) - ENGLAND: KOCHA mkuu wa timu ya taifa ya England, Thomas Tuchel amesema kiungo wa Real Madrid, Jude Bellingham anapaswa kupigania nafasi yake ili kuingia katika kikosi cha kwanza cha England katika Kombe la Dunia. Tuchel amesema kikosi chake cha sasa kina ushindani mkubwa sana, kiasi kwamba hata wachezaji wenye majina makubwa wanapaswa kuonesha ubora wa - [Eriksen apata nafuu baada ya kuanguka uwanjani](https://spotileo.co.tz/eriksen-apata-nafuu-baada-ya-kuanguka-uwanjani/) - DENMARK: KIUNGO wa zamani wa Manchester United na Tottenham, Christian Eriksen ameanguka uwanjani wakati wa mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Denmark na Ukraine uliochezwa mjini Odense juzi Juni 07,2026, hali iliyosababisha mchezo huo kusimamishwa katika dakika ya 65. Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Denmark, Eriksen alipoteza fahamu kwa muda mfupi lakini - [Antonelli bingwa Monaco Grand Prix, Lewis Hamilton nafasi ya pili](https://spotileo.co.tz/antonelli-bingwa-monaco-grand-prix-lewis-hamilton-nafasi-ya-pili/) - MONACO: MSHIRIKI wa mbio za magari Kimi Antonelli ameendelea kuandika historia kubwa katika msimu wa mashindano ya kimataifa ya mbio za magari (Formula 1) baada ya kushinda mbio za Monaco Grand Prix na kufikisha ushindi wake wa tano mfululizo msimu huu. Mbio hizo zilikuwa za kusisimua na zenye changamoto kubwa za kukatizwa mara kadhaa kutokana - [Tanzania yahitaji bwawa la wa watazamaji 5,000 kuimarisha mashindano ya kimataifa ya kuogelea](https://spotileo.co.tz/tanzania-yahitaji-bwawa-la-wa-watazamaji-5000-kuimarisha-mashindano-ya-kimataifa-ya-kuogelea/) - DAR ES SALAAM:MWENYEKITI wa Chama cha Kuogelea Tanzania, David Mwasioge, amesema kuna umuhimu mkubwa wa kujengwa bwawa la kisasa lenye uwezo wa kuchukua watazamaji kati ya 3,000 hadi 5,000 ili kuwezesha Tanzania kuandaa mashindano makubwa ya kimataifa na kukuza mchezo wa kuogelea nchini. Mwasioge amesema mwitikio wa vijana kushiriki mchezo wa kuogelea unaendelea kuongezeka kila - [CRDB Foundation kutunuku zaidi ya Milioni 100 kwenye Imbeju ndondo Cup 2026](https://spotileo.co.tz/crdb-foundation-kutunuku-zaidi-ya-milioni-100-kwenye-imbeju-ndondo-cup-2026/) - DAR ES SALAAM:BENKI ya CRDB kupitia CRDB Foundation imeahidi kutoa zawadi zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100 katika mashindano ya Imbeju Ndondo Cup 2026, yatakayokuwa msimu wa 13 tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo. Kwa mujibu wa mwaandaaji, Shafii Dauda amesema bingwa wa mashindano hayo atajinyakulia sh. milioni 30, huku mshindi wa pili akipata - [Ruben Dias:Ureno tunataka ubingwa wa Dunia](https://spotileo.co.tz/ruben-diasureno-tunataka-ubingwa-wa-dunia/) - LISBON:BEKI wa kimataifa wa Ureno, Ruben Dias , amesema kikosi cha taifa lake kinaingia kwenye mashindano ya Kombe la Dunia 2026 kikiwa na unyenyekevu lakini pia kikiwa na azma kubwa kuliko wakati wowote uliopita wa kuhakikisha wanachukua ubingwa. Akizungumza kuelekea mashindano hayo yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Duniani FIFA, Dias amesema hii itakuwa Kombe la - [Watatu Arsenal watajwa kuwania tuzo mchezaji bora](https://spotileo.co.tz/watatu-arsenal-watajwa-kuwania-tuzo-mchezaji-bora/) - LONDON: WACHEZAJI watatu wa mabingwa wa Ligi Kuu England, Arsenal wameingia kwenye orodha ya wanaowania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka ya Chama cha Wachezaji wa Kulipwa England (PFA). Walioteuliwa kutoka Arsenal ni kiungo Declan Rice, beki Gabriel Magalhaes na kipa David Raya, ambao walikuwa sehemu muhimu ya kikosi kilichoiongoza Arsenal kutwaa ubingwa wa Ligi - [Vitisho vyatamalaki kuelekea Dar Boxing Debi](https://spotileo.co.tz/vitisho-vyatamalaki-kuelekea-dar-boxing-debi/) - DAR ES SALAAM: MABONDIA mbalimbali wa ngumi za kulipwa nchini wameanza kurushiana vitisho na kutamba ushindi kuelekea tamasha kubwa la Ngumi maarufu kama Dar Boxing Debi litakalofanyika Julai 24, 2026 Dar es Salaam, huku wengi wakiahidi kuwamaliza wapinzani wao kwa njia ya KO. Tamasha hilo linaloratibiwa na Peak Time Media linatajwa kuwa moja ya matukio - [Mbunge Chamazi kuwa mgeni rasmi fainali za Ligi ya Maveterani](https://spotileo.co.tz/mbunge-chamazi-kuwa-mgeni-rasmi-fainali-za-ligi-ya-maveterani/) - DAR ES SALAAM: MBUNGE wa Jimbo la Chamazi, Abdallah Jafari Chaurembo, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika fainali za Ligi ya Maveterani Tanzania zitakazofanyika katika Uwanja wa Azam Complex, huku waandaaji wakijivunia mafanikio yaliyopatikana katika msimu wa kwanza wa mashindano hayo. Akizungumza na waandishi wa habari, mwakilishi wa mbunge huyo, Mussa Francis, amesema fainali hizo zitakazochezwa - [Cassie aaga Marekani baada ya kulipwa zaidi ya bilioni 2.5 kutoka kwa Didy](https://spotileo.co.tz/cassie-aaga-marekani-baada-ya-kulipwa-zaidi-ya-bilioni-2-5-kutoka-kwa-didy/) - NEW YORK: MPENZI wa zamani wa mwanamuziki Sean Combs (P.Didy), Cassie Ventura maarufu Cassie ameweka wazi kuwa kwa sasa hana mpango wa kurejea kuishi nchini Marekani baada ya kuhama nchi hiyo. Mwanadada huyo ambaye pia ni mwimbaji na mwanamitindo maarufu amesema uamuzi huo ameupata baada ya miaka mingi ya misukosuko ya kisheria iliyomuhusisha aliyekuwa mpenzi - [Toxic Lyrikal: Sikutaka kwenda kutumbuiza Ikulu](https://spotileo.co.tz/toxic-lyrikal-sikutaka-kwenda-kutumbuiza-ikulu/) - NAIROBI: RAPA maarufu kutoka Kayole, Nairobi nchini Kenya, Timothy Omondi maarufu Toxic Lyrikali amewaacha wengi wakishangaa baada ya kudai kwamba hakuwahi kuwa na mpango wa kuhudhuria hafla iliyofanyika Ikulu ya Nairobi Kenya licha ya kualikuwa kutumbuiza. Akizungumza katika mahojiano yaliyosambazwa mtandaoni, msanii huyo amesema awali alikataa mwaliko huo mara kadhaa na aliamua kutokwenda kabisa. Kwa - [Akshay Kumar auza nyumba zake mbili zaidi ya bilioni 2](https://spotileo.co.tz/akshay-kumar-auza-nyumba-zake-mbili-zaidi-ya-bilioni-2/) - MUMBAI: NYOTA wa Bollywood, Akshay Kumar, ameendelea kuonesha kuwa mbali na mafanikio ya filamu, pia ni bingwa wa uwekezaji baada ya kuuza nyumba zake mbili zilizopo katika jiji la Mumbai nchini India ambapo ameziuza kwa mamilioni ya fedha. Ripoti za mali isiyohamishika nchini India zinaeleza kuwa muigizaji huyo ameuza nyumba zake mbili zilizopo katika jengo - [Rambo arejea arekodi filamu yake nchini Thailand](https://spotileo.co.tz/rambo-arejea-arekodi-filamu-yake-nchini-thailand/) - THAILAND: MASHABIKI wa filamu za mapigano wana sababu ya kutabasamu baada ya taarifa kuthibitisha kuwa filamu mpya ya John Rambo imeanza rasmi kurekodiwa nchini Thailand, huku muigizaji Noah Centineo akitarajiwa kuvaa viatu vya gwiji wa movie za mapigano Sylvester Stallone kwa mara ya kwanza. Kampuni ya Lionsgate imetangaza kuwa uzalishaji wa filamu hiyo mpya umeanza - [Netflix kuachia filamu ya Michael Jackson, Lukas Podolsk mwezi huu](https://spotileo.co.tz/netflix-kuachia-filamu-ya-michael-jackson-lukas-podolsk-mwezi-huu/) - LOS ANGELES: JUKWAA kubwa la utazamaji duniani, Netflix, limewaandalia mashabiki wake mwezi wenye pilika nyingi baada ya kutangaza ujio wa makala nane mpya zitakazoanza kuoneshwa mwezi huu wa Juni 2026. Miongoni mwa kazi hizo zinazovutia zaidi ni makala inayomhusu nyota wa zamani wa soka la Ujerumani, Lukas Podolski, inayojulikana kwa jina la ‘Poldi’. Makala hiyo - [BMT yawataka waogeleaji kurejea na medali Mauritius](https://spotileo.co.tz/bmt-yawataka-waogeleaji-kurejea-na-medali-mauritius/) - DAR ES SALAAM:BARAZA la Michezo la Taifa (BMT) limewataka waogeleaji wa Tanzania wanaoshiriki Mashindano ya Kuogelea ya Wazi ya Afrika nchini Mauritius kurejea nyumbani na medali, likisisitiza kuwa safari yao si ya kushiriki tu bali ni ya kushindana na kuiletea nchi heshima. Ofisa Michezo Mwandamizi wa BMT, Ingrid Kimario, alitoa kauli hiyo wakati wa kuiaga - [Yanga hakuna kulala ni mwendo wa mazoezi](https://spotileo.co.tz/yanga-hakuna-kulala-ni-mwendo-wa-mazoezi/) - DAR ES SALAAM:KLABU ya Yanga imesema maandalizi ya kikosi chake yanaendelea vizuri kuelekea michezo iliyosalia ya Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na Kombe la Shirikisho, huku wachezaji wote wakiwa katika hali nzuri ya afya na utimamu wa mwili. Akizungumza kuhusu hali ya kikosi hicho, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe, amesema benchi la - [Opa: Ushirikiano ndiyo siri ya ushindi wa Twiga Stars](https://spotileo.co.tz/opa-ushirikiano-ndiyo-siri-ya-ushindi-wa-twiga-stars/) - DAR ES SALAAM:NAHODHA wa Timu ya Taifa ya Wanawake Tanzania, Twiga Stars, Opa Clement, amesema ushirikiano mkubwa miongoni mwa wachezaji ndio uliowezesha timu hiyo kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Malawi katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa KMC, Dar es Salaam. Twiga Stars iliibuka na ushindi huo kupitia bao pekee - [Nsangazelu aipa tano TFF kwa Mfumo wa kuzalisha vipaji](https://spotileo.co.tz/nsangazelu-aipa-tano-tff-kwa-mfumo-wa-kuzalisha-vipaji/) - DAR ES SALAAM:KOCHA Mkuu wa Serengeti Boys, Elieneza Nsangazelu, amesema mafanikio yaliyopatikana na timu hiyo katika michuano ya AFCON ya vijana ni matokeo ya maandalizi mazuri pamoja na uwekezaji uliofanywa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika kukuza vipaji vya vijana. Nsangazelu amesema awali watu wengi hawakuwa na imani kuwa Tanzania ingeweza kufanya - [Aliyeshinda ndege ya Mr. Beast akamatwa](https://spotileo.co.tz/aliyeshinda-ndege-ya-mr-beast-akamatwa/) - PARAGUAY:MAMBO yaligeuka filamu kwa rubani maarufu mwenye asili ya Jamaica na Marekani, Jabari Stephan Brown maarufu kama ‘Captain Treezy’, baada ya kukamatwa nchini Paraguay kuhusishwa na uchunguzi wa dawa za kulevya wenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 466. Brown, ambaye alipata umaarufu mkubwa duniani baada ya kushinda ndege binafsi kwenye shindano la YouTuber maarufu - [Muongoza filamu atunukiwa Tuzo ya Mafanikio ya Maisha](https://spotileo.co.tz/muongoza-filamu-atunukiwa-tuzo-ya-mafanikio-ya-maisha/) - MOMBASA: MTAYARISHAJI na mwongozaji mkongwe wa filamu kutoka Kenya, Judy Kibinge, ameendelea kuandika historia baada ya kutunukiwa Tuzo ya Mafanikio ya Maisha (Lifetime Achievement Award) katika tamasha la tano la Pridelands Wildlife Film Festival linaloendelea jijini Mombasa. Tuzo hiyo imekuja kwa heshima kwa mchango wake mkubwa katika kukuza tasnia ya filamu Afrika pamoja na juhudi - [Timu ya Taifa ya Kenya yakwama Hotelini Afrika Kusini](https://spotileo.co.tz/timu-ya-taifa-ya-kenya-yakwama-hotelini-afrika-kusini/) - PRETORIA: KIKOSI cha Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) kimejikuta kwenye sintofahamu nchini Afrika Kusini baada ya kukwama hotelini kutokana na mgogoro wa malazi na malipo wakati kikijiandaa na mechi mbili za kirafiki dhidi ya Lesotho. Taarifa zinaeleza kuwa mara baada ya kuwasili Pretoria, baadhi ya wachezaji walikataa kuingia katika hoteli ya kwanza waliyoandaliwa - [Bingwa wa R&B na mshindi wa Grammy Peabo Bryson afariki dunia](https://spotileo.co.tz/bingwa-wa-rb-na-mshindi-wa-grammy-peabo-bryson-afariki-dunia/) - NEW YORK: ULIMWENGI wa muziki wa R&B umeingia kwenye majonzi baada ya kupokea taarifa za kifo cha gwiji wa muziki huo Peabo Bryson, ambaye amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 75. Bryson aliyewahi kushinda tuzo za Grammy akiwa sambamba na Celine Dion kupitia wimbo wa ‘Beauty and the Beast’, atakumbukwa na nyimbo zake mbalimbali - [Idriss Elba atunukiwa hadhi: Sasa ni ‘Sir Idris Elba’](https://spotileo.co.tz/idriss-elba-atunukiwa-hadhi-sasa-ni-sir-idris-elba/) - UINGEREZA: MUIGIZAJI nyota wa kimataifa, Idris Elba, ameandika ukurasa mpya katika maisha yake baada ya kutunukiwa rasmi hadhi ya ‘Sir’ na Mfalme Charles III wa Uingereza kutokana na mchango wake mkubwa katika kuwasaidia vijana. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 53, ambaye amewahi kung'ara kupitia tamthilia maarufu za ‘The Wire na Luther’, alipokea heshima hiyo - [Andoni Iraola kutua Anfield: Enzi mpya Kuanza Liverpool](https://spotileo.co.tz/andoni-iraola-kutua-anfield-enzi-mpya-kuanza-liverpool/) - UINGEREZA: MABINGWA wa soka la England mara 20, Liverpool F.C., wapo kwenye hatua za mwisho za kufungua ukurasa mpya baada ya kufikia makubaliano ya kumteua Andoni Iraola kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili utakaodumu hadi Juni 2028. Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na mwandishi wa masuala ya soka duniani Fabrizio - [Napoli wamsajili Hojlund kwa mkataba wa kudumu](https://spotileo.co.tz/napoli-wamsajili-hojlund-kwa-mkataba-wa-kudumu/) - NAPLES:MABINGWA wa Italia, Napoli, wamemsajili mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund kwa mkataba wa kudumu kutoka Manchester United baada ya kuwa na msimu mzuri wa mkopo nchini Italia. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na klabu zote mbili, Napoli imelipa euro milioni 50 (takribani dola milioni 58) kukamilisha uhamisho wa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23. - [Mwakinyo kuwania mkanda wa IBO](https://spotileo.co.tz/mwakinyo-kuwania-mkanda-wa-ibo/) - DAR ES SALAAM: BONDIA nyota wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, anatarajiwa kupanda ulingoni Juni 10, 2026 nchini Ivory Coast kumenyana na bondia wa Ufaransa, Michel Soro, katika pambano la kuwania mkanda wa dunia wa International Boxing Organization wa uzani wa Middleweight. Pambano hilo litafanyika katika ukumbi wa Abidjan Arena na linatarajiwa kuvuta hisia za mashabiki wa - [Twiga Stars, Malawi kutafuta nguvu ya WAFCON](https://spotileo.co.tz/twiga-stars-malawi-kutafuta-nguvu-ya-wafcon/) - DAR ES SALAAM: TIMU ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, leo itashuka dimbani kuikabili timu ya taifa ya wanawake ya Malawi katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki utakaochezwa Uwanja wa KMC Complex kuanzia saa 10:00 jioni. Kocha Msaidizi wa Twiga Stars, Edna Lema, amesema mchezo huo una umuhimu mkubwa kwa timu zote mbili - [Makonda aonya klabu zinazoua vipaji vya wachezaji](https://spotileo.co.tz/makonda-aonya-klabu-zinazoua-vipaji-vya-wachezaji/) - RABAT:WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amevionya baadhi ya klabu vinavyopenda kuwasajili wachezaji wenye umri mdogo kisha kuwaweka benchi kwa muda mrefu bila kuwapa nafasi ya kucheza, akisema tabia hiyo huua vipaji vyao na kuathiri maendeleo ya soka la Tanzania. Makonda amesema hatua ya kuwasajili wachezaji vijana bila kuwapa muda wa kucheza - [Jaji wa American Got Talent, Sidemen waachana](https://spotileo.co.tz/jaji-wa-american-got-talent-sidemen-waachana/) - MMOJA wa majaji wa American Got Talent na nyota wa mtandaoni (YouTuber), Olajide Olayinka maarufu kama KSI ametangaza kuondoka katika kundi la Sidemen baada ya miaka 13 ya ushirikiano wao. Jaji huyo ambaye pia ni mwanamuziki, mfanyabiashara, na mwanamasumbwi wa Uingereza, walianzisha kundi hilo tangu mwaka 2013, amekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Sidemen kupitia - [Serena Williams arejea kwenye Tenisi baada ya miaka minne](https://spotileo.co.tz/serena-williams-arejea-kwenye-tenisi-baada-ya-miaka-minne/) - MALKIA wa tenisi duniani, Serena Williams, amethibitisha rasmi kurejea kwenye mchezo huo baada ya kukaa nje kwa karibu miaka minne, jambo lililowafurahisha mashabiki wake duniani kote. Serena, ambaye hakuwahi kucheza mechi rasmi tangu mwaka 2022, alitangaza kurejea kwake kupitia video ya matangazo ya Nike iliyokuwa na ujumbe wa "Guess everybody heard the news." Nyota huyo - [Gor Mahia waingiza zaidi ya milioni 110 siku ya Ubingwa Na Festo Polea](https://spotileo.co.tz/gor-mahia-waingiza-zaidi-ya-milioni-110-siku-ya-ubingwa-na-festo-polea/) - NAIROBI: MASHABIKI wa Mabingwa wa soka la Kenya 2025/26 Gor Mahia wameinufaisha timu yao iliingiza Nyayo kuwa bahari ya kijani na nyeupe huku klabu hiyo ikikusanya zaidi ya milioni 5.45 ambazo ni zaidi ya milioni 110 kupitia mauzo ya tiketi katika mechi ya kutawazwa mabingwa wa msimu wa 2025/26 wa SportPesa Premier League. Kwa mujibu - [Sabalenka amtoa Osaka, atinga robo fainali](https://spotileo.co.tz/sabalenka-amtoa-osaka-atinga-robo-fainali/) - PARIS:BINGWA namba moja duniani wa tenisi Aryna Sabalenka ameendelea kuonesha ubora wake katika michuano ya French Open baada ya kumtoa Naomi Osaka kwa ushindi wa seti 7-5, 6-3 na kutinga hatua ya robo fainali ya mashindano hayo yanayoendelea jijini Paris, Ufaransa. Sabalenka alipata upinzani mkali kutoka kwa Osaka katika mchezo huo wa hatua ya 16 - [Mmiliki wa Southampton amkingia kifua Kocha Mkuu](https://spotileo.co.tz/mmiliki-wa-southampton-amkingia-kifua-kocha-mkuu/) - SOUTHAMPTON: MMILIKI wa klabu ya Southampton nchini England Dragan Solak, amesema hatamfukuza kazi kocha mkuu wa timu hiyo Tonda Eckert, licha ya kuhusishwa na sakata la kupeleleza mazoezi ya timu pinzani katika Championship. Solak amesema Eckert anastahili kupewa nafasi ya pili kutokana na uwezo wake mkubwa wa ukocha na mchango alioutoa tangu alipopewa jukumu la - [Haji Manara: Hatuendi Morocco kufanya siasa](https://spotileo.co.tz/haji-manara-hatuendi-morocco-kufanya-siasa/) - DAR ES SALAAM:MSEMAJI wa timu za taifa za soka nchini, Haji Manara, amesema safari ya Watanzania zaidi ya 100 kuelekea Morocco kwa ajili ya fainali ya Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 (AFCON U-17) inalenga kuipa sapoti Timu ya Taifa ya Tanzania, Serengeti Boys, na si kufanya siasa kama ambavyo baadhi ya - [Michuano ya wanawake U17 Cecafa kuanza Juni 13](https://spotileo.co.tz/michuano-ya-wanawake-u17-cecafa-kuanza-juni-13/) - DAR ES SALAAM: MICHUANO ya Soka la Wanawake kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Afrika Mashariki na Kati inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka ukanda huo (Cecafa) imepangwa kufanyika Dar es Salaam kuanzia Juni 13 hadi 23, 2026. Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa jana, Tanzania, Kenya, Sudan na Somalia zipo Kundi - [Filamu 65 zatangazwa kuwania tuzo za ZIFF 2026o](https://spotileo.co.tz/filamu-65-zatangazwa-kuwania-tuzo-za-ziff-2026o/) - ZANZIBAR:TAMASHA Kimataifa la filamu Afrika Mashariki, Zanzibar International Film Festival (ZIFF), limeanza kuteka headlines baada ya waandaaji wake kutangaza rasmi filamu 65 pekee kutoka nchi mbalimbali duniani ndizo zitakazosshindanishwa katika tamasha hilo. Nchi ya Uganda imeongoza kwa kuwasilisha filamu 50 katika tamasha hilo huku Tanzania ikiwasilisha filamu 45 tu. Mkurugenzi Mtendaji wa Tamasha hilo Joseph - [Waandaaji wa filamu YouTube waitikisa Hollywood](https://spotileo.co.tz/waandaaji-wa-filanu-youtube-waitikisa-hollywood/) - LOS ANGELES:SEKTA ya filamu nchini Marekani inaendelea kushuhudia mabadiliko makubwa baada ya waandaaji wa maudhui waliotokea kwenye jukwaa la YouTube kuanza kupata nafasi katika uzalishaji wa filamu kubwa za Hollywood. Mafanikio yao katika kuvutia mamilioni ya watazamaji mtandaoni yamewafanya kuonekana kama nguvu mpya inayoweza kubadili mwelekeo wa tasnia hiyo yenye ushindani mkubwa duniani. Katika kipindi - [Harambee Stars yafanya mabadiliko kikosi chake](https://spotileo.co.tz/harambee-stars-yafanya-mabadiliko-kikosi-chake/) - NAIROBI:TIMU ya Taifa ya Kenya, Harambee Stars, imefanya mabadiliko kadhaa katika kikosi chake kinachoendelea kujiandaa kwa mechi za kirafiki za kimataifa zitakazochezwa mwezi Juni mwaka huu. Mabadiliko hayo yanalenga kuimarisha kikosi hicho huku benchi la ufundi likiendelea kutathmini uwezo wa wachezaji kabla ya majukumu muhimu ya mashindano yajayo. Katika maboresho hayo, baadhi ya wachezaji wameongezwa - [Milner akubali imetosha sasa](https://spotileo.co.tz/milner-akubali-imetosha-sasa/) - LONDON: ALIYEKUWA nyota wa timu ya taifa ya England, James Milner, ametangaza kustaafu soka baada ya kucheza kwa miaka 24 katika Ligi Kuu ya England. Kiungo huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi mbalimbali, ambaye sasa ana umri wa miaka 40, anaondoka uwanjani baada ya kumaliza mkataba wake na Brighton & Hove Albion, alikocheza kwa misimu - [Slot: Nimeiacha Liverpool ilipostahili](https://spotileo.co.tz/slot-nimeiacha-liverpool-ilipostahili/) - LONDON: ALIYEKUWA kocha mkuu wa Liverpool, Arne Slot, amesema anaondoka klabuni hapo akiwa na imani kuwa ameiacha katika nafasi yake sahihi miongoni mwa timu bora zaidi barani Ulaya baada ya kufutwa kazi mwishoni mwa wiki. Kocha huyo raia wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 47 alitoa kauli hiyo kupitia barua ya wazi aliyowaandikia mashabiki wa - [Simba hawana utani, wameingia kambini](https://spotileo.co.tz/simba-hawana-utani-wameingia-kambini/) - DAR ES SALAAM: KIKOSI cha Simba SC leo Jumatatu kimerejea mazoezini kuanza maandalizi ya michezo saba iliyosalia ya Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la CRDB kabla ya kuhitimishwa kwa msimu huu. Ofisa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema wachezaji wote ambao hawapo kwenye majukumu ya timu za taifa wameripoti kambini - [Class apata dili kufanya mazoezi nchini Marekani](https://spotileo.co.tz/class-apata-dili-kufanya-mazoezi-nchini-marekani-2/) - DAR ES SALAAM: BONDIA wa Tanzania, Ibrahim Class, amesema amepokea kwa furaha kubwa kukubaliwa kwenda kufanya mazoezi chini ya bondia bingwa wa Marekani, Terence Crawford, akieleza kuwa hatua hiyo ni ndoto aliyokuwa akiisubiri kwa muda mrefu. Akizungumza Dar es Salaam Class amesema nafasi hiyo ni mafanikio makubwa katika safari yake ya ngumi na itampa hamasa - [Mkali wa Jiko kuondoka na donge nono](https://spotileo.co.tz/mkali-wa-jiko-kuondoka-na-donge-nono/) - DAR ES SALAAM: MSHINDI wa shindano la Mkali wa Jiko msimu wa sita anatarajiwa kuondoka na zawadi ya Shilingi milioni tano pamoja na kusomeshwa Chuo cha Taifa cha Utalii, sambamba na fursa mbalimbali za ajira. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, mratibu wa shindano hilo, Zainabu Issa, amesema msimu wa sita wa - [Serena kurudi uwanjani baada ya miaka minne](https://spotileo.co.tz/serena-williams-karibu-kurejea-tenisi-baada-ya-miaka-minne/) - LONDON: NYOTA wa zamani wa tenisi duniani, Serena Williams, anatarajiwa kurejea tena kwenye mashindano ya ushindani baada ya taarifa kueleza kuwa huenda akacheza michuano ya Queen’s Club mwezi ujao nchini England. Serena mwenye umri wa miaka 44 hajacheza mchezo wa ushindani tangu mwaka 2022 alipostaafu baada ya michuano ya US Open, lakini sasa ameibua matumaini - [Wawili Serengeti Boys waula Stars](https://spotileo.co.tz/wawili-serengeti-boys-waula-stars/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Miguel Gamondi, amewaongeza wachezaji wawili wa Serengeti Boys katika kikosi cha timu ya taifa kuelekea michezo miwili ya kirafiki ya kalenda ya FIFA itakayochezwa nchini Morocco. Wachezaji walioitwa ni Luqman Mbalasalu na Kassim Juma ambao kwa sasa wapo na kikosi cha Serengeti Boys kinachoshiriki michuano ya Mataifa - [Madrid njia nyeupe kwa Konate](https://spotileo.co.tz/madrid-njia-nyeupe-kwa-konate/) - Real Madrid yapata nguvu kumsajili beki wa Liverpool MADRID: REAL Madrid imepata nguvu mpya katika harakati za kumsajili beki wa Liverpool, Ibrahima Konate, wakati klabu hiyo ikisaka mbadala wa David Alaba anayetarajiwa kuondoka mwishoni mwa msimu. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Hispania, Konate alikuwa mmoja wa malengo makubwa ya Real Madrid tangu msimu uliopita huku - [Messi yuko 'fiti' kwa Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/messi-yuko-fiti-kwa-kombe-la-dunia/) - BUENOS AIRES: NAHODHA wa Argentina, Lionel Messi anatarajiwa kucheza Kombe la Dunia la sita baada ya kutajwa kwenye kikosi cha nchi hiyo kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Dunia 2026. Messi, ambaye atakuwa na miaka 39 wakati wa mashindano hayo, ameendelea kuandika historia akiwa mmoja wa wachezaji bora kuwahi kutokea duniani baada ya kuiongoza Argentina kutwaa - [Stars kujiweka mguu sawa kwa AFCON 2027](https://spotileo.co.tz/stars-kujiweka-mguu-sawa-kwa-afcon-2027/) - DAR ES SALAAM: OFISA Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Clifford Ndimbo amesema michezo ya kirafiki ya kimataifa kati ya Taifa Stars dhidi ya Uganda na Rwanda ni sehemu ya maandalizi ya timu katika kujiweka tayari kwa mashindano mbalimbali yajayo ikiwemo Afcon. Akizungumza Dar es Salaam Ndimbo amesema mchezo wa kwanza utachezwa Juni 5 - [Azam FC yakanusha kupokea maombi ya Ibenge](https://spotileo.co.tz/azam-fc-yakanusha-kupokea-maombi-ya-ibenge/) - DAR ES SALAAM: OFISA Habari wa Azam FC, Hasheem Ibwe amesema klabu hiyo haijapokea taarifa yoyote rasmi kuhusu kuhitajika kwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Florent Ibenge, kutoka klabu nyingine zinazotajwa kumwania. Ibwe amesema pia kocha huyo mwenyewe hajawasilisha taarifa yoyote kwa uongozi wa Azam FC kupitia wawakilishi wake kuhusu nia ya kuondoka au kuhitajika - [Nsangazelu: Hatuendi Kombe la Dunia kinyonge](https://spotileo.co.tz/nsangazelu-hatuendi-kombe-la-dunia-kinyonge/) - RABAT: KOCHA wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, Elieneza Nsangazelu amesema ushindi walioupata dhidi ya Misri umeongeza imani kwa kikosi hicho kufanya makubwa zaidi katika michuano ya Kombe la Dunia. Serengeti Boys ilitinga fainali baada ya kuiondosha Misri kwa mikwaju ya penalti 4-3 kufuatia sare tasa ndani - [Barcelona yapania kumng'oa Alvarez ndani Atletico](https://spotileo.co.tz/barcelona-yapania-kumngoa-alvarez-ndani-atletico/) - BARCELONA: KLABU ya Barcelona inadaiwa kuandaa ofa ya Euro milioni 90 kwa ajili ya kumng’oa mshambuliaji wa Atletico Madrid, Julian Alvarez, baada ya kufanya mazungumzo na mawakala wa nyota huyo wa Argentina. Alvarez mwenye umri wa miaka 26 ametajwa kuwa chaguo kuu la Barcelona kuchukua nafasi ya mshambuliaji mkongwe Robert Lewandowski huku taarifa zikieleza kuwa - [JKT Queens kupewa ushindi wa mezani](https://spotileo.co.tz/jkt-queens-kupewa-pointi/) - DAR ES SALAAM: OFISA Habari wa JKT Queens, Masau Bwire, amesema kutochezwa kwa mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake kati ya timu yao na Ruangwa Queens kulitokana na wapinzani wao kushindwa kufika uwanjani kwa wakati uliopangwa. Akizungumza leo baada ya mchezo huo uliokuwa ufanyike jana Mei 27 katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Bwire amesema - [PSG yapewa nafasi kutwaa UCL](https://spotileo.co.tz/psg-yapewa-nafasi-kutwaa-ucl/) - BUDAPEST: PARIS Saint-Germain (PSG) imepewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mbele ya Arsenal kutokana na ubora wa kikosi chake pamoja na wachezaji wake kuwa na muda mkubwa wa kupumzika kabla ya fainali hiyo. Takwimu zinaonesha kuwa wachezaji wa Arsenal wamecheza dakika karibu 7,000 zaidi katika mechi za ligi msimu huu - [BSS yalamba donge nono](https://spotileo.co.tz/bss-yalamba-donge-nono/) - DAR ES SALAAM: BENKI ya CRDB imedhamini rasmi mashindano maarufu ya kusaka vipaji nchini, Bongo Star Search 2026, ambayo sasa yatakuwa yakifahamika kama CRDB Bank Bongo Star Search 2026. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya CRDB Bank, Palm Beach jijini Dar es Salaam, Madam Rita amesema ujio wa benki hiyo - [Clarke kuendelea kuinoa Scotland hadi 2030](https://spotileo.co.tz/clarke-kuendelea-kuinoa-scotland-hadi-2030/) - EDINBURG: KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Scotland, Steve Clarke, ameongeza mkataba mpya utakaomuweka madarakani hadi Kombe la Dunia la mwaka 2030 baada ya mafanikio ya kuifikisha nchi hiyo katika fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza baada ya miaka 28. Clarke mwenye umri wa miaka 62 alikuwa katika sintofahamu kuhusu hatma - [Dar City yawakumbuka watoto ikirejea kutoka Rwanda](https://spotileo.co.tz/dar-city-yawakumbuka-watoto-ikirejea-kutoka-rwanda/) - DAR ES SALAAM: TIMU YA Dar City Basketball Club imetoa msaada wa vyakula kwa Watoto wenye uhitaji maalum mara baada ya kurejea Dar es Salaam ikitokea nchini Rwanda ilikokuwa kwenye mashindano ya Basketball Africa League (BAL) . Dar City iliishia hatua yar obo fainali. Katika mapokezi yao yaliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward - [Oshibibi ya Gasper yatikisa Afrika Mashariki](https://spotileo.co.tz/oshibibi-ya-gasper-yatikisa-afrika-mashariki/) - MAREKANI: MSANII wa kizazi kipya anayeishi Marekani, Gasper Welongo, ameendelea kufanya vizuri kwenye anga la muziki baada ya wimbo wake mpya Oshibibi kupata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Gasper, ambaye ni Mtanzania anayeishi nchini Marekani, amesema mafanikio ya wimbo huo yamezidi matarajio yake kutokana na idadi kubwa ya - [Ilala yang'ara riadha UMITASHUMTA DAR](https://spotileo.co.tz/ilala-yangara-riadha-umitashumta-dar/) - DAR ES SALAAM: TIMU ya Riadha Kombaini ya Ilala, imeng'ara katika Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA), ngazi ya Mkoa wa Dar es Salaam. Mashindano yamefanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, jana na kushirikisha Wilaya tano, Ilala, Temeke, Kinondoni, Ubungo na Kigamboni. Vijana hao wa Shule - [Benfica yaongeza dau la kumbakisha Mourinho](https://spotileo.co.tz/benfica-yaongeza-dau-la-kumbakisha-mourinho/) - LISBON: KLABU ya Benfica imeongeza kiwango cha fedha kinachohitajika kwa Jose Mourinho kuondoka klabuni hapo na kujiunga na Real Madrid baada ya kipengele chake cha kuachiliwa kumalizika. Ripoti zinaeleza kuwa Real Madrid tayari imekubaliana mkataba wa miaka miwili na Mourinho ambaye anatajwa kuwa chaguo la rais wa klabu hiyo, Florentino Perez, kuchukua nafasi ya ukocha - [Knicks watinga Fainali za NBA kwa mara ya kwanza tangu 1999](https://spotileo.co.tz/knicks-watinga-fainali-za-nba-kwa-mara-ya-kwanza-tangu-1999/) - NEW YORK: TIMU ya New York Knicks ya Marekani imefuzu kucheza Fainali za Ligi ya Mpira wa Kikapu ya Marekani (NBA) kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1999 baada ya kuichapa Cleveland Cavaliers kwa pointi 130-93 katika mchezo wa nne wa fainali za Ukanda wa Mashariki uliochezwa mjini Cleveland. Ushindi huo umeifanya Knicks kumaliza kwa - [Mgunda: Makosa yetu yametugharimu dhidi ya Yanga](https://spotileo.co.tz/mgunda-makosa-yetu-yametugharimu-dhidi-ya-yanga/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Namungo FC, Juma Mgunda amesema makosa ya kujirudia yaliyofanywa na wachezaji wake ndiyo yaliyoigharimu timu hiyo katika mchezo waliopoteza mabao 3-1 dhidi ya Yanga jana. Mgunda amesema kucheza dhidi ya timu yenye wachezaji wenye ubora kama Yanga kunahitaji umakini mkubwa kwani kosa dogo linaweza kuadhibiwa haraka. “Mchezo wowote unapocheza - [Feisal: Azam FC tumebadilika, tunaonesha hadhi ya klabu](https://spotileo.co.tz/feisal-azam-fc-tumebadilika-tunaonesha-hadhi-ya-klabu/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO wa Azam FC, Feisal Salum amesema wao kama wachezaji waliamua kujipanga upya baada ya mwenendo usioridhisha katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, jambo ambalo sasa limeanza kuzaa matunda. Feisal amesema hayo baada ya Azam FC kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya KMC FC katika mchezo wa - [Kamwe: Mechi tano zilizobaki ni fainali](https://spotileo.co.tz/kamwe-mechi-tano-zilizobaki-ni-fainali/) - DAR ES SALAAM: MENEJA wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe, amesema mechi tano zilizobaki kwa timu hiyo katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara ni sawa na dabi kutokana na ushindani mkubwa uliopo. Yanga imetoka kushinda mchezo wake uliopita dhidi ya Namungo mabao 3-1 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja - [Timu za taifa zapata udhamini wa vinywaji](https://spotileo.co.tz/timu-za-taifa-zapata-udhamini-wa-vinywaji/) - DAR ES SALAAM: SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesaini mkataba mkubwa wa udhamini wa miaka miwili na kampuni ya Watercom Tanzania. Katika hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam, Rais wa TFF Wallace Karia na Meneja Masoko wa Watercom Mohamed Salim walisaini makubaliano yanayohusisha udhamini wa - [Odemba awachana walimbwende wa kisasa](https://spotileo.co.tz/odemba-awachana-walimbwende-wa-kisasa/) - DAR ES SALAAM : MLIMBWENDE wa zamani wa Tanzania, Miriam Odemba, ameibua mjadala mitandaoni baada ya kuwakosoa walimbwende wa kizazi cha sasa kwa madai kuwa wamepoteza uhalisia na mvuto wa asili uliokuwepo zamani. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Odemba amesema walimbwende wa sasa wamejikita zaidi kwenye muonekano wa kisasa usio wa asili badala ya kuonesha - [Filamu kuhimiza utalii wa ndani](https://spotileo.co.tz/filamu-kuhimiza-utalii-wa-ndani/) - DAR ES SALAAM: WASANII nchini wametakiwa kutumia filamu na makala kuhamasisha utalii wa ndani kwa kutangaza vivutio vya Tanzania, kama ilivyofanywa na onesho maalumu la Guardians of The Peak Season I linaloangazia safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro. Akizungumza katika uzinduzi wa kuelekea msimu wa pili wa makala hiyo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara - [Messi azua hofu Kombe la Dunia 2026](https://spotileo.co.tz/messi-azua-hofu-kombe-la-dunia-2026/) - MIAMI: Nyota wa timu ya taifa ya Argentina , Lionel Messi, amezua hofu kwa mashabiki wa timu hiyo baada ya kupata maumivu wakati akiichezea Inter Miami CF kwenye mchezo wa Ligi Kuu Marekani (MLS) dhidi ya Philadelphia Union. Messi mwenye umri wa miaka 38 alionekana kushika nyuma ya mguu wake wa kushoto kabla ya kuomba - [West Ham kukabiliwa na ukata wa fedha](https://spotileo.co.tz/west-ham-kukabiliwa-na-ukata-wa-fedha/) - LONDON: KLABU ya West Ham United imeanza kukabiliwa na presha kubwa ya kifedha kufuatia uamuzi wa English Football League (EFL) kuanzisha sheria mpya za matumizi ya vikosi kuanzia msimu wa 2026-27. Kwa mujibu wa sheria hizo mpya, klabu zitapaswa kutumia asilimia 85 tu ya mapato yao katika mishahara ya wachezaji pamoja na gharama nyingine za - [Mataifa saba kuchuana PickelBall](https://spotileo.co.tz/mataifa-saba-kuchuana-pickelball/) - DAR ES SALAAM : ZAIDI ya Mataifa Saba Duniani ikiwemo Kenya,Congo ,Rwanda ,Uganda,South Afrika ,Dubai kuja Nchini kwa ajili ya mashindano ya mchezo wa PickeBall yatakayoanza tarehe 27 hadi 31 mwezi huu. Hayo ameyasema leo Rais wa Chama Cha Pickeball Kartik Kapoor Nchini Tanzania na kusema kuwa mashindano hayo yatafanyika katika viwanja wa Gymkhana jijini - [David Rajabu kuja kivingine](https://spotileo.co.tz/david-rajabu-kuja-kivingine/) - MWANAMUZIKI muziki wa injili, David Rajabu, anatarajia kuachia wimbo wake mpya uitwao 'upendo' mwishoni mwa wiki hii, ukiwa na lengo la kuhamasisha upendo na mshikamano katika nchi za Afrika Mashariki. Rajabu, ambaye kwa sasa anaishi nchini Marekani, amewaomba mashabiki wa muziki wa injili kumuunga, amesema wimbo huo utapatikana katika majukwaa mbalimbali ya muziki kuanzia Mei - [Guardiola kuachana na Manchester City mwishoni mwa msimu](https://spotileo.co.tz/guardiola-kuachana-na-manchester-city-mwishoni-mwa-msimu/) - LONDON: KOCHA wa Manchester City, Pep Guardiola ametangaza kuondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu, akihitimisha safari ya miaka 10 iliyogubikwa na mafanikio makubwa katika soka la England. Guardiola mwenye umri wa miaka 55, ambaye alijiunga na City mwaka 2016 akitokea Bayern Munich, ameiongoza timu hiyo kutwaa mataji sita ya Premier League, likiwemo la misimu - [Wavu kutumika kutangaza AFCON 2027](https://spotileo.co.tz/wavu-kutumika-kutangaza-afcon-2027/) - DAR ES SALAAM: OFISA Michezo Mwandamizi wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Charles Maguzu, amewahamasisha Watanzania kutumia Mashindano ya Mpira wa Wavu Ufukweni Afrika Kanda ya Tano kama jukwaa la kuitangaza Tanzania kuelekea mashindano ya AFCON 2027. Maguzu ametoa kauli hiyo jana wakati wa ufunguzi rasmi wa mashindano hayo yanayofanyika katika Fukwe ya Sawa - [T9 yaonesha fursa za Afcon 2027](https://spotileo.co.tz/t9-yaonesha-fursa-za-afcon-2027/) - DAR ES SALAAM: WAKATI Tanzania ikijiandaa kuwa mwenyeji wa mashindano ya AFCON 2027, kampuni ya T9 imeibuka na mkakati wa kuhamasisha Watanzania kuzitumia fursa za kiuchumi zitakazoambatana na mashindano hayo kupitia uzinduzi wa jarida la T9 Magazine Opportunity Plus. Akizungumza katika uzinduzi huo Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa T9, Othman Razak, amesema AFCON - [Okello mchezaji bora Aprili](https://spotileo.co.tz/okello-mchezaji-bora-aprili/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Allan Okello amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Aprili wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuonesha kiwango bora katika michezo ya mwezi huo. Okello ameibuka na tuzo hiyo baada ya kuwa na mchango mkubwa kwa timu yake katika michezo mitatu aliyocheza, ambapo amefunga bao moja na kutoa - [Simba, Mashujaa watambiana](https://spotileo.co.tz/simba-mashujaa-watambiana/) - KIGOMA: KOCHA Mkuu wa Mashujaa FC, Jamhuri Kihwelu amesema hana hofu na Simba kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa kesho, akisisitiza timu yake ipo tayari kupambana kutafuta ushindi. Kihwelu amesema uzoefu wake ndani ya Simba unampa uelewa mkubwa wa mazingira ya klabu hiyo, licha ya kutofuatilia mechi zao za hivi karibuni. “Hii ligi - [TRA tumewazidi kila kitu- Bwire](https://spotileo.co.tz/tra-tumewazidi-kila-kitu-bwire/) - ARUSHA: JKT Tanzania imesema haiwezi kujifananisha na TRA United kwani wameizidi ubora, malengo na uimara wa kikosi. Akizungumza baada ya mchezo jana Ofisa Habari wa JKT Tanzania, Masau Bwire amesema mashabiki waliofuatilia mchezo huo wamejionea tofauti ya viwango kati ya timu hizo mbili huku akisisitiza kuwa wapinzani wao walinusurika kupata matokeo mabaya zaidi. “JKT Tanzania - [TRA ina nafasi ya kufanya vizuri - Mwagala](https://spotileo.co.tz/tra-ina-nafasi-ya-kufanya-vizuri-mwagala/) - ARUSHA: OFISA Habari wa TRA United Christina Mwagala amesema sare waliyoipata dhidi ya JKT Tanzania ni matokeo yaliyowaumiza kutokana na kuhitaji pointi tatu muhimu, lakini bado wanaamini wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika michezo iliyosalia. Mwagala amesema baada ya mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha kuwa matokeo hayo yanapaswa - [Washiriki 20 BSS watinga kambini](https://spotileo.co.tz/washiriki-20-bss-watinga-kambini/) - DAR ES SALAAM: WASHIRIKI 20 kutoka Kenya, Uganda, DR Congo na Tanzania waliochaguliwa kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania pamoja na nchi kadhaa za Afrika Mashariki na Kati wamewasili rasmi kambini katika ufukwe wa Ndege Beach jijini Dar es Salaam kuanza safari yao ya kutwaa ushindi vipaji la Bongo Star Search (BSS). Akizungumza na waandishi wa - [Pellegrini afurahia kurejea Ligi ya Mabingwa](https://spotileo.co.tz/pellegrini-afurahia-kurejea-ligi-ya-mabingwa/) - SEVILLA: KOCHA wa Real Betis, Manuel Pellegrini amesema ana furaha kubwa baada ya timu hiyo kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza baada ya miaka 20. Betis ilihakikisha nafasi hiyo baada ya kuifunga Elche mabao 2-1 katika mchezo wa LaLiga, ushindi uliowafanya kumaliza ndani ya nafasi tano za juu kwenye msimamo wa - [Yanga, Dodoma Jiji lazima kieleweke](https://spotileo.co.tz/yanga-dodoma-jiji-lazima-kieleweke/) - SINGIDA: KOCHA wa muda wa Yanga, AbdiHamid Moallin, amesema kikosi chake kiko tayari kupambana na Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa leo kwenye Uwanja wa Airtel mkoani Singida. Moallin amesema licha ya ratiba kuwa ngumu kutokana na muda mfupi kati ya mechi moja na nyingine, benchi la ufundi limejikita zaidi - [Ancelotti afunguka kuhusu nafasi ya Neymar Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/ancelotti-afunguka-kuhusu-nafasi-ya-neymar-kombe-la-dunia/) - BRASILIA: KOCHA wa timu ya taifa ya Brazil, Carlo Ancelotti amesema uamuzi wa kumjumuisha nyota Neymar Junior kwenye kikosi cha Kombe la Dunia 2026 utategemea uwezo wake wa kimwili na kiwango chake uwanjani, si hisia au umaarufu wake. Ancelotti amesema Neymar bado ni mchezaji muhimu kwa Brazil kutokana na kipaji chake kikubwa, lakini ameathiriwa na - [Yanga wameamua ishu ya uwanja wao!](https://spotileo.co.tz/yanga-wameamua-ishu-ya-uwanja-wao/) - DAR ES SALAAM: RAIS wa Klabu ya Yanga, Hersi Said, ameongoza kikao cha mwisho cha majadiliano kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa uwanja wa klabu hiyo. Kikao hicho kimefanyika leo Mei 12, 2026 jijini Dar es Salaam, kikiwa sehemu ya maandalizi ya kuanza rasmi kwa mradi wa uwanja wa Yanga SC, ambao unatarajiwa kuwa - [Ahmed Ally: Simba Tunakwenda Kigoma Kuchukua Pointi Tatu](https://spotileo.co.tz/ahmed-ally-simba-tunakwenda-kigoma-kuchukua-pointi-tatu/) - DAR ES SALAAM: MENEJA wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema timu hiyo inakwenda Kigoma ikiwa na lengo la kuchukua pointi tatu dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Alhamisi. Ahmed amesema Simba inautambua ugumu wa mchezo huo kutokana na ubora wa Mashujaa pamoja na benchi lao la - [Coastal: Kazi ipo kwa Mbeya City ila tutapambana](https://spotileo.co.tz/coastal-kazi-ipo-kwa-mbeya-city-ila-tutapambana/) - MANYARA: KOCHA Mkuu wa Coastal Union, Fikiri Elias amesema wanatarajia mchezo mgumu dhidi ya Mbeya City kesho kutokana na umuhimu wa pointi kwa timu zote mbili katika msimamo wa ligi. Fikiri amesema Coastal Union ipo nafasi ya 13 huku Mbeya City wakiwa nafasi ya 14, hali inayoufanya mchezo huo kuwa wa ushindani mkubwa kwa kila - [Gigy Money amuomba msamaha Zuchu ](https://spotileo.co.tz/gigy-money-amuomba-msamaha-zuchu/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Gigy Money, amemuomba msamaha msanii mwenzake Zuchu kupitia ujumbe aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram. Katika ujumbe huo, Gigy Money alisema ameandika kwa moyo wa kweli na unyenyekevu akieleza kuwa anatamani kuweka mambo sawa kati yao. “Natumaini uko salama na unaendelea vizuri. Nimechukua muda kuandika - [Southampton katika skendo ya ujasusi](https://spotileo.co.tz/southampton-katika-skendo-ya-ujasusi/) - LONDON: KLABU ya Southampton imeomba kuongezewa muda na EFL ili kukamilisha uchunguzi wa ndani kuhusu tuhuma za ujasusi dhidi ya wapinzani wao Middlesbrough kabla ya mchezo wa marudiano wa mtoano wa kuwania kupanda Ligi Kuu England. Southampton wanatuhumiwa baada ya mchambuzi mmoja wa timu hiyo kudaiwa kurekodi mazoezi ya Middlesbrough akiwa amejificha kwenye vichaka kabla - [Lebron James aweka kitendawili NBA](https://spotileo.co.tz/lebron-james-aweka-kitandawili-mustakabali-wake-nba/) - LOS ANGELES: NYOTA wa Los Angeles Lakers, LeBron James amesema bado hajafanya uamuzi kuhusu mustakabali wake wa kucheza NBA baada ya timu yake kutolewa kwenye hatua ya nusu fainali ya Kanda ya Magharibi dhidi ya Oklahoma City Thunder. Thunder waliibuka na ushindi wa pointi 115-110 na kukamilisha ushindi wa jumla wa 4-0 katika mfululizo huo - [De Zebri akerwa na sare dhidi ya Leeds](https://spotileo.co.tz/de-zebri-akerwa-na-sare-dhidi-ya-leeds/) - LONDON: KOCHA Mkuu wa Tottenham Hotspur, Roberto De Zerbi ameonesha wazi kukerwa baada ya timu yake kushindwa kuibuka na ushindi dhidi ya Leeds United kufuatia sare ya 1-1 iliyozidi kuiweka Spurs kwenye presha ya kushuka daraja katika Ligi Kuu England. Spurs walitangulia kupitia bao kali la Mathys Tel kabla ya makosa ya nyota huyo huyo - [Elimu ya usalama barabarani kusaidia maandalizi ya AFCON](https://spotileo.co.tz/elimu-ya-usalama-barabarani-kusaidia-maandalizi-ya-afcon-2027/) - DAR ES SALAAM: MBUNGE wa Jimbo la Mbagala, Burchard Kakulu amesema kampeni ya utoaji elimu ya usalama barabarani kwa waendesha bodaboda itakuwa sehemu muhimu ya maandalizi ya Tanzania kuelekea mashindano ya Mataifa ya Afrika 2027. Kakulu amesema hayo katika kampeni ya Usalama Daima iliyofanyika katika viwanja vya Zakhiem Mbagala, Temeke jijini Dar es Salaam, ikiwahusisha - [DSTV yazindua 'kila kitu kitasubiri' kuelekea Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/dstv-yazindua-kila-kitu-kitasubiri-kuelekea-kombe-la-dunia/) - DAR ES SALAAM: KAMPUNI ya DStv kupitia SuperSport imezindua kampeni yake mpya ya “Kila Kitu Kitasubiri” kuelekea fainali za Kombe la Dunia 2026 huku ikitangaza maboresho makubwa ya huduma kwa mashabiki wa soka nchini. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Masoko wa DStv, Ronald Shelukindo amesema Kombe la Dunia linaendelea kuwa mashindano makubwa zaidi - [Coastal haitacheza kinyonge dhidi ya Yanga](https://spotileo.co.tz/coastal-haitacheza-kinyonge-dhidi-ya-yanga/) - DAR ES SALAAM: COASTAL Union imewataka mabingwa watetezi Yanga kutarajia upinzani mkali watakapokutana katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kesho, huku Kocha wa Coastal Union, Fikiri Elias akisisitiza kuwa timu yake haitacheza kwa woga. Fikiri amesema kikosi chake kimeutumia vizuri muda wa maandalizi kwa kufanya maboresho muhimu ndani ya siku mbili zilizopita ili kuhakikisha - [Mavokali afunguka maumivu ya miaka miwili,](https://spotileo.co.tz/mavokali-afunguka-maumivu-ya-miaka-miwili/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Mavokali amefunguka kuhusu changamoto nzito alizopitia katika safari yake ya muziki, akieleza kuwa aliwahi kufikia hatua ya kutaka kukata tamaa na kuachana kabisa na muziki kutokana na maumivu na dhuluma alizokutana nazo. Mwanamuziki huyo aliyewahi kutamba na wimbo wa Commando amesema kwa kipindi cha takribani miaka miwili mfululizo - [Tuzo za wanamichezo bora kutolewa kesho](https://spotileo.co.tz/tuzo-za-wanamichezo-bora-kutolewa-kesho/) - DAR ES SALAAM: MSIMU wa nne wa Tuzo za Wanamichezo bora Tanzania unatarajiwa kufanyika kesho, huku waandaaji wakieleza kuwa maandalizi yote yamekamilika kwa ajili ya hafla hiyo ya kuwaenzi wanamichezo waliofanya vizuri ndani na nje ya nchi mwaka 2025. Akizungumza kuelekea hafla hiyo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha amesema - [Moallin: Tunazitaka pointi tatu kwa Coastal](https://spotileo.co.tz/moallin-tunazitaka-pointi-tatu-kwa-coastal/) - DAR ES SALAAM:KAIMU Kocha Mkuu wa Yanga, Abdihamid Moallin amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa kesho Mei 9,2026 dhidi ya Coastal Union utakaochezwa katika Uwanja wa KMC huku akisisitiza kuwa lengo kubwa ni kupata pointi tatu. Moallin amesema wachezaji wako kwenye hali nzuri kiakili na kimwili kuelekea mchezo huo muhimu, akieleza kuwa kila - [Ni Azam FC, TRA kusaka pointi tatu Leo](https://spotileo.co.tz/ni-azam-fc-tra-kusaka-pointi-tatu-leo/) - ARUSHA: MACHO na masikio ya wadau wa soka leo yataelekezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha ambapo TRA United itaikaribisha Azam FC katika mchezo muhimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara wenye vita ya pointi tatu na nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi. Azam FC wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa nafasi ya tatu - [Hii ndio sababu Pedro kutimuliwa Yanga](https://spotileo.co.tz/yanga-yaeleza-sababu-za-kumwondoa-kocha-pedro/) - DAR ES SALAAM: OFISA Habari wa Yanga SC, Ally Kamwe amefafanua sababu za uongozi wa klabu hiyo kufanya uamuzi wa kuachana na Kocha Mkuu Pedro Gonçalves, akibainisha kuwa uamuzi huo haukutokana na matokeo ya uwanjani pekee, bali tathmini ya kina ya mwenendo wa timu. Yanga ilitangaza kuachana na Pedro Jana baada ya kumalizika kwa mechi - [Miss Grand Beatrice: “Kuwa single kuna faida zake”](https://spotileo.co.tz/miss-grand-beatrice-kuwa-single-kuna-faida-zake/) - DAR ES SALAAM: Beatrice Alex ambaye ni Miss Grand Tanzania 2025, amesema kwa sasa yupo single na hajawa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa takribani miaka miwili. Mrembo huyo amesema mara ya mwisho kuwa na mpenzi ilikuwa mwaka 2024 kabla ya kuanza mwaka 2025, na tangu hapo ameendelea kuwa peke yake huku akiweka nguvu zaidi kwenye - [Uchebe: Nampenda Shilole, siyo adui yangu](https://spotileo.co.tz/uchebe-nampenda-shilole-siyo-adui-yangu/) - DAR ES SALAAM: MPENZI wa zamani wa Msanii Zuwena Mohamed 'Shilole' Uchebe ameweka wazi kuwa hana chuki na aliyekuwa mpenzi wake, Shishi, akieleza kuwa kuachana siyo vita ndiyo maana wakikutana husalimiana kwa heshima na upendo. Kuhusu uhusiano wao wa sasa, Uchebe amesema bado wanaheshimiana licha ya kuachana. “Salamu ni vizuri, mimi sina chuki na mtu. - [Chief Godlove amtambulisha msanii mpya](https://spotileo.co.tz/chief-godlove-amtambulisha-msanii-mpya/) - DAR ES SALAAM:MENEJA na mdau maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Godlove Mwakibete 'Chief Godlove', amemtabulisha rasmi msanii wake mpya anayefahamika kwa jina la Agness Silvester Samson kupitia ukurasa wake wa Instagram. Chief Godlove amesema kuwa ana imani kubwa na uwezo wa msanii huyo mpya kiasi cha kutoa ahadi nzito kwamba endapo hatofanikiwa kufanya vizuri - [Chief Godlove aweka rehani mali zake kisa msanii wake mpya](https://spotileo.co.tz/chief-godlove-aweka-rehani-mali-zake-kisa-msanii-wake-mpya/) - DAR ES SALAAM: MSANII na mfanyabiashara maarufu, Godlove Mwakibete 'Chief Godlove', ameibua mjadala mtandaoni baada ya kuweka wazi azma yake kuhusu mafanikio ya msanii wake mpya wa kike. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Chief Godlove amesema kuwa yuko tayari kugawa mali zake zote kwa watu wasiojiweza endapo msanii huyo hatapata mafanikio makubwa, ikiwemo kufika katika - [Pete ya uchumba ya Careen yaacha maswali](https://spotileo.co.tz/pete-ya-uchumba-ya-careen-yaacha-maswali/) - DAR ES SALAAM: MREMBO na mwanamitindo , Caren Simba, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuchapisha picha zake akiwa amevalishwa pete inayodhaniwa kuwa ya uchumba. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Caren ameonekana akiwa na furaha huku akionesha pete hiyo, jambo lililowafanya mashabiki na wadau wa mitandao ya kijamii kuanza kujiuliza kuhusu hatua hiyo mpya katika maisha - [Miaka 20 ya Christan Bella usipime!](https://spotileo.co.tz/miaka-20-ya-christan-bella-usipimey/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa dansi Christian Bella kesho anatarajia kufanya tamasha maalum la kuadhimisha miaka 20 ya safari yake ya muziki, litakalofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City. Tamasha hilo linafanyika kama sehemu ya shukrani kwa Watanzania kwa sapoti kubwa waliompa katika kazi yake ya muziki, pamoja na kushukuru baada ya kupewa rasmi - [Cassie:Lucy Komba ndiye alinifundisha kiswahili](https://spotileo.co.tz/cassielucy-komba-ndiye-alinifundisha-kiswahili/) - MSANII wa filamu kutoka nchini Zambia, Cassie Kabwita amesema mwigizaji mkongwe Lucy Komba ndiye aliyemsaidia kujifunza lugha ya Kiswahili pamoja na uigizaji alipokuwa akiendeleza safari yake ya sanaa nchini Tanzania. Cassie ambaye ameonekana katika kazi mbalimbali za filamu na tamthilia Tanzania, amesema Lucy Komba alikuwa mwalimu wake mkubwa katika hatua za mwanzo za kazi yake - [Drake aisaidia Venezia kupata uwekezaji Serie A](https://spotileo.co.tz/drake-aisaidia-venezia-kupata-uwekezaji-serie-a/) - ROME: RAPA maarufu wa Canada Aubrey Graham 'Drake' ameisaidia klabu ya Venezia FC ya nchini Italy kupata uwekezaji mkubwa kutoka kwa mfanyabiashara wa michezo Tim Leiweke. Venezia ambayo imefanikiwa kurejea katika ligi kuu ya Italy, Serie A msimu huu, imetangaza kupokea uwekezaji wa euro milioni 100 sawa na zaidi ya Sh bilioni 300 za Kitanzania. - [Dembélé amtaja Gavi baada ya kuimaliza Bayern](https://spotileo.co.tz/dembele-amtaja-gavi-baada-ya-kuimaliza-bayern/) - MUNICH: NYOTA wa Paris Saint-Germain, Ousmane Dembélé, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kusherehekea kufuzu kwa timu yake hatua ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kushiriki video ya kiungo wa Barcelona, Pablo Martin 'Gavi', kwenye akaunti yake ya mtandaao wa kijamii. PSG imefanikiwa kufuzu fainali hiyo itakayochezwa Budapest baada ya kutoka sare ya 1-1 - [Sule atangaza kustaafu soka](https://spotileo.co.tz/sule-atangaza-kustaafu-soka/) - BERLIN: BEKI wa Borussia Dortmund, Niklas Sule ametangaza kustaafu soka mwishoni mwa msimu huu baada ya kukumbwa na majeraha ya mara kwa mara. Sule mwenye umri wa miaka 30 amesema amefikia uamuzi huo baada ya kuumia goti katika mchezo dhidi ya TSG Hoffenheim mwezi uliopita. Beki huyo wa timu ya taifa ya Ujerumani- aliyewahi kucheza - ['Mtibwa Sugar lazima ipambane'](https://spotileo.co.tz/mtibwa-sugar-lazima-ipambane/) - DAR ES SALAAM: KOCHA wa Mtibwa Sugar FC, Yusuph Chipo amesema timu yake inapaswa kujipanga upya haraka kuelekea mchezo ujao dhidi ya Singida Black Stars baada ya kuendelea kupata matokeo mabaya kwenye ligi. Mtibwa Sugar imetoka kupoteza mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Dodoma Jiji kwa kichapo cha bao 1-0 jana. Chipo amesema kupoteza mchezo - [Amani Josiah afichua mbinu zilizowapa ushindi](https://spotileo.co.tz/amani-josiah-afichua-mbinu-zilizowapa-ushindi/) - DAR ES SALAAM: KOCHA wa Dodoma Jiji FC, Amani Josiah amesema maandalizi na kuisoma vizuri Mtibwa Sugar FC ndiyo siri ya ushindi wa bao 1-0 walioupata jana katika mchezo wa Ligi Kuu. Amesema benchi la ufundi la Dodoma Jiji lilifanya uchambuzi wa kina wa mchezo wa Mtibwa Sugar kabla ya kukutana nao na kubaini maeneo - [Chama: Haikuwa rahisi ila tumetoboa](https://spotileo.co.tz/chama-haikuwa-rahisi-ila-tumetoboa/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama amesema ushindi wa bao 1-0 walioupata dhidi ya JKT Tanzania jana kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo haukuwa rahisi kutokana na ugumu wa mchezo huo hasa kipindi cha kwanza. Chama ambaye ndiye aliyefunga bao pekee la ushindi, amesema walitarajia kupata bao la mapema ili kuwasaidia - [Okello: Tulipaswa kufunga mabao zaidi](https://spotileo.co.tz/okello-tulipaswa-kufunga-mabao-zaidi/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO mshambuliaji wa Yanga Allan Okello amesema ushindi wa bao 1-0 walioupata dhidi ya KMC jana haukuwa mwepesi kutokana na timu hiyo kukosa nafasi nyingi za wazi kipindi cha kwanza cha mchezo. Okello ambaye ndiye aliyefunga bao pekee la ushindi amesema walitengeneza nafasi nyingi lakini walishindwa kuzitumia kabla ya kurejea kipindi cha - [Davido anapewa $300,000 na baba yake](https://spotileo.co.tz/davido-anapewa-300000-na-baba-yake/) - LAGOS: MSANII maarufu wa muziki kutoka Nigeria, David Adeleke, 'Davido', amesema kwamba licha ya kuingiza mapato makubwa kupitia muziki wake, bado anapokea pesa kutoka kwa baba yake, bilionea Adedeji Adeleke. Davido amesema kuwa baba yake hufanya hivyo kwa sababu bado ni mtoto wake. Katika maelezo yake, amesema: 'Baba yangu bado ananipa pesa, mimi ni mtoto - [Simeone ajivunia Atlético Licha ya kutolewa na Arsenal](https://spotileo.co.tz/simeone-ajivunia-atletico-licha-ya-kutolewa-na-arsenal/) - LONDON: KOCHA Mkuu wa Atletico Madrid, Diego Simeone, ameonesha kujivunia kiwango cha timu yake licha ya kutolewa kwenye nusu fainali ya UEFA Champions League kufuatia kichapo kutoka kwa Arsenal Jumanne usiku. Simeone alikiri kuwa wapinzani wao walistahili kusonga mbele, akieleza kuwa walikuwa makini zaidi hasa kipindi cha kwanza, jambo lililowapa faida muhimu. Hata hivyo, alisisitiza - [Saka aibua mjadala kuhusu mpinzani wa Fainali ya Ulaya](https://spotileo.co.tz/20421-2/) - LONDON: NYOTA wa Arsenal, Bukayo Saka, amewaacha mashabiki wa soka kwenye sintofahamu baada ya kutoa kauli ya fumbo akidai kuwa timu hiyo ina mpinzani inayomtaka kwa ajili ya fainali ya UEFA Champions League msimu huu. Saka mwenye umri wa miaka 24 aliihakikishia Arsenal tiketi ya kufika fainali hiyo itakayofanyika Budapest baada ya kufunga bao katika - [Mashabiki Chelsea wawaka hasira, wamgeukia mmiliki](https://spotileo.co.tz/mashabiki-chelsea-wawaka-hasira-wamgeukia-mmiliki/) - LONDON: HALI ya sintofahamu imezidi kutanda ndani ya klabu ya Chelsea kufuatia kuongezeka kwa hasira za mashabiki dhidi ya umiliki wa BlueCo, huku kauli mbiu ya “Hatujali Clear lake, nao hawatujali sisi" ikiendelea kutawala majukwaa ya Stamford Bridge msimu huu. Hasira hizo zimechochewa zaidi na kipigo cha mabao 3-1 walichopata dhidi ya Nottingham Forest katika - [Yanga KMC mechi ya Presha](https://spotileo.co.tz/yanga-kmc-mechi-ya-presha/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga leo inatarajiwa kushuka dimbani kuikabili KMC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara mzunguko wa 21 utakaopigwa kwenye Uwanja wa KMC, huku ikiwa na dhamira ya kuendelea kulinda nafasi yake kileleni mwa msimamo wa ligi. Yanga inaingia katika pambano hilo ikiwa vinara wa ligi kwa pointi 48 baada ya - [Simba, JKT mechi ya jasho kusaka pointi tatu](https://spotileo.co.tz/simba-jkt-mechi-ya-jasho-kusaka-pointi-tatu/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Simba SC leo inatarajia kushuka dimbani kuikabili JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaopigwa saa 12:00 jioni kwenye Uwanja wa Jenerali Isamuhyo, huku ikiwa na lengo la kuendelea kusalia kwenye mbio za ubingwa. Simba inaingia katika mchezo huo ikiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi kwa - [Azam FC yamweka Feisal Salum kwenye kiti cha Ufalme](https://spotileo.co.tz/azam-fc-yamweka-feisal-salum-kwenye-kiti-cha-ufalme/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Azam FC imempa ufalme kiungo mshambuliaji wake Feisal Salum, baada ya kufikisha mabao 10 na kutoa pasi nane za mabao (assists) msimu huu Ligi ikiwa bado inaendelea. Feisal ameng'ara katika michezo ya Ligi iliyofuatana hivi karibuni akihusika kufunga na kutoa pasi za mabao. Katika mchezo wa jana dhidi ya Namungo - [Tanzania yajiandaa kushiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola](https://spotileo.co.tz/tanzania-yajiandaa-kushiriki-michezo-ya-jumuiya-ya-madola/) - DODOMA:SERIKALI inaendelea kuimarisha maandalizi ya wanamichezo wake watakaoiwakilisha nchi katika Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Glasgow, Scotland mwaka 2026, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuinua ushindani wa kimataifa wa michezo ya Tanzania. Akizungumza bungeni, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Tanzania itatuma jumla ya wanamichezo 11 kushiriki katika michezo - [Serikali imetenga bilioni 76 kwa AFCON 2027](https://spotileo.co.tz/serikali-imetenga-bilioni-76-kwa-afcon-2027/) - DODOMA: SERIKALI imetenga dola milioni 30 (zaidi ya Shilingi bilioni 76) kwa ajili ya ada ya uandaaji wa mashindano ya AFCON 2027, hatua inayoonesha dhamira ya dhati ya kuhakikisha Tanzania na washirika wake wanafanikisha maandalizi ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika. Akizungumza bungeni leo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema uwekezaji - [Zaidi ya wasanii 21,000 wasajiliwa](https://spotileo.co.tz/zaidi-ya-wasanii-21000-wasajiliwa/) - DODOMA: SERIKALI imeendelea kuimarisha usimamizi wa sekta ya sanaa nchini kwa kusajili zaidi ya wasanii 21,875 hadi kufikia Aprili 2026, hatua inayotajwa kuongeza uwazi, mipango na fursa za maendeleo kwa wadau wa sekta hiyo. Akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2026/27, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na - [Barca waisogelea taji, Real Madrid waichelewesha sherehe](https://spotileo.co.tz/barca-waisogelea-taji-real-madrid-waichelewesha-sherehe/) - MADRID:KLABU ya Real Madrid imeilazimisha Barcelona kusubiri kutwaa ubingwa wa La Liga baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Espanyol. Katika mchezo huo uliochezwa Uwanja wa RCDE, nyota wa Madrid, Vinícius Júnior, aliibuka shujaa kwa kufunga mabao yote mawili kipindi cha pili dakika ya 55 na 66, akimalizia pasi za Gonzalo García - [Mwamnyeto: Yanga hatukukata tamaa](https://spotileo.co.tz/mwamnyeto-yanga-hatukukata-tamaa/) - DAR ES SALAAM: NAHODHA wa Yanga, Bakari Mwamnyeto, amesema nidhamu na kutokata tamaa kuliwasaidia kusawazisha na kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya watani wao Simba katika dabi ya Kariakoo. Mwamnyeto, ambaye ndiye aliyefunga bao la kusawazisha katika mchezo huo, amesema walikutana na upinzani mkali huku wapinzani wao wakitangulia kuongoza kabla ya wao kurejea mchezoni. - [Simba yajilaumu, yajipongeza baada ya sare](https://spotileo.co.tz/simba-yajilaumu-yajipongeza-baada-ya-sare/) - DAR ES SALAAM: BAADA ya Simba kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Yanga katika dabi ya Kariakoo, Msemaji wa Simba, Ahmed Ally, amesema matokeo hayo yana pande mbili; kujilaumu kwa kukosa ushindi na kujipongeza kwa maendeleo ya timu. Akizungumza baada ya mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Jenerali Isamuhyo jana, Ahmed amesema Simba walikuwa - [Jokate awainua wasichana 120 sayansi](https://spotileo.co.tz/jokate-awainua-wasichana-120-sayansi/) - DAR ES SALAAM:MKURUGENZI wa Kidoti Foundation, Jokate Mwegelo, amewahamasisha wanafunzi wa kike nchini kujikita katika masomo ya sayansi, akisisitiza kuwa urembo haupaswi kuwa kikwazo cha kufanikiwa katika taaluma hizo. Jokate ametoa wito huo wakati wa ziara ya kielimu iliyolenga kuhamasisha ujifunzaji wa sayansi nje ya darasa, ambapo alisisitiza umuhimu wa kubadili mfumo wa ufundishaji kwa - [Atletico yapata pigo jipya la majeruhi](https://spotileo.co.tz/atletico-yapata-pigo-jipya-la-majeruhi/) - MADRID:KLABU ya Atletico Madrid imeingia katika taharuki ya majeruhi kwa wachezaji wake muhimu kuelekea mchezo wa marudiano wa UEFA Champions League dhidi ya Arsenal. Habari njema kwa kocha Diego Simeone ni kurejea salama kwa mshambuliaji Julian Alvarez aliyefunga bao katika mchezo wa jana dhidi ya Arsenal ambaye alionekana kupata maumivu ya kifundo cha mguu, lakini - [Pochettino aumizwa na mateso ya Spurs](https://spotileo.co.tz/pochettino-aumizwa-na-mateso-ya-spurs/) - LONDON:KOCHA wa zamani wa Tottenham Hotspur, Mauricio Pochettino, amesema anahuzunishwa kuona timu hiyo ikipitia kipindi kigumu huku ikipambana kujinusuru kushuka daraja kutoka Premier League. Pochettino, aliyeinoa Spurs kati ya mwaka 2014 hadi 2019 na kuifikisha fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, amesema bado ana mapenzi makubwa na klabu hiyo na anaguswa na hali wanayopitia kwa - [Parker aondoka Burnley baada ya kushuka daraja](https://spotileo.co.tz/parker-aondoka-burnley-baada-ya-kushuka-daraja/) - LONDON:KOCHA Mkuu wa Burnley, Scott Parker, ameondoka klabuni hapo kwa makubaliano ya pande zote, siku nane tu baada ya timu hiyo kuthibitisha kushuka daraja kutoka Premier League. Hatua hiyo inakuja kufuatia msimu mgumu kwa Burnley, ambao umeshuhudia timu hiyo ikishinda michezo minne pekee kati ya 34 ya ligi, huku ikikusanya pointi moja tu katika michezo - [DAREVA yajipanga kuboresha mzunguko wa pili wa Ligi](https://spotileo.co.tz/dareva-yajipanga-kuboresha-mzunguko-wa-pili-wa-ligi/) - DAR ES SALAAM: BODI ya Ligi ya Chama cha Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam (DAREVA) imesema imeanza mikakati ya kufanya maboresho mbalimbali yatakayolenga kuupa ubora zaidi mzunguko wa pili wa ligi hiyo pamoja na kuongeza ushindani kwa timu shiriki. Akizungumza kuhusu maandalizi hayo, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Peter Kahwaa, amesema maboresho yanayopangwa - [Pedro awatia moyo wachezaji wake, awapongeza](https://spotileo.co.tz/pedro-awatia-moyo-wachezaji-wake-awapongeza/) - ZANZIBAR:KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves ameonesha kujivunia kikosi chake licha ya kupoteza kwa bao 1-0 dhidi ya Simba katika fainali ya Kombe la Muungano, akisisitiza kuwa timu ilipambana hadi mwisho wa mashindano hayo. Pedro amesema anajivunia namna wachezaji walivyoonesha kujitoa, umoja na morali ya hali ya juu katika michuano yote, akibainisha kuwa hayo ni - [Magori: Simba bado haijafikia kiwango tunachotaka](https://spotileo.co.tz/magori-simba-bado-haijafikia-kiwango-tunachotaka/) - ZANZIBAR:MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Crescentius Magori, amesema licha ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Kombe la Muungano, bado hajaona kiwango kinachoridhisha kulingana na malengo ya klabu hiyo. Akizungumzia ushindi huo, Magori amesema mchezo ulikuwa mgumu kwa kuwa ulidumu kwa dakika 120 za “jasho na damu”, hali iliyowachosha wachezaji kuelekea mechi nyingine muhimu - [Seleman Mwalimu ajivunia kuweka historia baada ya kuifunga Yanga](https://spotileo.co.tz/seleman-mwalimu-ajivunia-kuweka-historia-baada-ya-kuifunga-yanga/) - ZANZIBAR: KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Seleman Mwalimu, amesema anajivunia mafanikio aliyoyapata baada ya kufunga bao muhimu katika mchezo wa dabi, akisisitiza kuwa ameandika historia ambayo haitasahaulika kirahisi. Mwalimu alitoa kauli hiyo mara baada ya mchezo huo mgumu uliomalizika kwa ushindi wa bao 1-0 na Simba kuchukua ubingwa wa Muungano. Amesema kuwa licha ya furaha aliyonayo, - [CAF na UEFA zasaini makubaliano kuendeleza soka Afrika na Ulaya](https://spotileo.co.tz/caf-na-uefa-zasaini-makubaliano-kuendeleza-soka-afrika-na-ulaya/) - VANCOUVER:SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeingia makubaliano ya kihistoria na Union of European Football Associations (UEFA) yenye lengo la kuimarisha ushirikiano, kukuza vipaji na kuendeleza mchezo wa soka katika mabara ya Afrika na Ulaya. Makubaliano hayo (MoU) yalisainiwa jijini Vancouver, Canada, yakiongozwa na Rais wa CAF, Patrice Motsepe, pamoja na Rais wa UEFA, Aleksander Čeferin. - [Kiduku: Mafanikio ya Ibrahim Class yatupa Moyo](https://spotileo.co.tz/kiduku-mafanikio-ya-ibrahim-class-yatupa-moyo/) - DAR ES SALAAM: BONDIA Twaha Kassim 'Kiduku amesema wao kama mabondia wametoka Morogoro hadi Dar es Salaam kwa lengo la kumpongeza Ibrahim Class kufuatia mafanikio yake makubwa aliyoyapata nchini Thailand kwa kutwaa mikanda miwili ya WBC. Kiduku na Karim Mandonga ni miongoni mwa mabondia waliojitokeza Jana kumpokea Class aliyepata mapokezi ya kifalme baada ya kufanya - [Simba , Yanga ni kisasi au dozi Kombe la Muungano Zanzibar](https://spotileo.co.tz/simba-yanga-ni-kisasi-au-dozi-kombe-la-muungano-zanzibar/) - ZANZIBAR:MIAMBA ya soka Tanzania, Simba na Yanga leo zinatarajiwa kumenyana katika mchezo wa fainali ya Kombe la Muungano utakaopigwa saa 2:15 usiku kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, huku ikiwa ni lazima mshindi apatikane ili kubeba taji hilo, hali inayotabiri pambano la nguvu na presha kubwa kwa - [Bayern yaiwinda PSG kwa kisasi baada ya kipigo cha mabao tisa](https://spotileo.co.tz/bayern-yaiwinda-psg-kwa-kisasi-baada-ya-kipigo-cha-mabao-tisa/) - MUNICH:KLABU ya Bayern Munich imeweka wazi dhamira ya kulipa kisasi dhidi ya Paris Saint-Germain (PSG) katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya UEFA Champions League baada ya kupoteza kwa mabao 5-4 katika mchezo wa kwanza uliochezwa Ufaransa. Mchezo huo uliingia kwenye rekodi kwa kuwa na mabao mengi zaidi katika hatua ya nusu fainali, huku - [Griezmann kumaliza hadithi yake Atletico kwa kishindo?](https://spotileo.co.tz/griezmann-kumaliza-hadithi-yake-atletico-kwa-kishindo/) - MADRID, Hispania — WAKATI Atletico Madrid wakijiandaa kuvaana na Arsenal leo katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya UEFA Champions League, macho yote yameelekezwa kwa mshambuliaji Antoine Griezmann, ambaye anatarajiwa kuhitimisha safari yake na klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu. Katika tukio lisilo la kawaida, kocha wa Atletico, Diego Simeone, alitumia mkutano na waandishi - [Heavenly Voice Gospel Band waanika mipango yao](https://spotileo.co.tz/heavenly-voice-gospel-band-waanika-mipango-yao/) - BENDI inayokuja kwa kasi kwenye muziki wa Injili, Heavenly Voice Gospel Band yenye makazi yake nchini Marekani imeweka wazi mipango yake ya kuwahudumia mashabiki. Akizungumza na Spoti Leo Mwanzilishi na mwalimu wa bendi hiyo, Maisha Manase, amesema baada ya Mungu kumpa maono ya kuanzisha Heavenly Voice Gospel Band, ameanza mipango ya kuwafikia mashabiki wengi ulimwenguni - [Wasanii, viongozi waomboleza kifo Hashim Kambi](https://spotileo.co.tz/wasanii-viongozi-waomboleza-kifo-hashim-kambi/) - DAR ES SALAAM- MWILI wa msanii mkongwe wa tasnia ya uigizaji, Hashim Kambi, uliagwa jana katika Msikiti wa Maamur jijini Dar es Salaam kabla ya kuzikwa katika makaburi ya Kisutu, huku wasanii, viongozi na wadau wa sanaa wakijitokeza kutoa heshima zao za mwisho. Akizungumza wakati wa mazishi hayo, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es - [FIFA yakutana Vancouver, Kombe la Dunia 2026 lakumbwa na maswali mazito](https://spotileo.co.tz/fifa-yakutana-vancouver-kombe-la-dunia-2026-lakumbwa-na-maswali-mazito/) - VANCOUVER:SHIRIKISHO la Soka Duniani, FIFA, linatarajiwa kufanya mkutano wake mkuu jijini Vancouver huku maandalizi ya FIFA World Cup 2026 yakikumbwa na changamoto kadhaa zikiwemo gharama, usafiri na masuala ya kisiasa. Mkutano huo unafanyika ikiwa zimebaki chini ya miezi miwili kabla ya kuanza kwa mashindano hayo makubwa zaidi kuwahi kufanyika, yatakayoshirikisha timu 48 kwa mara ya - [Man United yarudi mlangoni mwa Ligi ya Mabingwa, maamuzi mazito yaja](https://spotileo.co.tz/man-united-yarudi-mlangoni-mwa-ligi-ya-mabingwa-maamuzi-mazito-yaja/) - LONDON:KLABU ya Manchester United ipo hatua moja tu kurejea kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Brentford, lakini pamoja na mafanikio hayo, uongozi unakabiliwa na maamuzi magumu kuelekea msimu ujao. Kiungo mkongwe Carlos Casemiro, mwenye umri wa miaka 34, aliendelea kuwa mhimili wa timu hiyo baada - [Maema: Uvumilivu na nidhamu vimetupa ushindi](https://spotileo.co.tz/maema-uvumilivu-na-nidhamu-vimetupa-ushindi/) - ZANZIBAR: KIUNGO mshambuliaji wa Simba Neo Maema ameweka wazi sababu za ushindi wa mabao 3-0 walioupata dhidi ya Mlandege FC katika mchezo wa nusu fainali michuano ya Muungano, akisema mchezo huo ulikuwa mgumu hasa dakika za mwanzo lakini uvumilivu na nidhamu viliwabeba. Akizungumza baada ya mchezo huo, Maema amesema Mlandege waliingia na mpango maalum wa - [Raphinha mbioni kurejea mazoezini wiki hii](https://spotileo.co.tz/raphinha-mbioni-kurejea-mazoezini-wiki-hii/) - BARCELONA, Hispania: KLABU ya Barcelona imepata ahueni kubwa baada ya kurejea kwa wachezaji wawili muhimu wakati ikikaribia kutwaa ubingwa wa La Liga msimu huu. Taarifa zinaeleza kuwa nyota Raphael Belloli 'Raphinha' pamoja na kiungo chipukizi Marc Bernal wanatarajiwa kurejea mazoezini wiki hii, jambo linaloongeza nguvu kikosini mwa kocha Hansi Flick kuelekea mechi muhimu dhidi ya - ['Uzuri pekee hauwezi kumsaidia mwanamke'](https://spotileo.co.tz/uzuri-pekee-hauwezi-kumsaidia-mwanamke/) - DAR ES SALAAM: MWANAMITINDO Jasinta Makwabe ametoa rai kwa mabinti kutojitegemea kwenye uzuri wao pekee, akisisitiza umuhimu wa kuwa na akili na uwezo binafsi. Amesema kuwa uzuri bila maarifa na juhudi hauwezi kumsaidia mtu kujitegemea maishani. Jasinta amesema kuwa binti anayejikita kwenye uzuri tu bila kuwekeza kwenye maendeleo ya kiakili na kiuchumi anajiweka katika hatari - [Cole aipa silaha Chelsea kuiua Man City](https://spotileo.co.tz/20302-2/) - LONDON, England: KIUNGO wa zamani wa Chelsea, Joe Cole, amesema hofu ya kukutana na Manchester City inaweza kuisaidia timu hiyo kutoa kiwango bora katika fainali ya FA Cup mwezi ujao. Chelsea imefanikiwa kutinga fainali baada ya kuifunga Leeds United kwa bao 1-0 kwenye dimba la Wembley Stadium, bao lililofungwa na Enzo Fernández katika kipindi cha - [Cheka kurejea ulingoni Juni](https://spotileo.co.tz/cheka-kurejea-ulingoni-juni/) - DAR ES SALAAM: BONDIA Cosmas Cheka ametangaza kurejea tena ulingoni, akisema amerudi kwa dhamira ya kuwafundisha watu namna bora ya kucheza mchezo wa ngumi. Akizungumza kwa kujiamini na SpotiLeo Cheka amesema kurejea kwake si tu kwa ajili ya mashindano, bali pia kushirikisha uzoefu wake kwa chipukizi wanaotaka kufanikiwa katika mchezo huo. “Nimerudi tena, nimekuja kuwafundisha - [Chuji avutiwa kiwango Cha Abuya](https://spotileo.co.tz/chuji-avutiwa-kiwango-cha-abuya/) - DAR ES SALAAM: MCHEZAJI wa zamani wa Simba na Yanga , Athuman Idd ‘Chuji’, amempongeza kiungo wa Yanga Duke Abuya, kufuatia kiwango bora alichoonesha msimu huu. Kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa kijamii, Chuji ameandika maneno mafupi lakini yenye uzito mkubwa akisema: “Nakupa heshima ya juu 2024/2025”, akionesha kuvutiwa na mchango wa Abuya katika michuano - [Real Madrid yaweka dau nono kwa Gonzalo](https://spotileo.co.tz/real-madrid-yaweka-dau-nono-kwa-gonzalo/) - MADRID, Hispania: MABINGWA wa Hispania, Real Madrid, wameweka wazi kuwa hawako tayari kumuuza mshambuliaji wao chipukizi Gonzalo Garcia kwa bei yoyote chini ya euro milioni 60 katika dirisha lijalo la usajili wa majira ya kiangazi. Gonzalo (22) amekuwa na msimu wa kipekee licha ya kupata muda mchache wa kuanza kikosi cha kwanza, akishindwa kupenya mbele ya - [Lingard aandika historia Brazil](https://spotileo.co.tz/lingard-aandika-historia-brazil/) - BRASILIA, Brazil: KIUNGO mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Jesse Lingard, ameendelea kuandika historia baada ya kuwa Muingereza wa kwanza kucheza katika ligi kuu ya Brazil akikitumikia klabu ya Corinthians. Lingard (33) ambaye alijiunga na Corinthians akitokea FC Seoul, amesema anafurahia changamoto mpya huku akilenga kushinda mataji akiwa Brazil. Tayari amefunga bao lake la kwanza - [Simons nje msimu mzima, kukosa pia Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/simons-nje-msimu-mzima-kukosa-pia-kombe-la-dunia/) - LONDON, England: KIUNGO mshambuliaji wa kimataifa wa Uholanzi, Xavi Simons, ataukosa msimu uliosalia pamoja na michuano ya Kombe la Dunia 2026 kufuatia kuumia vibaya goti akiwa na klabu ya Tottenham Hotspur. Simons, mwenye umri wa miaka 23, alipata jeraha hilo la kano ya mbele ya goti (ACL) wakati wa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya - [Shime ataja kikosi cha kuiua Cameroon](https://spotileo.co.tz/shime-ataja-kikosi-cha-kuiua-cameroon/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya wanawake chini ya miaka 20 (Tanzanite Queens), Bakari Shime, ametaja kikosi cha wachezaji 27 kitakachoingia kambini kujiandaa na michezo miwili ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Cameroon. Akizungumza leo wakati wa kutangaza kikosi hicho, Shime amesema wachezaji aliowachagua wanafahamu uzito wa jukumu lililopo - [Simba, Mafunzo kuchuana Muungano leo Zanzibar](https://spotileo.co.tz/simba-mafunzo-kuchuana-muungano-leo-zanzibar/) - ZANZIBAR: WEKUNDU wa Msimbazi Simba na Mafunzo wanatarajiwa kushuka dimbani leo kuwania ushindi katika michuano ya Kombe la Muungano, utakaopigwa kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Mchezo huo ambao tayari umevuta hisia za mashabiki wengi wa soka, unatarajiwa kuanza saa 2:15 usiku. Wakizungumzia mchezo huo makocha wa timu hizo wamesema amejiandaa kikamilifu kwa ajili - [Serikali yasistiza wajibu wa kisheria kulipa mirabaha](https://spotileo.co.tz/serikali-yasistiza-wajibu-wa-kisheria-kulipa-mirabaha/) - DAR ES SALAAM: SERIKALI imesisitiza kuwa ulipaji wa mirabaha kwa matumizi ya kazi za ubunifu, ikiwemo muziki, si hiari bali ni wajibu wa kisheria, na imewataka watumiaji wote wa kazi hizo nchini kuzingatia sheria kikamilifu. Kauli hiyo imetolewa leo Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Sanaa katika Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, - [Simba yaingia Zanzibar kibabe](https://spotileo.co.tz/simba-yaingia-kibabe-zanzibar/) - ZANZIBAR: KIKOSI cha Simba kimewaili visiwani Zanzibar tayari kwa michuano ya Kombe la Muungano huku wakiahidi kuendelea kutoa burudani katika mchezo dhidi ya Mafunzo FC utakaochezwa kesho. Kwa mujibu wa Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, wamejipanga kuendelea kuhamishia burudani kwa mashabiki wao wa Zanzibar na kuhakikisha wanafanya vizuri katika hatua zote. Amesema michuano hiyo - [Singida kuivaa Mlendege kwa tahadhari](https://spotileo.co.tz/singida-kuivaa-mlendege-kwa-tahadhari/) - ZANZIBAR: KOCHA Mkuu wa Singida Black Stars, Muhibu Kanu, amesema kikosi chake kipo tayari kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Muungano dhidi ya Mlandege kesho, akisisitiza kuwa maandalizi yamekamilika kwa lengo la kufanya vizuri kwenye mashindano hayo. Akizungumza kuelekea mchezo huo, Kanu amesema licha ya kuutambua ugumu wa mechi hiyo, wamejipanga ipasavyo kuhakikisha wanapata - [Tanzania yaingia kwenye historia ya kuandaa Miss World Afrika](https://spotileo.co.tz/tanzania-yaingia-kwenye-historia-ya-kuandaa-miss-world-afrika/) - DAR ES SALAAM: TANZANIA imeandika historia mpya katika tasnia ya urembo duniani baada ya kuwa nchi ya pili Barani Afrika kuandaa mashindano ya 74 ya "Miss World' na kuwa ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ikitanguliwa na Afrika Kusini ambayo iliandaa mashindano hayo kwa mara ya mwisho mwaka 2009. Kauli hiyo imetolewa - [Mbio za Absa Dar City kumahisha mshikamano na afya njema](https://spotileo.co.tz/mbio-za-absa-dar-city-kumahisha-mshikamano-na-afya-njema/) - DAR ES SALAAM: The Runners Club kwa kushirikiana na benki ya Absa imezindua rasmi mbio za Absa Dar City Marathon 2026 zinazotarajiwa kufanyika Mei 17, 2026 Dar es Salaam. Hilo ni toleo la sita la mbio hizo, zikitarajiwa kuvutia zaidi ya washiriki 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi, huku zikilenga kuhamasisha mazoezi, mshikamano wa - [Odemba aja na ‘Sauti ya Mitindo’,](https://spotileo.co.tz/odemba-aja-na-sauti-ya-mitindo/) - DAR ES SALAAM: Mwanamitindo wa kimataifa, Miriam Odemba ametangaza kuanzisha jukwaa jipya la mitindo lijulikanalo kama Sauti ya Mitindo, litakalolenga kukuza vipaji vya wanamitindo wa kiume na wa kike nchini. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Odemba amesema jukwaa hilo ni sehemu ya kurejesha mchango wake katika tasnia ya urembo baada ya kunufaika na fursa mbalimbali - [Usain Bolt amuonya Gout](https://spotileo.co.tz/usain-bolt-amuonya-gout/) - ATLANTA, Marekani: MKONGWE wa mbio fupi duniani, Usain Bolt, amempa ushauri maalum nyota chipukizi wa Australia, Gout Gout, akimtaka asisahau mchezo wa riadha huku akisisitiza umuhimu wa kuwa na watu sahihi wa kumsaidia katika safari yake ya kimichezo. Bolt ametoa ushauri huo wakati mafanikio ya Gout yakiendelea kuvutia dunia, baada ya kutetea taji la mita - [Bosi West Ham aachia ngazi](https://spotileo.co.tz/bosi-west-ham-aachia-ngazi/) - LONDON, England: MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya West Ham United, Karren Brady, amejiuzulu rasmi nafasi yake baada ya kuhudumu kwa kipindi cha miaka 16, hatua iliyotangazwa Jumanne na klabu hiyo ya Ligi Kuu England. Brady ameondoka katika kipindi ambacho West Ham inapitia changamoto za matokeo uwanjani, ikiwa kwenye vita ya kushuka daraja, huku ikishika nafasi - [Yanga Muembe Makumbi City hapatoshi](https://spotileo.co.tz/yanga-kuvaana-na-muembe-makumbi-city/) - ZANZIBAR: MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga, wanatarajia kushuka dimbani leo saa 1:00 usiku kuikabili timu ya Muembe Makumbi City FC katika mchezo wa Kombe la Muungano utakaochezwa visiwani Zanzibar. Muembe Makumbi City, inayoshiriki Ligi Kuu ya Zanzibar, kwa sasa inashika nafasi ya nane kwenye msimamo ikiwa na pointi 33 baada ya michezo - [Babuu: Mkunga Marathon kuokoa maisha ya mama na mtoto](https://spotileo.co.tz/babuu-mkunga-marathon-kuokoa-maisha-ya-mama-na-mtoto/) - DAR ES SALAAM: MBIO za Mkunga Marathon zinatarajiwa kufanyika Mei 2 mkoani Kilimanjaro zikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani, huku zikilenga kukusanya fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za uzazi nchini. Akizungumzia katika tukio hilo, Cedou Mandingo maarufu kama ‘Babu wa Kitaa’ ameishukuru Chama cha Wakunga Tanzania (TAMA) kwa kumteua kuwa - [SuperSport kurusha mechi zote 104 za Kombe la Dunia 2026 mubashara](https://spotileo.co.tz/supersport-kurusha-mechi-zote-104-za-kombe-la-dunia-2026-mubashara/) - DAR ES SALAAM: KAMPUNI ya matangazo ya michezo ya SuperSport chini ya DStv, kampuni tanzu ya MultiChoice Group na kampuni ya CANAL+ imetangaza rasmi kuwa itarusha mubashara mechi zote 104 za FIFA World Cup 2026, tukio linalotarajiwa kuweka historia mpya katika soka la dunia. Taarifa hiyo iliyotolewa Aprili 17, 2026, inaeleza kuwa mashindano hayo yatakayofanyika - [Pedro: Tuko tayari kuivaa Mbeya City](https://spotileo.co.tz/pedro-tuko-tayari-kuivaa-mbeya-city/) - DAR ES SALAAM: KOCHA mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema kikosi chake kiko imara na tayari kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mbeya City, huku akisisitiza kuwa lengo kuu ni kuondoka na alama tatu kesho. Akizungumzia mchezo huo Dar es Salaam leo Pedro amesema mchezo wa mwisho ugenini ulikuwa mgumu kutokana na - [Mbeya City siyo kinyonge dhidi ya Yanga](https://spotileo.co.tz/mbeya-city-siyo-kinyonge-dhidi-ya-yanga/) - DAR ES SALAAM: WAKATI presha ikizidi kuelekea mchezo wao dhidi ya Yanga utakaopigwa kesho kwenye Uwanja wa KMC, mabosi na wachezaji wa Mbeya City wameweka wazi dhamira yao ya kusaka ushindi bila kuyumba. Ofisa Habari wa Mbeya City, Gwamaka Mwankota, amesema kelele zinazoendelea nje ya uwanja haziwatishi, badala yake zimewapa ari zaidi ya kupambana. “Tumekuwa - [Simeone awapa tano wachezaji wake](https://spotileo.co.tz/simeone-awapa-tano-wachezaji-wake/) - MADRID, Hispania: KOCHA wa Atletico Madrid, Diego Simeone, ameisifu timu yake kwa kuonesha moyo wa kupambana na kufanikiwa kulinda matokeo muhimu yaliyoipeleka klabu hiyo hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Simeone Amesema wachezaji wake walionesha nidhamu na kujituma mbele ya mashabiki wao, jambo lililochangia mafanikio hayo makubwa ambapo Atletico sasa wanasubiri kumenyana - [Simba, Fountain Gate vitani leo](https://spotileo.co.tz/simba-fountain-gate-vitani-leo/) - ARUSHA. TIMU ya Simba SC leo inatarajiwa kushuka dimbani kuvaana na Fountain Gate FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaopigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Simba inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na morali nzuri baada ya kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho la CRDB. Kocha Mkuu wa - [Masaki: Amani inachochea mafanikio sekta ya mitindo](https://spotileo.co.tz/masaki-amani-inachochea-mafanikio-sekta-ya-mitindo/) - MBUNIFU wa mavazi kutoka AMFashion, Agusta Masaki, amesema amani iliyopo nchini Tanzania ni nguzo muhimu inayowezesha wabunifu na wafanyabiashara kufanya kazi zao kwa utulivu na ubunifu mkubwa. Akizungumza na SpotiLEO kuhusu mtazamo wake, Masaki ameeleza kuwa tofauti na baadhi ya nchi nyingine, Tanzania inatoa mazingira rafiki yanayoruhusu watu kufikiria, kuunda na kukuza vipaji vyao bila - [Raphina awalalamikia waamuzi](https://spotileo.co.tz/raphina-awalalamikia-waamuzi/) - MADRID, Hispania: WINGA wa Barcelona, Raphael Dias ‘Raphinha’, amewashambulia waamuzi kufuatia timu yake kuondolewa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Atletico Madrid. Barcelona ilitolewa kwa jumla ya mabao 3-2 licha ya kushinda 2-1 katika mchezo wa marudiano uliochezwa Jumanne, huku wakimaliza michezo yote miwili wakiwa na wachezaji 10 uwanjani. Raphinha, ambaye hakushiriki michezo - [Slot ahofia majeraha ya Ekitike](https://spotileo.co.tz/slot-ahofia-majeraha-ya-ekitike/) - LONDON, England: Kocha wa Liverpool FC, Arne Slot, amesema ana hofu kubwa kuhusu hali ya mshambuliaji Hugo Ekitike kufuatia kupata jeraha baya katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Paris Saint-Germain. Ekitike alitolewa nje kwa machela dakika ya 30 ya mchezo wa robo fainali mkondo wa pili baada ya kuanguka bila kuguswa na - [Miss Tanzania yakabidhiwa Lamata Village](https://spotileo.co.tz/miss-tanzania-yakabidhiwa-lamata-village/) - DAR ES SALAAM. MASHINDANO ya urembo ya Miss Tanzania yameingia katika sura mpya baada ya jukumu la kuyaendesha kukabidhiwa rasmi kwa taasisi ya Lamata Village, hatua inayotarajiwa kurejesha hadhi na mvuto wa shindano hilo lenye historia kubwa nchini. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo Leo Aprili 14, mwaka huu, Mkurugenzi wa Kampuni ya The Look, - [Lufingo: Amani ni tunda la haki](https://spotileo.co.tz/lufingo-amani-ni-tunda-la-haki/) - MSANII wa filamu, Daniel Lufingo, amesema kuwa uwepo wa amani katika jamii ni jambo muhimu kwa wasanii, kwani kazi zao hutegemea mazingira tulivu pamoja na ushirikiano mzuri kati ya jamii na serikali. Akizungumza na Spoti Leo, Lufingo maarufu kama “Adam” kutoka tamthilia ya Noma, amesisitiza kuwa amani ya kweli hujengwa juu ya msingi wa haki, - [Balozi Kibesse awataka wasanii kutangaza Kiswahili kimataifa kupitia sanaa](https://spotileo.co.tz/balozi-kibesse-awataka-wasanii-kutangaza-kiswahili-kimataifa-kupitia-sanaa/) - NAIROBI, Kenya: Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk Bernard Kibesse, amewataka wasanii wa Tanzania kuendelea kutumia sanaa zao kutangaza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi. Dk Kibesse ametoa kauli hiyo jijini Nairobi baada ya kukutana na wasanii waliotembelea ubalozi wa Tanzania nchini humo, mara baada ya kushiriki Kongamano la The East African Art - [Steve Nyerere: Acheni siasa zisizo na tija](https://spotileo.co.tz/steve-nyerere-acheni-siasa-zisizo-na-tija/) - DAR ES SALAAM. MCHEKESHAJI mkongwe na Mwenyekiti wa taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steve Nyerere, amewataka Watanzania hususanI vijana kuacha kujikita kupita kiasi kwenye siasa zisizoleta matokeo, badala yake kuelekeza nguvu kwenye shughuli za maendeleo. Akizungumzia mwenendo wa jamii kwa sasa, Nyerere amesema kumekuwa na hali ya watu wengi kupoteza mwelekeo wa kufanya kazi - [BASATA kuchochea uchumi wa ubunifu kupitia mashindano ya uchoraji](https://spotileo.co.tz/basata-kuchochea-uchumi-wa-ubunifu-kupitia-mashindano-ya-uchoraji/) - DAR ES SALAAM: KAIMU Katibu wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Edward Buganga, amesema mashindano ya uchoraji yanayoshirikisha wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali nchini ni mkakati muhimu wa kukuza, kuinua na kuendeleza vipaji vya sanaa sambamba na kuchangia uchumi wa ubunifu nchini. Akizungumza na Spoti Leo Buganga ameeleza kuwa BASATA itaendelea kuandaa mashindano hayo ili - [Diarra kukiwasha dhidi ya Mbeya City](https://spotileo.co.tz/diarra-kukiwasha-dhidi-ya-mbeya-city/) - DAR ES SALAAM: KIPA namba moja wa Yanga, Djigui Diarra atarajiwa kuonekana tena uwanjani baada ya kumaliza adhabu yake ya kufungimiwa michezo mitatu. Nyota huyo huenda akarejea uwanjani katika mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Mbeya City utakaochezwa Alhamis kwenye Uwanja wa KMC. Diarra alitumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu ambayo ni dhidi ya - [Wasanii Afrika Mashariki  kuungana kuimarisha sanaa](https://spotileo.co.tz/wasanii-afrika-mashariki-kuungana-kuimarisha-sanaa/) - KENYA: Wasanii wa fani mbalimbali za sanaa katika Ukanda wa Afrika Mashariki wametakiwa kuungana na kuwa na sauti moja ili kuleta mabadiliko chanya na kukuza sekta ya sanaa katika kanda hiyo. Akizungumza wakati wa kuwasilisha mada katika kongamano la The East African Art Nexus (TEANEX) lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Nairobi, Rais wa Shirikisho la - [Sanaa za uoni zaiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia](https://spotileo.co.tz/sanaa-za-uoni-zaiweka-tanzania-kwenye-ramani-ya-dunia/) - KENYA: Sanaa za uoni/ufundi ni miongoni mwa sekta chache nchini Tanzania na duniani zinazochangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya urithi wa sanaa ya kipekee unaoitangaza nchi kimataifa. Akizungumza na Spoti Leo baada ya kuwasilisha mada katika kongamano la The East African Art Nexus (TEANEX) lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Nairobi, Msanii Safina Kimbokota amesema kuwa - [Simba yatamba kuichapa Dodoma Jiji](https://spotileo.co.tz/simba-yatamba-kuichapa-dodoma-jiji/) - ARUSHA: KLABU ya soka ya Simba kupitia kwa Meneja wa Habari na Mawasiliono wa timu hiyo, Ahmed Ally amesema Dodoma Jiji sio timu daraja la Simba baada ya ushindi waliopata wa mabao 3-1 katika mchezo wa Kombe la Shirikisho la CRDB. Simba ni miongoni mwa timu zilizofuzu hatua ya nane bora baada ya kushinda katika - [Simba yatamba baada ya kufuzu robo fainali](https://spotileo.co.tz/simba-yatamba-baada-ya-kufuzu-robo-fainali/) - Grace Mkojera ARUSHA: KLABU ya soka ya Simba kupitia kwa Meneja wa Habari na Mawasiliono wa timu hiyo, Ahmed Ally amesema Dodoma Jiji sio timu daraja la Simba baada ya ushindi waliopata wa mabao 3-1 katika mchezo wa Kombe la Shirikisho la CRDB. Simba ni miongoni mwa timu zilizofuzu hatua ya nane bora baada ya - [Samatta gari limewaka Ligue 1](https://spotileo.co.tz/samatta-gari-limewaka-ligue-1/) - PARIS, Ufaransa: MSHAMBULIAJI wa Tanzania, Mbwana Samatta amefunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) akiwa na timu yake ya Le Havre. Mchezaji huyo wa zamani wa Genk ya Ubelgiji ameandika historia nyingine ya kuwa Mtanzania wa kwanza ambaye amefanikiwa kufunga goli katika ligi kuu kubwa mbili barani Ulaya ambapo alifunga - [Mpira wa Wavu wapata msukumo kukuza vipaji](https://spotileo.co.tz/mpira-wa-wavu-wapata-msukumo-kukuza-vipaji/) - DAR ES SALAAM: MPIRA wa wavu nchini umepata msukumo mpya wa kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana baada ya kampuni ya mawasiliano ya Yas kuingia ushirikiano na Chama cha Mpira wa Wavu nchini. Ushirikiano huo unalenga kuinua kiwango cha mchezo huo kupitia udhamini unaolenga kutoa motisha kwa wachezaji pamoja na waamuzi, sambamba na kuhamasisha ushiriki - [Taliss IST yatwaa Ubingwa wa Kuogelea Taifa](https://spotileo.co.tz/taliss-ist-yatwaa-ubingwa-wa-kuogelea-taifa/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Taliss IST imeibuka bingwa wa Mashindano ya 18 ya Kuogelea ngazi ya Klabu baada ya kujikusanyia pointi nyingi zaidi katika michuano hiyo iliyohitimishwa jana katika Bwawa la Kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika. Katika matokeo ya jumla, Taliss IST ilitwaa ubingwa kwa kujikusanyia alama 448.5, ikifuatiwa na Dar Swim - [Msigwa: Afcon ni jukumu letu sote Watanzania](https://spotileo.co.tz/msigwa-afcon-ni-jukumu-letu-sote-watanzania/) - DAR ES SALAAM: SERIKALI imewataka Watanzania kuchukua umiliki wa pamoja wa mashindano ya Africa Cup of Nations 2027 (AFCON 2027), ikisisitiza kuwa mashindano hayo ni fursa ya kitaifa ambayo manufaa yake hayatabaki serikalini pekee, bali yataenea kwa wananchi na sekta mbalimbali nchini. Akizungumza wakati wa kikao cha wadau kujadili maandalizi ya fainali hizo zitakazofanyika mwaka - [Mwasyoge: Michezo ni nguzo ya kuimarisha amani](https://spotileo.co.tz/mwasyoge-michezo-ni-nguzo-ya-kuimarisha-amani/) - DAR ES SALAAM: MWENYEKITI wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA), David Mwasyoge, amesema michezo ina nafasi kubwa katika kuimarisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania. Mwasyoge ameyasema hayo wakati akizungumza na Dailynews Digital kuhusu nafasi ya michezo katika amani ambapo amesema kuwa michezo hujenga mshikamano wa kijamii bila kujali tofauti za kidini, kisiasa au - [Robertson kuondoka Anfield mwishoni mwa msimu](https://spotileo.co.tz/robertson-kuondoka-anfield-mwishoni-mwa-msimu/) - LIVERPOOL:KLABU ya Liverpool imethibitisha kuwa beki wao wa kushoto na nahodha wa Scotland, Andy Robertson, ataondoka mwishoni mwa msimu huu baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka tisa yenye mafanikio makubwa sana. Robertson alijiunga na Liverpool akitokea Hull City mwaka 2017, na tangu hapo amekuwa sehemu muhimu ya moja ya vipindi bora zaidi kwenye historia - [Mwagala ajivunia “TRA Effect”](https://spotileo.co.tz/mwagala-ajivunia-tra-effect/) - ARUSHA: MSEMAJI wa TRA, Christina Mwagala, amesema hakuna timu yenye uwezo wa kuifunga TRA wanapocheza nyumbani Arusha kufuatia sare tasa waliyoipata dhidi ya Simba katika mchezo wa Ligi Kuu uliopigwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jana. Mwagala amesema matokeo hayo yanaonesha uimara wa kikosi chao, akisisitiza kuwa walijiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huo licha - [Azam FC haifungiki kiurahisi](https://spotileo.co.tz/azam-fc-haifungiki-kiurahisi/) - MANYARA: TIMU ya Azam FC imeendelea kuonesha sura mbili tofauti ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya Mbeya City katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara jana. Matokeo hayo yanaifanya Azam kufikisha jumla ya sare 10 katika michezo 18 ya ligi msimu huu, ikiwa ndiyo - [Simba hakuna kukata tamaa!](https://spotileo.co.tz/simba-hakuna-kukata-tamaa/) - ARUSHA: MENEJA Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally, amesema sare ya bila kufungana dhidi ya TRA haijaathiri malengo ya timu hiyo katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu. Akizungumza baada ya mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Ahmed amekiri kuwa matokeo hayo hayakuwa ya kuridhisha lakini hayajapunguza ari - [JKT yawahofia Mbuni, yajipanga](https://spotileo.co.tz/jkt-yawahofia-mbuni-yajipanga/) - DAR ES SALAAM: KOCHA wa JKT Tanzania, Ahmed Ally, amesema kikosi chake kimejipanga vizuri kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Mbuni FC, huku akisisitiza kuwa hawataidharau timu hiyo licha ya kucheza ligi ya chini. JKT Tanzania itavaana na Mbuni FC hatua ya 16 bora kesho katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, huku - [Presha yahamia Yanga Princess baada ya kuporomoka](https://spotileo.co.tz/presha-yahamia-yanga-princess-baada-ya-kuporomoka/) - DAR ES SALAAM: MBIO za ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara zimechukua sura mpya baada ya Yanga Princess kuanza kudondosha alama muhimu, kufuatia kuchapwa mabao 2-0 na Tausi katika mchezo wa mzunguko wa 13 uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Azam Complex. Kupoteza huko kumeifanya Yanga Princess kuendelea kubaki nyuma ya vinara Simba Queens, - [Jarjou: Nitafunga mabao mengi](https://spotileo.co.tz/jarjou-nitafunga-mabao-mengi/) - SINGIDA: BAADA ya kuibuka shujaa wa Singida Black Stars kwa bao lililoizamisha KMC kwa ushindi wa bao 1-0, mchezaji Lamin Jarjou ametuma salamu nzito kwa wapinzani wake akiahidi kuwa bado hajamaliza kazi na kwamba ataendelea kufunga mabao mengi zaidi. Jarjou alikuwa nyota wa mchezo huo uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Airtel, Singida, baada ya kufunga - [Pedro: Tulibadili mfumo kutokana na mazingira ya mchezo](https://spotileo.co.tz/pedro-tulibadili-mfumo-kutokana-na-mazingira-ya-mchezo/) - MWANZA: KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Gonçalves, amesema walilazimika kubadili mfumo wa uchezaji katika mechi yao dhidi ya Pamba kutokana na tofauti ya mazingira ya mchezo, aina ya uwanja pamoja na hali ya mpinzani. Akizungumza jijini Mwanza baada ya mchezo dhidi ya Pamba walioshinda mabao 3-0 Pedro amesema timu yake inaendelea kujengwa hatua kwa hatua, - [Barker, Imoro wang'ara Machi](https://spotileo.co.tz/barker-imoro-wangara-machi/) - DAR ES SALAAM: KOCHA wa Simba Steven Barker, amechaguliwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Machi wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2025/26 baada ya kuiongoza timu yake kupata matokeo mazuri. Barker aliiwezesha Simba kushinda michezo miwili na kutoka sare miwili, matokeo yaliyoifanya timu hiyo kupanda kutoka nafasi ya tatu hadi ya nafasi ya pili - [Kompany: Tuna kila sababu ya kujiamini](https://spotileo.co.tz/kompany-tuna-kila-sababu-ya-kujiamini/) - MADRID, Hispania: KOCHA wa Bayern Munich, Vincent Kompany, amesema kikosi chake kina kila sababu ya kuwa na imani kubwa baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 ugenini dhidi ya Real Madrid katika mchezo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League. Kompany amesema jambo muhimu kwa sasa si kulewa ushindi huo, bali ni - [JKT wanawake mambo safi DAREVA](https://spotileo.co.tz/jkt-wanawake-mambo-safi-dareva/) - DAR ES SALAAM: LIGI ya Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam (DAREVA) imeendelea kushika kasi huku ushindani ukizidi kupamba moto, katika michezo inayoendelea kupigwa kwenye Uwanja wa KIUT, jijini Dar es Salaam. Katika michezo ya jana, timu ya JKT imeendelea kuonesha ubora wake baada ya kuibuka na ushindi wa seti 3-0 dhidi ya - [Arbeloa amjia juu mwamuzi](https://spotileo.co.tz/arbeloa-amjia-juu-mwamuzi/) - MADRID, Hispania KOCHA wa Real Madrid, Álvaro Arbeloa, ameonesha kutoridhishwa na maamuzi ya mwamuzi baada ya kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya FC Bayern Munich kwenye robo fainali ya Ligi ya Mabingwa. Arbeloa amesema beki wa Bayern, Jonathan Tah, alipaswa kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya rafu aliyomfanyia Kylian Mbappé. “Sielewi kwa nini mchezaji - [KMC: Tutafufukia kwa Singida BS](https://spotileo.co.tz/kmc-tutafufukia-kwa-singida-bs/) - SINGIDA: IKIWA imetoka kupoteza michezo minne mfululizo, Klabu ya KMC FC imesema ipo tayari kupambana na kuhakikisha inapata matokeo mazuri katika mchezo unaokuja dhidi ya Singida katika Ligi Kuu ya Tanzania kesho. Ofisa Habari wa KMC, Khalid Chukuchuku, amesema:“Tunataka kufufukia kwa Singida, kupambana kuhakikisha tunapata matokeo mazuri na inawezekana," "Huu ni mchezo mgumu ambao kila - [Barker: Simba ni ngumu kufungwa](https://spotileo.co.tz/barker-simba-ni-ngumu-kufungwa/) - ARUSHA: KOCHA Mkuu wa Simba, Steven Barker amesema kikosi chake kinapaswa kuendelea kuwa imara kwa dakika zote 90 za mchezo ili kuepuka kuruhusu mabao ya kizembe, kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya TRA utakaochezwa kesho mkoani Arusha. Akizngumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo, Barker amesema moja ya maeneo muhimu ambayo - [Curry ainusuru Warriors](https://spotileo.co.tz/curry-ainusuru-warriors/) - SAN FRANCISCO, Marekani: Nyota Stephen Curry ameiwezesha timu yake ya Golden State Warriors katika dakika za mwisho baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa pointi 110-105 dhidi ya Sacramento Kings katika mchezo wa Ligi ya Kikapu Marekani (NBA) uliochezwa usiku wa kuamkia leo jijini San Francisco. Curry, aliyemaliza mchezo akiwa na pointi 17, aliibuka - [Arsenal yainufaisha Ligi Kuu ya England](https://spotileo.co.tz/arsenal-yainufaisha-ligi-kuu-ya-england/) - LONDON, Ligi Kuu England (EPL) imehakikishiwa kuwa na timu tano zitakazoshiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao, baada ya kupata rasmi nafasi ya ziada ya Ulaya maarufu kama European Performance Spot (EPS) kwa mwaka wa pili mfululizo. Nafasi hiyo ilipatikana jana usiku baada ya Arsenal kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Sporting katika - [Serengeti Girls wanalitaka Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/serengeti-girls-wanalitaka-kombe-la-dunia/) - MONASTIR: TIMU ya soka ya Taifa ya Wanawake chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Girls), imemaliza kambi yake ya mazoezi mjini Monastir kwa sare ya bila kufungana dhidi ya wenyeji wao Tunisia kwenye Uwanja wa MustaphaBen Jannet Monastir leo. Mechi hiyo ilikuwa ya pili kwa Serengeti Girls dhidi ya Tunisia, ya kwanza ilichezwa Machi - [Simba yaapa kulipa kisasi kwa Coastal Union](https://spotileo.co.tz/simba-yaapa-kulipa-kisasi-kwa-coastal-union/) - DAR ES SALAAM: Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema mchezo wa kesho dhidi ya Coastal Union ni miongoni mwa mechi ngumu kutokana na kumbukumbu ya msimu uliopita ambapo wapinzani hao walichangia kuinyima Simba nafasi ya kutimiza malengo yake ya ubingwa. Ahmed amesema sare ya mabao 2-2 waliyolazimishwa na Coastal Union katika - [Depu, Boka, Bacca warejea](https://spotileo.co.tz/depu-boka-bacca-warejea/) - DAR ES SALAAM: KIKOSI cha Yanga kimepata ahueni baada ya baadhi ya wachezaji waliokuwa nje kutokana na majeraha kurejea mazoezini, hatua inayoongeza nguvu kuelekea michezo ijayo ya mashindano mbalimbali. Wachezaji waliorejea rasmi mazoezini ni Laurindo Aurelio ‘Depu’, Ibrahim Bacca na Chadrack Boka, ambao kwa nyakati tofauti walikuwa nje ya uwanja wakikabiliwa na changamoto za kiafya. - [DR Congo yarejea Kombe la Dunia baada ya miaka 52](https://spotileo.co.tz/dr-congo-yarejea-kombe-la-dunia-baada-ya-miaka-52/) - GUADALAJARA, Mexico: JAMHURI ya Kidemokrasia ya Congo (DR Congo) imefuzu kucheza Kombe la Dunia 2026 kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1974, baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Jamaica katika mchezo wa mchujo wa mabara uliochezwa Jumanne usiku. Bao pekee la ushindi lilifungwa na Axel Tuanzebe katika dakika ya 100 ya - [Italia yapigwa tena, yashindwa kufuzu Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/italia-yapigwa-tena-yashindwa-kufuzu-kombe-la-dunia/) - ZENICA, Bosnia na Herzegovina: Italia imeendelea kuandamwa na jinamizi la kutofuzu Kombe la Dunia baada ya usiku wa kuamkia leo kuchapwa kwa penalti 4-1 na Bosnia na Herzegovina kufuatia sare ya 1-1 katika mchezo wa mchujo wa kufuzu fainali hizo. Matokeo hayo yanaifanya Italia, mabingwa mara nne wa dunia, kukosa nafasi ya kucheza Kombe la - [Woods ajiondoa gofu kutafuta matibabu](https://spotileo.co.tz/woods-ajiondoa-gofu-kutafuta-matibabu/) - FLORIDA, Marekani: Mchezaji wa Gofu wa kulipwa, Tiger Woods, ametangaza kujiondoa kwa muda kwenye mchezo huo ili kutafuta matibabu na kuangazia afya yake, kufuatia kukamatwa baada ya kuhusishwa na ajali ya gari iliyotokea Florida, Marekani. Woods mwenye umri wa miaka 50, ambaye amewahi kutwaa mataji 15 ya mashindano makubwa ya gofu (majors), alikamatwa na kufunguliwa - [Singida BS, Azam FC hapatoshi](https://spotileo.co.tz/singida-bs-azam-fc-hapatoshi/) - SINGIDA: SINGIDA Black Stars inatarajiwa kushuka dimbani kesho kuikabili Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC utakaochezwa kwenye Uwanja wa Airtel, mkoani Singida. Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na historia ya timu hizo mbili pamoja na nafasi zao kwenye msimamo wa ligi. Takwimu zinaonesha kuwa katika michezo 10 ya mwisho - [Ngorongoro kutumia AFCON kutangaza utalii](https://spotileo.co.tz/ngorongoro-kutumia-afcon-kutangaza-utalii/) - DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesema imejipanga kutumia fursa ya mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) kutangaza vivutio vya utalii na historia ya kipekee ya eneo hilo, ikiwemo chimbuko la mwanadamu katika eneo la Laetoli mkoani Arusha. Akizungumzia msimu wa 11 WA shindano la Safari Field Chalenji linalohusisha waongoza watalii, - [Max Nzengeli afunguka kushuka kwa kiwango](https://spotileo.co.tz/max-nzengeli-afunguka-kushuka-kwa-kiwango/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO wa Yanga, Max Nzengeli, amesema kucheza kwa muda mrefu na kutumia nguvu nyingi uwanjani ni miongoni mwa sababu zinazoweza kufanya kiwango cha mchezaji kupungua na kilivyokuwa mwanzoni mwa msimu. Nzengeli amesema ni jambo la kawaida kwa mchezaji ambaye amekuwa akicheza mara kwa mara kwa dakika nyingi kushindwa kuwa na ubora ule - [Shetta apongeza majukwaa ya ubunifu](https://spotileo.co.tz/shetta-apongeza-majukwaa-ya-ubunifu/) - DAR ES SALAAM: MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Nurdin Bilal Juma 'Shetta', amesema majukwaa ya ubunifu kama Her Creative Spark yana mchango mkubwa katika kukuza sekta ya ubunifu nchini kwa kuwapa vijana fursa ya kujifunza na kuonesha vipaji vyao. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Shetta amewapongeza waandaaji wa tukio hilo kwa juhudi zao - [Tanzania atwaa ubingwa wa ICC T20 Qualifier B](https://spotileo.co.tz/tanzania-atwaa-ubingwa-wa-icc-t20-qualifier-b/) - ACCRA, Ghana TANZANIA imeandika historia baada ya kutwaa ubingwa wa mashindano ya kufuzu Kombe la Dunia la Kriketi la T20 kwa wanaume, Kanda ya Afrika B (ICC Men’s T20 World Cup Sub Regional Africa Qualifier B), yaliyomalizika nchini Ghana. Kwa ushindi huo, Tanzania imefanikiwa kufuzu hatua inayofuata ya 2028 T20 World Cup Regional Qualifiers, baada - [Serengeti girls ya motooo!](https://spotileo.co.tz/serengeti-girls-ya-motooo/) - MONASTIR: TIMU ya soka ya Taifa ya Wanawake chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Girls), imeanza vyema kambi yake ya mazoezi kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tunisia kwenye Uwanja wa Mustapha Ben Jannet Monastir nchini Tunisia jana. Serengeti Girls imeweka kambi mjini Monastir nchini Tunisia kwa ajili ya maandalizi ya mechi za - [Vipaji vya riadha vyang’aa Dar](https://spotileo.co.tz/vipaji-vya-riadha-vyangaa-dar/) - DAR ES SALAAM:MWENYEKITI wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam, Amani Ngoka, amesema mashindano ya vijana yanayoendelea jijini humo yameanza kuonesha mwanga mkubwa wa kupata vipaji vya baadaye kwa ajili ya timu za taifa. Akizungumza na SpotiLeo, Ngoka amesema mwitikio wa vijana umeanza vizuri na anaamini hadi kesho vipaji vingi vitaendelea kuibuka. Amesema - [Atiki kuipambania Dar City kesho](https://spotileo.co.tz/atiki-kuipambania-dar-city-kesho/) - PRETORIA, Afrika Kusini: DAR CITY itaanza rasmi safari yake ya kusaka mafanikio kwenye michuano ya Basketball Africa League (BAL) Kalahari Conference kesho, itakapomenyana na Johannesburg Giants nchini Afrika Kusini. Mabingwa hao wa Tanzania wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa wamejipanga kuonesha ushindani mkubwa, huku wakiimarisha kikosi chao kwa kusajili wachezaji wenye uzoefu wa kimataifa. Katika kujiandaa - [Vijana 3000 kuchuana Riadha](https://spotileo.co.tz/vijana-3000-kuchuana-riadha/) - DAR ES SALAAM: ZAIDI ya wanariadha 3,000 wanatarajiwa kushiriki mashindano makubwa ya vijana yatakayofanyika kesho jijini Dar es Salaam, huku waandaaji wakitarajia kuvutia zaidi ya mashabiki 10,000. Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam, Amani Ngoka, amewaambia waandishi wa habari Leo kuwa mashindano hayo yatahusisha vijana wenye umri wa chini ya miaka - [Jeuri ya Yanga kwa Simba bado ipo](https://spotileo.co.tz/jeuri-ya-yanga-kwa-simba-bado-ipo/) - DAR ES SALAAM: LICHA ya Ligi Kuu Tanzania Bara kusimama kwa muda kupisha ratiba ya timu ya taifa inayoshiriki michezo ya FIFA Series nchini Rwanda, vita ya ubingwa baina ya watani wa jadi Yanga na Simba imeendelea kuwa gumzo kubwa miongoni mwa mashabiki wa soka nchini. Hadi ligi iliposimama, Yanga bado imeendelea kuonyesha jeuri yake - [Gamondi: tupo tayari kucheza na Liechtenstein](https://spotileo.co.tz/gamondi-tupo-tayari-kucheza-na-liechtenstein/) - KIGALI, Rwanda: KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Miguel Gamondi amesema kikosi chake kipo tayari kuanza vyema michuano ya FIFA Series kwa kucheza soka kuvutia na lenye matokeo watakaposhuka dimbani dhidi ya Liechtenstein leo nchini Rwanda. Taifa Stars inatarajiwa kucheza mchezo huo wa kimataifa saa 11:30 jioni, huku pambano la ufunguzi wa michuano hiyo likitarajiwa kuchezwa - [Tenisi walemavu yaomba Milioni 40 kushiriki mashindano Morocco](https://spotileo.co.tz/tenisi-walemavu-yaomba-milioni-40-kushiriki-mashindano-morocco/) - DAR ES SALAAM: TIMU ya Taifa ya wachezaji wa tenisi kwa walemavu imeomba msaada wa Shilingi milioni 40 ili kufanikisha safari ya kwenda kushiriki mashindano ya kimataifa yatakayofanyika nchini Morocco kuanzia Machi 30 hadi Aprili 3, 2026. - Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kocha wa timu hiyo ambaye pia ni Katibu, - [Kasiga ahimiza nidhamu kwa wasanii wa filamu](https://spotileo.co.tz/kasiga-ahimiza-nidhamu-kwa-wasanii-wa-filamu/) - DAR ES SALAAM: KATIBU Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk Gervas Kasiga, amesema tofauti kubwa kati ya kizazi cha sasa cha waigizaji na vizazi viwili vilivyotangulia ni kiwango cha nidhamu kilichojengwa kupitia vikundi mbalimbali vya sanaa hapo awali. Dk Kasiga ameeleza kuwa zamani wasanii walipitia mafunzo na makuzi ya sanaa ndani ya vikundi maalum, - [Vanillah awaonya wachambuzi](https://spotileo.co.tz/vanillah-awaonya-wachambuzi/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Fanuel Peter 'Vanillah' amesema hataki kupokea ushauri wala maoni kutoka kwa wachambuzi wa muziki kuhusu kazi yake mpya anayotarajia kuiachia hivi karibuni. Kupitia ujumbe wake aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, msanii huyo alieleza kuwa kuna mambo mengi yamejitokeza nyuma ya pazia ambayo watu hawafahamu, lakini mara - [Wanariadha wa Tanzania wang’ara Kili Half Marathon 2026](https://spotileo.co.tz/wanariadha-wa-tanzania-wangara-kili-half-marathon-2026/) - KILIMANJARO: Wanariadha wa Tanzania wameendelea kuonesha kiwango cha juu cha ushindani katika mashindano ya Kili International Half Marathon 2026. Mashindano hayo ya kilomita 21, ambayo ni sehemu ya tamasha kubwa la kila mwaka la Kili International Marathon, yameendelea kuwa jukwaa la kuhamasisha afya kupitia mazoezi pamoja na kukuza vipaji vya wanariadha wa ndani na nje - [Marioo, Matata kutangaza utamaduni wa Afrika kupitia ‘Nyongi’](https://spotileo.co.tz/marioo-matata-kutangaza-utamaduni-wa-afrika-kupitia-nyongi/) - NAIROBI: MSANII wa Tanzania Omary Mwanga 'Marioo' ameungana na kundi maarufu la muziki wa pop kutoka Kenya, Matata na wameachia wimbo wao unaoitwa nyongi. Wimbo huo ni utangulizi wa EP ya kundi hilo itakayoitwa ERA (East Rise Again) inayotarajiwa kutoka mwezi Juni ikiwa na nyimbo sita pamoja na wimbo wa ‘Kanairo’ unaotarajiwa kutoka Mei - [Gueye: Tulishinda Afcon uwanjani](https://spotileo.co.tz/gueye-tulishinda-afcon-uwanjani/) - SENEGAL: NYOTA wa Everton na Senegal, Idrissa Gueye amesema walishinda Kombe la Mataifa ya Afrika uwanjani na bingwa hawezi kuamuliwa ofisini. Aidha, alisema yuko tayari kurejesha medali ya ubingwa kwa Morocco ikiwa hatua hiyo itasaidia kupunguza mvutano kati ya mataifa hayo mawili.Akizungumza baada ya mechi ya klabu yake ya Everton kushinda 3-0 dhidi ya Chelsea, - [Mariga aeleza alivyoshindwa kucheza EPL](https://spotileo.co.tz/mariga-aeleza-alivyoshindwa-kucheza-epl/) - NAIROBI: KIUNGO wa zamani wa Kenya, McDonald Mariga, ameelezea tena jinsi ndoto yake ya kuwa Mkenya wa kwanza kucheza Ligi Kuu ya England ilivyovunjika miaka 16 iliyopita. Mariga alizungumzia kwa mara nyingine kuhusu uhamisho wake ulioshindikana kwenda klabu ya Manchester City mwaka 2010. Mnamo Januari mwaka huo, alikuwa karibu kuandika historia baada ya City, iliyokuwa - [Polisi waondoa video 154 za YouTube, reels 703 za wimbo ‘Tateeree’](https://spotileo.co.tz/polisi-waondoa-video-154-za-youtube-reels-703-za-wimbo-tateeree/) - HARYANA, India: POLISI wa jimbo la Haryana nchini India wameondoa jumla ya video 857 kutoka mitandao ya kijamii zinazohusiana na wimbo “Tateeree” wa msanii Badshah kufuatia kuzuka kwa utata kuhusu wimbo huo. Wimbo huo umekosolewa vikali kwa madai ya kuwa na maneno na picha zisizofaa, hasa zinazodaiwa kudhalilisha wanawake na watoto. Msanii huyo, anayejulikana pia - [Tamasha la Shakira India laahirishwa](https://spotileo.co.tz/tamasha-la-shakira-india-laahirishwa/) - INDIA: TAMASHA la msanii maarufu duniani, Shakira Mebarak maarufu Shakira, lililokuwa lifanyike nchini India limeahirishwa bila kutangazwa tarehe mpya kutokana na mvutano wa kisiasa na hali ya kijiografia, ikiwemo mgogoro kati ya Marekani na Iran. Shakira, mshindi wa tuzo za Grammy, alikuwa amewapa mashabiki hamu kubwa baada ya kutangaza ziara yake ya kurejea India mwezi - [Mpanzu yupo sana Msimbazi](https://spotileo.co.tz/mpanzu-yupo-sana-msimbazi/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Simba imeondoa sintofahamu kuhusu hatma ya kiungo mshambuliaji wake, Elie Mpanzu, baada ya kumsainisha mkataba mpya wa miaka miwili wa kuendelea kuitumikia timu hiyo. Mpanzu, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), amekamilisha usajili huo leo Jumatatu, Machi 23, 2026, hatua inayomuweka Msimbazi hadi Desemba 2028. Awali, kiungo huyo - [Makonda aitaka Dar City iandike historia mpya Afrika](https://spotileo.co.tz/makonda-aitaka-dar-city-iandike-historia-mpya-afrika/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, ameikabidhi bendera ya taifa timu ya mpira wa kikapu ya Dar City na kuitaka kwenda kufanya vizuri katika michuano ya Afrika BAL Kalahari Conference 2026, akisema mafanikio yao yamefungua ukurasa mpya kwa mchezo huo nchini. Akizungumza wakati akiiaga timu hiyo inayokwenda Pretoria, Afrika - [Halima apigwa nyundo miaka 3, faini milioni 3](https://spotileo.co.tz/halima-apigwa-nyundo-miaka-3-faini-milioni-3/) - DAR ES SALAAM: BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limetangaza kumfungia msanii Halima Haji kujihusisha na shughuli za sanaa kwa kipindi cha miaka mitatu, kufuatia kukiuka maadili katika kazi zake za kisanii. Katika taarifa rasmi iliyotolewa na BASATA, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Leonidas Tibanga, imeelezwa kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kusambaa kwa - [Lady JayDee amesema umri si kikwazo cha kupendeza](https://spotileo.co.tz/lady-jaydee-amesema-umri-si-kikwazo-cha-kupendeza/) - DAR ES SALAAM: Msanii wa Bongo Fleva, Judith Wambura 'Lady JayDee', amezungumzia mabadiliko ya mwili yanayokuja kadri umri unavyosonga, huku akisisitiza kuwa hilo halitamzuia kuendelea kupendeza na kufurahia maisha. Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Lady JayDee ameandika kuwa kuna wakati unafika mambo ya kubana tumbo hayawezekani tena, na badala yake mtu anatakiwa kuukubali - [Msanii Irene Robert, afariki dunia](https://spotileo.co.tz/msanii-irene-robert-afariki-dunia/) - DAR ES SALAAM:TASNIA ya muziki wa Injili nchini Tanzania imepata pigo kufuatia kifo cha muimbaji maarufu Irene Robert, aliyeripotiwa kufariki dunia leo Ijumaa baada ya kuugua ghafla. Taarifa za msiba huo zimethibitishwa na msanii mwezake, Walter Chilambo kupitia ukurasa wake wa Instagram, ambapo ameeleza masikitiko yake na kuomboleza msanii huyo aliyegusa maisha ya wengi kupitia - [Dogo Rema aomba sapoti ya mashabiki](https://spotileo.co.tz/dogo-rema-aomba-sapoti-ya-mashabiki/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Dogo Rema, amewaomba mashabiki wake kuendelea kumsapoti katika kazi zake za muziki pamoja na kumpatia fursa za kushiriki katika maonesho mbalimbali. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo ameeleza kuwa mafanikio aliyoyapata yametokana na mchango mkubwa wa mashabiki wake waliomuinua kutoka maisha ya kawaida hadi kufikia - [Lady Jaydee aingia mkataba mkubwa na Universal Music Group East Africa](https://spotileo.co.tz/lady-jaydee-aingia-mkataba-mkubwa-na-universal-music-group-east-africa/) - DAR ES SALAAM:MSANII mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura maarufu kama Lady Jaydee, amepata dili kubwa baada ya Kampuni ya Universal Music Group East Africa kutangaza rasmi ushirikiano wake na nyota huyo wa Afrika Mashariki. Lady Jaydee anatambulika kama mmoja wa wasanii wenye sauti yenye ushawishi mkubwa na iliyodumu kwa muda mrefu katika - [BASATA yamuita Halima Haji](https://spotileo.co.tz/basata-yamuita-halima-haji/) - DAR ES SALAAM: BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limemuita msanii Halima Haji pamoja na meneja wake, Rahma Pascal, kufuatia kusambaa kwa kipande cha video ya muziki kinachodaiwa kukiuka maadili ya Kitanzania. Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na BASATA, kikao hicho ambapo wahusika walifika mbele ya Baraza na kukiri kufanya kosa hilo. Kufuatia kukiri - [Barker: hatukutarajia matokeo ya sare](https://spotileo.co.tz/barker-hatukutarajia-matokeo-ya-sare/) - MWANZA: KOCHA Mkuu wa Simba, Steven Barker, amesema sare ya bao 1-1 dhidi ya Pamba haikuwa matokeo waliyoyatarajia, kwani kila wanapoingia uwanjani lengo lao ni kushinda na kupata pointi tatu. Akizungumza baada ya mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza jana Barker amesema walijua mapema kuwa mchezo huo usingekuwa mwepesi kwa sababu Pamba - [Jay-Z aibuka na mabadiliko ya jina lake la muziki](https://spotileo.co.tz/jay-z-aibuka-na-mabadiliko-ya-jina-lake-la-muziki/) - NEWYORK : RAPAnguli wa Marekani Shawn Corey Carter maarufu Jay-Z ameibua gumzo kubwa baada ya kufanya mabadiliko madogo lakini yenye maana katika jina lake la kisanii, hatua inayotafsiriwa na wengi kama kurejea kwenye mizizi ya mwanzo wa safari yake ya muziki. Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, Jay-Z ameongeza tena alama ya umlaut (¨) katika jina - [LeBron James afikia rekodi ya Parish](https://spotileo.co.tz/lebron-james-afikia-rekodi-ya-parish/) - LOS ANGELES:NYOTA wa Los Angeles Lakers, LeBron James, ameifikia rekodi ya kihistoria ya Robert Parish ya kucheza mechi 1,611 katika Ligi ya NBA, rekodi ambayo ilikuwa imedumu kwa karibu miaka 30. LeBron, mwenye umri wa miaka 41, alifikia idadi hiyo ya mechi Alhamisi usiku katika mchezo dhidi ya Miami Heat, akilingana na Parish ambaye alicheza - [Venus Williams 'apigwa' na kinda](https://spotileo.co.tz/venus-williams-apigwa-na-kinda/) - MIAMI: GWIJI wa mchezo wa tenisi Venus Williams ameshindwa kuonesha umwamba wake katika mchezo huo baada ya kushindwa vibaya na mchezaji chipukizi Francesca Jones katika mashindano ya Miami Open yaliyofanyika nchini Marekani usiku wa kuamkia leo Machi 20. Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa, Francesca Jones aliibuka na ushindi wa seti mbili mfululizo kwa - [Tanzania yajiunga rasmi na world Boxing](https://spotileo.co.tz/tanzania-yajiunga-rasmi-na-world-boxing/) - DAR ES SALAAM: SHIRIKISHO la Ngumi Tanzania (BFT) limesema Tanzania imekuwa rasmi mwanachama wa World Boxing, Shirikisho la Kimataifa la Ngumi linalotambuliwa na Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC). Kwa mujibu wa Rais wa BFT Lukelo willilo, uamuzi wa kuipokea Tanzania ulifikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya World Boxing kilichofanyika Machi 15, 2026, - [Forest na historia yatinga robo fainali Europa League](https://spotileo.co.tz/forest-na-historia-yatinga-robo-fainali-europa-league/) - LONDON, England: NOTTINGHAM Forest imeandika historia mpya barani Ulaya baada ya kutinga robo fainali ya Europa League kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1996, licha ya kupitia msimu mgumu katika Ligi Kuu England. Forest ilifanikiwa kusonga mbele baada ya kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penalti 3-0 dhidi ya Midtjylland ya Denmark, kufuatia jumla ya - [Singida wakubali mziki wa Prisons](https://spotileo.co.tz/singida-waikubali-prisons/) - DODOMA: Meneja wa Singida Black Stars, Othmen Najjar amesema anashukuru kwa timu yake kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Prisons, akieleza kuwa haikuwa mechi rahisi kutokana na ushindani mkubwa walioupata uwanjani. Akizungumza baada ya mchezo huo jana kocha huyo amesema walikuwa wanatarajia upinzani mkali kutoka kwa Tanzania Prisons, hasa kutokana na uwezo wao - [Wachezaji Chess Tanzania wajipanga Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/wachezaji-chess-tanzania-wajipanga-kombe-la-dunia/) - DAR ES SALAAM: CHAMA cha mchezo wa Chess Tanzania kimesema kimeanza maandalizi ya kushiriki mashindano makubwa ya dunia yanayofanana na Olimpiki yanayotarajiwa kufanyika nchini Uzbekistan kati ya Septemba na Oktoba mwaka huu. Akizungumza na SpotiLeo kuhusu maandalizi hayo, msemaji wa chama hicho Mussa Mangula amesema wanatarajia kuandaa mashindano ya Taifa ya Chess yatakayofanyika Mei Mosi - [Maskini Yanga limewakuta jambo](https://spotileo.co.tz/maskini-yanga-limewakuta-jambo/) - DAR ES SALAAM: Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe amesema mshambuliaji wa timu hiyo, Prince Dube, amelazimika kubaki Dar es Salaam kwa ajili ya kufanyiwa vipimo zaidi kufuatia kuumia katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya TRA uliochezwa jana. Kamwe amesema wakati Dube akibaki jijini Dar es Salaam kwa uangalizi wa kitabibu, - [Liverpool watinga robo fainali kibabe](https://spotileo.co.tz/liverpool-watinga-robo-fainali-kibabe/) - LONDON, England KLABU ya Liverpool imefuzu hatua ya robo fainali ya UEFA Champions league baada ya kuichapa Galatasaray mabao 4-0 , ambapo sasa itakutana na mabingwa watetezi Paris St-Germain. Baada ya kufungwa 1-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa Istanbul, kikosi cha kocha Arne Slot kilirejea kwa nguvu na kusawazisha jumla ya mabao kupitia kiungo Dominik - [Ludacris kusherehesha tuzo za muziki 2026](https://spotileo.co.tz/ludacris-kusherehesha-tuzo-za-muziki-2026/) - LOS ANGELES: RAPA, muigizaji na mfanyabiashara maarufu nchini Marekani Christopher Brian ametangazwa rasmi kuwa mtangazaji mkuu wa tuzo za muziki za iHeartRadio 2026, tukio linalosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki duniani. Tukio hilo linatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Dolby Theatre uliopo jijini Los Angeles, nchini Marekani. Katika tuzo hizo mwanamuziki na muigizaji Miley Cyrus - [Kevin Hart akosoa sanamu lake](https://spotileo.co.tz/kevin-hart-akosoa-sanamu-lake/) - WASHINGTON DC: Mchekeshaji maarufu duniani Kevin Hart ameibua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kushangazwa na sanamu yake ya wax iliyowekwa kwenye makumbusho nchini Marekani. Kupitia video aliyochapisha, Hart aliikosoa sanamu hiyo akidai haifanani naye, kauli iliyosababisha mashabiki na mastaa wengine kuingia kwenye mjadala huo kwa utani na vichekesho. Kevin Hart aliichapisha video hiyo akionesha sanamu - [Mkongwe Madona ajitupa kwenye Uigizaji](https://spotileo.co.tz/mkongwe-madona-ajitupa-kwenye-uigizaji/) - LOS ANGELES: MWANAMUZIKI mkongwe Louise Ciccone maarufu Madonna amethibitisha kurejea kwenye uigizaji baada ya kutoonekana katika tasnia hiyo kwa zaidi ya miaka 20. Nyota huyo alionekana nchini Italy akisoma script ya kazi mpya ya tamthilia ‘The Studio’, jambo lililowasisimua mashabiki wake duniani. Tamthilia hiyo inayorushwa na Apple TV+ imekuwa maarufu kwa kushinda tuzo nyingi nje - [Barcelona yatinga robo fainali kwa kishindo](https://spotileo.co.tz/barcelona-yatinga-robo-fainali-kwa-kishindo/) - BARCELONA, Hispania: KLABU ya FC Barcelona imeonesha ubora barani Ulaya baada ya kuichapa Newcastle United mabao 7-2 katika mchezo wa marudiano wa hatua ya 16 bora ya UEFA Champions League uliopigwa katika dimba la Spotify Camp Nou. Ushindi huo mkubwa uliifanya Barcelona kusonga mbele kwa jumla ya mabao 8-3, ikiweka wazi dhamira yake ya kutwaa - [Wanasiasa wataka uchunguzi kuuzwa kwa Kampuni ya Warner Bro](https://spotileo.co.tz/wanasiasa-wataka-uchunguzi-kuuzwa-kwa-kampuni-ya-warner-bro/) - NEW YORK: KATIKA hatua kubwa ya kihistoria, kampuni ya Warner Bros. Discovery inayojishughulisha na utengenezaji wa filamu, vipindi vya televisheni na maudhui ya kidigitali imekubali kununuliwa na Kampuni ya Paramount Skydance kwa takribani dola bilioni 110. Dili hilo linaelezwa kuwa moja ya makubwa kuwahi kutokea katika tasnia ya burudani duniani. Kinachovuta zaidi hisia ni kwamba - [Messi aingia kwenye historia afikisha mabao 900](https://spotileo.co.tz/messi-aingia-kwenye-historia-afikisha-mabao-900/) - MIAMI, Marekani: NYOTA wa soka duniani, Lionel Messi, ameingia rasmi kwenye kundi la wachezaji wachache waliofunga mabao 900 katika maisha yao ya soka, akimfuata mpinzani wake wa muda mrefu, Cristiano Ronaldo. Messi alifikisha bao lake la 900 baada ya kufunga katika mchezo wa marudiano wa hatua ya 16 bora dhidi ya Nashville SC uliochezwa Machi - [EACLC yafungua milango wasanii wa filamu](https://spotileo.co.tz/eaclc-yafungua-milango-wasanii-wa-filamu/) - DAR ES SALAAM: MKURUGENZI wa Kituo cha Biashara na Usafirishaji Afrika Mashariki (EACLC), Dk. Cathy Wang, amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Gervas Kasiga, kwa lengo la kufungua fursa mpya za ushirikiano zitakazonufaisha tasnia ya filamu nchini. Mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, yamelenga kuimarisha mahusiano kati ya EACLC - [Wasanii watakiwa kutangaza utalii kupitia filamu](https://spotileo.co.tz/wasanii-watakiwa-kutangaza-utalii-kupitia-filamu/) - DAR ES SALAAM: WASANII wa filamu nchini wametakiwa kuhakikisha kazi wanazozalisha zinatumika kama jukwaa la kutangaza vivutio vya utalii, hatua itakayosaidia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Tanzania. Wito huo umetolewa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Gervas Kasiga, wakati wa hafla ya ugawaji tuzo na vyeti kwa wanafunzi walioshinda shindano la Guardians - [Barker: Simba tuko tayari kuivaaa Pamba](https://spotileo.co.tz/barker-simba-tuko-tayari-kuivaaa-pamba/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Simba SC, Steven Barker, amethibitisha kuwa kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Pamba kesho kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza. Barker amesema timu iko katika hali nzuri kimwili na kisaikolojia, licha ya kuchelewa kucheza mechi iliyopita mwishoni mwa wiki. “Kutocheza mechi iliyopita kunatupa - [Gamondi amrejesha Manula Taifa Stars](https://spotileo.co.tz/gamondi-amrejesha-manula-taifa-stars/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Taifa Stars Miguel Gamondi amemrejesha kikosini kipa wa Azam Aishi Manula kwenye kikosi cha wachezaji 25 kitakachoingia kambini kujiandaa na michezo ya Fifa Series 2026. Manula aliwahi kutumikia Taifa Stars akiwa Simba baadaye akapata majeraha yaliyomweka nje kwa muda mrefu n a hata alivyopona hakupata nafasi hadi alipojiunga na - [Britney ahofia kuwekwa chini ya uangalizi](https://spotileo.co.tz/britney-ahofia-kuwekwa-chini-ya-uangalizi/) - CALIFORNIA: MSANII maarufu wa muziki wa pop, Britney Spears anaripotiwa kukumbwa na hofu kubwa kufuatia kukamatwa kwake kwa tuhuma za kuendesha gari akiwa amelewa, huku akihofia kurejea katika kipindi cha maisha ya uangalizi. Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya karibu, nyota huyo mwenye umri wa miaka 44 anadaiwa kuwa katika hali ya wasiwasi mkubwa - [PSG haikamatiki UEFA,](https://spotileo.co.tz/psg-haikamatiki-uefa/) - LONDON, England BINGWA mtetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Paris Saint-Germain (PSG) wameonesha ubora wao kwa kuichapa Chelsea mabao 3-0 katika mchezo wa marudiano wa hatua ya 16 bora ya michuano hiyo katika Uwanja wa Stamford Bridge. Ushindi huo umeifanya PSG kusonga mbele kwa jumla ya mabao 8-2, ikiwa ni moja ya vipigo vizito - [Manchester City taabani Ligi ya Mabingwa Ulaya](https://spotileo.co.tz/manchester-city-taabani-ligi-ya-mabingwa-ulaya/) - MANCHESTER, England KLABU ya Manchester City ya England wametolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kipigo cha jumla ya mabao 5-1 kutoka kwa Real Madrid. City walikubali kipigo cha mabao 3-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliochezwa katika Uwanja wa Santiago Bernabeu nchini Hispania kabla ya kufungwa mabao 2-1 jana katika - [Morocco bingwa AFCON 2025](https://spotileo.co.tz/morocco-bingwa-afcon-2025/) - MARRAKECH, Morocco TIMU ya Taifa ya Morocco imetangazwa rasmi mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kubatilisha matokeo ya fainali iliyokuwa imeipa ushindi Senegal. Awali, Senegal ilishinda fainali hiyo kwa bao 1-0 dhidi ya Morocco katika mchezo uliochezwa Januari 18, 2026, lakini ushindi huo sasa - [Budju aibuka na wimbo mpya ‘Safe In You’](https://spotileo.co.tz/jonathan-budju-aibuka-na-wimbo-mpya-safe-in-you/) - DAR ES SALAAM: STAA wa muziki wa Injili anayeishi Canada, Jonathan Budju, amewataka mashabiki wake wakae tayari kwa ajili ya ujio wa wimbo wake mpya unaoitwa Safe In You, unaotarajiwa kutoka hivi karibuni. Msanii huyo ambaye alifanya vizuri kwenye chati za muziki wa Injili kupitia wimbo wake wa sifa zake, amekamilisha maandalizi ya kazi yake - [Neymar atemwa kikosi cha Brazil](https://spotileo.co.tz/neymar-atemwa-kikosi-cha-brazil/) - BRASILIA, Brazil MCHEZAJI wa timu ya taifa ya soka ya Brazil, Neymar Junior, ametemwa kwa mara nyingine kwenye kikosi kilichotangazwa na kocha mkuu Carlo Ancelotti kwa ajili ya mechi za kirafiki za kimataifa za kalenda ya FIFA kuelekea maandalizi ya FIFA World Cup 2026. Brazil inatarajiwa kucheza mechi mbili za kirafiki, ikianza kwa kuchuana na - [Barker, Depu wang'ara Februari](https://spotileo.co.tz/barker-depu-wangara-februari/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Simba, Steve Barker, amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi Februari wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2025/2026. Aidha, Mshambuliaji wa Yanga, Laurindo Aurelio 'Depu' amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Februari wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2025/2026, Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi yq - [Mabondia wanawake kuchuana Tanga](https://spotileo.co.tz/mabondia-wanawake-kuchuana-tanga/) - DAR ES SALAAM: Shirikisho la Ngumi Tanzania (BFT) limetangaza kuandaa mashindano maalum ya ngumi kwa wanawake yatakayofanyika Aprili 6 na 7 mwaka huu mkoani Tanga. Akizungumza na SpotiLeo, Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, amesema mashindano hayo awali yalipangwa kufanyika mwezi huu lakini yalilazimika kusogezwa mbele kutokana na kipindi cha Ramadan. Mashaga amesema baada - [Yanga kuwakosa Bacca, Depu dhidi ya TRA](https://spotileo.co.tz/yanga-kuwakosa-bacca-depu-dhidi-ya-tra/) - ARUSHA: Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema mapokezi makubwa waliyoyapata kutoka kwa mashabiki wa timu hiyo walipowasili jijini Arusha yamewapa nguvu na motisha zaidi ya kuendelea kupambana katika michezo ijayo. Kupitia ujumbe wake, kocha huyo amesema sapoti na upendo mkubwa waliouonesha mashabiki umeongeza morali kwa wachezaji na benchi la ufundi, huku akisisitiza kuwa kikosi - [Majizo: Sikumchagua Ssebo kwa bahati mbaya](https://spotileo.co.tz/majizo-sikumchagua-ssebo-kwa-bahati-mbaya/) - DAR ES SALAAM :MKURUGENZI wa Kituo cha EFM , Francis Siza maarufu kama Mhimili, ameeleza masikitiko yake kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi wa Biashara na Uendeshaji wa Kituo Cha EFM, Dennis Busulwa aliyefariki dunia. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mtangazaji na DJ wa kituo hicho, Majizzo, ameandika ujumbe wa kugusa hisia akimkumbuka marehemu kama mtu - [Kanye West kulipa fidia ya Sh18 milioni](https://spotileo.co.tz/kanye-west-kulipa-fidia-ya-sh18-milioni/) - LOS ANGELES: MAHAKAMA ya majaji jijini Los Angeles imemuamuru rapa maarufu Kanye West kulipa fidia ya takribani shilingi milioni 18 kwa aliyekuwa meneja wa mradi wake, Tony Saxon, kufuatia mgogoro wa kazi katika nyumba ya kifahari ya rapa huyo iliyopo Malibu. Kesi hiyo ilihusisha madai ya kutolipwa mishahara, mazingira hatarishi ya kazi na kufukuzwa kazi - [Filamu ya Priyanka Chopra ‘The Bluff’ yavunja rekodi](https://spotileo.co.tz/filamu-ya-priyanka-chopra-the-bluff-yavunja-rekodi/) - INDIA: FILAMU mpya ya muigizaji wa Bollywood Priyanka Chopra iitwayo ‘The Bluff’ imefanikiwa kuwa filamu ya asili iliyotazamwa zaidi katika majukwaa ya utiririshaji (OTT) duniani licha ya kupokea maoni mchanganyiko kutoka kwa wakosoaji. Filamu hiyo iliyotolewa Februari 25 kwenye jukwaa la Amazon Prime Video, imekusanya takribani dakika milioni 300.3 za watazamaji katika kipindi cha wiki - [Makonda: Ole wao wanaokiuka katiba](https://spotileo.co.tz/makonda-ole-wao-wanaokiuka-katiba/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema baadhi ya viongozi wa mashirikisho ya michezo wamekuwa wakibadilisha katiba za taasisi zao ili kulinda nafasi zao madarakani. Makonda alitoa kauli hiyo katika mkutano wa Baraza la Michezo la Taifa uliofanyika kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam Leo. Amesema taarifa - [Makonda: Tutawang'oa viongozi wasiowajibika](https://spotileo.co.tz/makonda-tutawangoa-viongozi-wasiowajibika/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amewaonya viongozi wa mashirikisho ya michezo nchini wanaoshindwa kutekeleza ahadi walizozitoa kwa wanachama wao kuwa wako hatarini kung’olewa madarakani. Makonda amesema ofisi yake itaanza kufuatilia utekelezaji wa ahadi hizo na endapo itabainika kuwa hazijafikia hata asilimia 20 ya yale waliyoahidi wakati wa uchaguzi, - [Makonda: Tumieni fursa ya AFCON kuonesha vipaji](https://spotileo.co.tz/makonda-tumieni-fursa-ya-afcon-kuonesha-vipaji/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amewataka viongozi wa mashirikisho ya michezo kutumia fursa ya mashindano makubwa ya soka barani Afrika kuitangaza Tanzania na kuonesha vipaji vya michezo mingine. Makonda amesema maandalizi ya mashindano hayo yanapaswa kuwa fursa kwa michezo yote nchini, siyo soka pekee. Akizungumza kwenye mkutano wa - [Makonda awaonya viongozi wa michezo](https://spotileo.co.tz/makonda-awaonya-viongozi-wa-michezo/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amewaonya viongozi wa mashirikisho ya michezo nchini wanaoshindwa kutekeleza ahadi walizozitoa kwa wanachama wao kuwa wako hatarini kung’olewa madarakani. Makonda amesema ofisi yake itaanza kufuatilia utekelezaji wa ahadi hizo na endapo itabainika kuwa hazijafikia hata asilimia 20 ya yale waliyoahidi wakati wa uchaguzi, - [Baba Levo kuokota milioni 100 kwa Wakazi](https://spotileo.co.tz/baba-levo-kuokota-milioni-100-kwa-wakazi/) - DAR ES SALAAM: MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Mjini, na Msanii Clayton Revocatus Chiponda 'Baba levo,, ametangaza kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imemhukumu msanii wa hip hop, Wakazi, kumlipa fidia ya Shilingi milioni 100 kufuatia kusambaza taarifa za uongo na za kashfa dhidi yake. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Babalevo - [Mwili wa Ssebo kuagwa Jumamosi](https://spotileo.co.tz/mwili-wa-ssebo-kuagwa-jumamosi/) - DAR ES SALAAM; MWILI wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Uendeshaji na Biashara wa kampuni ya E-Media, marehemu Denis Busulwa maarufu kama Ssebo, unatarajiwa kuagwa rasmi Jumamosi, Machi 14, 2026 katika viwanja vya Sanyansi vilivyopo eneo la Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Taarifa za ratiba ya mazishi zimetolewa na Mratibu wa Vipindi wa E-Media, Dizzo, ambaye amesema - [Gigy Money: Maisha yamenifundisha mtu anaweza kubadilika](https://spotileo.co.tz/gigy-money-maisha-yamenifundisha-mtu-anaweza-kubadilika/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Gift Stanford 'Gigy Money', amesema maisha yamemfundisha kuwa mtu anaweza kubadilika na kuwa bora zaidi pale anapopata mwongozo sahihi katika maisha. Kupitia ujumbe aliyouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, msanii huyo amesema anatambua kuwa zamani hakuwa kama alivyo sasa, kwani alipitia changamoto na kufanya makosa mbalimbali yaliyomjengea - [Maandalizi ya tamasha la sarakasi Tanzania yaanza rasmi](https://spotileo.co.tz/maandalizi-ya-tamasha-la-sarakasi-tanzania-yaanza-rasmi/) - DAR ES SALAAM: WATAALAM kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) leo wamekutana na viongozi wa Chama cha Sarakasi Tanzania (CHASATA) kujadili maandalizi ya kuanzishwa kwa Tamasha la Sarakasi nchini. Akizungumza na SpotiLEO Mkurugenzi Msaidizi wa Tafiti na Masoko wa BASATA Mrisho Mrisho katika ukumbi wa mikutano wa BASATA uliopo Dar es Salaam, wataalamu wa - [Ibenge ainua mapanga Dar Dabi](https://spotileo.co.tz/ibenge-ainua-mapanga-dar-dabi/) - DODOMA: KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge amesema hawana sababu ya kuficha mbinu zao kuelekea mchezo ujao dhidi ya Yanga akisisitiza kuwa wapinzani wao tayari wanaifahamu vizuri timu yake kutokana na mechi nyingi walizocheza msimu huu. Ibenge amesema ni jambo la kawaida kwa timu pinzani kufuatilia michezo ya wapinzani wao ili kujua mbinu na - [Aucho: Tulipoteza umakini](https://spotileo.co.tz/aucho-tulipoteza-umakini/) - SINGIDA: KIUNGO wa Singida Black Stars, Khalid Aucho amesema kupoteza umakini katika dakika za mwisho kumeigharimu timu yake baada ya kufungwa mabao 2-1 na Simba katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Airtel. Aucho amesema licha ya kupoteza mchezo huo, timu yao ilicheza vizuri na ilitengeneza nafasi kadhaa za kufunga lakini walishindwa - [Kocha Simba ampa heko Mpanzu](https://spotileo.co.tz/kocha-simba-ampa-heko-mpanzu/) - SINGIDA: KOCHA Mkuu wa Simba Steven Barker amesema haikuwa rahisi kwa Simba kupata ushindi dhidi ya Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa kwenye Uwanja wa Airtel, lakini juhudi na mapambano ya wachezaji hadi dakika za mwisho yaliwapa ushindi wa mabao 2-1. Akizungumza baada ya mchezo huo, Barker, amesema ulikuwa mchezo mgumu na - [Christina Mwagala azitumia Salamu Simba, Yanga](https://spotileo.co.tz/christina-mwagala-azitumia-salamu-simba-yanga/) - ARUSHA: OFISA Habari wa TRA, Christina Mwagala, amezitumia salamu klabu za Simba na Yanga akisisitiza kuwa ni vyema zikawa tayari kucheza michezo yao ya Ligi Kuu katika viwanja vya mikoani badala ya kuonekana kama hazitaki kusafiri nje ya Dar es Salaam. Mwagala amesema TRA imechagua Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kuwa uwanja wake - [Ibenge akubali muziki wa wachezaji wake](https://spotileo.co.tz/ibenge-akubali-muziki-wa-wachezaji-wake/) - DODOMA: KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema ameridhishwa na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. Ibenge amesema ushindi huo ni matokeo ya juhudi kubwa na mabadiliko ya kimkakati waliyoyafanya katika - [Yanga tayari kuivaa Tanzania Prisons](https://spotileo.co.tz/yanga-tayari-kuivaa-tanzania-prisons/) - DODOMA: KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema kikosi chake kipo tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Tanzania Prisons utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, huku akisisitiza malengo yao makubwa ni kuondoka na alama tatu. Goncalves amesema leo watafanya mazoezi ya mwisho kabla ya mchezo huo, huku akili za wachezaji - [Anunobi asimulia kifo cha mwanawe](https://spotileo.co.tz/anunobi-asimulia-kifo-cha-mwanawe/) - NIGERIA: MUIGIZAJI mkongwe wa Nigeria, Eucharia Anunobi amefunguka kwa mara nyingine kuhusu maumivu aliyopitia kuhusu kifo cha mwanawe mwenye umri wa miaka 15. Akizungumza katika mahojiano kwenye podikasti ya ‘The Honest Bunch Podcast’, Anunobi alidai kuwa uzembe wa kitabibu ulihusika katika kifo cha mwanawe. Kwa mujibu wa mwigizaji huyo, mwanawe ambaye alikuwa katika hali mbaya - [Don Jazzy afunguka kuhusu mwanamke anayemtaka:](https://spotileo.co.tz/don-jazzy-afunguka-kuhusu-mwanamke-anayemtaka/) - ABUJA: MTAYARISHAJI wa muziki kutoka Nigeria, Michael Collins Ajereh 'Don Jazzy' amefunguka hadharani kuhusu sifa anazozitafuta kwa mwanamke anayetarajia kuwa naye kwenye mahusiano na kutengeneza maisha. Don Jazzy alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza kwenye podikasti ya ‘Is This Seat Taken’ inayoendeshwa na muigizaji Chinasa Anukam. Katika mazungumzo hayo, Don Jazzy alieleza kuwa anapendelea mwanamke mwenye - [Rihanna aikimbia nyumba yake baada ya shambulio la risasi](https://spotileo.co.tz/rihanna-aikimbia-nyumba-yake-baada-ya-shambulio-la-risasi/) - LOS ANGELES: MWANAMUZIKI maarufu duniani Rihanna amelazimika kuondoka katika jumba lake la kifahari jijini Los Angeles baada ya mtu mwenye silaha kufyatua risasi kadhaa katika eneo la makazi hayo. Kwa mujibu wa polisi wa Los Angeles, mshukiwa aliyetambuliwa kama Ivanna Lisette Ortiz alifika kwenye nyumba hiyo akiwa na bunduki aina ya semi-automatic na kufyatua takribani - [O’Hara ataka Spurs imfute kazi Igor](https://spotileo.co.tz/ohara-amtaka-tudor-afukuzwe-baada-ya-kipigo-cha-aibu-cha-spurs/) - LONDON: England ALIYEKUWA kiungo wa Tottenham Hotspur 'Spurs', Jamie O'Hara, amemtaka uongozi wa klabu hiyo kumfuta kazi kocha Igor Tudor kufuatia kipigo kikubwa cha mabao 5-2 dhidi ya Atlético Madrid katika mchezo wa UEFA Champions League. O’Hara, ambaye kwa sasa ni mchambuzi wa redio ya talkSPORT, alionesha kukerwa na kiwango cha Tottenham Hotspur baada ya - [Paris kusaidia wafanyabiashara wanawake](https://spotileo.co.tz/paris-kusaidia-wafanyabiashara-wanawake/) - LOS ANGELES: Mjasiriamali na nyota wa burudani Paris Hilton amezindua mfuko maalumu wa kusaidia wanawake wamiliki wa biashara ndogo waliokumbwa na majanga mbalimbali ikiwemo moto. Hilton ametoa dola 350,000 kuanzisha mfuko huo uitwao ‘Back in Business Recovery Fund’ kwa kushirikiana na taasisi ya GoFundMe. Paris amesema lengo la mfuko huo ni kukusanya angalau dola milioni - [Utabiri washindi wa Oscars 2026 waanza kutikisa Hollywood](https://spotileo.co.tz/utabiri-washindi-wa-oscars-2026-waanza-kutikisa-hollywood/) - LOS ANGELES: Wakati maandalizi ya tuzo za Academy Awards za mwaka 2026 yakifikia kilele, wachambuzi wa filamu wameanza kutoa utabiri wa nani anaweza kuibuka mshindi. Filamu ya One Battle After Another inayoongozwa na Paul Thomas Anderson inaonekana kuwa na nafasi kubwa ya kushinda tuzo ya filamu bora ikiwa na takribani asilimia 60. Katika kipengele cha - [Rais wa soka DR Congo ahukumiwa kifungo cha maisha](https://spotileo.co.tz/mkuu-wa-soka-dr-congo-ahukumiwa-kifungo-cha-maisha-kwa-ufisadi/) - DR CONGO: Rais wa Shirikisho la Soka la Jamhuri ya Congo FECOFOOT, Jean-Guy Blaise Mayolas, amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya ubadhirifu wa fedha za maendeleo ya soka. Mahakama ya jinai mjini Brazzaville ilitoa hukumu hiyo baada ya uchunguzi wa miezi kadhaa kubaini kuwa Mayolas alihusika katika ubadhirifu wa zaidi - [Katy Perry ashindwa kisheria na Katie Perry](https://spotileo.co.tz/katy-perry-ashindwa-kisheria-na-katie-perry/) - AUSTRALIA : Mahakama Kuu ya Australia imetoa ushindi kwa mbunifu wa mavazi wa nchini humo Katie Perry, katika mgogoro wa muda mrefu wa nembo ya biashara dhidi ya nyota wa muziki wa pop kutoka nchini Marekani Katy Perry. Mbunifu huyo alikuwa amemshtaki mwanamuziki huyo maarufu duniani akidai kuwa alikiuka haki ya matumizi ya jina ‘Katie - [Vipimo vya afya vyamliza Dipika Kakar](https://spotileo.co.tz/vipimo-vya-afya-vyamliza-dipika-kakar/) - MUMBAI: Muigizaji wa India Dipika Kakar ameshindwa kuzuia hisia zake alipomwaga machozi wakati mumewe Shoaib Ibrahim alipokumbusha kuhusu vipimo vipya vya damu atakavyofanyiwa baada ya sikukuu ya Eid. Katika video mpya waliyochapisha kwenye YouTube, Shoaib alieleza kuwa Dipika amekuwa akifuata ratiba maalum ya lishe na mazoezi, ikiwemo kuamka mapema asubuhi kwa ajili ya matembezi na - [Meneja Uwanja wa Mkwakwani kusimamishwa kazi](https://spotileo.co.tz/meneja-uwanja-wa-mkwakwani-kusimamishwa-kazi/) - TANGA: Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Tanga, Rajabu Abdallah ameiagiza kamati ya siasa mkoa kumsimamisha kazi meneja wa uwanja wa CCM Mkwakwani kwa madai ya kushindwa kusimamia uwanja huo. Maagizo hayo ameyatoa wakati wa ziara yake ya kutembelea kukagua maendeleo ya uwanja huo Jumatano Machi 11,2026 ambapo ametoa mwezi mmoja kuhakikisha uwanja - [Job afanyiwa upasuaji, Rais Hersi amtia moyo](https://spotileo.co.tz/job-afanyiwa-upasuaji-rais-hersi-amtia-moyo/) - DAR ES SALAAM: Nahodha Msaidizi wa Yanga, Dickson Job, amefanyiwa upasuaji wa goti nchini Afrika Kusini kufuatia majeraha aliyoyapata katika mchezo wa Kariakoo Dabi dhidi ya Simba uliochezwa Machi 1, 2026. Job alipata majeraha hayo katika kipindi cha kwanza baada ya kugongana na kiungo wa Simba, Inno Loemba wakati wakigombea mpira, hali iliyomlazimu kutolewa uwanjani - [Yanga yabaki Njia Panda Kusubiri Uthibitisho](https://spotileo.co.tz/yanga-yabaki-njia-panda-kusubiri-uthibitisho/) - DAR ES SALAAM:KLABU ya Yanga ipo njia panda kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons baada ya hadi sasa kutosafiri kuelekea mkoani Tabora ambako mechi hiyo imepangwa kuchezwa. Awali mchezo huo ulipangwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, lakini Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) ilitangaza kuufungia uwanja huo juzi - [Tiwa Savage: Sina mpango wa kuacha muziki](https://spotileo.co.tz/tiwa-savage-sina-mpango-wa-kuacha-muziki/) - ABUJA: Nyota wa muziki kutoka Nigeria Tiwa Savage amesema hana mpango wa kuacha muziki licha ya kuanzisha taasisi mpya ya kusaidia vipaji chipukizi barani Afrika. Savage alisema wazo la kuanzisha taasisi hiyo lilitokana na uzoefu wake binafsi alipokuwa mwanafunzi wa ufadhili katika Berklee College of Music nchini Marekani. Alieleza kuwa msaada alioupata wakati huo uliibadilisha - [Omotola: Nilikataa mikataba mikubwa ya fedha ili kujilinda](https://spotileo.co.tz/omotola-nilikataa-mikataba-mikubwa-ya-fedha-ili-kujilinda/) - NIGERIA: Muigizaji mkongwe wa Nollywood, Omotola Jalade amesema angekuwa bilionea kama angekubali baadhi ya mikataba yenye faida kubwa iliyowahi kutolewa kwake katika maisha yake ya sanaa ya uigizaji. Akizungumza katika kipindi cha The Afropolitan Show, Omotola alisema alikataa ofa kadhaa za kifedha kwa sababu zilikuwa zinakinzana na maadili na misimamo yake binafsi. Alieleza kuwa ingawa - [Shakira anogewa ziara ya India](https://spotileo.co.tz/shakira-anogewa-ziara-ya-india/) - INDIA: Mwanamuziki maarufu duniani Shakira ameongeza tamasha jingine katika ziara yake ya muziki nchini India kufuatia mahitaji makubwa ya tiketi kutoka kwa mashabiki. Kwa mujibu wa waandaaji, tamasha jipya litafanyika Aprili 11 katika uwanja wa Mahalaxmi Racecourse jijini Mumbai, siku moja baada ya tamasha la kwanza lililopangwa Aprili 10 katika eneo hilo hilo. Mbali na - [Mwanamke anaswa kwa kufyatua risasi karibu na nyumba ya Rihanna](https://spotileo.co.tz/mwanamke-anaswa-kwa-kufyatua-risasi-karibu-na-nyumba-ya-rihanna/) - LOS ANGELES: Polisi wa Los Angeles wamemkamata mwanamke mwenye umri wa miaka 35 baada ya kufyatua risasi karibu na nyumba ya mwanamuziki maarufu Rihanna katika eneo la Beverly Hills huko Marekani. Kwa mujibu wa polisi, tukio hilo lilitokea majira ya saa saba mchana, baada ya kupokea taarifa kuhusu milio ya risasi katika eneo hilo. Mwanamke - [Filamu ya Ranveer Singh yakutana na ushindani sokoni](https://spotileo.co.tz/filamu-ya-ranveer-singh-yakutana-na-ushindani-sokoni/) - INDIA: Filamu mpya ya muigizaji wa India Ranveer Singh inayojulikana kama ‘Dhurandhar 2’’ inatarajiwa kukutana na ushindani mkali katika soko la filamu baada ya kupangwa kuachiwa siku moja na filamu ya Pawan Kalyan, ‘Ustaad Bhagat Singh’. Hapo awali, filamu ya Yash iitwayo ‘Toxic ‘ ilikuwa itolewe Machi 19, lakini iliahirishwa hadi Juni 4, hatua iliyofungua - [Arijit Singh kuacha kuimba nyimbo za filamu](https://spotileo.co.tz/arijit-singh-kuacha-kuimba-nyimbo-za-filamu/) - MUMBAI: Mwanamuziki wa India Madhubanti Bagchi ametoa maoni yake kuhusu uamuzi wa mwanamuziki maarufu Arijit Singh aliyetangaza kuachana na uimbaji wa nyimbo za filamu. Akizungumza katika mahojiano, Bagchi alisema tasnia ya uimbaji wa filamu mara nyingi huwaweka waimbaji katika makundi maalumu na kuwazuia kufanya ubunifu wao binafsi. Alieleza kuwa mara nyingi waimbaji hulazimika kuimba aina - [Alvaro Carreras, Mbappe kuwakosa Manchester City](https://spotileo.co.tz/alvaro-carreras-mbappe-kuwakosa-manchester-city/) - MADRID, Hispania: Klabu ya Real Madrid imethibitisha kuwa beki wake Álvaro Carreras na Kylian Mbappé wataukosa mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City utakaochezwa kesho Jumatano. Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo, Carreras amepata majeraha ya misuli mguu wake wa kulia, hali itakayomlazimu kukaa nje ya uwanja kwa muda ambao - [JESHI Stars, TPDC zashinda Ligi ya Wavu Dar](https://spotileo.co.tz/jeshi-stars-tpdc-zashinda-ligi-ya-wavu-dar/) - DAR ES SALAAM: TIMU ya JESHI Stars imeibuka na ushindi wa seti 3-1 dhidi ya JKT katika mchezo wa Ligi ya Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam uliochezwa Jana. Katika mchezo mwingine wa wanaume, TPDC iliibuka na ushindi wa seti 3-0 dhidi ya Airforce katika pambano lililoonyesha ushindani mkubwa miongoni mwa timu hizo. - [Simba yaifuata Singida BS kibabe](https://spotileo.co.tz/simba-yaifuata-singida-bs-kibabe/) - SINGIDA: Simba imetua mkoani Singida kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Singida Black Stars unaotarajiwa kuchezwa Jumatano ya wiki hii kwenye Uwanja wa Airtel. Akizungumza na SpotiLeo, Msemaji wa Simba, Ahmed Ally, amesema wanautambua ugumu wa mchezo huo lakini wamejipanga kuhakikisha wanapata matokeo mazuri. “Tunajua tunakwenda kucheza na timu imara ambayo - [Dodoma Jiji yajivika mabomu mechi dhidi ya Azam](https://spotileo.co.tz/dodoma-jiji-yajivika-mabomu-mechi-dhidi-ya-azam/) - DODOMA: KLABU YA Dodoma Jiji imesema haiihofii Azam kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa kesho, ikieleza tayari imeshakutana na timu zenye uwezo unaofanana na huo na kupata matokeo chanya. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Kocha Mkuu wa Dodoma Jiji Amani Josiah amesema anaitambua Azam kama timu bora, lakini hawana sababu - [Rais Samia ampatia Bitchuka Sh milioni 10](https://spotileo.co.tz/rais-samia-ampatia-bitchuka-sh-milioni-10/) - DAR ES SALAAM; Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ amemtembelea na kumjulia hali Mwanamuziki nguli nchini, Hassan Bitchuka nyumbani kwake Sinza Mori, jijini Dar es Salaam. Mwana FA alimtembelea mwanamuziki huyo jana na kufikisha salamu kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan za kumtakia kila la heri na kumuombea afya - [16 Bora Shirikisho, mambo hadharani](https://spotileo.co.tz/16-bora-shirikisho-mambo-hadharani/) - BINGWA mtetezi wa Kombe la Shirikisho la CRDB, Yanga atacheza dhidi ya TMA Stars inayoshiriki Ligi ya Championship katika hatua ya 16 bora ya michuano hiyo. Katika michezo mingine, Simba watamenyana na Dodoma Jiji, huku Singida Black Stars wakicheza dhidi ya Mbeya City. Matajiri wa Dar es Salaam, Azam watacheza na Fountain Gate, wakati Namungo - [Rais Samia ampa pole Mzee Zorro](https://spotileo.co.tz/rais-samia-ampa-pole-mzee-zorro/) - DAR ES SALAAM: RAIS Samia Suluhu Hassan amempa mkono wa pole Mwanamuziki mkongwe wa Muziki wa Dansi nchini, Zahir Ally Zorro. Kwa niaba ya Rais Samia, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’, jana alimtembelea mwanamuziki huyo kumjulia hali nyumbani kwake Kigamboni jijini Dar es Salaam. Mwana FA amemkabidhi Mzee - [Loemba: Kila mchezo kwetu ni fainali](https://spotileo.co.tz/loemba-kila-mchezo-kwetu-ni-fainali/) - MCHEZAJI wa Simba SC, Ino Loemba, amesema kwao kila mchezo ni kama fainali jambo linalowafanya wasimdharau mpinzani yeyote wanayekutana naye. Loemba aliyasema hayo baada ya Simba kutinga hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho la CRDB kufuatia kuifunga timu ya Championship B19 mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Jenerali Isamuhyo juzi. Mchezaji huyo - [Messi bado mtamu! rekodi zinatisha](https://spotileo.co.tz/messi-bado-mtamu-rekodi-zinatisha/) - MIAMI: Nahodha wa timu ya taifa ya Argentina na mshambuliaji wa Inter Miami, Lionel Messi, anakaribia kufikisha bao lake la 900 katika soka la kulipwa, hatua itakayoongeza rekodi nyingine kubwa katika maisha yake ya soka. Hii inakuja kufuatia ushindi wa mabao 2-1 walioupata Inter Miami dhidi ya D.C. United katika mchezo wa ligi kuu ya - [YANGA HAICHEKESHI!](https://spotileo.co.tz/yanga-haichekeshi/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga imeonesha ubora wake kwa kishindo baada ya kuibuka na ushindi mkubwa wa mabao 7-1 dhidi ya Polisi Tanzania na kutinga hatua ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho. Mchezo huo ulipigwa jana katika Uwanja wa KMC Complex uliopo jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo, Yanga ilianza kwa kasi - [Zari awaombea waislamu](https://spotileo.co.tz/zari-awaombea-waislamu/) - DAR ES SALAAM: MSANII na Mfanyabiashara, Zari Hassan ‘Zari The Boss Lady’, amefanya dua maalumu waumini wa dini ya kiislamu katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani. Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram, Zari amechapisha picha mpya akiambatanisha na ujumbe wa kuwatakia mema waumini wote wanaotekeleza ibada ya funga. Katika ujumbe huo, - [Mbosso awaandaa mashabiki wake](https://spotileo.co.tz/mbosso-awaandaa-mashabiki-wake/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva Mbwana Kilungi ‘Mbosso’, ameweka wazi kwa mashabiki wake kuwa kwa sasa wanapaswa kutarajia kazi bora zaidi kutoka kwake kila wanaposikia jina lake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo aliandika ujumbe unaoonesha dhamira yake ya kuendelea kutoa muziki wenye ubora na maudhui mazuri kwa mashabiki wake. - [Mobetto amwagia sifa Aziz Ki](https://spotileo.co.tz/mobetto-amwagia-sifa-aziz-ki/) - DAR ES SALAAM: MWANAMITINDO, Hamisa Mobetto, amemwagia sifa mume wake Stephane Aziz Ki, alipokuwa akimtakia heri ya siku yake ya kuzaliwa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mobetto ameandika ujumbe mrefu wa upendo na shukrani akimpongeza mumewe kwa umri mpya, huku akieleza namna anavyothamini uwepo wake katika maisha yake. “Nakupenda sana mume wangu halali wa ndoa - [Mwalimu afungiwa michezo mitatu](https://spotileo.co.tz/mwalimu-afungiwa-michezo-mitatu/) - DAR ES SALAAM : MCHEZAJI wa Simba, Seleman Mwalimu amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kumpiga kiwiko kwa makusudi mchezaji wa Dodoma Jiji Andy Bikoko wakati mchezo wa Ligi Kuu uliokutanisha timu hizo. Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 41:5(5.2) ya Ligi Kuu kuhusu - [Waamuzi Dabi ya Kariakoo vilio](https://spotileo.co.tz/waamuzi-dabi-ya-kariakoo-vilio/) - DAR ES SALAAM: MWAMUZI Msaidizi namba moja (1) wa mchezo dabi ya Simba na Yanga, Kassim Mpanga kutoka Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita (6) kwa kosa la kushindwa kutafsiri vema sheria za mpira wa miguu ambapo katika dakika ya 70 ya mchezo alikataa bao halali la klabu ya Simba kwa kile alichoonesha kwamba kulikuwa - [Simba, Yanga zatozwa faini](https://spotileo.co.tz/simba-yanga-zatozwa-faini/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Simba imetozwa faini ya jumla Sh milioni 20 na Yanga Sh milioni tano kutokana na makosa tofauti katika mechi mbili tofauti ikiongozwa na Dabi iliyochezwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa New Amaan Zanzibar. Simba ilitozwa sh milioni tano kwa kosa la kuingia kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar kupitia mlango usio - [Shabiki aiponza Madrid yatozwa faini](https://spotileo.co.tz/shabiki-aiponza-madrid-yatozwa-faini/) - MADRID: SHIRIKISHO la Soka Barani Ulaya (UEFA) limeitoza faini Real Madrid pamoja na kuamuru kufungwa kwa muda sehemu ya viti katika Uwanja wa Santiago Bernabéu baada ya shabiki mmoja kuonekana akifanya ishara inayofanana na saluti ya Nazi. Shirikisho hilo la soka barani Ulaya limetangaza kuwa Real Madrid italazimika kulipa faini ya euro 15,000 (takribani pauni - [Shimmuta yaikabidhi BMT sera ya Michezo](https://spotileo.co.tz/shimmuta-yaikabidhi-bmt-sera-ya-michezo/) - DAR ES SALAAM: MWENYEKITI wa Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) Roselyne Massam, leo amekabidhi rasmi Sera ya Michezo kwa Wafanyakazi “Sports for the Well-Being of Workers” kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Neema Msitha yenye lengo la kuimarisha sekta hiyo kwa wanachama wake - [Ulevi wamponza Britney Spears](https://spotileo.co.tz/ulevi-wamponza-britney-spears/) - NEWYORK: MWANAMUZIKI maarufu wa Marekani Britney Spears amekamatwa na polisi katika Jimbo la California baada ya kuripotiwa kuendesha gari kwa hatari barabarani kwa takribani saa moja kabla ya kusimamishwa na kukamatwa kwa tuhuma za kuendesha gari akiwa amelewa. Kwa mujibu wa taarifa za polisi, Spears mwenye umri wa miaka 44 alikamatwa majira ya saa 3:30 - [Fury amuonya mwanawe Prince John](https://spotileo.co.tz/fury-amuonya-mwanawe-prince-john/) - BANGKOK: BINGWA wa zamani wa ngumi wa uzito wa juu duniani, Tyson Fury amesema mwanawe mkubwa, Prince John James, ana ndoto ya kufuata nyayo zake na kuwa bondia wa kulipwa siku za usoni. Fury, ambaye ni baba wa watoto saba, amesema mwanawe huyo mwenye umri wa miaka 15 tayari ameanza kujifunza masuala ya ndondi na - [Ibenge alia na Uwanja wa Sokoine](https://spotileo.co.tz/ibenge-alia-na-uwanja-wa-sokoine/) - MBEYA: KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema ni vigumu kucheza mpira mzuri kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya kutokana na hali ya uwanja huo, baada ya timu yake kutoka sare ya bila kufungana na Tanzania Prisons jana. Akizungumza baada ya mchezo huo, Ibenge amesema aina ya uwanja huo inafanya timu ishindwe kucheza mpira - [Simba, B19 mchezo wa jasho na heshima](https://spotileo.co.tz/simba-b19-mchezo-wa-jasho-na-heshima/) - DAR ES SALAAM: WEKUNDU wa Msimbazi Simba kesho Jumamosi watashuka dimbani kuikaribisha timu ya Championship ya B19 katika mchezo wa Kombe la Shirikisho la CRDB utakaochezwa kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo Dar es Salaam. Kuelekea katika mchezo huo wa mtoano hatua ya 32 bora, Kocha Mkuu wa Simba Steven Barker amesema anaamini utakuwa mchezo - [Okello: Nimefurahi kufungua akaunti ya mabao](https://spotileo.co.tz/okello-nimefurahi-kufungua-akaunti-ya-mabao/) - SINGIDA: KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Allan Okello, ameeleza furaha yake baada ya kufunga bao lake la kwanza kwa timu hiyo katika ushindi wa mabao 3-0 walioupata dhidi ya Singida Black Stars. Okello, ambaye alijiunga na Yanga katika dirisha dogo la usajili akitokea Vipers ya Uganda, alikuwa miongoni mwa wafungaji katika ushindi huo uliopatikana jana ugenini - [Pedro awapa tano wachezaji wake](https://spotileo.co.tz/pedro-awapa-tano-wachezaji-wake/) - SINGIDA: KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, ameipongeza timu yake kwa kuonesha kujituma na kujitoa kwa kiwango kikubwa baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Singida Black Stars. Akizungumza baada ya mchezo huo wa Ligi Kuu uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Airtel jana, Goncalves amesema kikosi chake kilionesha nidhamu, kujitoa na umoja - [Wafcon 2026 yasogezwa mbele](https://spotileo.co.tz/wafcon-2026-yasogezwa-mbele/) - CAIRO: SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), limesogeza mbele mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON 2026) ikiwa zimesalia siku 12 kabla ya mashindano hayo kuanza nchini Morocco. Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika kuanzia Machi 17 hadi Aprili 3 mwaka huu, sasa yatafanyika kuanzia Julai 25 hadi Agosti 16, mwaka huu. - [Tottenham “Ni Janga”’](https://spotileo.co.tz/tottenham-ni-janga/) - LONDON: MSHAMBULIAJI wa kulia wa Tottenham Hotspur, Pedro Porro, ameeleza kuwa msimu wa klabu hiyo katika Ligi Kuu ya England ni “janga” huku akiweka lawama kwa majeraha na ukosefu wa wachezaji wa akiba. Tottenham, ambayo kwa sasa haina wachezaji 10 kutokana na majeraha, haijashinda mechi ya ligi katika michezo 10 iliyopita na ipo nafasi ya - [Loemba akabidhiwa gari, wengine kufuata](https://spotileo.co.tz/loemba-akabidhiwa-gari-wengine-kufuata/) - DAR ES SALAAM : KIUNGO mshambuliaji wa Simba SC, Inno Loemba, amekabidhiwa gari aina ya Toyota Crown New Model na kampuni ya Jayerutty Investment moja ya wadhamini wa klabu hiyo. Loemba ni miongoni mwa wachezaji wa Simba waliosajiliwa kwa ushirikiano na kampuni hiyo, kufuatia makubaliano ya kimkataba kati yao na Simba SC ambayo yanaitaka kusaidia - [Lizer Classic: Acheni kuchanganya mambo](https://spotileo.co.tz/lizer-classic-acheni-kuchanganya-mambo/) - DAR ES SALAAM: Muandaaji maarufu wa muziki nchini, Lizer Classic, amesema kuwa uwekezaji unaofanywa kwa wasanii katika tasnia ya muziki unalenga kazi zao za muziki pekee na si maisha yao binafsi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Lizer Classic ameandika ujumbe akieleza kuwa wasanii wengi husahau mipaka iliyopo kati ya uwekezaji wa muziki na maisha binafsi. - [Arbeloa: Haijulikani lini Mbappe atarudi kucheza](https://spotileo.co.tz/arbeloa-haijulikani-lini-mbappe-atarudi-kucheza/) - MADRID: KOCHA wa Real Madrid, Álvaro Arbeloa, amesema hali ya Kylian Mbappé imeanza kuimarika baada ya kuumia goti la kushoto licha ya kutokuwa muda sahihi wa nyota huyo kurejea. Mbappé amekuwa nje ya uwanja kutokana na kukabiliwa na majeraha hayo yanayomsumbua tangu Desemba. “Ninasalimiana naye kila siku,” Arbeloa alisema katika mkutano na waandishi wa habari. - [Maguire agoma kutoa hongo](https://spotileo.co.tz/maguire-agoma-kutoa-hongo/) - ATHENS: MLINZI wa timu ya taifa ya England na Manchester United, Harry Maguire, amekataa kutoa hongo ya Pauni 43,500 kwa polisi wa Ugiriki ili kesi yake ya shambulio iishe, siku chache kabla ya kutolewa hukumu ya miezi 15 iliyosimamishwa. Maguire, 33, alikutwa na hatia ya shambulio dogo, baada ya kupigana akiwa likizo ya kifamilia Agosti - [Simba haiwachukulii poa B19](https://spotileo.co.tz/simba-haiwachukulii-poa-b19/) - DAR ES SALAAM : WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamesema sare waliyopata kwenye dabi dhidi ya Yanga umeipa timu hiyo kujiamini na kurejesha heshima, huku akisisitiza kuwa sasa nguvu zao zinaelekezwa katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho la CRDB dhidi ya timu ya Championship B19. Akizungumzia mchezo huo Dar es Salaam leo, Meneja Habari na - [Singida BS yamrejesha kundini Aucho](https://spotileo.co.tz/singida-bs-yamrejesha-kundini-aucho/) - SINGIDA: KLABU ya Singida Black Stars imetangaza kumsamehe na kumrejesha kundini kiungo wake Khalid Aucho. Awali, klabu hiyo ilitangaza kumfungia mchezaji huyo miezi mitatu kwa utovu wa nidhamu na utoro kazini. Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo leo kwa vyombo vya habari, kufuatia barua ya kukiri na kuomba radhi kwa makosa kutoka kwa mchezaji - [Tanzania kupanua utambuzi wa ujuzi sekta bunifu](https://spotileo.co.tz/tanzania-kupanua-utambuzi-wa-ujuzi-sekta-bunifu/) - MOROGORO: TANZANIA imeanza rasmi mchakato wa kupanua mfumo wa utambuzi wa ujuzi nje ya elimu rasmi ili kuwanufaisha vijana na wanawake wanaojihusiha kwenye sekta ya utamaduni na ubunifu. Hatua hiyo inalenga kuwatoa vijana katika ajira zisizo rasmi na kuwaingiza katika ajira zenye staha na ulinzi wa kisheria. Mchakato huo, uliyowakutanisha wawakilishi 42 kutoka wizara zinazoshughulikia - [B19 yajipanga kuing’oa Simba Kombe la Shirikisho](https://spotileo.co.tz/b19-yajipanga-kuingoa-simba-kombe-la-shirikisho/) - DAR ES SALAAM: TIMU ya Championship ya B19 imepania mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Simba ikisema imeweka fungu maalum ili kuiondosha Simba katika hatua hiyo ya 32 bora. Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa timu ya B19, Felix Makota, amesema amesema wanautambua ugumu wa mchezo huo dhidi ya moja ya timu - [Tambwe: Yanga na Singida wote ni mafundi](https://spotileo.co.tz/tambwe-yanga-na-singida-wote-ni-mafundi/) - SINGIDA : MENEJA wa timu ya Singida Black Stars na mchezaji wa zamani wa Simba na Yanga, Amis Tambwe, amesema kikosi chao kiko tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Yanga utakaopigwa kesho, akisisitiza kuwa ni pambano la “mafundi” litakalojaa burudani ya soka safi. Tambwe amesema mkoani hapa kuwa wanautazama mchezo huo kama fursa - [Prisons: Hatuwaogopi Azam tunawaheshimu](https://spotileo.co.tz/prisons-hatuwaogopi-azam-tunawaheshimu/) - MBEYA: KOCHA Mkuu wa Tanzania Prisons, Shadrack Nsajigwa, amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC huku akisisitiza kuwa wanawaheshimu wapinzani wao lakini hawataingia uwanjani kwa hofu. Akizungumza jijini Mbeya kuelekea katika mchezo huo utakaopigwa kesho kwenye Uwanja wa Sokoine, Nsajigwa amesema Azam ni timu yenye uzoefu na - [Wadau wajadili sanaa zenye staha](https://spotileo.co.tz/wadau-wajadili-sanaa-zenye-staha/) - MOROGORO :WAKATI sekta ya sanaa na ubunifu ikiendelea kukua kwa kasi na kutoa ajira kwa maelfu ya vijana nchini, wadau wameonya kuwa bila kuwepo kwa kazi zenye staha, mchango wake katika kukuza uchumi wa Taifa unaweza kubaki kwenye takwimu zisizogusa maisha halisi ya wasanii. Kauli hiyo imetolewa katika warsha ya siku tatu ya kusambaza matokeo - [UNI challenge yaibuka kidedea](https://spotileo.co.tz/uni-challenge-yaibuka-kidedea/) - MECHI ya kirafiki iliyochezwa hivi karibuni kati ya Timu ya Guardian of the Peak na Uni Challenge imehitimishwa kwa timu ya Uni Challenge kutoka kifua mbele, ambapo timu hiyo ilijinyakulia Kombe la Guardian of the Peak Season Two, baada ya ushindi wa mikwaju ya penalti. Katika dakika 90 za mchezo huo, timu hizo zilitoshana nguvu - [Gwajima: Wanawake wapewe nafasi michezo na biashara](https://spotileo.co.tz/gwajima-wanawake-wapewe-nafasi-michezo-na-biashara/) - DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk Dorothy Gwajima, ametoa wito wa kuendelea kumpa nafasi mwanamke kushiriki kikamilifu kwenye majukwaa ya michezo na biashara akisisitiza mchango wake katika uchumi na maendeleo ya familia. Akizungumza katika mbio za riadha za kuadhimisha miaka 20 ya Tanzania Women Chamber of Commerce - [Ibenge: Uwanja ulituzuia kucheza Vizuri](https://spotileo.co.tz/ibenge-uwanja-ulituzuia-kucheza-vizuri/) - MWANZA: KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema sare ya mabao 2-2 dhidi ya Pamba FC si matokeo mabaya, licha ya kukiri timu yake kuanza vibaya kutokana na Uwanja. Akizungumza baada ya mchezo huo uliochezwa jana, Ibenge amesema walianza kwa presha kubwa kutokana na mazingira ya uwanja ambayo hayakuruhusu timu yake kucheza soka lao - [Dodoma itasimama kupisha Bunge Marathon](https://spotileo.co.tz/dodoma-itasimama-kupisha-bunge-marathon/) - DAR ES SALAAM: MWENYEKITI wa Bunge Marathon na Bunge Bonanza, Festo Sanga, ametangaza kuwa mbio za Bunge Marathon msimu wa tatu zinatarajiwa kufanyika Aprili 18, 2026 katika Viwanja vya Jamhuri mkoani Dodoma. Akizungumza na waandishi wa habari Februari 28, 2026 jijini Dar es Salaam, Sanga amesema maandalizi ya tukio hilo yamekamilika na lengo kuu ni - [Arsenal kukutana na Leverkusen hatua ya 16](https://spotileo.co.tz/arsenal-kukutana-na-leverkusen-hatua-ya-16/) - NYON:ARSENAL wamepangwa kukutana na Bayer Leverkusen katika hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2025/26, droo ambayo tayari imeanza kuvuta hisia kutokana na stori inayomuhusu Kai Havertz. Havertz, ambaye ni zao la akademi ya Leverkusen, alipandishwa kikosi cha kwanza mwaka 2016 kabla ya kuhamia Chelsea majira ya kiangazi 2020. Mwaka 2023 akasajiliwa na - [Barcelona kuumana na Newcastle raundi ya 16](https://spotileo.co.tz/barcelona-kuumana-na-newcastle-raundi-ya-16/) - NYON:KLABU ya BARCELONA watakutana na Newcastle United katika hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya droo kufanyika leo kwenye makao makuu ya UEFA mjini Nyon, Uswisi. Barça walikuwa na uwezekano wa kukutana na timu mbili ambazo ni Newcastle au PSG, na hatimaye wakapangwa dhidi ya klabu hiyo ya Ligi Kuu England. - [Ni Man City na Real Madrid tena!](https://spotileo.co.tz/ni-man-city-na-real-madrid-tena/) - NYON:DROO ya hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imethibitisha pambano lingine kubwa kati ya Manchester City na Real Madrid katika hatua ya 16 bora. Huu ni mchuano ambao sasa umegeuka kuwa kama “fainali kabla ya fainali” kutokana na historia yao ya hivi karibuni. Tangu mwaka 2020, timu hizi zimekutana mara kwa mara katika - [Khalid Aucho afunguka Sakata la kufungiwa](https://spotileo.co.tz/khalid-aucho-afunguka-sakata-la-kufungiwa/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO wa Singida Black Stars, Khalid Aucho, amevunja ukimya kufuatia uamuzi wa klabu yake kumfungia kwa muda wa miezi mitatu kwa tuhuma za utovu wa nidhamu. Kupitia ujumbe wake, Aucho ameeleza kuwa katika maisha yake yote ya soka amekuwa akijiheshimu na kuzingatia taaluma, akidai hajawahi kuhusishwa na tukio lolote la utovu wa - [BASATA yazindua “Rising Star Award” kukuza vipaji vya muziki nchini](https://spotileo.co.tz/basata-yazindua-rising-star-award-kukuza-vipaji-vya-muziki-nchini/) - DAR ES SALAAM: BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limezindua rasmi programu mpya ya BASATA Rising Star Award, jukwaa maalumu litakalolenga kuibua na kukuza vipaji vya wanamuziki chipukizi nchini. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa BASATA, Kelvin Stansilausi, amesema hii ni hatua muhimu katika safari ya kuimarisha sekta ya - [Dulla Makabila akanusha mahusiano na mama wa Hamisa Mobetto](https://spotileo.co.tz/dulla-makabila-akanusha-mahusiano-na-mama-wa-hamisa-mobetto/) - DAR ES SALAAM: Msanii wa Bongo Fleva, Dulla Makabila, ameibuka na kuvunja ukimya kuhusu taarifa zilizokuwa zikisambaa mitandaoni zikimdai aliwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mama wa Hamisa Mobetto. Dulla amesema amewahi kusikia tetesi hizo lakini hazina ukweli wowote, akisisitiza kuwa anamuheshimu sana mama mzazi wa Hamisa na hawezi kufanya jambo la namna hiyo. - [Dabi ya Kariakoo takwimu zinaibeba Yanga, Simba presha tupu](https://spotileo.co.tz/dabi-ya-kariakoo-takwimu-zinaibeba-yanga-simba-presha-tupu/) - ZANZIBAR:KIPUTE cha watani wa jadi kati ya Yanga na Simba kinatarajiwa kupigwa Jumapili, Machi 01, 2026, kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar kuanzia saa 2:15 usiku. Mchezo huo unakuja katika kipindi ambacho Yanga wanaingia wakiwa na rekodi bora dhidi ya watani wao, baada ya kushinda mechi sita mfululizo za mwisho za Dabi ya Kariakoo. - [Clement Mzize kufanyiwa upasuaji leo](https://spotileo.co.tz/clement-mzize-kufanyiwa-upasuaji-leo/) - JOHANNESBURG: MSHAMBULIAJI wa YANGA Clement Mzize, anatarajiwa kufanyiwa upasuaji leo kufuatia changamoto ya kiafya inayomkabili. Taarifa za kufanyiwa upasuaji kwake zimewekwa wazi na aliyekuwa mtaalam wa masuala ya misuli na utimamu wa mwili wa Yanga, Seroto Sekhwela maarufu kwa jina la SK Seroto, aliyewapokea nchini Afrika Kusini. Kupitia ujumbe wake, Sekhwela alionesha mshikamano na upendo - [Singida black Stars yamfungia Khalid Aucho](https://spotileo.co.tz/singida-black-stars-yamfungia-khalid-aucho/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Singida Black Stars SC imetangaza kumfungia miezi mitatu kiungo Khalid Aucho kwa kosa la utovu wa nidhamu na kuchelewa kazini. Aidha, imemsimamisha kazi kipa Amas Obasogie kwa kipindi cha miezi mitatu ili kuruhusu uchunguzi wa tuhuma zinazohusiana na upangaji wa matokeo. Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo iliyolewa leo - [Frenkie De Jong nje wiki 6](https://spotileo.co.tz/frenkie-de-jong-nje-wiki-6/) - BARCELONA:KLABU ya BARCELONA wamepata pigo zito baada ya Frenkie de Jong kupata majeraha yatakayomuweka nje kwa takribani wiki tano hadi sita. Kiungo huyo wa miaka 28 alilazimika kusitisha mazoezi baada ya kuhisi maumivu makali, na vipimo vya kitabibu vimeonesha kuwa ameumia misuli ya nyuma ya paja la mguu wa kulia. Katika taarifa rasmi, klabu imethibitisha - [Fahyma: “Nilimshonea Wema gauni, nikaishia getini!”](https://spotileo.co.tz/fahyma-nilimshonea-wema-sepetu-gauni-maalum-nikaishia-getini/) - DAR ES SALAAM, Mwanamitindo na mfanyabiashara, Fahyma 'Fahyvanny', ambaye pia ni mzazi mwenza wa msanii wa Bongo Fleva Rayvanny, ameweka wazi simulizi ya tukio lililowahi kumkuta alipokusudia kumpatia zawadi staa wa filamu Tanzania, Wema Sepetu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Fahyma ameeleza kuwa aliwahi kushona gauni maalum kwa ajili ya Wema Sepetu kama ishara ya - [Bwire: Yanga walituchanganya, Dube ni mwanariadha](https://spotileo.co.tz/bwire-yanga-walituchanganya-dube-ni-mwanariadha/) - DAR ES SALAAM : Ofisa Habari wa JKT Tanzania, Masau Bwire, amesema kasi na mbio za mshambuliaji Dube zimewapa wakati mgumu vijana wake, akidai ni kama ameandaliwa rasmi kuwa nwanariadha kutokana na namna alivyokuwa akikimbia kuwania mipira mirefu. Kauli hiyo ni baada ya timu yake kupoteza kwa kichapo cha mabao 5-0 dhidi ya Yanga katika - [Wolper awaza kesho ya wanae](https://spotileo.co.tz/wolper-awaza-kesho-ya-wanae/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa filamu za nchini, Jackline Wolper amesema hana haraka ya kutafuta maisha ya kifahari, kwani anachokipa kipaumbele ni watoto wake kupata malezi na msingi imara wa maisha yao ya baadaye. “Sijawahi kufikiri kuwa nikifikisha umri fulani niwe na maisha ya namna fulani au ya kifahari. Kwa sasa nina watoto wananiangalia mimi,” - [Kocha Yanga alia ugumu wa ratiba](https://spotileo.co.tz/kocha-yanga-afurahia-ushindi-alia-ratiba-ngumu/) - DAR ES SALAAM : KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Gonçalves, amesema ushindi walioupata haukuwa rahisi licha ya matokeo kuonekana makubwa, akisisitiza umuhimu wa umoja wa kikosi kizima pamoja na mchango wa wachezaji wa akiba. Kauli yake hiyo imekuja baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa - [Pedro ampakulia 'minyama' Shekhan](https://spotileo.co.tz/pedro-ampakulia-minyama-shekhan/) - DAR ES SALAAM : KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Gonçalves, amemmwagia sifa kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Shekhan Ibrahim kuwa ni miongoni mwa wachezaji wenye vipaji vikubwa ndani ya kikosi hicho. Pamoja na sifa hizo, amemtaka Shekhan kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia kiwango cha juu zaidi. Nyota huyo alikuwa ni miongoni mwa wachezaji - [Ibenge awapa heko wachezaji wake](https://spotileo.co.tz/ibenge-awapa-heko-wachezaji-wake/) - DAR ES SALAAM : KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema ameridhishwa na ushindi wa mabao 3-0 walioupata dhidi ya Mtibwa Sugar jana kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi. Ibenge amewapongeza wachezaji wake kwa kutengeneza nafasi nyingi na kucheza soka la kuvutia. Aidha, Ibenge amesema timu yake imeonesha uimara mkubwa kwa kufunga mabao matatu - [Sowah bado hakijaeleweka Simba](https://spotileo.co.tz/sowah-bado-hakijaeleweka-simba/) - DODOMA: MENEJA wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema mshambuliaji Jonathan Sowah yupo nje ya kikosi na hatma yake ya kusafiri na timu kuelekea Zanzibar bado haijafahamika. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma jana baada ya mchezo dhidi ya Dodoma Jiji, Ally ameeleza kuwa mara baada ya mchezo dhidi ya - [Simba na kibonde, Yanga mwendo wa wanajeshi](https://spotileo.co.tz/simba-na-kibonde-yanga-mwendo-wa-wanajeshi/) - DAR ES SALAAM : DROO ya hatua ya 32 bora ya Kombe la Shirikisho la CRDB 2025/2026 imetangazwa leo, ambapo Simba, Yanga na Azam FC zimeangukia kwa wapinzani wanaoshiriki ligi ya Championship. Katika droo hiyo iliyochezeshwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Azam Media, Simba inatarajia kucheza na kibonde kwenye Championship B19 - [Nancy Sumari aipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa](https://spotileo.co.tz/nancy-sumari-aipeperusha-bendera-ya-tanzania-kimataifa/) - DAR ES SALAAM: Miss Tanzania 2006 na Miss World Africa, ambaye kwa sasa ni mbunifu wa teknolojia, Nancy Sumari, ameendelea kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa baada ya kushinda tuzo ya Ubunifu kutoka Zero Project nchini Austria. Nancy ametunukiwa tuzo hiyo kwa kutambua mchango wake kupitia Taasisi ya JengaHub katika kuendeleza elimu jumuishi kwa watoto - [Uwoya: “Usinichokoze, siongei ngumi zinaruka!”](https://spotileo.co.tz/uwoya-usinichokoze-siongei-ngumi-zinaruka/) - DAR ES SALAAM :MSANII wa filamu za Bongo Movie, Irene Uwoya, amesema kuwa huwa hapendi kukaa kimya anapokasirishwa, akieleza kuwa hasira zake ziko karibu na mara nyingi huishia kutumia nguvu pale anapochokozwa kupitiliza. Akizungumza kuhusu tabia yake, Uwoya amesema kuwa si mtu wa kubishana kwa maneno kwa muda mrefu, kwani akishajibiwa mara kadhaa hushindwa kuendelea - [Rakeem wa Jux atimiza miezi sita, amchagua baba yake](https://spotileo.co.tz/rakeem-wa-jux-atimiza-miezi-sita-amchagua-baba-yake/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Juma Mkambala (Jux), pamoja na mke wake Priscilla, wanasherehekea kutimia kwa miezi sita tangu kuzaliwa kwa mtoto wao, Rakeem. Kupitia kurasa zao za Instagram, familia hiyo imechapisha video inayoonesha tukio la furaha wakiwa pamoja na mtoto wao. Katika video hiyo, Rakeem anaonekana akicheza mchezo wa kuchagua kati ya - [Samatta mwili Ulaya, moyo upo Tanzania](https://spotileo.co.tz/samatta-mwili-ulaya-moyo-upo-tanzania/) - DAR ES SALAAM; Baridi ya jioni, ikiambatana na mvua za barafu barani Ulaya humkuta akipambana kwenye viwanja vya kisasa, taa zikimulika kila hatua yake. Ajabu iliyoje ndani ya kifua chake, kuna joto la Bahari ya Hindi, sauti za Mbagala, na ndoto za vijana wa Kitanzania. Huyo ndiye Mbwana Ally Samatta, nahodha wa Timu ya Taifa - [Rayvanny anatukumbusha kitu kuhusu maisha!](https://spotileo.co.tz/rayvanny-anatukumbusha-kitu-kuhusu-maisha/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Raymond Mwakyusa 'Rayvanny', amewaachia mashabiki wake na gumzo mitandaoni baada ya kuchapisha picha yake ya zamani na kuambatanisha ujumbe wa kutia moyo kuhusu safari ya maisha. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo aliandika: “Ukifumba macho jione mwingine, sio yule yule wa jana!!! Kwa (On God) - [Neo Maema akoshwa na umoja Simba](https://spotileo.co.tz/neo-maema-akoshwa-na-umoja-simba/) - DODOMA: UMOJA na morali kubwa ndani ya kikosi cha Simba ndivyo vinavyompa furaha zaidi kiungo Neo Maema, akiamini kuwa mshikamano wa timu hiyo ndiyo silaha muhimu katika safari ya kusaka ubingwa msimu huu. Maema amesema pamoja na kufurahia mwenendo mzuri wa timu, anaona kitu cha pekee ni namna wachezaji wanavyokuwa kitu kimoja ndani na nje - [Duwaa atema madini!](https://spotileo.co.tz/duwaa-atema-madini/) - DAR ES SALAAM: MSANII na Mtengeneza maudhui anayefanya vizuri kwa sasa, Abigael Duwaa, amewakumbusha wanajamii umuhimu wa kuwatunza wazazi wao wakiwa bado hai, akisisitiza kuwa fursa hiyo ni ya kipekee na haijirudii. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Abigael ameandika ujumbe wenye kugusa hisia za wengi akisema: “Tutunze wazazi wetu pindi wanapokuwa hai, maana - [Yanga, JKT wanaingia vita ya uongozi](https://spotileo.co.tz/yanga-jkt-wanaingia-vita-ya-uongozi/) - DAR ES SALAAM: YANGA na JKT Tanzania wanaingia kwenye vita ya uongozi watakapokutana kesho katika mchezo wa Ligi Kuu utakaochezwa kwenye Uwanja wa KMC . JKT ndiye kinara kwa pointi 28 katika michezo 16 tofauti ya pointi tatu dhidi ya Yanga ambaye pia, yuko nyuma michezo saba. Huenda wanajeshi wakashushwa kama wataruhusu kufungwa maana yake - [Zaylissa humbuambii kitu kwenye stara](https://spotileo.co.tz/zaylissa-humbuambii-kitu-kwenye-stara/) - DAR ES SALAAM:MUIGIZAJI wa filamu za Bongo, ambaye ni bibi harusi Zaylissa Said, amezua mjadala mzito mitandaoni baada ya kuzungumzia suala la uvaaji wa stara na namna unavyoweza kumpendezesha mtu kuliko mavazi ya kuacha maungo wazi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zaylissa alishiriki picha akiwa amevalia mavazi ya heshima na kuambatanisha ujumbe uliowavutia wengi. “Hivi - [Mtibwa Sugar yahamishia hasira kwa Azam](https://spotileo.co.tz/mtibwa-sugar-yahamishia-hasira-kwa-azam/) - DAR ES SAAAM: MTIBWA Sugar imesema hasira zao za kupoteza mchezo uliopita wanazihamishia katika mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi. Wakatamiwa hao wa Morogoro wametoka kupoteza dhidi ya Singida Black Stars mabao 3-1 mwishoni mwa wiki na sasa wana kibarua Kizito cha kusaka pointi - [Ahmed: Dodoma Jiji ni mziki mnene](https://spotileo.co.tz/ahmed-dodoma-jiji-ni-mziki-mnene/) - DODOMA: KLABU ya Simba imesema inatarajia kukumbana na upinzani mkubwa dhidi ya Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kesho. Imesema mpinzani huyo ana ubora wa juu kuliko waliokutana nao katika mchezo uliopita wa Tanzania Prisons walioibuka na ushindi wa mabao 2-0. Akizungumza kuelekea pambano hilo, - [Pipi Jojo aachana na Chief Godlove](https://spotileo.co.tz/pipi-jojo-aachana-na-chief-godlove/) - DAR ES SALAAM: MENEJA na Mkurugenzi wa Chief Loot Music, Chief Godlove, ametangaza rasmi kuvunjwa kwa mkataba wa usimamizi kati ya lebo hiyo na msanii Pipi Jojo, hatua inayomfanya msanii huyo kuwa huru kuanzia leo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Chief Godlove ameweka wazi kuwa makubaliano ya kusimamia kazi za Pipi Jojo yamefikia tamati rasmi - [Wavu Dar kufanyika Februari 28](https://spotileo.co.tz/wavu-dar-kufanyika-februari-28/) - DAR ES SALAAM: TIMU 20 za Seria A na B kwa wanawake na wanaume zinatarajia kushiriki Ligi ya Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam itakayoanza kutimua vumbi Februari 28 mwaka huu katika viwanja vya Kampala International University Tanzania (KIUT). Katibu wa Chama cha Wavu Dar es Salaam DAREVA, Clement Athanas, amesema kuwa kati - [Baraka The Prince amkataa Dudu Baya](https://spotileo.co.tz/baraka-the-prince-amkataa-dudu-baya/) - DAR ES SALAAM: Msanii wa Bongo Fleva, Baraka The Prince, amezua mjadala mzito baada ya kutoa kauli kali kuhusu wasanii wawili wakubwa kutoka Mwanza, Farid Kubanda (FID Q) na Godfrey Tumaini (Dudu Baya), akieleza mtazamo wake kuhusu nani ana heshima na mamlaka ya kimuziki katika Jiji la Mwanza. Akizungumza kupitia mahojiano na mitandao ya kijamii, - [Mr Blue aweka tiki kwa Marioo mbele ya Mbosso](https://spotileo.co.tz/mr-blue-aweka-tiki-kwa-marioo-mbele-ya-mbosso/) - DAR ES SALAAM: MKALI wa muziki wa hip hop nchini, Khery Sameer Rajab (Mr Blue), amesema wazi kuwa kati ya wasanii wawili wakubwa wa Bongo Fleva, Omary Mwanga (Marioo) na Mbosso Khan, angechagua kumsapoti Marioo akieleza kuwa ni msanii jasiri kwa kuthubutu kushindana na Mbosso. Akizungumza katika mahojiano yake, Mr Blue amesema kuwa Mbosso ana - [Wolper aibua mjadala kuhusu malezi ya watoto](https://spotileo.co.tz/wolper-aibua-mjadala-kuhusu-malezi-ya-watoto/) - DAR ES SALAAM: STAA wa filamu nchini, Jacqueline Wolper, ameibua mjadala mpana mitandaoni baada ya kuweka wazi hisia zake za ndani kuhusu dini ya Kiislamu, akieleza kuvutiwa kwake kwa kiasi kikubwa na imani hiyo pamoja na matamanio ya kuona watoto wake wakikua wakiifahamu na kuiheshimu. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Wolper amefunguka kuwa - [Ibenge: Tunahitaji kushinda kila mchezo](https://spotileo.co.tz/ibenge-tunahitaji-kushinda-kila-mchezo/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema lengo kuu la timu hiyo katika michuano ya Kombe la Shirikisho la CRDB ni kushinda kila mchezo ulioko mbele yao na kufuzu hatua zinazofuata licha ya ushindani kuwa mkubwa na muda kuwa mfupi. Akizungumza baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Endumenti FC - [Muigizaji mkongwe Tom Noonan amefariki Dunia](https://spotileo.co.tz/muigizaji-mkongwe-tom-noonan-amefariki-dunia/) - MUIGIZAJI mkongwe wa filamu za Hollywood, Tom Noonan, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 74. Kifo chake kimethibitishwa na mtayarishaji wa filamu Fred Dekker kupitia chapisho la Facebook alilolitoa Februari 18, akieleza kuwa Noonan alifariki Februari 14, 2026. Noonan alikuwa maarufu kwa kuigiza wahusika wenye mvuto wa kipekee, wa kina na mara nyingi waliokuwa - [Tabitha ateuliwa Singida Black Stars](https://spotileo.co.tz/tabitha-ateuliwa-singida-black-stars/) - DAR ES SALAAM :UONGOZI wa Singida Black Stars, umetangaza kumteua Tabitha Kidawawa kuwa Mkurugenzi wa Masoko na Mashindano kuanzia leo Februari 19, 2026. Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mtendaji Mkuu Jonathan Kassano, Kidawawa ana uzoefu wa kutumikia klabu mbalimbali hapa nchini hivyo wana imani na uzoefu wake. - [Geay: Nipo tayari kwa mbio za Daegu](https://spotileo.co.tz/geay-nipo-tayari-kwa-mbio-za-daegu/) - DAR ES SALAAM: MWANARIADHA nyota wa Tanzania, Gabriel Geay, ameweka wazi kuwa yupo tayari kutetea heshima yake katika mbio za kimataifa za Daegu Marathon zitakazofanyika Jumapili ya wiki hii nchini Korea Kusini. Geay alithibitisha kurejea huko katika mazungumzo na Spotileo akisema amejipanga vizuri kwenda kushindana na kutetea nafasi hiyo kwa mara nyingine. Mbio hizo zinatarajiwa - [Siri ya mabao ya Buba iko kwa Mama yake](https://spotileo.co.tz/siri-ya-mabao-ya-buba-iko-kwa-mama-yake/) - DAR ES SALAAM: WINGA mpya wa Yanga Buba Jammeh amesema alitabiri kufunga katika mchezo wake wa kwanza baada ya kuzungumza na mama yake kabla ya mechi, aliyempa ushuri uliomtia nguvu ya kuifungia timu yake mabao mawili katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Cosmopolitan ya First League uliochezwa jana kwenye Uwanja wa KMC. Akizungumza baada ya - [Kidao aibukia TRA United](https://spotileo.co.tz/kidao-aibukia-tra-united/) - DAR ES SALAAM: Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Juma Mwenda amezindua Bodi ya Usimamizi wa timu ya mpira wa miguu “TRA United Sports Club na kuitaka kuisimamia kikamilifu timu hiyo na kuifanya kuwa bora na tishio katika ligi ya ndani na Kimataifa. Pamoja na mambo mengine ameisisitiza kwenda kusimamia nidhamu ya - [Serikali yaidhinisha katiba mpya ya Simba](https://spotileo.co.tz/serikali-yaidhinisha-katiba-mpya-ya-simba/) - DAR ES SALAAM: SERIKALI kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) imetangaza rasmi kuidhinishwa kwa marekebisho ya Katiba ya Klabu ya Simba Sports Club, hatua inayohitimisha mchakato wa muda mrefu wa mageuzi ya uendeshaji wa klabu hiyo na kuweka mazingira rafiki kwa uwekezaji huku ikilinda maslahi ya wanachama. Akizungumza na Waandishi wa habari Dar es - [Yanga kazini Leo kuivaa Cosmopolitan](https://spotileo.co.tz/yanga-kazini-leo-kuivaa-cosmopolitan/) - DAR ES SALAAM: MABINGWA watetezi wa Kombe la Shirikisho la CRDB, Yanga, leo wanatarajiwa kushuka dimbani katika Uwanja wa KMC Complex kuanza rasmi kampeni ya kutetea taji hilo kwa kuvaana na Cosmopolitan katika mchezo wa hatua ya 64 bora utakaopigwa saa 1:00 usiku. Yanga wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na morali ya juu baada ya - [Zaiylissa afunga ndoa tena](https://spotileo.co.tz/zaiylissa-afunga-ndoa-tena/) - DAR ES SALAAM:MUIGIZAJI wa filamu za Kibongo, Zaiylissa, ametangaza rasmi kufunga ndoa na mpenzi wake anayejulikana kwa jina la Mr. Said, hatua inayofungua ukurasa mpya katika maisha yake ya ndoa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zaiylissa ameshirikisha video fupi ikimuonyesha akiwa karibu na mume wake katika hali ya furaha na mapenzi, akiambatanisha na ujumbe mfupi - [Shilole aadhimisha miaka minne ya Penzi lake](https://spotileo.co.tz/shilole-aadhimisha-miaka-minne-ya-penzi-lake/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed 'Shilole', ameonesha furaha na upendo wake hadharani kwa kumpongeza mpenzi wake katika siku yake ya kuzaliwa, sambamba na kusherehekea miaka minne ya uhusiano wao. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shilole alichapisha picha akiwa katika mjongeo wa kimahaba na mpenzi wake, akiambatanisha na ujumbe mzito wa - [Diamond Platnumz awaombea wasio na ndoa](https://spotileo.co.tz/diamond-platnumz-awaombea-wasio-na-ndoa/) - DAR ES SALAAM: MSANII maarufu wa Bongo Fleva nchini, Diamond Platnumz, ametuma ujumbe maalum kwa wanandoa na wale ambao bado hawajabahatika kuingia kwenye ndoa, akihamasisha upendo na amani kuelekea Mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, staa huyo alichapisha ujumbe mzito wenye maombi na dua kwa Waislamu na jamii kwa ujumla, akisisitiza umuhimu - [Nandy: Billnass ataka mtoto mwingine,](https://spotileo.co.tz/nandy-billnass-ataka-mtoto-mwingine/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Nandy, ameweka wazi kuwa mume wake, Billnass, amemuomba mwaka huu amzalie mtoto mwingine, akieleza kuwa ni wakati muafaka kwani binti yao, Naya, anakaribia kutimiza miaka minne. Akizungumza kwa furaha, Nandy amesema mume wake anaona ni muda sahihi wa kuongeza mtoto katika familia yao. “Mume wangu anataka - [Aziz Ki amzawadia Hamisa G-Wagon](https://spotileo.co.tz/aziz-ki-amzawadia-hamisa-g-wagon/) - DAR ES SALAAM :MCHEZAJI wa kimataifa wa Burkina Faso, Stéphane Aziz Ki, ameendelea kuonesha mapenzi ya dhati kwa mke wake, Hamisa Mobetto, baada ya kumzawadia gari la kifahari aina ya G-Wagon ikiwa ni sehemu ya kusherehekea mwaka mmoja tangu wafunge ndoa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, nyota huyo aliambatanisha video ya tukio hilo la kimapenzi - [Lulu na Majizzo watimiza miaka mitano ya ndoa](https://spotileo.co.tz/lulu-na-majizzo-watimiza-miaka-mitano-ya-ndoa/) - DAR ES SALAAM: MREMBO wa filamu za Bongo, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, amesherehekea kwa furaha kubwa miaka mitano ya ndoa yake na mumewe kipenzi, Francis Siza ‘Majizzo’, wakiwa tayari wamebarikiwa watoto wawili. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Lulu alifunguka kwa hisia kali akimshukuru Mungu kwa kuwavusha salama katika safari ya ndoa yao na kuomba - [Clara Luvanga hashikiki Saudi Arabia](https://spotileo.co.tz/clara-luvanga-hashikiki-saudi-arabia/) - RIYADH: NYOTA wa Twiga Stars, Clara Luvanga, anaendelea kuonesha kiwango cha juu katika Ligi Kuu ya Wanawake Saudi Arabia baada ya kuongoza orodha ya wafungaji bora hadi kufikia raundi ya 10 ya michuano hiyo. Mshambuliaji huyo hatari tayari ameshafunga mabao 18, akimuacha mbali mpinzani wake wa karibu Adriana Silva mwenye mabao 12, huku Leale Garrec - [Simba kuhamishia vita yao kwa Greenland leo](https://spotileo.co.tz/simba-kuhamishia-vita-yao-kwa-greenland-leo/) - DAR ES SALAAM: TIMU ya soka ya Simba leo inaanza rasmi kampeni ya michuano ya Kombe la Shirikisho la CRDB kwa kumenyana na Greenland katika mchezo utakaochezwa saa moja usiku kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam. Wekundu wa Msimbazi wanaingia kwenye mashindano hayo wakiwa na morali kubwa baada ya kutoka kushinda bao - [Allan Okello avunja ukimya](https://spotileo.co.tz/allan-okello-avunja-ukimya/) - DAR ES SALAAM: KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Allan Okello amesema wameumizwa na kushindwa kutinga hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika lakini bado wana malengo makubwa ya kupigania katika msimu huu. Okello ametoa kauli hiyo kupitia ujumbe mfupi baada ya Yanga kuhitimisha safari yake katika hatua ya makundi, akieleza kuwa matokeo hayo hayafuti - [KOTI JEUPE’ kuzinduliwa Dar, mastaa kibao ndani!](https://spotileo.co.tz/koti-jeupe-kuzinduliwa-dar-mastaa-kibao-ndani/) - DAR ES SALAAM: WASANII wa Filamu za Bongo Movie nchini, Rihama Ally na Shamila Rashid maarufu kama Bi Staa, wamekutanishwa katika filamu mpya ya Koti Jeupe inayotarajiwa kuzinduliwa Februari 17, 2026 katika ukumbi wa Dar Free Market, jijini Dar es Salaam. Akizungumza na Spoti leo jijini, Mwongozaji na mwandishi wa filamu hiyo, Sylvia Lyimo, amesema - [Kazi mnayo, Gamondi apewa stars mazima!](https://spotileo.co.tz/kazi-mnayo-gamondi-apewa-stars-mazima/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Miguel Gamondi amesaini mkataba rasmi wa kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, kwa mkataba wa miaka miwili. Hafla ya utiaji saini wa mkataba huo imefanyika leo, Februari 16, 2026, katika Uwanja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na Waziri wa Habari, - [Ratcliffe: Kutokuwa maarufu Man United kunaanza kuzaa matunda](https://spotileo.co.tz/ratcliffe-kutokuwa-maarufu-man-united-kunaanza-kuzaa-matunda/) - MANCHESTER: Mwenyekiti wa kampuni ya INEOS na mmiliki mwenza wa timu ya Manchester United, Jim Ratcliffe, amesema maamuzi magumu aliyoyachukua ambayo yalimfanya asiwe maarufu miongoni mwa mashabiki sasa yanaanza kuonesha matokeo chanya ndani ya klabu hiyo. Ratcliffe, ambaye alinunua hisa katika klabu hiyo ya Ligi Kuu England miaka miwili iliyopita, amefanya mabadiliko kadhaa yenye utata - [Waghana Wazindua ‘Fugu Day’ vazi lao la asili, Rais apongeza](https://spotileo.co.tz/waghana-wazindua-fugu-day-vazi-lao-la-asili-rais-apongeza/) - ACCRA, Ghana: Waghana duniani kote wamegeuza kejeli za mitandaoni kuwa sherehe ya kimataifa kwa kulirejesha kwa fahari vazi lao la asili kupitia maadhimisho mapya yanayojulikana kama ‘Fugu Day.’ Kwa mujibu wa BBC, harakati hizo zilichochewa na vita ya kidijitali mtandaoni kati ya watumiaji wa mitandao ya kijamii kutoka Ghana na Zambia kuhusu vazi la fugu - [Tottenham ni timu ndogo sana- Postecoglou](https://spotileo.co.tz/19323-2/) - LONDON:KOCHA wa zamani w Tottenham Hotspur, Ange Postecoglou ameizungumzia Tottenham kwa maneno ya moja kwa moja bila kuficha chochote, akisema wazi kuwa klabu hiyo bado haijafika kiwango cha kuitwa “klabu kubwa”, hasa kwenye suala la matumizi ya fedha. Kocha huyo aliyeiongoza Spurs kushinda Europa League msimu uliopita kabla ya kutimuliwa, amesema tatizo kubwa la klabu - [Mwanamitindo wa TikTok afariki kwa kula sumu](https://spotileo.co.tz/mwanamitindo-wa-tiktok-afariki-kwa-kula-sumu/) - UFILIPINO: Mwanamitandao maarufu wa masuala ya vyakula nchini Ufilipino, Emma Amit mwenye miaka 51, amefariki dunia baada ya kula kaa mwenye sumu anayejulikana kama ‘devil crab’. Mwanamtandao huyo alikula kaa huyo mwenye sumu akiwa anaandaa maudhui ya mitandao ya kijamii. Kwa mujibu wa taarifa ya tukio hilo lilitokea Februari katika makazi yake ya pwani mkoani - [Lady Jay Dee kupamba usiku wa Valentine ](https://spotileo.co.tz/lady-jay-dee-kupamba-usiku-wa-valentine/) - DAR ES SALAAM: MSANII nguli wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura maarufu kama Lady Jay Dee, anatarajiwa kupamba na kunogesha Usiku wa Wapendanao (Valentine’s Day) katika ukumbi wa Brake Point, Makumbusho jijini Dar es Salaam. Akizungumza kuhusu tukio hilo, Lady Jay Dee amesema anafahamu jinsi Watanzania wanavyompenda na amewaahidi burudani ya hali ya juu - [Aggy Baby atoa ushauri wa Valentine:](https://spotileo.co.tz/aggy-baby-atoa-ushauri-wa-valentine/) - DAR ES SALAAM:MREMBO na mwanamitindo maarufu, Aggy Baby, amewataka wanawake kuhakikisha wanapokea zawadi za Valentine zinazoendana na thamani yao halisi. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Aggy Baby amesisitiza kuwa siku ya wapendanao ni muhimu kuthaminiwa kwa vitendo vinavyoonesha upendo wa kweli. “Hakikisha anakupa zawadi ya Valentine inayoendana na thamani yako. Akikupa maua, ujue - [Wahalifu wavunja na kuiba ghala la rapa Central Cee](https://spotileo.co.tz/wahalifu-wavunja-na-kuiba-ghala-la-rapa-central-cee/) - LONDON: RAPA maarufu wa Uingereza Oakley Caesar-Su maarufu Central Cee, ameripotiwa kupoteza mali ya thamani kubwa baada ya wahalifu kuvamia ghala lake la kuhifadhia mizigo na kuiba sehemu kubwa ya mkusanyiko wake wa viatu (sneakers) aliokuwa amekusanya kwa zaidi ya miaka 12. Msanii huyo mwenye umri wa miaka 27 alithibitisha tukio hilo kupitia ukurasa wake - [Simba: Hatutapoteza mara mbili kwa mpinzani mmoja](https://spotileo.co.tz/simba-hatutapoteza-mara-mbili-kwa-mpinzani-mmoja/) - DAR ES SALAAM: SIMBA imesema haitakubali kupoteza mara mbili dhidi ya mpinzani mmoja, ikiahidi kupambana hadi mwisho kuhakikisha inapata ushindi dhidi ya Stade Malien katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika utakaochezwa Februari 14 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es - [Twiga Stars kushiriki Pink Ladies Cup](https://spotileo.co.tz/twiga-stars-kushiriki-pink-ladies-cup/) - DAR ES SALAAM:TIMU ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, inatarajiwa kushiriki mashindano ya kimataifa ya Pink Ladies Cup yatakayofanyika Dubai, Falme za Kiarabu kuanzia Februari 28 hadi Machi 6, 2026. Mashindano hayo yatazikutanisha timu nne za taifa ambazo ni Tanzania, Russia, Ghana na Hong Kong, huku yakitarajiwa kuwa sehemu ya maandalizi muhimu ya - [Yanga yaenda Zanzibar kwa Maandalizi ya kuivaa JS Kabylie](https://spotileo.co.tz/yanga-yaenda-zanzibar-kwa-maandalizi-ya-kuivaa-js-kabylie/) - DAR ES SALAAM: KIKOSI cha Yanga SC leo kimewasili Zanzibar kwa ajili ya kuweka kambi ya mwisho kuelekea mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya JS Kabylie ya Algeria. Mchezo huo muhimu utapigwa Jumapili katika Uwanja wa New Amaan, Zanzibar, ukiwa ni wa kuamua hatma ya Wananchi katika michuano - [Rihanna aweka ubilionea pembeni, aingia dukani kama mama wa kawaida](https://spotileo.co.tz/rihanna-aweka-ubilionea-pembeni-aingia-dukani-kama-mama-wa-kawaida/) - MAREKANI: Licha ya kuwa bilionea na mmoja wa mastaa wakubwa wa muziki duniani, Rihanna ameonesha kuwa linapokuja suala la familia, yeye ni mama wa kawaida tu kama wanawake wengine. Muimbaji huyo maarufu alionekana Jumatatu, Februari 9, 2026, akifanya manunuzi ya mboga mboga na mahitaji ya jikoni yeye mwenyewe katika supermarket ya Bristol Farms, West Hollywood, - [Britney Spears auza muziki wake kwa Sh Bilioni 26](https://spotileo.co.tz/britney-spears-auza-muziki-wake-kwa-sh-bilioni-26/) - LOS ANGELES:MWANAMUZIKI maarufu wa pop duniani, Britney Spears, ameripotiwa kuuza katalogi yake yote ya muziki kwa kampuni huru ya uchapishaji wa muziki ya Primary Wave kwa makubaliano yanayokadiriwa kufikia Sh26 bilioni saw ana dola milioni 200. Kwa mujibu wa BBC, dili hilo lilikamilishwa mwishoni mwa mwezi Desemba na linaweka alama kubwa ya kifedha kwa msanii - [BMT yawataka viongozi wapya Chaneta kuwa wabunifu](https://spotileo.co.tz/bmt-yawataka-viongozi-wapya-chaneta-kuwa-wabunifu/) - DAR ES SALAAM: BARAZA la Michezo la Taifa (BMT) limewataka viongozi wapya wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) kuwa wabunifu ili kukuza vipaji vya vijana na kurudisha heshima ya mchezo wa netiboli nchini. Akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa vya chama hicho yaliyofanyika leo Februari 11, 2026, katika ukumbi wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini - [Sean Dyche afutwa kazi Nottingham Forest](https://spotileo.co.tz/sean-dyche-afutwa-kazi-nottingham-forest/) - KLABU ya Nottingham Forest imeendelea na utamaduni wake wa kubadilisha makocha mara kwa mara baada ya kumuondoa Sean Dyche, ambaye anakuwa kocha wa tatu kufukuzwa ndani ya msimu huu mmoja. Dyche ameondoka baada ya kudumu kwa siku 114 pekee madarakani, huku taarifa zikithibitisha kuwa uamuzi huo ulifanyika usiku wa manane, saa chache tu baada - [Kibu Denis ndio basi tena Simba](https://spotileo.co.tz/kibu-denis-ndio-basi-tena-simba/) - DAR ES SALAAM: MSHAMBULIAJI wa Simba SC, Kibu Denis, ameaga rasmi klabu hiyo baada ya kuitumikia kwa miaka minne na nusu, akieleza kuwa amepata changamoto mpya ya kwenda “kutengeneza familia” katika klabu ya Al Nasr ya Libya. Kibu amejiunga na Al Nasr kwa ada ya uhamisho ya dola za Marekani 300,000 (takribani Sh milioni 776) - [Vera Sidika:Nawapenda wanaume wa Tanzania](https://spotileo.co.tz/vera-sidika-nawapenda-wanaume-wa-tanzania/) - DAR ES SALAAM:MWANAMITANDAO maarufu kutoka nchini Kenya, Vera Sidika, amesema kuwa anavutiwa zaidi na wanaume wa Tanzania akieleza kuwa wanapendelea vitendo kuliko maneno mengi. Vera, ambaye kwa sasa yupo California, Marekani, ameyasema hayo kupitia mahojiano aliyofanya na Vidyfy_us chini Jacchalz. Katika mahojiano hayo, Vera ameweka wazi kuwa kwa sasa yupo single. Hata hivyo, alibainisha kuwa - [TANZIA: Mama mzazi wa msanii Chid Benz afariki dunia](https://spotileo.co.tz/tanzia-mama-mzazi-wa-msanii-chid-benz-afariki-dunia/) - DAR ES SALAAM:MAMA mzazi wa msanii wa Hip Hop nchini Tanzania, Rashid Abdallah maarufu kama Chid Benz, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo, Februari 11, 2026. Taarifa zilizothibitishwa na familia zinaeleza kuwa marehemu, Bi. Hawa, amefariki na kwa sasa msiba upo nyumbani kwa familia eneo la Chanika, jijini Dar es Salaam. Familia imesema kuwa taarifa - [Mahakama yatupilia mbali pingamizi la Jux,](https://spotileo.co.tz/mahakama-yatupilia-mbali-pingamizi-la-jux/) - DAR ES SALAAM: MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imetupilia mbali pingamizi la msanii Juma Musa maarufu kama Jux, katika kesi ya madai inayomkabili, na kuamuru shauri hilo kuendelea kusikilizwa Februari 26, 2026. Kesi hiyo imefunguliwa na mtayarishaji na msanii Shabani Abdalla Shaban maarufu kama Keizer Pie, anayodai kuwa ni mwandishi mwenza - [Eric Omondi apata Jeraha la yonga siku ya kwanza ya matembezI ya hisani](https://spotileo.co.tz/eric-omondi-apata-jeraha-la-yonga-siku-ya-kwanza-ya-matembezi-ya-hisani/) - NAIROBI:MCHEKESHAJI maarufu wa Kenya, Eric Omondi, amepata jeraha la nyonga katika siku ya kwanza ya matembezi yake ya hisani kutoka Nairobi hadi Mombasa. Eric, anayefanya safari hiyo ya kilomita 486 kwa lengo la kuchangisha fedha za kujenga Kituo kipya cha ‘Help and Rescue’, alifanikiwa kutembea kilomita 68 katika siku ya kwanza na kuhitimisha safari yake - [Kuelekea Valentine, Diamond aonesha Saa ya Sh Bilioni 1.2](https://spotileo.co.tz/kuelekea-valentine-diamond-aonesha-saa-ya-sh-bilioni-1-2/) - DAR ES SALAAM: MSANII nyota wa muziki wa Bongo Fleva na Mkurugenzi Mtendaji wa Wasafi Media, Diamond Platnumz, anajiandaa kuachia wimbo wake mpya wa kimahaba uitwao ‘Natulizana’ ikiwa ni maalumu kwa msimu wa Valentine. Hata hivyo, mbali na mashabiki kusubiri kwa hamu kazi hiyo mpya, gumzo kubwa limeibuka kuhusu saa ya kifahari inayoonekana kwenye video - [Leonardo: Mwanaume unapaswa kumuamini mpenzi wako](https://spotileo.co.tz/leonardo-mwanaume-unapaswa-kumuamini-mpenzi-wako/) - DAR ES SALAAM: MKALI wa vichekesho, Leonard Butindi, amesema kuwa kuwa na mpenzi mzuri wakati mwingine kunaweza kumfanya mwanaume kuwa na wasiwasi, hasa kutokana na mazingira ya jamii na namna watu wanavyomzunguka. Leonard amesema mwanamke wake ni mtu anayejitambua na anayejiheshimu katika kila jambo, jambo linalompa amani lakini pia kumfanya awe makini zaidi. “Mwanamke wangu - [Azam FC yaifuata Wydad kusaka robo fainali](https://spotileo.co.tz/azam-fc-yaifuata-wydad-kusaka-robo-fainali/) - DAR ES SALAAM: KIKOSI cha wachezaji 25 wa Azam FC kimeondoka mapema leo kuelekea Morocco kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Wydad Athletic Club, utakaopigwa Jumapili. Mchezo huo unasubiriwa kwa hamu kubwa kwani ndio utakaoamua hatma ya Azam FC katika michuano hiyo. Azam FC - [Nana Dollz abadili msimamo: “Sitaki Tena mwanaume mwenye pesa”](https://spotileo.co.tz/nana-dollz-abadili-msimamo-sitaki-tena-mwanaume-mwenye-pesa/) - DAR ES SALAAM:MREMBO wa filamu za Bongo Movie, Nana Dollz, ameibua mjadala mzito mitandaoni baada ya kuweka wazi mabadiliko ya msimamo wake kuhusu mwanaume anayemtaka katika maisha yake ya kimapenzi. Nana Dollz amesema kuwa kwa muda mrefu alikuwa akitamani mwanaume aliyemzidi kipato, lakini sasa ameamua kubadili kabisa mtazamo huo. Kwa mujibu wa msanii huyo, suala - [Kim Kayndo asema Muziki wa bongo hauthaminiwi,](https://spotileo.co.tz/kim-kayndo-asema-muziki-wa-bongo-hauthaminiwi/) - DAR ES SALAAM:MENEJA wa msanii Zuhura Othman ‘Zuchu’, anayefahamika kwa jina la Kim Kayndo, amesema kuwa muziki wa Bongo haupati thamani inayostahili kutoka kwa Watanzania wenyewe, hali inayowakatisha tamaa wasanii wa ndani. Kauli hiyo ameitoa baada ya kuonyesha kutoridhishwa na mijadala ya vyombo vya habari pamoja na mashabiki kufuatia onyesho la msanii wa Nigeria, Davido, - [Asmah Majed akemea maswali: “Msiniulize kwa nini natembea kwa miguu”](https://spotileo.co.tz/asmah-majed-akemea-maswali-msiniulize-kwa-nini-natembea-kwa-miguu/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa vichekesho, Asmah Majed, ameweka wazi msimamo wake kwa mashabiki na wadau wa mitandao ya kijamii kuhusu maisha yake binafsi, hususani suala la kutembea kwa miguu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Asmah Majed amesema kuanzia sasa hataki kuulizwa au kushangazwa anapokutwa akitembea kwa miguu, akisisitiza kuwa ni jambo la kawaida kwake - [Elyston Angay awasili Tanzania kwa shoo ya Valentine](https://spotileo.co.tz/elyston-angay-awasili-tanzania-kwa-shoo-ya-valentine/) - DAR ES SALAAM: MWANAMUZIKI mkongwe wa muziki wa dansi, Elyston Angay, amewasili nchini Tanzania kwa ajili ya kushiriki katika shoo maalum itakayofanyika usiku wa Siku ya Wapendanao (Valentine Day) katika Ukumbi wa Las Carinyo, uliopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Ujio wa Elyston Angay unatarajiwa kuipa shoo hiyo mvuto wa kipekee, hasa kwa mashabiki wa - [Marais watatu wa muziki wa Dansi kutumbuiza jukwaa moja](https://spotileo.co.tz/marais-watatu-wa-muziki-wa-dansi-kutumbuiza-jukwaa-moja/) - DAR ES SALAAM: MASHABIKI wa muziki wa dansi nchini wanatarajiwa kushuhudia shoo kubwa ya kihistoria itakayofanyika jijini Dar es Salaam, ikiwakutanisha marais watatu wa muziki wa dansi Tanzania katika jukwaa moja. Shoo hiyo iliyopewa jina la “3 Kubwa” itawakutanisha wasanii wakubwa wa muziki wa dansi ambao ni Chalz Baba, Christian Bella na Nyoshi El Saadat, - [Simba kurejea kibaruani kesho](https://spotileo.co.tz/simba-kurejea-kibaruani-kesho/) - DAR ES SALAAM: WEKUNDU wa Msimbazi Simba wanatarajia kurejea Ligi Kuu kesho watakapovaana na wenyeji KMC kwenye Uwanja wa KMC Complex Dar es Salaam. Morali ya Simba katika mchezo huo iko juu hasa baada ya kutoka kuonesha kiwango bora ugenini katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Petro Atletico ya Angola walikotoka sare - [Barker: Hakuna mchezo mwepesi Ligi Kuu](https://spotileo.co.tz/barker-hakuna-mchezo-mwepesi-ligi-kuu/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Simba SC, Steven Barker, amesema kikosi chake kina hamasa kubwa kurejea katika michezo ya Ligi Kuu baada ya kumaliza ratiba ya michezo ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF). Barker amesema tayari timu imerejea mazoezini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo dhidi ya KMC unaotarajiwa kuchezwa kesho jioni, akisisitiza kuwa - [Zari atupa jiwe gizani!](https://spotileo.co.tz/zari-atupa-jiwe-gizani/) - DAR ES SALAAM: MFANYABIASHARA na mzazi mwenza wa msanii wa Bongo Fleva Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’, amezua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kueleza tofauti anayoiona kati ya mwanamke tajiri na mwanaume tajiri katika malezi ya watoto. Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X, Zari ameandika kuwa mwanamke anapokuwa - [K2ga afunguka sababu za wasanii kuondoka kwenye lebo](https://spotileo.co.tz/k2ga-afunguka-sababu-za-wasanii-kuondoka-kwenye-lebo/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Karim Rashid, 'K2ga', amesema kuwa sababu kubwa inayowafanya wasanii wengi kuondoka kwenye lebo zao za muziki ni kutafuta ukuaji binafsi na kipato kikubwa. K2ga amesema kuwa kila msanii anakumbana na changamoto tofauti akiwa ndani ya lebo, hali inayowasukuma baadhi yao kuchagua kujitegemea. “Kila mtu ana changamoto - [Yanga yaja na kampeni “Tutafuzu Nyumbani”](https://spotileo.co.tz/yanga-yaja-na-kampeni-tutafuzu-nyumbani/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga SC imezindua imekuja na kampeni maalum iliyopewa kaulimbiu “Tutafuzu Nyumbani” ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha mashabiki kuelekea mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika utakaochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa New Amaan, Zanzibar. Kampeni hiyo inakuja baada ya Wananchi kupoteza mchezo uliopita ugenini dhidi ya - [Twiga Stars waanza maandalizi ya Wafcon](https://spotileo.co.tz/twiga-stars-waanza-maandalizi-ya-wafcon/) - DAR ES SALAAM: TIMU ya Taifa ya Wanawake, Twiga Stars, imeanza rasmi mazoezi katika Uwanja wa Kituo cha Ufundi cha Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Kigamboni, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 zitakazofanyika nchini Morocco. Tanzania imepangwa Kundi B - [Ugonjwa wamfanya Salif Keita ashindwe kutumbuiza Sauti za Busara 2026](https://spotileo.co.tz/ugonjwa-wamfanya-salif-keita-ashindwe-kutumbuiza-sauti-za-busara-2026/) - ZANZIBAR : MWANAMUZI mkongwe Salif Keita ameshindwa kufika Zanzibar na kutumbuiza katika Tamasha la Sauti za Busara 2026 kutokana na kuugua. Mkurugenzi wa Tamasha hilo, Journey Ramadhani amesema taarifa ya kuugua kwa mwanamuziki huyo aliyekuwa akitarajiwa kutumbuiza siku ya mwisho ya tamasha hilo wameipokea kutoka kwa mwanamuziki huyo baada ya kushauriwa na daktari wake kutosafiri - [Tamasha la Sauti za Busara 2027 kupisha Mfungo](https://spotileo.co.tz/tamasha-la-sauti-za-busara-2027-kupisha-mfungo/) - ZANZIBAR: TAMASHA la Sauti za Busara linalofanyika mwezi Februari kila mwaka kwa mwaka 2027 litafanyika mwezi Machi ili kupisha mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani utakaofanyika ndani ya mwezi wa Februari. Mwenyekiti wa Tamasha hilo, Journey Ramadhani ametaja tarehe ya Tamasha hilo kwa mwakani kuwa ni Machi 11 hadi 14. “Tamasha huwa likifanyika kila mwezi - [Man Fongo kutetea wanawake, watoto](https://spotileo.co.tz/man-fongo-kutetea-wanawake-watoto/) - ZANZIBAR: MSANII wa singeli,Man Fongo ameweka wazi kuwa anaandaa nyimbo zenye jumbe maalumu za kutetea haki za Wanawake na Watoto dhidi ya ukatili wa kijinsia. Man Fongo amesema hayo katika mjadala ulioandaliwa na UNICEF kwa kushirikiana na Sauti za Busara, uliojikita katika namna wasanii wanavyoweza kutumia sauti na ushawishi wao kukemea ukatili na kutetea haki - [Silva: Kushindwa Anfield kungeua mbio za ubingwa](https://spotileo.co.tz/silva-kushindwa-anfield-kungeua-mbio-za-ubingwa/) - MANCHESTER: NAHODHA wa Manchester City, Bernardo Silva, amesema kuwa chochote tofauti na ushindi dhidi ya Liverpool kingeua kabisa matumaini ya timu yake katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England. Kauli hiyo ilitolewa baada ya kikosi cha Pep Guardiola kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Liverpool katika uwanja wa Anfield. City walikuwa hatarini - [Khaligraph Jones kutumbuiza baada ya mechi za HSBC SVNS 2 Nyayo Stadium](https://spotileo.co.tz/khaligraph-jones-kutumbuiza-baada-ya-mechi-za-hsbc-svns-2-nyayo-stadium/) - NAIROBI: MSISIMKO wa burudani katika mashindano ya raga ya HSBC SVNS 2 Nairobi umeendelea kupanda baada ya waandaaji kuthibitisha rasmi kuwa mastaa wakubwa wa muziki wa Kenya, Khaligraph Jones na Vijana Barubaru, wataongoza sherehe za burudani za baada ya mechi (afterparty) zitakazofanyika katika Uwanja wa Nyayo. Burudani hiyo ya siku mbili inawezeshwa na kampuni ya - [Makonda awataka Watanzania kuunga mkono vipaji vya ndani](https://spotileo.co.tz/makonda-awataka-watanzania-kuunga-mkono-vipaji-vya-ndani/) - DAR ES SALAAM:WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewataka Watanzania kuwa wazalendo kwa kupenda na kuunga mkono vipaji vya ndani, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika ujenzi wa shule na viwanja vya michezo kwa lengo la kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Makonda amesema maendeleo ya michezo - [Serikali kujenga shule 56 za kuinua vipaji vya michezo nchini](https://spotileo.co.tz/serikali-kujenga-shule-56-za-kuinua-vipaji-vya-michezo-nchini/) - DAR ES SALAAM: SERIKALI ina mpango wa kujenga shule 56 maalumu za kukuza vipaji vya watoto kuanzia umri mdogo, ambapo ujenzi utaanza kwa shule saba katika kila halmashauri nchini. Akizungumza na waandishi wa habari Leo jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake katika Uwanja wa Taifa wa Benjamin Mkapa, Waziri Habari wa Utamaduni, Sanaa - [Tanzania kupokea ugeni wa viongozi wakuu CAF](https://spotileo.co.tz/tanzania-kupokea-ugeni-wa-viongozi-wakuu-caf/) - DAR ES SALAAM:TANZANIA inatarajia kupokea ugeni wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Patrice Motsepe, anayekuja nchini kuongoza Mkutano wa Kamati Tendaji wa CAF, utakaofanyika Februari 13, 2026 jijini Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 9, 2026 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, - [ Mwandambo atoa onyo kwa vijana kurudiana na “Ex”](https://spotileo.co.tz/mwandambo-atoa-onyo-kwa-vijana-kurudiana-na-ex/) - DAR ES SALAAM: Mwanamitandao maarufu, Clemence Mwandambo, amewapa somo vijana kuhusu masuala ya mahusiano, akisisitiza kuwa si busara kurudiana na mpenzi wa zamani (Ex). Akizungumza kupitia mitandao ya kijamii, Mwandambo amedai kuwa mwanamke hapendi kuachwa mara mbili, hivyo endapo mwanaume atarudiana na mpenzi wake wa zamani, anaweza kukumbana na changamoto au madhara makubwa baadaye. “Ex - [Simba wala haina presha ikiivaa Petro Atletico kesho](https://spotileo.co.tz/simba-wala-haina-presha-ikiivaa-petro-atletico-kesho/) - LUANDA- NAHODHA wa Simba SC, Shomari Kapombe, amesema wanataka kuutumia mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Petro Atletico kama sehemu ya maandalizi ya mechi zijazo za Ligi Kuu na Mashindano mengine. Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kesho Jumamosi nchini Angola ambapo tayari wekundu ni kama wamepoteza matumaini ya kusonga mbele kutokana na Mwenendo wa - [Gumbo: Morali Yanga juu, tunahitaji matokeo chanya](https://spotileo.co.tz/gumbo-morali-yanga-juu-tunahitaji-matokeo-chanya/) - DAR ES SALAAM: UONGOZI wa Yanga SC umeeleza kuwa timu ipo katika hali nzuri kisaikolojia na kiufundi kuelekea mchezo wa kesho Jumamosi dhidi ya FAR Rabat utakaochezwa nchini Morocco. Akizungumza akiwa Morocco Mkuu wa Msafara wa Yanga na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Rogers Gumbo, alisema viongozi, benchi la ufundi na wachezaji - [KMC yapumua baada ya ushindi wa pili](https://spotileo.co.tz/kmc-yapumua-baada-ya-ushindi-wa-pili/) - DAR ES SALAAM: KMC FC hatimaye imepata ahueni baada ya kuibuka na ushindi wake wa pili wa mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu, ikiifunga Mashujaa FC katika mchezo wa raundi ya 13, ushindi uliopatikana kupitia bao la mpira wa adhabu lililofungwa na Daruweshi Saliboko jana. Ushindi huo ni wa pili kwa KMC baada - [Masanza: Singida hakuna kulala Zanzibar](https://spotileo.co.tz/masanza-singida-hakuna-kulala-zanzibar/) - ZANZIBAR: SINGIDA Black Stars imesema haina muda wa kupumzika tayari imewasili Zanzibar tangu jana ikitokea Jamhuri ya Congo, ikianza mara moja mazoezi ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya CR Belouizdad ya Algeria. Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Jumapili kwenye Uwanja wa New Amaan Zanzibar. Akizungumzia maandalizi ya mchezo - [Chanuo afunguka maisha magumu ya utotoni](https://spotileo.co.tz/chanuo-afunguka-maisha-magumu-ya-utotoni/) - DAR ES SALAAM:MREMBO wa Bongo Movie anayefanya vizuri kupitia tamthilia maarufu ya Kombolela, Chanuo Nchakali, 'Mwamini' amefunguka kuhusu maisha magumu aliyopitia alipokuwa darasa la saba, akisema kuwa hakuwa na rafiki wa kike wala wa kiume kutokana na hali duni ya maisha iliyomsababisha kushindwa kuoga na kupiga mswaki. Akizungumza kwa hisia, Chanuo amesema kuwa kipindi hicho - [TFF yawataka Futsal kukamilisha kazi Ivory Coast](https://spotileo.co.tz/tff-yawataka-futsal-kukamilisha-kazi-ivory-coast/) - DAR ES SALAAM: KAIMU Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Oscar Mirambo, ameihimiza Timu ya Taifa ya wanaume ya Futsal kuhakikisha inalinda ushindi na kumaliza kazi vizuri katika mchezo wa pili wa kufuzu Futsal AFCON 2026 dhidi ya Ivory Coast. Mirambo aliyasema hayo alipozungumza na wachezaji pamoja na benchi la ufundi - [Rotimi, Vanessa penzi la mwendokasi](https://spotileo.co.tz/rotimi-vanessa-penzi-la-mwendokasi/) - MUIGIZAJI na mwanamuziki maarufu kutoka Marekani, Rotimi, ambaye ni mume wa staa wa muziki wa Tanzania Vanessa Mdee 'V Money', amewahakikishia Watanzania kuwa ndoa yake na mkewe ipo imara na hawana mpango wowote wa kuachana. Rotimi ametoa kauli hiyo kufuatia maneno mengi yaliyoenea mitandaoni baada ya yeye kuonekana akigawa namba yake ya simu kwa mwanamuziki - [Simba yajipanga kurejesha heshima yake](https://spotileo.co.tz/simba-yajipanga-kurejesha-heshima-yake/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Simba, Steven Barker, amesema bado kuna matumaini kwa kikosi chake katika Ligi ya Mabingwa Afrika licha ya maumivu ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 kwenye mchezo uliopita dhidi ya Esperance ya Tunisia mwishoni mwa wiki. Barker alisema Simba bado ina michezo miwili ya hatua ya makundi, ambayo itatoa fursa - [Mwanamuziki wa taarabu afariki dunia](https://spotileo.co.tz/mwanamuziki-wa-taarabu-afariki-dunia/) - DAR ES SALAAM: MWANAMUZIKI mkongwe na mtunzi wa muziki wa taarabu nchini, Ally Hemed 'Ally Star' amefariki dunia leo, Februari 3, 2026 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa. Ally Star ambaye amefanya kazi kwa muda mrefu akiwa na bendi ya Tanzania One Theatre (TOT), alikuwa amelazwa Muhimbili kwa zaidi ya mwezi mmoja. Msanii - [Yanga waifuata Far Rabat na silaha zote!](https://spotileo.co.tz/yanga-waifuata-far-rabat-na-silaha-zote/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga inatarajiwa kusafiri leo kuelekea Rabat, Morocco, kwa ajili ya mchezo muhimu wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya AS FAR Rabat utakaochezwa Jumamosi. Mchezo huo utakuwa wa tano kwa Yanga katika kundi hilo na ni wa kuamua hatima yao ya kufuzu hatua ya robo fainali, - [Collins Sichanje ajiunga na klabu ya Charton Athletic](https://spotileo.co.tz/collins-sichanje-ajiunga-na-klabu-ya-charton-athletic/) - LONDON, UINGEREZA BEKI wa heshima wa soka la Kenya Collins Sichenje amefanikiwa kujiunga na klabu ya Charlton Athletic ya nchini Uingereza. Sichanje amefanikiwa kiutia saini mkataba wa miaka miwili na nusu baada ya kukamilisha uhamisho wake kutoka klabu ya FK Vojvodina ya nchini Serbia. Hii ni hatua kubwa katika safari ya mchezaji huyo mwenye miaka - [Ibenge: Tunahitaji umakini michezo ijayo](https://spotileo.co.tz/ibenge-tunahitaji-umakini-michezo-ijayo/) - DAR ES SALAAM- KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesisitiza haja ya wachezaji wake kuongeza umakini wa kiuchezaji, uimara wa kisaikolojia na matumizi sahihi ya nafasi katika michezo ijayo, akisema timu yake bado ina nafasi ya kufanya vizuri zaidi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika. Ibenge amesema pamoja na ushindi walioupata katika mchezo - [Star wa filamu ya Apocalypto Gerardo Taracena, afariki dunia](https://spotileo.co.tz/star-wa-filamu-ya-apocalypto-gerardo-taracena-afariki-dunia/) - MEXICO: TASNIA ya filamu na sanaa ya maigizo nchini Mexico imekumbwa na pigo kubwa baada ya kifo CHA mmoja wa waigizaji wa fiamu ya Apocalypto iliyotoka mwaka 2006, Gerardo Taracena, kufariki dunia. Muigizaji huyo na densa maarufu nchini humo amefariki akiwa na umri wa miaka 55. Awali hawakutoa maelezo rasmi kuhusu sababu ya kifo, lakini - [Tyla aandika historia Grammy](https://spotileo.co.tz/tyla-aandika-historia-grammy/) - LOS ANGELES: MSANII chipukizi wa muziki wa pop kutoka Afrika Kusini, Tyla, ameandika historia mpya katika tuzo za Grammy 2025 baada ya kushinda tuzo yake ya pili, akiwashinda mastaa wakubwa wa Afrika akiwemo Burna Boy, Davido, Ayra Starr pamoja na Eddy Kenzo wa Uganda. Tyla mwenye miaka 24 alitwaa tuzo ya Best African Music Performance - [Tamasha la Sauti za Busara 2026 kufanyika Mnazi Mmoja](https://spotileo.co.tz/tamasha-la-sauti-za-busara-2026-kufanyika-mnazi-mmoja/) - ZANZIBAR: TAMASHA la 23 la Kimataifa la Muziki, Sauti za busara linatarajiwa kuanza Februari 5 hadi 8, 2026 visiwani Zanzibar zikiwa siku nne za kuburudika na muziki wa live kutoka kwa wasanii zaidi ya 400 kutoka kote duniani. Mkurugenzi wa Tamasha hilo Journey Ramadhani amesema kwa mwaka huu tamasha hilo linatarajiwa kufanyika katika Viwanja vya - [Yanga Princess yamrejesha Oluwayemisi](https://spotileo.co.tz/yanga-princess-yamrejesha-oluwayemisi/) - DAR ES SALAAM- TIMU ya Yanga Princess imeendelea kuimarisha kikosi chake baada ya kutangaza rasmi kumrejesha mshambuliaji wake wa zamani, Oluwayemisi Samwel, raia wa Nigeria. Mchezaji huyo anarejea ndani ya kikosi hicho baada ya msimu uliopita kuitumikia TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako alipata uzoefu muhimu katika mashindano ya ngazi ya juu - [Wabunifu wa mitindo wapigwa msasa elimu ya fedha](https://spotileo.co.tz/wabunifu-wa-mitindo-wapigwa-msasa-elimu-ya-fedha/) - DAR ES SALAAM: WABUNIFU wa mavazi, wanamitindo na washonaji nchini wamepewa mafunzo ya elimu ya fedha yenye lengo la kuinua biashara zao, kuongeza ajira kwa vijana na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa. Mafunzo hayo yalitolewa jana jijini Dar es Salaam katika Jukwaa la Mitindo Tanzania (Tanzania Fashion Forum), yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa taasisi za - [Kiswahili Kung’ara Paris: BAKITA yatoa wito wadau kujisajili](https://spotileo.co.tz/kiswahili-kungara-paris-bakita-yatoa-wito-wadau-kujisajili/) - DAR ES SALAAM: BARAZA la Kiswahili la Taifa (BAKITA) limewataka wadau wote wa Kiswahili wenye nia ya kushiriki katika Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili, litakalofanyika jijini Paris, Ufaransa, kuanzia Aprili 27 hadi 30, 2026, kujisajili mapema ili kuwezesha maandalizi ya kongamano hilo. Akizungumza, jijini Dar es Salaam, Mhariri Mkuu wa BAKITA, Richard Mtambi, - [Timu nane zenye makombe mengi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya](https://spotileo.co.tz/timu-nane-zenye-makombe-mengi-ya-ligi-ya-mabingwa-ulaya/) - ULAYA:LIGI ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) ni mashindano makubwa zaidi ya klabu barani Ulaya. Ndani yake ndipo historia ya kweli ya soka la Ulaya ilipoandikwa. Timu zinazofanikiwa kubeba kombe hili mara nyingi zimekuwa zikionesha ukubwa wao sio tu kwa vikosi walivyokuwa navyo, bali pia kwa namna walivyotawala vizazi tofauti vya soka.Kiufupi ni kwamba, si - [AFCON 2025: Ni Senegal na Morocco fainali Jumapili](https://spotileo.co.tz/afcon-2025-ni-senegal-na-morocco-fainali-jumapili/) - RABAT: TIMU ya taifa ya Senegal itakutana na wenyeji Morocco katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada ya michezo miwili ya nusu fainali iliyojaa presha, ushindani mkali na matokeo yaliyopatikana kwa njia tofauti. Morocco walijihakikishia nafasi ya kucheza fainali itakayofanyika Jumapili jijini Rabat baada ya kuibuka na ushindi wa penalti 4–2 - [Kocha Yanga akoshwa kiwango cha wachezaji wake](https://spotileo.co.tz/kocha-yanga-akoshwa-kiwango-cha-wachezaji-wake/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Pedro Goncalves, amekoshwa na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake akisema wataendelea kupambana kushinda na kulinda heshima ya rangi zake. Kauli yake hiyo inakuja baada ya Yanga kuibuka na ushindi mnono wa mabao 6-0 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa jana kwenye - [“Mimi sio wa mazoea!”-Barnaba Classic aweka msimamo mkali](https://spotileo.co.tz/mimi-sio-wa-mazoea-barnaba-classic-aweka-msimamo-mkali/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Barnaba Elias maarufu kama Barnaba Classic, ametoa ujumbe mzito kwa watu wanaojitambulisha kuwa ni marafiki au watu wake wa karibu, akiwataka kupunguza mazoea na kulinda heshima katika mahusiano yao. Barnaba ameeleza hayo kupitia Insta Story yake, akisisitiza kuwa kuzoeana hakupaswi kuwa sababu ya kudharau heshima, hadhi na - [Ahmed Ally:tumpe ushirikiano Kibabage](https://spotileo.co.tz/ahmed-allytumpe-ushirikiano-kibabage/) - DAR ES SALAAM: MSEMAJI wa Klabu ya Simba SC, Ahmed Ally, amewaomba mashabiki wa klabu hiyo kumpokea na kumpa ushirikiano beki wa kushoto Nikson Kibabage, akisisitiza kuwa ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa wa kuisaidia timu. Katika taarifa yake aliyoitoa leo, Ahmed amesema Kibabage ana ubora na uwezo ambao, endapo atapewa sapoti inayostahili, ataifanyia makubwa Simba. - [Safari ya Aaliyah: Nyota iliyoangaza vikali kwa muda mfupi](https://spotileo.co.tz/safari-ya-aaliyah-nyota-iliyoangaza-vikali-kwa-muda-mfupi/) - SAFARI ya muziki ya Aaliyah Dana Haughton ni hadithi ya kipaji, ujasiri, mafanikio makubwa na majonzi yasiyosahaulika. Alizaliwa Januari 16, 1979 huko Brooklyn, Marekani, na akalelewa Detroit, ambako vipaji vyake vilianza kuonekana akiwa mdogo. Kutoka kwenye televisheni hadi studio za muziki, safari yake ilikuwa na kasi ya ajabu lakini pia iliandamana na changamoto nzito ambazo - [Fahamu siri iliyojificha uchekeshaji wa Mr. Bean](https://spotileo.co.tz/fahamu-siri-iliyojificha-uchekeshaji-wa-mr-bean/) - KATIKA ulimwengu wa uigizaji, Rowan Atkinson, anayefahamika zaidi kama Mr. Bean, ameweka alama isiyofutika kupitia uhusika wake wa kipekee anayevaa koti la rangi ya kahawia na tai nyekundu, huku rafiki yake mkuu akiwa ni dubu wa mdoli anayeitwa Teddy. Uigizaji wake ni wa kipekee na wa aina yake ambao unapendwa na watu wa rika zote, - [Coming to America:Eddie Murphy alituliza akili humu](https://spotileo.co.tz/coming-to-americaeddie-murphy-alituliza-akili-humu/) - COMING to America ni moja ya filamu ambazo mpaka leo bado zinaangaliwa na watu wanacheka kama mara ya kwanza. Hii ni filamu ya vichekesho lakini ndani yake kuna ujumbe mzito kuhusu maisha, mapenzi na kutafuta uhuru wa kuwa wewe mwenyewe. Filamu inamzungumzia Prince Akeem, mrithi wa ufalme wa nchi ya kubuni inayoitwa Zamunda barani Afrika. Akeem - [Twende  kilioni: Nywele za mkono sasa ofisini na kila kona](https://spotileo.co.tz/twende-kilioni-nywele-za-mkono-sasa-ofisini-na-kila-kona/) - KARIBU kwa mara nyingine upate ladha ya mitindo na mvuto wa kipekee, na leo ukurasa wetu wa urembo na mitindo unakuletea mwelekeo unaoendelea kuitikisa jamii kwa kasi kubwa, usukaji wa nywele za mkono maarufu kama Twende Kilioni, sambamba na mitindo ya kuchora maumbo, mistari na hata maneno kichwani. Zamani watu walizoea kuona nywele za mkono - [Phina aeleza maana mpya ya wimbo wa wawili](https://spotileo.co.tz/phina-aeleza-maana-mpya-ya-wimbo-wa-wawili/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Saraphina Michael maarufu kama Phina, amesema kuwa wimbo wake “Wawili” sasa una maana ya kipekee na ya kweli katika maisha yake ya mapenzi, baada ya kuuhusisha moja kwa moja na mpenzi wake, Eni Edo, raia wa Nigeria. Wimbo huo wa “Wawili” uliotoka rasmi Februari 16, 2024, uliwasilisha simulizi - [Lazaro Suda aiweka wazi 'Maadui'](https://spotileo.co.tz/lazaro-suda-aiweka-wazi-maadui/) - MOROGORO: MWIMBAJI wa muziki wa Injili anayekuja kwa kasi kutoka mkoani Morogoro, Lazaro Suda, amewaomba wadau na mashabiki wa muziki huo kuupokea kwa mikono miwili wimbo wake mpya unaoitwa “Maadui”, ambao amesema una ujumbe mzito unaogusa jamii. Suda amesema dhamira yake kubwa ni kuitangaza Injili ya Yesu Kristo, huku akiitambulisha Morogoro kama moja ya ngome - [Ligi Kuu kurejea kesho baada ya AFCON](https://spotileo.co.tz/ligi-kuu-kurejea-kesho-baada-ya-afcon/) - DAR ES SALAAM: LIGI Kuu Tanzania Bara inarejea rasmi kesho baada ya mapumziko yaliyotokana na majukumu ya timu ya Taifa katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) pamoja na kukamilika kwa mashindano ya Kombe la Mapinduzi. Ratiba ya kurejea kwa ligi hiyo inaanza kesho kwa mchezo wa kusisimua kati ya Dodoma Jiji FC - [Yanga yamtambulisha Depu](https://spotileo.co.tz/yanga-yamtambulisha-depu/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga imemtambulisha rasmi mshambuliaji mpya Laurindo Dilson Maria Aurélio maarufu kama Depu, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha kikosi chake katika dirisha dogo la usajili. Depu amesajiliwa akitokea Ligi ya Poland, hatua inayodhihirisha dhamira ya mabingwa hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji kuelekea nusu ya - [CAF yamfungia Etoo mechi nne na faini juu](https://spotileo.co.tz/caf-yamfungia-etoo-mechi-nne-na-faini-juu/) - RABAT: SHIRIKISHO la Soka Barani Afrika (CAF) limemfungia Rais wa Shirikisho la Soka Cameroon (FECAFOOT), Samuel Eto’o mechi nne, kufuatia matukio yaliyojitokeza katika robo fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 kati ya Morocco na Cameroon. Kwa mujibu wa uamuzi wa kamati ya nidhamu ya CAF, Eto’o pia, ametozwa faini ya dola 20,000 - [Faiza Ally:Diamond hajazaliwa kutatua matatizo ya watu](https://spotileo.co.tz/faiza-allydiamond-hajazaliwa-kutatua-matatizo-ya-watu/) - DAR ES SALAAM:MWANAMITINDO na mfanyabiashara Faiza Ally ameweka wazi msimamo wake kuhusu matarajio ya jamii kwa msanii maarufu Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz, akisisitiza kuwa msanii huyo hajaja duniani kwa ajili ya kutatua matatizo ya watu wengine. Faiza ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram, ambapo ameeleza kuwa msaada wowote - [Rose Muhando alalamikia hakimiliki](https://spotileo.co.tz/rose-muhando-alalamikia-haki-miliki/) - DAR ES SALAAM:MALKIA wa muziki wa Injili nchini Tanzania, Rose Muhando, ameiomba Serikali kuingilia kati kwa haraka mgogoro wa hakimiliki unaomhusu, akimtaja moja kwa moja Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, ili kuhakikisha anapata haki yake ya mapato kutokana na kazi zake za muziki. Kupitia taarifa yake, ukurasa wa istagramu Rose Muhando - [Kinachoendelea Bernabeu hakinihusu- Klopp](https://spotileo.co.tz/kinachoendelea-bernabeu-hakinihusu-klopp/) - MALLORCA:JÜRGEN Klopp ameweka wazi msimamo wake kuhusu tetesi zinazomhusisha na Real Madrid, akitumia nafasi hiyo kuzungumzia kwa kina zaidi kuondoka kwa Xabi Alonso ndani ya muda mfupi tangu ateuliwe. Akizungumza na Sport Talk, Klopp amesema kuondoka kwa Alonso baada ya miezi sita tu ni ishara tosha kwamba kuna matatizo ndani ya Real Madrid, na si - [Kuna uwezekano Sterling na Disasi kurejea kikosini](https://spotileo.co.tz/19049-2/) - LONDON:HATMA ya Axel Disasi na Raheem Sterling ndani ya Chelsea inaweza kubadilika chini ya kocha mpya Liam Rosenior, ambaye ameacha wazi mlango wa kurejea kwao kwenye kikosi cha kwanza. Rosenior amesema ana heshima kubwa kwa Sterling kutokana na kazi kubwa aliyofanya katika soka, huku akimuelezea Disasi kama mchezaji ambaye amemvutia kwa muda mrefu. “Raheem ana - [Shamsa Ford atoa ya Moyoni kuhusu 'kupost' mpenzi](https://spotileo.co.tz/shamsa-ford-atoa-ya-moyoni-kuhusu-kupost-mpenzi/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa filamu za Bongo, Shamsa Ford, ameibuka na ujumbe mzito wa funzo kwa mabinti, akitumia uzoefu wa maisha yake ya mahusiano kama somo kwa jamii. Shamsa amesema kuwa kama angepata nafasi ya kurudisha nyuma miaka, asingeposti wala kuweka wazi mahusiano yake ya kimapenzi alipokuwa bado hajaolewa, bali angemruhusu mume wake wa ndoa - [D voice: Aeleza kwa nini hakumchangia matibabu mkubwa fella](https://spotileo.co.tz/d-voice-aeleza-kwa-nini-hakumchangia-matibabu-mkubwa-fella/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva kutoka lebo ya Wasafi, Abdul Khamis Mtambo maarufu kama D Voice, amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu ziara aliyofanya pamoja na Diamond Platnumz kwenda kumtembelea Mkubwa Fella wakati alipokuwa amelazwa hospitalini. Akizungumza na waandishi wa habari, D Voice amesema kuwa licha ya kufika hospitalini mara moja - [Hassan Mwakinyo: Hakuna Bondia wa kunizidi](https://spotileo.co.tz/hassan-mwakinyo-hakuna-bondia-wa-kunizidi/) - DAR ES SALAAM:MPIGANAJI wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania, Hassan Mwakinyo, amesema kuwa baadhi ya mapromota wasio na uwezo wanamtazama kama bondia mwenye madai makubwa ya malipo kuliko wapiganaji wengine wote wa ngumi za kulipwa. Kupitia ujumbe aliouchapisha leo, instagramu, Mwakinyo amesema mtazamo huo unatokana na ukweli kwamba hakujawahi kutokea bondia wa kiwango chake kwa - [Simba wahusishwa na usajili wa wachezaji watatu wa kigeni](https://spotileo.co.tz/simba-wahusishwa-na-usajili-wa-wachezaji-watatu-wa-kigeni/) - DAR ES SALAAM:KLABU ya Simba SC imeendelea kuhusishwa na usajili wa wachezaji watatu wa kigeni katika dirisha hili la usajili, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha kikosi chake kuelekea michezo ya kimataifa na ya ndani. Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya soka zinaeleza kuwa Wekundu wa Msimbazi wanamfuatilia kwa karibu winga wa kimataifa wa Senegal, - [Okello hakuna kuchelewa ameanza kazi rasmi](https://spotileo.co.tz/okello-hakuna-kuchelewa-ameanza-kazi-rasmi/) - PEMBA: MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga SC, Allan Okello, hakuna kuchelewa tayari ameanza mazoezi Leo ( jana ) na wenzake mara baada ya kuwasili na kujiunga rasmi na klabu hiyo. Okello anaonekana mwenye hamasa kubwa na ari ya kufanya mazoezi Gym akionesha kuwa yupo tayari kwa changamoto mpya ndani ya Ligi Kuu ya NBC. Mchezaji huyo - [Mshery awashukuru mashabiki Yanga kwa sapoti](https://spotileo.co.tz/mshery-awashukuru-mashabiki-yanga-kwa-sapoti/) - PEMBA: GOLIKIPA wa Yanga SC, Abutwalibu Mshery, amewashukuru mashabiki wa klabu hiyo kwa sapoti kubwa waliyoipa timu yao, baada ya Yanga kutwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi jana, huku akisisitiza kuwa msimu bado ni mrefu na malengo makubwa bado yapo mbele. Akizungumza mara baada ya kutwaa taji hilo, Mshery alisema mashindano ya mwaka huu yamekuwa - [Kriketi Tanzania yaichapa Ireland U19](https://spotileo.co.tz/kriketi-tanzania-yaichapa-ireland-u19/) - WINDHOEK:TIMU ya Taifa ya kriketi ya vijana chini ya umri wa miaka 19 (Tanzania U19) imeendelea kung’ara katika mechi za maandalizi ya Kombe la Dunia baada ya kuibuka na ushindi wa kusisimua wa wiketi moja dhidi ya Ireland U19 katika mechi ya pili ya maandalizi. Katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa hadi mpira wa mwisho, - [Rose Muhando achumbiwa nchini Kenya](https://spotileo.co.tz/rose-muhando-achumbiwa-nchini-kenya/) - NAIROBI: MSANII maarufu wa nyimbo za Injili kutoka Tanzania, Rose Muhando, anayejulikana kama Malkia wa Gospel, ametangaza rasmi kuolewa na Bishop Robert Bob Lumbasi, raia wa Kenya ambaye ni Bishop, Msanii wa Injili na askari wa cheo cha juu nchini humo. Bishop Lumbasi alitangaza habari hizo baada ya kumvisha pete ya uchumba Rose Muhando katika - [Mke wa Mkubwa Fella awajibu wakosoaji:](https://spotileo.co.tz/mke-wa-mkubwa-fella-awajibu-wakosoaji/) - DAR ES SALAAM:MKE wa Mkubwa Fella maarufu kama Sweet Fella amevunja ukimya na kuwajibu wanaomchokonoa kupitia mitandao ya kijamii, akidai kuwa tayari amechukua hatua dhidi yao na athari zake zinaonekana hadi sasa. Kupitia Instagram Story yake, Sweet Fella amesema kuwa licha ya kumpiga “moja tu”, tayari baadhi ya watu wameanza kuonekana kupoteza mwelekeo, huku akionya - [Simba yaanza maandalizi ya kuivaa Esperance](https://spotileo.co.tz/simba-yaanza-maandalizi-ya-kuivaa-esperance/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Simba SC imerejea rasmi katika uwanja wa mazoezi kuanza maandalizi ya mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance ya Tunisia, huku uongozi wa klabu hiyo ukiwataka mashabiki wake kuwa watulivu kuhusu masuala ya usajili. Wekundu hao wametoka Zanzibar na kurejea Dar es Salaam tangu juzi walikokuwa wanashiriki - [KMC yatambulisha Kocha wa Makipa](https://spotileo.co.tz/kmc-yatambulisha-kocha-wa-makipa/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya KMC FC imeendelea kufanya maboresho katika benchi la ufundi na idara ya uendeshaji baada ya kuwatambulisha rasmi Raphael Mpangala kuwa Kocha wa Makipa na Dalton Mgala kama Msimamizi wa vifaa wa timu hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuimarisha kikosi chake. Kupitia taarifa iliyotolewa na klabu hiyo, uongozi wa - [Phina:Mimi na Eni tulikuwa tunaandaa mambo mazuri](https://spotileo.co.tz/phinamimi-na-eni-tulikuwa-tunaandaa-mambo-mazuri/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa Bongo Fleva, Saraphina Michaeli ‘Phina’, amesema ukimya wake wa hivi karibuni kwenye shughuli za muziki umetokana na maandalizi ya mambo makubwa aliyokuwa akiyafanya kwa kushirikiana na mpenzi wake, Eni kutoka Nigeria. Phina ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii baada ya kuchapisha picha akiwa pamoja na Eni, akieleza kuwa - [Mama Dangote, Esma Platnumz wasisitiza shukrani katika msaada wa Mkubwa Fella](https://spotileo.co.tz/mama-dangote-esma-platnumz-wasisitiza-shukrani-katika-msaada-wa-mkubwa-fella/) - DAR ES SALAAM;SANURA Kasimu maarufu kama Mama Dangote amethibitisha kuwa alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kushiriki moja kwa moja katika harakati za matibabu ya Mkubwa Fella, akisisitiza umuhimu wa kuthamini na kushukuru msaada unaotolewa na watu mbalimbali katika nyakati za shida. Kupitia ujumbe aliouchapisha, Mama Dangote amekumbusha jamii kuhusu thamani ya shukrani pale mtu - [Mwamuzi wa Stars mechi ya Morocco aondolewa](https://spotileo.co.tz/mwamuzi-wa-stars-mechi-ya-morocco-aondolewa/) - RABAT:SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemuondoa mwamuzi wa kimataifa wa Mali, Boubou Traoré, katika orodha ya watakaosalia kuchezesha mechi zilizobaki za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 zinazoendelea nchini Morocco. Mbali na Traoré, mwamuzi mwingine aliyeripotiwa kuondolewa ni Abdou Abdel Medire kutoka Cameroon aliyechezesha mechi ya hatua ya 16 bora kati ya - [Usiogope hapana ya Mungu– Miriam Mauki](https://spotileo.co.tz/usiogope-hapana-ya-mungu-miriam-mauki/) - DAR ES SALAAM:MWIMBAJI wa nyimbo za Injili nchini Tanzania, Miriam Mauki, amesema kuwa mara nyingi kile ambacho binadamu hukiona kama hapana kutoka kwa Mungu, huwa ndicho jibu sahihi na salama kwa wakati husika. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mauki aliwaasa waumini na mashabiki wake kumruhusu Mungu abaki kuwa Mungu, hata pale ambapo majibu yao ya - [Azam, Yanga yasaka historia mpya Mapinduzi Cup](https://spotileo.co.tz/azam-yanga-yasaka-historia-mpya-mapinduzi-cup/) - PEMBA:MABINGWA watarajiwa wa Kombe la Mapinduzi 2026 watapatikana leo jioni saa 10:30, wakati vigogo wa soka nchini Azam FC na Yanga SC watakapovaana kwenye fainali ya michuano hiyo itakayopigwa katika Uwanja wa Gombani, Pemba. Ni fainali yenye historia yake, kwani kwa mara ya kwanza tangu Kombe la Mapinduzi lilipoanza kushirikisha timu kutoka nje ya Zanzibar, - [Carrick kuibeba United hadi mwisho wa msimu](https://spotileo.co.tz/carrick-kuibeba-united-hadi-mwisho-wa-msimu/) - MANCHESTER:MANCHESTER United wamethibitisha rasmi kumteua Michael Carrick kuwa kocha wa muda wa kikosi cha kwanza hadi msimu utakapomalizika. Carrick anachukua nafasi hiyo baada ya Darren Fletcher aliyekuwa anakaimu kwa muda mfupi kufuatia kufutwa kazi kwa Ruben Amorim wiki iliyopita. Carrick, ambaye pia alikuwa akiwania nafasi hiyo na Ole Gunnar Solskjaer, amechaguliwa kutokana na uzoefu wake - [Okello: Nina furaha kuwa Mwananchi](https://spotileo.co.tz/okello-nina-furaha-kuwa-mwananchi/) - DAR ES SALAAM: MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga SC, Allan Okello, amesema ana furaha kubwa kujiunga na klabu hiyo huku akisisitiza kuwa yuko tayari kupigania mafanikio ya timu. Kupitia ujumbe wake mfupi aliouandika kwenye mitandao ya kijamii mara baada ya kutambulishwa rasmi, Okello alisema: “Nina furaha kuwa Mwananchi. Daima mbele, nyuma mwiko,” akiambatanisha na alama ya - [Real Madrid yaachana na Alonso](https://spotileo.co.tz/real-madrid-yaachana-na-alonso/) - MADRID:REAL Madrid wametangaza kuachana na kocha Xabi Alonso kwa makubaliano ya pande zote, siku moja tu baada ya kupoteza fainali ya Spanish Super Cup kwa kufungwa mabao 3-2 na wapinzani wao wakubwa Barcelona. Taarifa ya klabu imesema Alonso ataendelea kubaki kuwa sehemu ya familia ya Real Madrid, lakini safari yake kama kocha wa kikosi cha - [Arbeloa kocha mpya Real Madrid](https://spotileo.co.tz/arbeloa-kocha-mpya-real-madrid/) - MADRID:REAL Madrid wamemtangaza rasmi Alvaro Arbeloa kuwa kocha mpya wa kikosi cha kwanza, akichukua nafasi ya Xabi Alonso aliyeondoka kwa makubaliano ya pande zote. Arbeloa amepandishwa kutoka timu ya akiba (Castilla), hatua inayomrudisha rasmi kwenye jukwaa kubwa la klabu aliyotumikia kwa mafanikio makubwa akiwa mchezaji. Arbeloa amekuwa kocha wa Castilla tangu Juni 2025, na kabla - [Hansi Flick:Fainali 8, makombe 8](https://spotileo.co.tz/hansi-flickfainali-8-makombe-8/) - JEDDAH:HANSI Flick anaendelea kujijengea heshima ya kipekee kwenye dunia ya soka, hasa linapokuja suala la fainali. Popote anapofika, akifika hatua ya mwisho, mara nyingi hadithi huwa ile ile,Flick anatoka na kombe. Kocha huyo sasa ameweka rekodi ya kushangaza baada ya kushinda fainali nane kati ya nane alizowahi kusimamia katika maisha yake ya ukocha. Ushindi wake - [Umuhimu wa Raphinha Barcelona haupimiki](https://spotileo.co.tz/umuhimu-wa-raphinha-barcelona-haupimiki/) - JEDDAH:KAMA bado kulikuwa na mtu anajiuliza Raphinha ana umuhimu gani ndani ya Barcelona, basi majibu yako wazi kabisa. Tangu arejee kwenye kikosi cha kwanza baada ya kupona maumivu ya misuli ya paja, Barca imegeuka mashine ya ushindi, ikipeleka kibindoni mechi zote wanazocheza. Takwimu zinasema kila kitu. Barcelona imeshinda mechi zote 10 mfululizo tangu Raphinha aliporudi - [Alonso:Kombe lile halikuwa na umuhimu mkubwa kwetu](https://spotileo.co.tz/alonsokombe-lile-halikuwa-na-umuhimu-mkubwa-kwetu/) - JEDDAH:BAADA ya kupoteza fainali ya Super Cup dhidi ya Barcelona, kocha Xabi Alonso amesema wazi kuwa kwa mtazamo wake, hilo lilikuwa shindano lisilo na uzito mkubwa ukilinganisha na mengine wanayoshiriki msimu huu. Akizungumza baada ya mechi hiyo ngumu na yenye ushindani mkubwa, Alonso ameonesha kutokukatishwa tamaa na matokeo, akisisitiza kuwa timu yake inapaswa kufunga ukurasa - [Mafia boxing yafungua milango kwa mabondia](https://spotileo.co.tz/mafia-boxing-yafungua-milango-kwa-mabondia/) - DAR ES SALAAM:PROMOTA wa ngumi za kulipwa, Ally Zayumba, amesema fursa zipo wazi kwa mabondia kutoka mikoa mbalimbali nchini wanaotaka kusimamiwa chini ya Mafia Boxing, akibainisha kuwa kipaumbele kikubwa ni nidhamu, mapenzi ya dhati kwa mchezo wa ngumi na kujitoa kikamilifu. Katika mazungumzo na SpotiLeo Zayumba amesema Mafia Boxing imejipanga kuibua vipaji vipya na kuvilea - [Timu ya kriketi U19 waichapa Japan](https://spotileo.co.tz/timu-ya-kriketi-u19-waichapa-japan/) - TIMU ya Taifa ya kriketi ya vijana chini ya umri wa miaka 19 (Tanzania U19) imeshinda mchezo wa Kimataifa wa kirafiki wa maandalizi ya Kombe la Dunia dhidi ya Japan U19 kwa mikimbio 81. Tanzania iliweka alama mapema baada ya kukusanya mikimbio 204 kwa kupoteza wiketi tisa katika overs 50, ikionesha ubora wa kupiga mpira - [Lulu Diva:Whozu si mpenzi wangu, ni rafiki yangu tu](https://spotileo.co.tz/lulu-divawhozu-si-mpenzi-wangu-ni-rafiki-yangu-tu/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva Lulu Abas ‘Lulu Diva’ ameweka wazi msimamo wake kuhusu urafiki wake na msanii Whozu, ambaye aliwahi kuwa mpenzi wa Wema Sepetu, akikanusha vikali madai yanayosambaa mitandaoni kuwa amemsaliti rafiki yake kwa kuanzisha mahusiano ya kimapenzi na Whozu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Lulu Diva amesema anasikitishwa na namna - [Dayna Nyange avunja ukimya:](https://spotileo.co.tz/dayna-nyange-avunja-ukimya/) - DAR ES SALAAM: MREMBO anayetikisa anga la muziki wa Bongo Fleva, Dayna Nyange, hatimaye amevunja ukimya wake na kuweka wazi maisha yake ya mapenzi, baada ya tetesi nyingi kusambaa mitandaoni. Daina amewathibitishia mashabiki kuwa yupo kwenye penzi zito, ambalo wengi wameanza kuliita “penzi kilo 150”, baada ya kuchapisha picha mpya akiwa na mpenzi wake kupitia - [Elia Mtishibi, Boaz Danken kupamba ‘The Night of Revelation 2026’](https://spotileo.co.tz/elia-mtishibi-boaz-danken-kupamba-the-night-of-revelation-2026/) - DAR ES SALAAM: WAIMBAJI maarufu wa nyimbo za Injili nchini, Boaz Danken na Elia Mtishibi, wanatarajiwa kuwa miongoni mwa waimbaji watakaopamba Mkesha wa Vijana wa Kusifu na Kuabudu unaojulikana kama “The Night of Revelation 2026”, utakaofanyika Januari 16, 2026 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Mabibo External. Mkesha huo unakwenda sambamba - [Bongo Star Search msimu wa 16 kuanza rasmi Februari 7](https://spotileo.co.tz/bongo-star-search-msimu-wa-16-kuanza-rasmi-februari-7/) - DAR ES SALAAM:MASHINDANO makubwa ya kusaka vipaji nchini, Bongo Star Search (BSS) Msimu wa 16, yanatarajiwa kuanza rasmi Februari 7 na 8, 2026 katika Ukumbi wa La Kairo Hotel, jijini Mwanza, baada ya kuahirishwa kwa muda. Akizungumza na waandishi wa habari Januari 9, 2027, Mkurugenzi wa Bench Mack, Madam Rita Paulsen, amesema mashindano hayo yalisitishwa - [Prince Dube mchezaji bora wa Yanga mwezi Desemba](https://spotileo.co.tz/prince-dube-mchezaji-bora-wa-yanga-mwezi-desemba/) - DAR ES SALAAM: MSHAMBULIAJI wa Yanga SC, Prince Dube, ameibuka mchezaji bora wa klabu hiyo kwa mwezi Desemba, tuzo inayodhaminiwa na NIC Insurance, baada ya kuonesha kiwango bora na mchango mkubwa katika michuano ya Ligi Kuu na Ile ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Dube alichaguliwa kufuatia mwendelezo wa kiwango chake kizuri cha ufungaji, kujituma uwanjani - [Semenyo atua Man City](https://spotileo.co.tz/semenyo-atua-man-city/) - MANCHESTER:KLABU ya Manchester City imefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa Ghana, Antoine Semenyo, kutoka Bournemouth ili kuongeza nguvu kwenye safu yao ya ushambuliaji kabla ya msimu wa EPL na UCL kumalizika.City imemsajili mchezaji huyo kwa mkataba wa miaka mitano na nusu na atavaa jezi namba 42, namba iliyowahi kuvaliwa na mkongwe Yaya Toure. Semenyo, mwenye umri wa - [Unai Simon aendelea kumkosha kocha Spain](https://spotileo.co.tz/unai-simon-aendelea-kumkosha-kocha-spain/) - BILBAO:GOLIKIPA Unai Simón anaendelea kujiweka juu ya wenzake wote ndani ya timu ya taifa ya Hispania, huku akionekana kuwa chaguo la kwanza la kocha Luis de la Fuente kuelekea Kombe la Dunia 2026, licha ya Uhispania kuwa na kizazi kingine hatari cha magolikipa. Tangu aitwe kwenye kikosi cha taifa mwaka 2020, Simón amekuwa namba moja - [Ndidi:Wasipolipa posho nitawalipa mimi](https://spotileo.co.tz/ndidiwasipolipa-posho-nitawalipa-mimi/) - RABAT:NAHODHA wa Nigeria, Wilfred Ndidi, ameamua kubeba jukumu zito ndani ya timu ya taifa baada ya kutangaza kuwa yuko tayari kulipa mwenyewe bonasi za wachezaji na benchi la ufundi iwapo Shirikisho la Soka Nigeria (NFF) litashindwa kufanya hivyo kabla ya robo fainali ya AFCON dhidi ya Algeria. Ndidi amesema tayari amekuwa akihamasisha kikosi kizima kuacha - [Mutimawangu awasili Tanzania](https://spotileo.co.tz/mutimawangu-awasili-tanzania/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa kwanza wa kike kutoka lebo ya Kings Music Records, Mutimawangu, amewasili nchini Tanzania akitokea nchini Rwanda, ambapo kwa mara ya kwanza tangu atue amezungumza na waandishi wa habari kueleza hisia zake baada ya kutambulishwa rasmi kama msanii mpya wa lebo hiyo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mutimawangu - [Alikiba: Mutimawangu yuko huru kufanya kazi na msanii yeyote](https://spotileo.co.tz/alikiba-mutimawangu-yuko-huru-kufanya-kazi-na-msanii-yeyote/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa Bongo Fleva, Ali Kiba, amesema msanii wake mpya, Mutimawangu, yuko huru kufanya kazi na msanii yeyote mwenye uwezo mzuri wa kuimba, ilimradi makubaliano yatakayofikiwa yawe na maslahi kwa pande zote. Amesisitiza kuwa lebo yake ya Kings Music haina mipaka ya ushirikiano, bali inalenga kukuza vipaji na kutoa uhuru wa ubunifu kwa - [Wema Sepetu-Mimi si wa kwanza kukosa mtoto](https://spotileo.co.tz/wema-sepetu-mimi-si-wa-kwanza-kukosa-mtoto/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa filamu nchini, Wema Sepetu, amewaomba mashabiki wake kuacha kumhurumia kuhusu suala la kukosa mtoto, akisema si yeye wa kwanza kupitia hali hiyo na anataka mjadala uelekezwe kwenye mambo mengine ya maisha. Kupitia ukurasa wake wa Snapchat, Wema amechapisha ujumbe akieleza wazi msimamo wake na kusema tayari amekubali hali hiyo na kufanya - [Tuzo za Tamasha la Filamu Tanzania kufanyika Februari 14](https://spotileo.co.tz/tuzo-za-tamasha-la-filamu-tanzania-kufanyika-februari-14/) - DAR ES SALAAM:TUZO za Tamasha la Filamu Tanzania (Tanzania Film Festival Awards) zinatarajiwa kufanyika Februari 14, 2016 katika ukumbi wa The Super Dome, uliopo Masaki jijini Dar es Salaam. Akizungumza wakati wa kutangaza vipengele vya tuzo hizo, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Gervas Kasiga, alisema kuwa tuzo hizo zinatarajiwa kuacha alama kubwa katika - [Boaz Danken kupamba The Night of Revelation 2026](https://spotileo.co.tz/boaz-danken-kupamba-the-night-of-revelation-2026/) - DAR ES SALAAM:MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za Injili nchini, Boaz Danken, anatarajiwa kuwa miongoni mwa waimbaji watakaopamba mkesha wa vijana wa kusifu na kuabudu unaojulikana kama 'The Night of Revelation 2026', utakaofanyika Januari 16, 2026 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Mabibo External. Mkesha huo unakwenda sambamba na kaulimbiu isemayo “New - [Amshaamsha za mashabiki mapokezi Stars](https://spotileo.co.tz/amshaamsha-za-mashabiki-mapokezi-stars/) - DAR ES SALAAM: AMSHAAMSHA za mashabiki Uwanja wa Ndege ya Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, ambako timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inatarajiwa kuwasili Dar es Salaam asubuhi hii, ikitokea nchini Morocco ambako ilikwenda kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025). - [Watanzania wajitokeza kuipokea Stars](https://spotileo.co.tz/watanzania-wajitokeza-kuipokea-stars/) - DAR ES SALAAM:SHAMRASHAMRA za mashabiki wa Taifa Stars waliokuja Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere kuwapokea Taifa Stars wanaorudi Leo kutoka Morocco walikokuwa wanashiriki michuano ya mataifa ya Afrika Afcon ambapo walitolewa hatua ya 16 bora. - [Mac Allister aanika ya moyoni kuhusu Liverpool](https://spotileo.co.tz/18881-2/) - LIVERPOOL:KIUNGO wa Liverpool, Alexis Mac Allister, amekiri wazi kuwa matumaini ya timu yake kutetea ubingwa wa Ligi Kuu England yanaonekana kuyeyuka, akisema kwa sasa haoni kabisa dalili za Liverpool kurejea kileleni msimu huu. Akizungumza kwa huzuni, Mac Allister amesema ni vigumu kukubali lakini uhalisia unaonesha wazi kuwa nafasi ya Liverpool kubeba tena taji ni ndogo - [Neila Manga aanzisha kampeni ya “Freedom For Men”](https://spotileo.co.tz/neila-manga-aanzisha-kampeni-ya-freedom-for-men/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa vichekesho nchini, Neila Manga, ametangaza kuanzisha kampeni maalum ya kuwatetea wanaume ili wapate uhuru wao katika jamii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Neila Manga alichapisha video akieleza rasmi kuanzishwa kwa kampeni hiyo aliyoiita “Freedom for Men”, yenye lengo la kusimamia haki na nafasi ya mwanaume katika familia na jamii kwa ujumla. - [Kiasi cha pesa walichotumia United kwa Amorim](https://spotileo.co.tz/kiasi-cha-pesa-walichotumia-united-kwa-amorim/) - MANCHESTER:SAA chache tu baada ya kufutwa kazi na Manchester United, Ruben Amorim alionekana akitembea taratibu huku akiwa anatabasamu na kufurahi pamoja na mke wake, Maria, tukio lililogusa hisia za wengi mitandaoni. Hata hivyo, nje ya picha za furaha, utekelezaji wa uamuzi wa klabu umewalazimisha United kukabili bili kubwa ya kifedha kutokana na kusitisha mkataba wake. - [Chelsea yamtangaza kocha mpya](https://spotileo.co.tz/chelsea-yamtangaza-kocha-mpya/) - LONDON:KLABU ya Chelsea imemtangaza rasmi Liam Rosenior kama kocha mkuu mpya wa timu hiyo, akitia saini mkataba wa miaka sita utakaomweka Stamford Bridge hadi mwaka 2032. Rosenior mwenye umri wa miaka 41 anachukua nafasi ya Enzo Maresca aliyeondoka Chelsea siku ya Mwaka Mpya. Kupitia taarifa yao, Chelsea wamesema msisitizo utaendelea kuwa kwenye kukuza na kuendeleza - [Enzo Maresca na Chelsea sasa basi!](https://spotileo.co.tz/enzo-maresca-na-chelsea-sasa-basi/) - LONDON:ENZO Maresca ameondoka rasmi Chelsea baada ya uongozi wa klabu na kocha huyo wa Italia kufikia makubaliano ya pande zote kuvunja ushirikiano wao, kufuatia matokeo mabaya na mvutano wa ndani uliodumu kwa muda. Maamuzi hayo yamethibitishwa na Chelsea siku ya Mwaka Mpya, wakisema mabadiliko hayo yamelenga kuipa timu nafasi bora ya kurekebisha msimu. Maresca anakumbukwa - [Goti lamuweka Victor Boniface matatani](https://spotileo.co.tz/goti-lamuweka-victor-boniface-matatani/) - BREMEN:TAARIFA zinaeleza kuwa Werder Bremen na Bayer Leverkusen wamekubaliana kuwa mshambuliaji wa Nigeria, Victor Boniface, atalazimika kufanyiwa upasuaji mwingine wa goti, hali inayoweka hatarini mustakabali wa maisha yake ya soka. Boniface, mwenye umri wa miaka 25, ameripotiwa kuwa na uharibifu mkubwa wa goti ambao hauwezi kurekebishwa kirahisi, jambo lililowafanya madaktari kupendekeza afanyiwe operesheni nyingine. Kwa - [Serikali ya Gabon yaisimamisha timu ya taifa](https://spotileo.co.tz/serikali-ya-gabon-yaisimamisha-timu-ya-taifa/) - RABAT:SERIKALI ya Gabon imetangaza kuisimamisha kwa muda timu ya taifa, kumfuta kazi kocha pamoja na kuwaondoa kwenye kikosi wachezaji wakubwa akiwemo Pierre-Emerick Aubameyang, baada ya timu hiyo kufanya vibaya kwenye fainali za Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) zinazoendelea Morocco. Tangazo hilo limetolewa na Waziri wa Michezo wa Gabon, Simplice-Desire Mamboula, kupitia televisheni ya taifa, baada - [Mama Lisa ampongeza Professor Jay kutimiza miaka 50](https://spotileo.co.tz/mama-lisa-ampongeza-professor-jay-kutimiza-miaka-50/) - DAR ES SALAAM:MKE wa msanii wa Hip Hop Joseph Haule maarufu kama Professor Jay, anayefahamika kwa jina la Mama Lisa, amempongeza mume wake kwa kutimiza umri wa miaka 50, akieleza upendo wake mkubwa, shukrani na imani yake kwa Mungu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mama Lisa aliandika ujumbe maalumu wa kumtakia heri ya siku ya - [Harmonize na Kajala warudiana tena](https://spotileo.co.tz/harmonize-na-kajala-warudiana-tena/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Rajab Abdul maarufu Harmonize, na mpenzi wake Frida Kajala, wamezua gumzo kubwa baada ya kurudiana tena na kuvishana pete ya uchumba kwa mara ya pili, hatua iliyorejesha matumaini mapya kwa mashabiki wao. Harmonize na Kajala waliwahi kuvishana pete ya uchumba mwaka 2022, lakini kabla ya kufikia - [Irene Uwoya atangaza kutubu na kuanza maisha mapya](https://spotileo.co.tz/irene-uwoya-atangaza-kutubu-na-kuanza-maisha-mapya/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Irene Uwoya, ameomba msamaha kwa Mungu baada ya kukiri kukosea katika mawazo, maneno na matendo yake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, muigizaji huyo maarufu nchini Tanzania alichapisha ujumbe wenye kuonesha unyenyekevu na majuto makubwa akisema: “Mungu naomba unisamehe (GOD please forgive me)… nimekosa sana kwa - [Dogo Paten aomba msamaha kwa aliyemkosea](https://spotileo.co.tz/dogo-paten-aomba-msamaha-kwa-aliyemkosea/) - DAR ES SALAAM:MSANII maarufu wa muziki wa Singeli, Dogo Paten, ameomba msamaha kwa mtu yeyote aliyemkosea kwa namna yoyote ile, huku akihimiza amani na upendo kuelekea mwishoni mwa mwaka. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo amesema kuwa kama binadamu si mkamilifu na huenda kwa makusudi au bila kukusudia aliwakwaza watu katika kipindi cha mwaka - [Dulla Makabila awekeza Milioni 20 kwenye video](https://spotileo.co.tz/dulla-makabila-awekeza-milioni-20-kwenye-video/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa muziki wa Singeli na Bongo Fleva, Dulla Makabila, amesema ameandika historia mpya katika kazi yake ya muziki baada ya kutumia kiasi cha Sh milioni 20 kwa ajili ya kutengeneza video ya wimbo mmoja. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo amesema hiyo ni mara ya kwanza kwake kutumia bajeti kubwa kiasi - [PSG yatawala usiku wa tuzo za Globe Soccer](https://spotileo.co.tz/psg-yatawala-usiku-wa-tuzo-za-globe-soccer/) - DUBAI:USIKU wa jana Jumapili, Desemba 28, 2025, macho ya dunia ya soka yalikuwa Dubai ambako tuzo za Globe Soccer zilitolewa, na Paris Saint-Germain (PSG) ikaondoka kifua mbele baada ya kufanya vizuri kupita kiasi. PSG, ambayo ilimaliza mwaka 2025 kwa kutwaa mataji sita ikiwemo Ligi ya Mabingwa Ulaya, ilikusanya jumla ya tuzo saba na kuthibitisha ubora - [Pogba abeba tuzo baada ya kipindi kigumu](https://spotileo.co.tz/pogba-abeba-tuzo-baada-ya-kipindi-kigumu/) - DUBAI:KIUNGO wa Ufaransa Paul Pogba ametwaa tuzo ya 'Best Comeback' kwenye hafla ya Globe Soccer Awards 2025, baada ya kurejea tena uwanjani kufuatia kipindi kigumu nje ya soka. Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Pogba alisema safari yake haikuwa rahisi hata kidogo, lakini ilimfundisha kutambua watu waliokuwa karibu naye kwa dhati wakati hakuwa tena kwenye - [Yamal ang'ara tuzo za Globe Soccer](https://spotileo.co.tz/yamal-angara-tuzo-za-globe-soccer/) - DUBAI:FC Barcelona na Paris Saint-Germain ndizo klabu zilizotawala tuzo za Globe Soccer Awards zilizofanyika Dubai, huku macho yote yakielekezwa kwa kinda wa Barcelona, Lamine Yamal, aliyeibuka nyota wa usiku huo. Yamal, ambaye bado ni kijana mdogo , alikusanya tuzo tatu kubwa ambazo ni Mchezaji Bora wa chini ya umri wa miaka 23 LaLiga, Mshambuliaji Bora - [Usimchukie aliyekutangulia, jifunze kwake – Gabo Zigamba](https://spotileo.co.tz/usimchukie-aliyekutangulia-jifunze-kwake-gabo-zigamba/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa Bongo Movie, Gabo Zigamba, amewataka watu kuacha chuki kwa wale waliowatangulia katika maisha au taaluma zao, badala yake wawachukulie kama mfano wa kujifunza ili kufikia mafanikio makubwa zaidi. Gabo ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram, ambapo amesema mtu aliyekutangulia hapaswi kuchukiwa, bali atumike kama darasa la kukuza maarifa na - [Zuchu amshukuru Shamira kwa upendo wa dhati](https://spotileo.co.tz/zuchu-amshukuru-shamira-kwa-upendo-wa-dhati/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa Bongo Fleva nchini, Zuhura Othuman 'Zuchu', ameonesha hisia zake za dhati kwa rafiki yake Shamira, mke wa meneja wake, Kim Kyando akimtaja kuwa ni miongoni mwa watu wachache wanaomjali na kumpenda bila kutarajia faida yoyote. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Zuchu ameweka wazi namna Shamira alivyo mtu wa pekee - [Hamadi Kikala: Ndoto ya soka iliyoishia jukwaa la uigizaji](https://spotileo.co.tz/hamadi-kikala-ndoto-ya-soka-iliyoishia-jukwaa-la-uigizaji/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa filamu za Kitanzania, John Elisha maarufu kama Boneka na anayefahamika pia kwa jina la Hamadi Kikala, amesema kuwa ndoto yake ya awali haikuwa uigizaji bali ilikuwa ni kuwa mchezaji wa mpira wa miguu wa kulipwa. Akizungumza kuhusu safari ya maisha yake, Hamadi amesema kuwa aliwahi kuwa na ndoto kubwa ya kuitegemea - [Inspector Haroun kufanya kazi na Jux](https://spotileo.co.tz/inspector-haroun-kufanya-kazi-na-jux/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa muziki anayefahamika kwa jina la Haroun Rashid ‘Inspector Haroun Babu’ ameweka wazi matarajio yake ya kuendelea kufanya kazi na wasanii mbalimbali wanaofanya vizuri katika muziki wa Bongo Fleva kwa sasa. Akizungumza na SpotiLeo, Inspector Haroun Babu amesema tayari ana miradi kadhaa ya muziki inayoendelea, huku mingine ikiwa tayari imekamilika. Miongoni mwa - [Ambwene Mwasongwe awapa ujumbe wa tumaini mashabiki](https://spotileo.co.tz/ambwene-mwasongwe-awapa-ujumbe-wa-tumaini-mashabiki/) - DAR ES SALAAM:MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili Tanzania, Ambwene Mwasongwe, amewapa ujumbe wa faraja na matumaini mashabiki wake akisisitiza umuhimu wa kumtegemea Mungu katika kila hatua ya maisha. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ambwene ameandika ujumbe wenye kugusa nyoyo za wengi akisema kuwa bila msaada wa Mungu hakuna binadamu anayeweza kusaidia kwa ukamilifu, lakini - [Inspector Haroun aachia nyimbo mbili mpya](https://spotileo.co.tz/inspector-haroun-aachia-nyimbo-mbili-mpya/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Haroun Rashidi maarufu kama ‘Inspector Haroun Babu’, ameendelea kudhihirisha uimara wake katika tasnia ya muziki baada ya kuachia nyimbo mbili mpya zenye majina “AI” na “Maisha Ndo Haya Haya.” Inspector Haroun Babu ameeleza kuwa wimbo wa “AI” ameutoa kwa mfumo wa audio pekee, huku wimbo wa “Maisha - [Wastara: Umaskini ni kitu kibaya na chakudhalilisha](https://spotileo.co.tz/wastara-umaskini-ni-kitu-kibaya-na-chakudhalilisha/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa filamu nchini, Wastara Juma, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kueleza kwa hisia kali namna umaskini unavyoweza kumdhalilisha mtu na kumfanya ajisikie kutengwa katika jamii. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Wastara ameandika ujumbe mrefu akieleza machungu anayoyaona au kuyashuhudia yanayoletwa na hali ngumu ya maisha. Amesema kuwa licha ya - [Msuva: Kuna kitu kitatokea dhidi ya Nigeria](https://spotileo.co.tz/msuva-kuna-kitu-kitatokea-dhidi-ya-nigeria/) - RABAT: WINGA wa Taifa Stars, Simon Msuva, ameibua matumaini kwa Watanzania kuelekea mchezo wa kwanza wa Kundi C wa Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) leo usiku dhidi ya Nigeria, akisisitiza kuwa pamoja na ukubwa wa mpinzani, kuna kitu kizuri kitatokea. Akizungumza kuelekea mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa saa 2:30 usiku kwenye Uwanja wa Fez, Morocco, - [Yanga Princess yapanda mlima kwa kasi](https://spotileo.co.tz/yanga-princess-yapanda-mlima-kwa-kasi/) - DAR ES SALAAM: MSIMAMO wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania umebadilika kwa kasi baada ya mechi za jana, huku Yanga Princess ikiibuka kinara mpya wa ligi baada ya ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Geita Queens. Ushindi huo umeiwezesha Yanga kupanda hadi nafasi ya kwanza kwa pointi 12, ikitimiza ushindi wa mechi zote nne - [Dube: hatujakata tamaa, tutajaribu tena](https://spotileo.co.tz/dube-hatujakata-tamaa-tutajaribu-tena/) - RABAT: MSHAMBULIAJI wa timu ya Taifa ya Zimbabwe, Prince Dube, amesema kikosi hicho hakitakata tamaa licha ya kuanza vibaya fainali za Afrika baada ya kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Misri katika mchezo wa kwanza wa Kundi B uliochezwa jana nchini Morocco. Akizungumza kupitia ujumbe aliouandika baada ya mchezo huo, Dube alisema: “Imekuwa ni Mungu - [Maresca akanusha kuitaka Man City](https://spotileo.co.tz/maresca-akanusha-kuitaka-man-city/) - LONDON: KOCHA wa Chelsea Enzo Maresca amezima kabisa tetesi zinazomuhusisha na nafasi ya ukocha Manchester City, akisema uvumi huo haumtikisi hata kidogo na bado amejikita kikamilifu kuitumikia klabu ya Chelsea. Maresca, ambaye aliwahi kufanya kazi kama kocha msaidizi Manchester City, alijiunga na Chelsea mwaka 2024 na mara moja akaacha alama baada ya kuiongoza klabu hiyo - [Salah, Slot 'wamemalizana'](https://spotileo.co.tz/salah-slot-wamemalizana/) - LIVERPOOL: KOCHA wa Liverpool Arne Slot amesema hakuna tena mvutano kati yake na mshambuliaji wa klabu hiyo Mohamed Salah, akisisitiza kuwa wawili hao wamemaliza tofauti zao baada ya mshambuliaji huyo kuikosoa klabu hadharani hivi karibuni. Akizungumza leo Ijumaa kuelekea mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Tottenham Hotspur utakaochezwa kesho Jumamosi, Slot amesema suala hilo - [Kakuta akutana na zali DRC](https://spotileo.co.tz/kakuta-akutana-na-zali-drc/) - KINSHASA: TIMU ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imemuita kikosini kiungo Gael Kakuta kuchukua nafasi ya Mario Stroeykens aliyeondolewa kwenye kikosi cha Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) kutokana na jeraha. Kakuta mwenye umri wa miaka 34, aliyewahi kutambulika kama kipaji kikubwa alipokuwa kijana katika klabu ya Chelsea, kwa sasa anacheza soka - [Ni Messi Vs Yamal ‘Finalissima’ 2026](https://spotileo.co.tz/ni-messi-vs-yamal-finalissima-2026/) - DOHA: SHIRIKISHO la Soka Ulaya (UEFA) limetangaza kuwa Mabingwa wa Ulaya, timu ya Taifa ya Hispania watakutana na mabingwa wa Copa America timu ya Taifa ya Argentina katika mchezo wa ‘Finalissima’ utakaochezwa nchini Qatar mwezi Machi mwaka ujao. Mchezo huo unaowakutanisha mabingwa wa mabara mawili ulirejeshwa mwaka 2021 baada ya UEFA na Shirikisho la Soka - [Kimeeleweka, Milan V Como kupigwa Australia](https://spotileo.co.tz/kimeeleweka-milan-v-como-kupigwa-australia/) - MILAN: RAIS wa Serie A Ezio Simonelli amethibitisha kuwa mechi ya Serie A kati ya AC Milan na Como iliyopangwa kuchezwa mjini Perth nchini Australia, mwezi Februari mwakani itaendelea kama ilivyopangwa. Kauli hiyo inakuja baada ya ripoti za vyombo vya habari vya Italia wiki iliyopita kudai kuwa mchezo huo ulikuwa hatarini kuahirishwa, kufuatia wasiwasi wa - [Hojlund ashiriki kikamilifu ‘maangamizi’ ya AC Milan](https://spotileo.co.tz/hojlund-ashiriki-kikamilifu-maangamizi-ya-ac-milan/) - RIYADH: MSHAMBULIAJI wa Napoli Rasmus Hojlund alikuwa mhimili muhimu wa ushindi baada ya kuisaidia timu yake kuifunga AC Milan mabao 2-0 katika nusu fainali ya Super Cup ya Italia Alhamisi usiku. Mchezaji huyo raia wa Denmark alihusika moja kwa moja katika mabao yote mawili, akitengeneza bao la kwanza kipindi cha kwanza kabla ya kufunga mwenyewe - [Morocco yaenda AFCON na kombe](https://spotileo.co.tz/morocco-yaenda-afcon-na-kombe/) - LUSAIL: TIMU ya Taifa ya Morocco imetwaa ubingwa wa Kombe la Nchi za Kiarabu baada ya kuifunga Jordan mabao 3-2, kwa msaada wa mabao mawili ya Abderrazzaq Hamed Allah yaliyofuata bao la kusisimua la mbali la Oussama Tannane. Morocco ilianza vyema mchezo huo kwa kupata bao mapema dakika ya nne, Tannane akifunga kwa shuti la - [Haller mguu nje, mguu ndani AFCON 2025](https://spotileo.co.tz/haller-mguu-nje-mguu-ndani-afcon-2025/) - RABAT: MSHAMBULIAJI Sebastien Haller, aliyefunga bao muhimu lililoipa Ivory Coast taji la Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) lililopita, yupo hatarini kukosa michuano ya mwaka huu nchini Morocco kutokana na majeraha. Haller alipata jeraha la msuli wa paja (hamstring) alipokuwa akiichezea klabu ya Utrecht katika ligi ya Uholanzi mwishoni mwa wiki, na tangu ajiunge na - [Makonda kuongoza kambi ya Taifa Stars AFCON Morocco](https://spotileo.co.tz/makonda-kuongoza-kambi-ya-taifa-stars-afcon-morocco/) - CAIRO: NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, atakuwa sehemu ya viongozi wa kambi ya Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, itakayokuwa nchini Morocco katika maandalizi na ushiriki wa Michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) itakayoanza Desemba 21 mwaka huu. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi, amesema - [Hamadi Furahisha atuma salamu kwa Mmalawi](https://spotileo.co.tz/hamadi-furahisha-atuma-salamu-kwa-mmalawi/) - DAR ES SALAAM: BONDIA Hamadi Furahisha amewaahidi Watanzania ushindi mnono dhidi ya mpinzani wake Hannock Phiri wa Malawi katika pambano litakalopigwa Desemba 26, 2025 Dar es Salaam. Akizungumza mapema leo Yombo Dovya Dar es Salaam, Furahisha amesema anatambua ubora na hatari ya mpinzani wake ambaye ameshawapiga mabondia kadhaa wa Tanzania bila kupigwa, lakini safari hii - [Yanga warejea mazoezini, macho yote kimataifa](https://spotileo.co.tz/yanga-warejea-mazoezini-macho-yote-kimataifa/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Yanga SC imerejea mazoezini leo kuanza maandalizi ya awamu ya kwanza, ambapo itafanya mazoezi kwa wiki moja kabla ya kuingia mapumziko mafupi. Baada ya hapo, kikosi hicho kinatarajiwa kurejea tena kambini tarehe 29, mara baada ya wachezaji wote waliokuwa na majukumu mbalimbali kurejea, ili kuingia kwenye maandalizi mazito zaidi. Kwa - [Vigogo washika usukani Ligi Kuu Wanawake](https://spotileo.co.tz/vigogo-washika-usukani-ligi-kuu-wanawake/) - DAR ES SALAAM: BAADA ya michezo ya wikiendi, timu kubwa za Ligi Kuu ya Wanawake zimeanza kuonesha makucha yao, huku ushindani ukiwa mkali kileleni mwa msimamo wa ligi. JKT Queens, Simba Queens na Yanga Princess, ambazo ni miongoni mwa vigogo wa soka la wanawake nchini, zinaungana kileleni zikiwa na pointi sita, sambamba na Alliance Girls. - [Mabula atua Misri kuongeza nguvu Stars](https://spotileo.co.tz/mabula-atua-misri-kuongeza-nguvu-stars/) - CAIRO: KIUNGO mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania, Alphonce Mabula, amewasili nchini Misri kuungana na wenzake wa Taifa Stars kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON). Mabula anajiunga na kikosi hicho akiwa katika kiwango kizuri, baada ya kuifungia bao timu yake ya FC Shamakhi katika mchezo - [Aziz Ki: Wengi hawamjui Hamisa Mobetto wa ndani](https://spotileo.co.tz/aziz-ki-wengi-hawamjui-hamisa-mobetto-wa-ndani/) - DAR ES SALAAM: MCHEZAJI wa mpira wa miguu, Stephen Aziz Ki, amesema kuwa taswira inayowafanya baadhi ya watu kumhukumu mke wake, mwanamitindo Hamisa Mobetto, si kielelezo halisi cha maisha yake ya ndani. Aziz Ki amesema kuwa watu wengi humtazama Hamisa kupitia picha na maudhui yanayosambaa kwenye mitandao ya kijamii na kudhani kuwa ndivyo alivyo hata - [Billnass ampamba Nandy zawadi zaidi ya Dola 20,000](https://spotileo.co.tz/billnass-ampamba-nandy-zawadi-zaidi-ya-dola-20000/) - DAR ES SALAAM:MSANII wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, William Lyimo maarufu kama Billnass, amemnunulia mke wake Faustina Mfinanga ‘Nandy’ zawadi zenye thamani ya zaidi ya Dola 20,000 za Kimarekani, sawa na takribani sh. milioni 69 za Kitanzania. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nandy ameposti video akionesha zawadi alizopokea kutoka kwa mume wake, jambo - [Rosey Manfere: Mimi Bado mdogo, bado sifikirii ndoa](https://spotileo.co.tz/rosey-manfere-mimi-bado-mdogo-bado-sifikirii-ndoa/) - DAR ES SALAAM: MISS Tanzania 2020, Rosey Manfere, amesema bado ni mdogo kiumri na anajivunia kuwa sehemu ya kizazi cha Generation Z, akieleza kuwa vijana wa kizazi hicho wamekuwa wachangamfu na kufanya vizuri katika nyanja mbalimbali ikilinganishwa na kizazi cha Millennial. Rosey amesema kwa sasa hana shinikizo la kuingia kwenye ndoa, akisisitiza kuwa kauli zake - [Marioo apongeza upendo wa mashabiki](https://spotileo.co.tz/marioo-apongeza-upendo-wa-mashabiki/) - DAR ES SALAAM: MSANII Omary Mwanga maarufu kama Marioo amewashukuru mashabiki wake kwa upendo mkubwa wanaoendelea kumuonyesha, kufuatia mapokezi mazuri ya kazi yake mpya ya muziki. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Marioo amendika:“Kusema ukweli mko na upendo mkubwa sana. Last night hata hao Wasauzi wenyewe walishangaa hayo mawe yalivyokuwa yanalia,” ameandika Marioo. Hatua - [Miss Tanzania 2020: Napenda kuvaa nadhifu bila kuacha mwili wazi](https://spotileo.co.tz/miss-tanzania-2020-napenda-kuvaa-nadhifu-bila-kuacha-mwili-wazi/) - DAR ES SALAAM: MISS Tanzania 2020, Rosey Manfere, amesema kuwa katika maisha yake anapenda sana kuvaa vizuri na kupendeza, lakini hapendi kuvaa mavazi yanayoacha mwili wake wazi. Akizungumza na Spoti Leo kuhusu suala la mavazi, Rosey amesema mtu anaweza kuvaa kwa staha na akaonekana mrembo bila kuacha mwili wazi, kinachohitajika ni kuzingatia aina ya sehemu - ["Tunaendelea kumtathmini Rodri" - Toure](https://spotileo.co.tz/tunaendelea-kumtathmini-rodri-toure/) - MANCHESTER: MANCHESTER City wataendelea kummkosa kiungo wao muhimu, Rodrigo Hernandez Cascante maarufu ‘Rodri’, katika mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Crystal Palace Jumapili, huku mshindi huyo wa Ballon d’Or akiendelea kuimarika baada ya majeraha ya nyama za misuli ya paja yaliyomweka nje tangu Oktoba. Man City wangependa kumrejesha uwanjani kiungo huyo raia wa Hispania - [Arteta aweka mtego kwa ‘mastraika’ Arsenal](https://spotileo.co.tz/arteta-aweka-mtego-kwa-mastraika-arsenal/) - LONDON: KOCHA wa Arsenal, Mikel Arteta, amesema mshambuliaji wa klabu hiyo Gabriel Jesus ana uwezo wa kuwa mshambuliaji namba moja wa timu hiyo, baada ya kurejea uwanjani wiki hii kufuatia kuwa nje kwa miezi 11. Mshambuliaji huyo raia wa Brazil, mwenye umri wa miaka 28, alicheza dakika zake za kwanza tangu Januari alipoumia goti, akiingia - [Wikiendi ya shangwe na majanga kwa Chelsea](https://spotileo.co.tz/wikiendi-ya-shangwe-na-majanga-kwa-chelsea/) - LONDON: WENYEJI wa Darajani Chelsea wamepokea habari mseto kabla ya kuvaana na Everton kwenye Premier League Jumamosi, baada ya kocha Enzo Maresca kuthibitisha kuwa mshambuliaji Cole Palmer na beki wa kati Wesley Fofana wako tayari kurejea uwanjani, huku mshambuliaji Liam Delap akikabiliwa na hadi wiki nne nje kwa majeraha. Palmer, aliyerejea hivi karibuni kutoka kwenye - [Arteta aendelea kumtetea Gyökeres](https://spotileo.co.tz/arteta-aendelea-kumtetea-gyokeres/) - LONDON: KOCHA wa Arsenal Mikel Arteta ameendelea kuutetea ubora wa mshambuliaji Viktor Gyökeres, akisema ana imani kubwa kwamba staa huyo wa Sweeden atafunguka licha ya mwanzo mgumu tangu kuwasili Emirates. Gyökeres, aliyeng’ara kwa kufunga mabao 54 akiwa Sporting msimu uliopita, ametikisa nyavu mara sita tu katika mechi 18 tangu kusajiliwa kwa paundi milioni 64, huku - [Licha ya kutocheza msimu huu, Bissouma Mali](https://spotileo.co.tz/licha-ya-kutocheza-msimu-huu-bissouma-mali/) - BAMAKO: KOCHA wa timu ya taifa ya Mali amemjumuisha kiungo wa taifa hilo Yves Bissouma kwenye kikosi cha kombe la mataifa ya Afrika (AFCON) licha ya kutokucheza mechi yoyote ya klabu msimu huu, hatua iliyoibua mjadala lakini pia kuonesha kiwango cha imani aliyojengewa na benchi la ufundi. Kocha Tom Saintfiet alimtaja Bissouma mwenye umri wa - [Mtanzania ang’ara Tuzo za Kwanza za TikTok 2025](https://spotileo.co.tz/mtanzania-angara-tuzo-za-kwanza-za-tiktok-2025/) - JOHANNESBURG: MOJA ya matukio yaliyosubiriwa kwa hamu kubwa mwaka huu ni pamoja na Tuzo za TikTok Afrika zilizofanyika kwa mafanikio makubwa katika jiji la Johannesburg nchini Afrika Kusini. Tuzo hizo zinadaiwa kuibua vipaji, kuburudisha na kuthibitisha ukuaji wa upeo wa ubunifu barani Afrika licha ya kufanyika kwa mara ya kwanza. Muigizaji kutoka Tanzania Fanuel Masamaki - [Mercedes-Benz 560 SEL la Rais Moi kivutio Jamhuri Day](https://spotileo.co.tz/mercedes-benz-560-sel-la-rais-moi-kivutio-jamhuri-day/) - NAIROBI: WAKATI Kenya ikiadhimisha sherehe za Miaka 62 ya Uhuru (Jamhuri Day), gari la kifahari aina ya Mercedes-Benz 560 SEL, iliyokuwa katika utawala wa Rais wa zamani Daniel arap Moi lenye rangi ya bluu iliyong’aa, lilikuwa kivutio kikubwa katika maadhimisho hayo. Gari hilo limezungushiwa kamba maalumu na kung’aa kana kwamba linamngoja kiongozi, gari hilo lilikuwa - [Majibu ya Chalamet yawachanganya mashabiki](https://spotileo.co.tz/majibu-ya-chalamet-yawachanganya-mashabiki/) - CALIFORNIA: MUIGIZAJI Timothee Chalamet ambaye pia ni mwanamuziki akiwa kwenye mahojiano na Samuel Goldwyn Theatre huko Beverly Hills, azidisha uvumi kwamba anaweza kuwa rapper wa Uingereza asiyejulikana EsDeeKid. Tetesi mbalimbali zinahusu utambulisho wa mwanamuziki huyo maarufu, ambaye amekua akifananishwa na rapa EsDeeKid ameonekana akisuasua na majibu yake akiwa na mtangazaji Samuel alipomuuliza “Mashabiki wako wamepoteza - [Diarra kimeeleweka AFCON](https://spotileo.co.tz/diarra-kimeeleweka-afcon/) - BAMAKO: Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Mali, Tom Saintfiet, ametangaza kikosi cha wachezaji 28 kuelekea Fainali za AFCON 2025, huku golikipa wa Yanga, Djigui Diarra, akiendelea kuitwa kwa mara nyingine. Diarra amekuwa akiitwa mara kwa mara kwenye timu ya taifa kutokana na ubora wake usiochuja ndani ya klabu yake ya Yanga na timu - [Mabadiliko makubwa yanakuja Simba - Ahmed](https://spotileo.co.tz/mabadiliko-makubwa-yanakuja-simba-ahmed/) - DAR ES SALAAM: MSEMAJI wa Simba, Ahmed Ally, amesema klabu hiyo imegeuza kipindi hiki cha mapumziko ya ligi kuwa fursa ya kufanya mabadiliko makubwa ndani ya kikosi, ikianzia na tathmini ya mechi zote walizocheza msimu huu hadi mchakato wa kupata benchi jipya la ufundi. Akizungumzia kinachoendelea ndani ya klabu hiyo, Ahmed alisema ligi imesimama kupisha - [Azam FC yaelekeza jicho michuano ya Mapinduzi](https://spotileo.co.tz/azam-fc-yaelekeza-jicho-michuano-ya-mapinduzi/) - DAR ES SALAAM: AZAM FC ni miongoni mwa timu zinazotarajia kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi Zanzibar msimu huu baada ya kueleza mipango yake ya kujiandaa na mashindano hayo. Timu hiyo inayowakilisha nchi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho imesema inatarajia kuweka kambi Desemba 29, 2025 Visiwani Zanzibar ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa - [Golikipa Livakovic apigwa ‘stop’ Girona](https://spotileo.co.tz/golikipa-livakovic-apigwa-stop-girona/) - MADRID: KOCHA wa Girona, Miguel Ángel Sánchez Muñoz maarufu Míchel, amemkosoa vikali kipa wa klabu hiyo raia wa Croatia Dominik Livakovic, akidai mchezaji huyo hana uzalendo na haipi kipaumbele klabu na kusema kuwa hatachezea timu hiyo tena. Míchel amesema kipa huyo wa akiba alikataa kucheza mechi ya hivi karibuni na ameeleza wazi kutaka kuondoka klabuni - [Wachezaji Madrid matatani kwa kumbughudhi refa](https://spotileo.co.tz/wachezaji-madrid-matatani-kwa-mumbughudhi-refa/) - MADRID: WACHEZAJI watatu wa Real Madrid Dani Carvajal, Álvaro Carreras na Endrick wamepigwa marufuku ya mechi mbili kila mmoja kufuatia utovu wa nidhamu waliouonesha kwa waamuzi katika mechi ya LaLiga dhidi ya Celta Vigo iliyochezwa mwishoni mwa wiki. Carreras alilimwa kadi nyekundu dakika za jioni kwenye kipigo hicho cha mabao 2-0 katika Uwanja wa Bernabéu, - [Aston Villa mwendo mdundo UEL](https://spotileo.co.tz/aston-villa-mwendo-mdundo-uel/) - BASEL: WABABE wa Arsenal, Aston Villa wameendeleza mwendo mzuri kwenye UEFA Europa League (UEL) baada ya kuishushia kipigo cha mabao 2-1 kwa FC Basel ya Switzerland, Alhamisi usiku, kupitia mabao ya Evann Guessand na Youri Tielemans. Ushindi huo umeifikisha Villa kwenye pointi 15, sawa na vinara wa ligi hiyo Olympique Lyonnais na Midtjylland walio nafasi - [Vilio na vicheko kikosi cha Nigeria AFCON](https://spotileo.co.tz/vilio-na-vicheko-kikosi-cha-nigeria-afcon/) - LAGOS: TIMU ya taifa ya Nigeria (Super Eagles) inaingia kwenye michuano ya kombe la mataifa ya Afrika AFCON 2025 kikiwa na sura mpya na maamuzi ya kushangaza baada ya kocha Eric Chelle kutangaza kikosi cha wachezaji 28, ambacho kinajumuisha nyota wapya watano ambao hawajawahi kuichezea Super Eagles. Kikosi hicho, kitakachoshiriki AFCON nchini Morocco kuanzia Desemba - [Mawazo ya salah sasa ni AFCON](https://spotileo.co.tz/mawazo-ya-salah-sasa-ni-afcon/) - CAIRO: KIUNGO mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah, atapumzika presha ya Anfield wiki ijayo atakapojiunga na timuu ya Taifa ya Misri kuelekea Morocco kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), licha ya sintofahamu iliyozuka baada ya kutofautiana na kocha wake Arne Slot. Kocha wa Misri Hossam Hassan alimhakikishia nahodha huyo nafasi kwenye - [Mashabiki walia na bei za tiketi WC 2026](https://spotileo.co.tz/mashabiki-walia-na-bei-za-tiketi-wc-2026/) - WASHINGTON: MASHABIKI wa soka duniani wameishambulia FIFA vikali wakilaani kile walichokiita usaliti mkubwa baada ya bei mpya za tiketi za Kombe la Dunia kuanza kuzunguka mitandaoni mapema Alhamisi. Kwa utaratibu wa kawaida, FIFA hutenga asilimia 8 ya tiketi kwa mashirikisho ya kitaifa ili ziuzwe kwa mashabiki wa timu husika. Hata hivyo, orodha iliyochapishwa na Shirikisho - [BMT, TFF na Blueberry kuwapeleka mashabiki](https://spotileo.co.tz/bmt-tff-na-blueberry-kuwapeleka-mashabiki/) - DAR ES SALAAM: BARAZA la Michezo la Taifa (BMT) kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Wakala wa Usafirishaji Blueberry Travels, wametangaza mpango maalum wa kuwasafirisha mashabiki watakaosafiri kwenda Morocco kuisapoti Taifa Stars kwenye michuano ya fainali za mataifa ya Afrika ‘AFCON 2025’ inayoanza Desemba 21, 2025. Akizungumza na waandishi wa - [Harmonize Amjia juu Baba Levo](https://spotileo.co.tz/harmonize-amjia-juu-baba-levo/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Rajab Abdul ‘Harmonize’, amemjibu vikali msanii mwenzake Baba Levo baada ya Baba Levo kum-post na kudai kuwa Diamond Platnumz ndiye “baba” yao na mtu aliyewainua wasanii wengi nchini. Katika sehemu ya maoni kupitia ukurasa wa Instagram, Harmonize ameibua gumzo baada ya kumrushia maneno mazito Baba Levo, akisisitiza kuwa - [Marioo: Lazima tumalize mwaka kwa kishindo](https://spotileo.co.tz/marioo-lazima-tumalize-mwaka-kwa-kishindo/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Omary Mwanga maarufu kama Marioo, ameahidi kumaliza mwaka kwa kishindo baada ya kufanya vizuri kwenye majukwaa mbalimbali ya kidijitali kwa miaka mfululizo. Kupitia ukurasa wake, Marioo amesema mafanikio yake yametokana na upendo na sapoti ya mashabiki wake ambao wameendelea kusikiliza kazi zake na kumfanya aongoze kwa muda mrefu - [United yaripoti tena hasara](https://spotileo.co.tz/united-yaripoti-tena-hasara/) - MANCHESTER: MSHETANI wekundu Manchester United wameripoti hasara ya robo ya kwanza ya mwaka baada ya kukumbwa na upungufu wa mapato ya matangazo ya Televisheni na mauzo ya tiketi, kufuatia kukosa kushiriki mashindano ya Ulaya msimu huu. Klabu hiyo ya Old Trafford imetangaza hasara ya pauni milioni 6.6 kwa robo iliyoishia Septemba 30, ikilinganishwa na faida - [Dube kimeeleweka Afcon](https://spotileo.co.tz/dube-kimeeleweka-afcon/) - HARARE: MSHAMBULIAJI wa Yanga Prince Dube ni miongoni mwa majina yaliyotangazwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Zimbabwe kitakachoshiriki mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025. Dube amekuwa na kiwango kizuri hivi karibuni kwenye klabu yake huenda ni sababu ya kuendelea kuaminiwa kwenye kikosi cha Zimbabwe. Kikosi kamili cha Zimbabwe: MAKIPA: Washington - [Shakira afurahia kucheza na watoto wake jukwaani](https://spotileo.co.tz/shakira-afurahia-kucheza-na-watoto-wake-jukwaani/) - ARGENTINA: MWANAMUZIKI mashuhuri Shakira Isabel Mebarak Ripoll amewashukuru watoto wake wawili kwa kumtia nguvu baada ya kupanda jukwaani na kuimba naye katika onesho lake huko Buenos Aires. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Shakira ameeleza: Buenos Aires asante kwa wakati huu ambao utadumu milele sikutegemea kuimba na watoto wangu na kuwaona wakitoa muziki walionao ndani huku - [Masalanga: Nigeria wagumu ila tutapambana](https://spotileo.co.tz/masalanga-nigeria-wagumu-ila-tutapambana/) - CAIRO: GOLIKIPA wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Hussein Masalanga amesema mchezo wao wa ufunguzi wa Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) dhidi ya Nigeria utakuwa mgumu kutokana na kiwango cha wachezaji wa timu hiyo wengi wanacheza soka la kulipwa Ulaya. Akizungumza Leo katika maandalizi yao yanayoendelea nchini Misri, golikipa huyo amesema, “Tunakutana - [Mwandishi nguli wa vitabu afariki dunia](https://spotileo.co.tz/mwandishi-nguli-wa-vitabu-afariki-dunia/) - LONDON: MWANDISHI wa riwaya mashuhuri Kinsell, ambaye jina lake halisi ni Madeleine Sophie Wickham, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kutokana na ugonjwa saratani ya ubongo uliokuwa ukimsumbua aliofunguka kuwa nao mwaka 2022. Taarifa ya kifo chake iliyochapishwa kwenye akaunti yake ya Instagram usiku kuamkia leo ilisoma: "Tunasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wetu Sophie (anayejulikana - [Aston Villa kuendeleza ubabe UEL leo?](https://spotileo.co.tz/aston-villa-kuendeleza-ubabe-uel-leo/) - BASEL: KLABU ya Aston Villa, iliyoko kwenye kiwango bora na ikija juu baada ya kuwachabanga vinara wa Ligi Kuu England Arsenal, inatarajiwa kuvaana na FC Basel kwenye UEFA Europa League (UEL) usiku wa leo Alhamisi. Baada ya kuanza msimu kwa kusuasua, Villa imegeuka tishio na sasa ipo kwenye mwendelezo wa ushindi katika mechi saba mfululizo - [Guardiola akoshwa na kiwango Man City, amtaja Doku](https://spotileo.co.tz/guardiola-akoshwa-na-kiwango-man-city-amtaja-doku/) - MADRID: KOCHA wa Manchester City, Pep Guardiola, amewasifu wachezaji wake kwa ustahimilivu na ari ya kupambana baada ya kufanya ‘comeback’ na kushinda mabao 2-1 dhidi ya Real Madrid kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano usiku katika dimba la Bernabeu. Licha ya kuanza mchezo kwa kusuasua na kuonekana kuwa hatarini mbele ya mashambulizi ya mara kwa - [Howard Stern amjibu Kim Kardashian kauli ya wizi](https://spotileo.co.tz/howard-stern-amjibu-kim-kardashian-kauli-ya-wizi/) - PARIS: MTANGAZAJI maarufu wa redio na Jaji wa American Got Talent Howard Stern amejibu vikali madai ya Kim Kardashian kwamba alimshutumu kughushi tukio lake la wizi la mwaka 2016 mjini Paris. Kim, mwenye miaka 45, aliwahi kushambuliwa na wanaume waliovamia chumba chake cha hoteli jijini Paris na kumshikilia kwa bunduki, wakimvua vito vyenye thamani ya - [“Tutajitahidi kurejesha kiwango chetu” – Alonso](https://spotileo.co.tz/tutajitahidi-kurejesha-kiwango-chetu-alonso/) - MADRID: KOCHA wa Real Madrid, Xabi Alonso, amesema wachezaji wake wanajitahidi kadiri ya uwezo wao kurejesha kiwango chao licha ya kuendelea kwa mwenendo mbaya baada ya kupoteza mabao 2-1 dhidi ya Manchester City katika Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano. Alonso, aliyechukua timu hiyo mwezi Juni, yuko chini ya shinikizo baada ya kushinda mara mbili tu - [“Madueke ni mtu na nusu” – Arteta](https://spotileo.co.tz/madueke-ni-mtu-na-nusu-arteta/) - BRUGGE: KOCHA wa Arsenal, Mikel Arteta, amemmiminia sifa nyingi winga wa klabu hiyo Noni Madueke baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-0 wa Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) dhidi ya Club Brugge nchini Ubelgiji usiku wa kuamkia leo. Madueke alifungua ukurasa wa mabao kwa shuti kali dakika ya 25, likiwa bao la kuvutia - [Netflix, Majumba ya Sinema kimeumana](https://spotileo.co.tz/netflix-majumba-ya-sinema-kimeumana/) - LOS ANGELES: MUONGOZAJI filamu mashuhuri huko Hollywood ambaye aliongoza filamu ya ‘Brick’, Rian Johnson, ametetea majukwaa ya utoaji filamu mtandaoni (streaming), akieleza kuwa watu wengi hawaelewi changamoto na ugumu uliopo kati ya majumba ya sinema na kampuni za huduma za mtandao kama Netflix. Johnson amesema: “Sio tu Netflix kusema hawatatoa filamu nyingi kwenye sinema. Kuna - [James Cameron aigomea Ai](https://spotileo.co.tz/james-cameron-aigomea-ai/) - LOS ANGELES: MUONGOZAJI filamu maarufu, James Cameron, amesema kuwa hatoitumia AI katika kazi zake za filamu na wala hana maslahi binafsi kutumia teknolojia hiyo. Cameron, mwenye miaka 71, amesema hatotumia AI kuchukua nafasi ya ubunifu wa kibinadamu licha ya kuwa kiongozi mkubwa wa kutumia teknolojia za kisasa kwenye ulimwengu wa filamu zake. Akizungumza kwenye Tamasha - [Gamondi: Tutaingia Afcon kama timu iliyokomaa](https://spotileo.co.tz/gamondi-tutaingia-afcon-kama-timu-iliyokomaa/) - CAIRO: KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Miguel Gamondi, amesema maandalizi ya kuelekea Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) za Morocco 2025 yamejaa dhamira moja kubwa—kuiwakilisha Tanzania kwa heshima, nidhamu na ari ya kupambana. Akizungumza katika kikao cha tathmini ya maandalizi, Gamondi alisisitiza kuwa anataka kuona Taifa Stars inaingia AFCON kama timu iliyokomaa, yenye umoja na - [Leila ‘Macho’ amchimba mkwara Hidaya Zahoro](https://spotileo.co.tz/leila-macho-amchimba-mkwara-hidaya-zahoro/) - DAR ES SALAAM: BONDIA wa kike kutoka Kambi ya Kivita Mburahati, Leila Macho, amemchimba mkwara mkali mpinzani wake Hidaya Zahoro wa Morogoro kuelekea pambano lao linalosubiriwa kwa hamu litakalofanyika Desemba 26, 2025 Dar es Salaam. Akizungumza wakati akiendelea na mazoezi yake, Macho alisema Hidaya amekuwa akijifariji kwa “ndoto za mchana,” akisisitiza kuwa siku ya pambano - [Leverkusen yanusurika kwa Newcastle](https://spotileo.co.tz/leverkusen-yanusurika-kwa-newcastle/) - LEVERKUSEN: WINGA wa Bayer Leverkusen Alex Grimaldo aliinusuru klabu hiyo na kichapo cha nyumbani baada ya kufunga bao la dakika ya 88 lililoiwezesha klabu hiyo kuambulia sare ya mabao 2-2 dhidi ya Newcastle United kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano usiku. Newcastle, ambao pia waligonga mwamba mara mbili, walidhani wamechukua pointi tatu baada - [Man City yatamba Bernabeu](https://spotileo.co.tz/man-city-yatamba-bernabeu/) - MADRID: BAO la kinda Nico O’Reilly na penalti ya Erling Haaland vimeipa Manchester City ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Real Madrid katika mchezo wa kukata na shoka wa Ligi ya Mabingwa ulaya uliopigwa uwanjani Bernabéu Jumatano usiku. Real Madrid walikuwa wa kwanza kutangulia kupitia Rodrygo dakika ya 28, akiimalizia kwa utulivu shambulizi la kushtukiza - [Jesus mambo safi UCL](https://spotileo.co.tz/jesus-mambo-safi-ucl/) - BRUGES: KOCHA wa Arsenal Mikel Arteta amesema mshambuliaji wa klabu hiyo Gabriel Jesus anaweza kurejea katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya leo Jumatano baada ya kukosekana kwa muda mrefu, lakini atawakosa tena nyota kadhaa muhimu akiwemo Declan Rice na Leandro Trossard. Mshambuliaji huyo wa Brazil amekuwa nje tangu Januari baada ya kupata jeraha la - [Man City yamtia ‘kiwewe’ Alonso](https://spotileo.co.tz/man-city-yamtia-kiwewe-alonso/) - MADRID: PRESHA imezidi kumpanda kocha wa Real Madrid, Xabi Alonso, kuelekea mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City utakaopigwa katika dimba la Bernabeu leo Jumatano saa 5 usiku. Madrid imekuwa kwenye mwenendo wa kutatanisha, ikishinda mechi mbili pekee kati ya saba ilizocheza katika mashindano yote, ikiwemo kipigo cha 2-0 kutoka kwa - [Sakata la Mo Salah lachukua sura mpya, mashabiki wasimama na Slot](https://spotileo.co.tz/sakata-la-mo-salah-lachukua-sura-mpya-mashabiki-wasimama-na-slot/) - MILAN: MASHABIKI wa Liverpool wameweka wazi upande wanaounga mkono katika kile kinachoonekana kama mvutano unaoendelea kati ya nyota wa klabu hiyo, Mohamed Salah, na kocha Arne Slot. Zaidi ya mashabiki 5,000 waliosafiri na timu hiyo kwenda nchini Italia waliimba kwa nguvu jina la Slot kabla na baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Inter Milan - [Misri yaishika pabaya FIFA](https://spotileo.co.tz/misri-yaishika-pabaya-fifa/) - CAIRO: SHIRIKISHO la Soka nchini Misri (EFA) limethibitisha kuwa limetuma barua kwenda shirikisho la soka duniani FIFA likitaka kuzuia shughuli zozote zinazohusiana na maudhui ya wapenzi wa jinsia moja (LGBTQ+) wakati wa mchezo wa Kombe la Dunia kati ya timu ya taifa ya Misri na Iran utakaopigwa mjini Seattle Juni mwakani. Kwa mujibu wa EFA, - [Jonathan Budju kufunga mwaka na wimbo mpya Ituri amani](https://spotileo.co.tz/jonathan-budju-kufunga-mwaka-na-wimbo-mpya-ituri-amani/) - KINSHASA: MSANII nyota wa Injili kutoka Canada, Jonathan Budju, ame­tangaza kuachia wimbo mpya unaolenga kuhamasisha amani katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Budju, ambaye amejipatia umaarufu mkubwa kupitia kazi zake za Injili na shughuli za kijamii kupitia taasisi yake ya JB Foundation inayofanya kazi katika nchi mbalimbali za Afrika Mashariki, - [Afande Sele: Nimetumia miaka 10 kumpata mke bora](https://spotileo.co.tz/afande-sele-nimetumia-miaka-10-kumpata-mke-bora/) - MOROGORO: RAPA Selemani Msindi maarufu Afande Sele amesema ametumiaka miaka 10 ili kumpata mke mwingine bora baada ya kifo cha mke wake wa kwanza. Afande Sele amefunga ndoa ya kiserikali na Mwandishi wa Habari wa gazeti la Mwananchi Iman Makongoro. Amesema baada ya kifo cha mke wake wa kwanza na Watoto alikuwa nao aliamua kusubiri - [Sunny Deol amkumbuka baba yake, aachia ujumbe](https://spotileo.co.tz/sunny-deol-amkumbuka-baba-yake-aachia-ujumbe/) - MUMBAI: Sunny Deol ambaye ni mtoto wa muigizaji wa filamu kutoka India aliyefariki dunia hivi karibuni Dharmendra amechapisha ujumbe wa kumkumbuka baba yake ikiwa ni siku kadhaa tangu kifo chake. Dharmendra aliaga dunia mnamo Novemba 24 mwaka huu, siku chache tu kabla ya siku yake ya kuzaliwa ya kutimiza miaka 90, Desemba 8. Sunny akimkumbuka - [Picha la Salah, Liverpool linatisha!](https://spotileo.co.tz/picha-la-salah-liverpool-linatisha/) - LIVERPOOL: MAISHA yanaenda kasi sana, ni kama Mohamed Salah yupo ndotoni hivi, lakini huu ndio ukweli mchungu ambao anakutana nao sasa. Msimu uliopita Liverpool walimpigia magoti asaini mkataba mpya wa kuendelea kuwatumikia, Salah aliwasumbua mno hadi alipokuja kusaini mkataba huo. Kilichompa kiburi Salah ni kiwango chake kwani alikuwa mchezaji bora wa EPL msimu uliopita na - [Maresca aanika sababu za kufanya ‘rotation’](https://spotileo.co.tz/maresca-aanika-sababu-za-kufanya-rotation/) - BOURNEMOUTH: KOCHA wa Chelsea, Enzo Maresca, amesema ni lazima wafanye ‘rotation’ ya wachezaji ili kuwalinda wale wasioweza kucheza kila baada ya siku tatu, timu ikijiandaa na safari ya kuelekea Bournemouth baada ya kupoteza 3-1 dhidi ya Leeds United Jumatano. Maresca alikosolewa vikali kufuatia kichapo hicho kutoka kwa Leeds wanaopambana kuepuka kushuka daraja, ambapo alifanya mabadiliko - [“Merino ana haki ya kuwa mshambuliaji” - Arteta](https://spotileo.co.tz/merino-ana-haki-ya-kuwa-mshambuliaji-arteta/) - LONDON: KOCHA wa Arsenal, Mikel Arteta, amesema kiungo wake Mikel Merino amejitengenezea haki ya kuangaliwa kama mshambuliaji hata pale wachezaji wote wa safu ya mbele watakapokuwa fiti. Merino, raia wa Hispania aliyesajiliwa kutoka Real Sociedad Agosti 2024, hakuwahi kutumika kama namba 9 kabla ya kuwasili London, lakini alifunga mabao tisa katika msimu wake wa kwanza - [Aston Villa kuzima moto wa arsenal wikiendi hii?](https://spotileo.co.tz/aston-villa-kuzima-moto-wa-arsenal-wikiendi-hii/) - MANCHESTER: KLABU ya Aston Villa inaonekana kama timu yenye moto zaidi kwa timu za Daraja la kati katika Ligi Kuu England kwa sasa, na Jumamosi watakuwa na kazi ya kuipima tena Arsenal katika safari yake ya kuwania ubingwa. Mexhi hiyo inapata ladha ya kipekee kutokana na kukutana tena kwa kocha Unai Emery na Arsenal klabu - [Slot aitamani ‘Top four’ ya EPL](https://spotileo.co.tz/slot-aitamani-top-four-ya-epl/) - LIVERPOOL: Kocha wa Liverpool, Arne Slot, amesema kikosi chake kiko katika hali mbaya na kinalazimika kupambana kurejea kwenye ‘Top Four’ ya Ligi Kuu England, baada ya kushinda mechi mbili pekee kati ya tisa zilizopita. Liverpool wanaendelea kusota katika nafasi ya tisa wakiwa na pointi 22 kutokana na mechi 14, wakiachwa kwa pointi 11 na vinara - [Wachezaji Galatasaray, Fenerbahçe matatani kwa ‘kubeti’](https://spotileo.co.tz/wachezaji-galatasaray-fenerbahce-matatani-kwa-kubeti/) - ISTANBUL: WAENDESHA mashtaka jijini Istanbul wametoa hati za kukamatwa kwa makumi ya wachezaji na maofisa wa soka kufuatia kashfa ya upangaji na ushawishi wa matokeo kupitia michezo ya kubeti, ambayo imeitikisa nchi hiyo. Katika misako ya alfajiri iliyofanywa mapema leo Ijumaa, wachezaji kadhaa kutoka klabu kongwe za Uturuki wamekamatwa, akiwemo Mert Hakan Yandaş wa Fenerbahçe - ['Staa' wa filamu za mapigano wa Japan afariki](https://spotileo.co.tz/staa-wa-filamu-za-mapigano-wa-japan-afariki/) - TOKYO: CARY-Hiroyuki Tagawa, mmoja wa waigizaji waliotamba kwa zaidi ya miongo minne katika filamu za mapigano, amefariki dunia akiwa na miaka 75 kutokana na matatizo yaliyotokana na kiharusi. Tagawa amefariki jana Desemba 05 huko Santa Barbara akiwa amezungukwa na familia yake, kwa mujibu wa taarifa ya mwakilishi wake. - Tagawa, ambaye wengi wanamkumbuka kama mchawi(adui) - [Linah Sanga: “Sitamani ndoa kwa sasa"](https://spotileo.co.tz/linah-sanga-sitamani-ndoa-kwa-sasa/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Linah Sanga, amesema kwa sasa hana kabisa shauku ya kuingia kwenye ndoa, na kwamba anahitaji muda wa kupumzika na kufurahia ujana wake. Amesema hayo ikiwa ni miaka michache tangu kutangaza kuachana na baba wa mtoto wake, ambaye pia aliwahi kuwa meneja wake katika kazi zake za muziki. Linah - [Mr. P Afichua hofu yake kubwa maishani](https://spotileo.co.tz/mr-p-afichua-hofu-yake-kubwa-maishani/) - LAGOS: MSANII mashuhuri wa R&B kutoka Nigeria, Peter Okoye 'Mr. P'—amefunguka kuhusu jambo ambalo linamtisha zaidi maishani, akisema kuwa si kifo kinachomtia hofu bali ni umaskini. Mr. P amesema kuwa hofu hiyo imejengwa na maisha magumu aliyowahi kupitia katika utoto wake, ikiwa ni pamoja na tukio walilowahi kukumbana nalo la kubomolewa nyumba waliyokuwa wakiishi. “Siogopi - [Mr. Chuzi aliyempika mkude simba akapikika](https://spotileo.co.tz/mr-chuzi-aliyempika-mkude-simba-akapikika/) - DAR ES SALAAM: KATIKA upepo wa simulizi za Instagram, nyota mwenye sura nyingi katika sanaa muigizaji, mchekeshaji, mwandishi wa tamthilia na mbadili-sauti mahiri, Mussa Kitale ‘Mkude Simba’, maarufu kama Bwakila, amefungua ukurasa wa kumbukizi za safari yake ya ubunifu. Safari ambayo chanzo chake hakikuwa studio, bali mikono ya mtu mmoja muhimu sana katika tasnia ya - [“Soka la Afrika linastahili heshima” – kocha wa Mali](https://spotileo.co.tz/soka-la-afrika-linastahili-heshima-kocha-wa-mali/) - BAMAKO: KOCHA wa timu ya Taifa ya Mali, Tom Saintfiet, amesema soka la Afrika linastahili kuheshimiwa zaidi, baada ya hatua ya ghafla ya FIFA kuchelewesha muda wa kuachiliwa kwa wachezaji kuelekea Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika baadae mwezi huu nchini Morocco. FIFA ilitangaza Jumatano kwamba klabu zitalazimika kuachia wachezaji kuanzia Desemba - [Roy Keane aikosoa vikali Man U](https://spotileo.co.tz/roy-keane-aikosoa-vikali-man-u/) - MANCHESTER: NAHODHA wa zamani wa Manchester United, Roy Keane, amesema kikosi cha sasa cha United kinaonekana kuwa na hofu na hakikuwa na ukali unaohitajika ili kupata pointi tatu, baada ya kuruhusu bao la dakika za mwisho na kulazimishwa sare ya 1-1 na West Ham United Alhamisi usiku Uwanjani Old Trafford. United walikosa nafasi ya kupanda - [“Salaha kukaa benchi kunaashiria hakuna mkubwa Liverpool” – Van Dijk](https://spotileo.co.tz/salaha-kukaa-benchi-kunaashiria-hakuna-mkubwa-liverpool-van-dijk/) - LIVERPOOL: Nahodha wa mabingwa watetezi wa EPL Liverpool, Virgil van Dijk, amesema uamuzi wa kumuweka Mohamed Salah benchi katika mechi mbili mfululizo za Ligi Kuu England ni ishara tosha kwamba hakuna mchezaji mwenye uhakika wa namba kikosini bila kuonyesha kiwango cha kutosha. Winga huyo raia wa Misri, mwenye umri wa miaka 33, hakuingia kabisa uwanjani - [United yakwama nafasi ya nane](https://spotileo.co.tz/united-yakwama-nafasi-ya-nane/) - MANCHESTER: mashetani wekundu Manchester United wameshindwa kupanda hadi nafasi ya tano kwenye msimamo Ligi Kuu England baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na West Ham United katika mchezo wa Alhamisi usiku uliopigwa nyumbani kwao Old Trafford, matokeo ambayo yaliwaacha wageni wakiendelea kusota kwenye eneo la kushuka daraja. Baada ya kipindi cha kwanza kisicho na mvuto, - [Bajaber: Nimepitia wakati mgumu benchi](https://spotileo.co.tz/bajaber-nimepitia-wakati-mgumu-benchi/) - DAR ES SALAAM: MSHAMBULIAJI wa Simba SC Mohamed Bajaber amefunguka baada ya kufunga bao lake la kwanza tangu ajiunge na Wekundu wa Msimbazi, akisema alikuwa akipita kwenye kipindi kigumu cha kukosa nafasi kutokana na majeraha yaliyomuweka nje kwa muda mrefu. Mchezaji huyo, aliyesajiliwa msimu huu akitokea Polisi Kenya, hakuweza kuanza kuitumikia Simba mapema kutokana na - [Mau Music atamba na EP yake mpya Still Mshua](https://spotileo.co.tz/mau-music-atamba-na-ep-yake-mpya-still-mshua/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva anayeishi nchini Afrika Kusini, Maulidi Lukwale ‘Mau Music’, ameendelea kutikisa anga la muziki punde tu baada ya kuachia albamu yake fupi (EP) iitwayo Still Mshua. Kwa muda mrefu Mau Music amekuwa mstari wa mbele kutetea na kutangaza muziki wa Bongo Fleva nchini Afrika Kusini, akiuonyesha kwa mchanganyiko wa - [Yanga yaifunga 2-0 Fountain Gate](https://spotileo.co.tz/anga-yaifunga-2-0-fountain-gate/) - DAR ES SALAAM: MABINGWA watetezi Yanga SC wameendelea kujiimarisha kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Fountain Gate, mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa KMC, Dar es Salaam. Mabao ya Yanga yalifungwa na Prince Dube dakika ya 28 kwa mkwaju wa penalti na Pacome - [Trent aiweka njiapanda Madrid](https://spotileo.co.tz/trent-aiweka-njiapanda-madrid/) - MADRID: Beki wa mabingwa wa kihistoria wa Ligi Ya Mabingwa Ulaya Real Madrid, Trent Alexander-Arnold amepata jeraha kwenye mguu wa kushoto siku chache kabla ya klabu yake kukutana na Manchester City. Beki huyo wa kulia aliumia misuli ya juu ya mguu wa kushoto na akifanyiwa mabadiliko muda mfupi baada ya kipindi cha pili kuanza katika - [Spalletti ajawa hisia mesto Napoli](https://spotileo.co.tz/spalletti-ajawa-hisia-mesto-napoli/) - MILAN: KOCHA wa zamani wa SSC Napoli, Luciano Spalletti anatarajia kurejea jijini Napoli Jumapili kwa mara ya kwanza tangu aiwezeshe klabu hiyo kutwaa taji lake la kwanza la Serie A baada ya zaidi ya miaka 30. Spalletti amesema tayari anahisia kali kuhusu kurejea huko. Safari hii akirejea si tena kama rafiki na mkufunzi wa kikosi - [UEFA yawafungia mashabiki wa Young Boys](https://spotileo.co.tz/uefa-yawafungia-mashabiki-wa-young-boys/) - NYON: Mashabiki wa klabu ya soka ya Young Boys wamezuiwa kuhudhuria mchezo wa Europa League wa alhamisi Alhamisi ijayo kama adhabu kwa vurugu zao zilizokatisha mchezo dhidi ya Aston Villa wiki iliyopita. Mashabiki wa Young Boys walirusha chupa za plastiki zilizompiga mfungaji wa Aston Villa, Donyell Malen, na kugombana na walinzi wa uwanjani walipopokea kichapo - [Neymar Jr apiga 'hat-tick' akiwa majeruhi](https://spotileo.co.tz/neymar-jr-apiga-hat-tick-akiwa-majeruhi/) - CAXIAS DO SUL: KIUNGO mshambuliaji wa klabu ya Santos Neymar Jr ameonesha uzalendo wa hali ya juu kwa klabu hiyo iliyomlea baada ya kucheza akiwa na jeraha la goti na kufanikiwa kufunga hat-trick iliyoiinua klabu yake hiyo ya utotoni, kutoka kwenye hatari ya kushuka daraja katika Ligi Kuu ya Brazil, Serie A. Mchezaji huyo mwenye - [“Mashabiki tulieni” – Maresca](https://spotileo.co.tz/mashabiki-tulieni-maresca/) - LEEDS: BAADA ya kupoteza mechi ya Ligi Kuu ya England dhidi ya Leeds United kwa kufungwa mabao 3-1, kocha mkuu wa Chelsea, Enzo Maresca, amewataka baadhi ya mashabiki wanaolalamikia uamuzi wa kocha huyo wa kutowatumia baadhi ya wachezaji wake muhimu kutomuingilia kwenye majukumu yake. Chelsea imepoteza mechi hiyo ya usiku wa Jumatano ikicheza ugenini katika - [Kim Kardashian alia kuhisiwa mwizi na Kanye West](https://spotileo.co.tz/kim-kardashian-alia-kuhisiwa-mwizi-na-kanye-west/) - CALIFORNIA: MREMBO mwenye umri wa miaka 45 Kim Kardashian amerudi Paris mapema mwaka huu ili kutoa ushahidi kwenye kesi ya uhalifu wa silaha uliofanyika takriban muongo mmoja uliopita huku akisema kuwa hata mume wake wa zamani alikuwa na shaka kuhusu wizi huo kama umetokea kweli ama la. Akiwa katika kipindi cha ‘The Kardashians’, Kim alizungumza - [Anupam Kher apoteza wafuasi laki 9 ndani ya siku 15.](https://spotileo.co.tz/anupam-kher-apoteza-wafuasi-laki-9-ndani-ya-siku-15/) - MUMBAI: ANUPAM KHER alishiriki wasiwasi wake na kukata tamaa kwenye mtandao wake wa kijamii wa Twitter ujulikanao kama X baada ya kupoteza wafuasi 900,000 ndani ya siku 15 zilizopita. Baada ya kumshirikisha mtu tajiri zaidi duniani Elon Musk, mwigizaji huyo aomba mabadiliko makubwa. Akitoa mfano kwamba wadhifa huo ulikuwa wa uchunguzi na sio malalamiko, Kher - [Miss World Tanzania Yarudi Upya](https://spotileo.co.tz/miss-world-tanzania-yarudi-upya/) - DAR ES SALAAM: MASHINDANO ya Miss World Tanzania yamerudi kwa sura mpya baada ya kampuni ya 361 Degrees Africa kuzindua rasmi mwongozo mpya wa uendeshaji unaoangazia kwa kiasi kikubwa dhana ya “Urembo wenye Malengo.” Mashindano Hayo yanalenga kuinua hadhi ya mashindano haya nchini pamoja na kutoa nafasi pana zaidi kwa vijana wa kike kuonyesha vipaji, - [Tuzo za Wanawake katika Filamu zaiva](https://spotileo.co.tz/tuzo-za-wanawake-katika-filamu-zaiva/) - NAIROBI: TUZO za Wanawake katika Filamu zimetangaza kufungua usahili wa toleo la saba, zikialika usahili katika takriban jumla ya makundi 30 yanayosherehekea mchango wa wanawake kwenye sekta ya filamu nchini Kenya. Waandaaji wa tuzo hizo walibaini kuwa mwito wa usahili utaendeshwa hadi Desemba 15, 2025, na wanahamasishwa waandaaji wa filamu na wataalamu wa tasnia hiyo - [Niffer awashukuru Mastaa waliotembelea Mahabusu](https://spotileo.co.tz/niffer-awashukuru-mastaa-waliotembelea-mahabusu/) - DAR ES SALAAM: MFANYABIASHARA Jennifer Jovin maarufu kama Niffer ametoa shukrani za dhati kwa watu waliomfariji na kumtembelea kipindi alipokuwa gerezani, akiwemo Paula Paul, Marioo na mama yake Kajala Masanja. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Niffer aliandika ujumbe mrefu akionyesha namna alivyoguswa na upendo na ukaribu aliopata kutoka kwa familia hiyo. “Thank you! Ulikuwa wa - [Muigizaji wa Kenya Bilal Wanjau afariki dunia](https://spotileo.co.tz/muigizaji-wa-kenya-bilal-wanjau-afariki-dunia/) - NAIROBI: SEKTA ya filamu na maigizo nchini Kenya imetangaza kusikitishwa na kifo cha muigizaji mahiri, Bilal Wanjau. Muigizaji Sandra Dacha, amesema Wanjau alifariki dunia leo, Desemba 4, 2025, wakati akipatiwa matibabu katika hospitali moja huko Nairobi kutokana na matatizo ya kisukari. “Ni kwa huzuni kubwa kwamba napenda kuwatangazia kumpoteza ghafla mwenzetu Bilal Wanjau asubuhi hii - [Amber Lulu aanza kuuza mboga mboga](https://spotileo.co.tz/amber-lulu-aanza-kuuza-mboga-mboga/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Amber Lulu, ameibuka na kufichua kuwa kwa sasa ameanza biashara ya kuuza mboga mboga ikiwemo mchicha, matembele na kisamvu ili kujikimu kimaisha. Akizungumza na Spoti Leo, Amber Lulu alisema hali ya maisha imekuwa ngumu, hivyo ameamua kutafuta mbinu mbadala ya kujipatia kipato licha ya changamoto mbalimbali anazopitia. “Kuna - [Mrembo wa Sudan aibuka Mwanamitindo Bora wa mwaka 2025](https://spotileo.co.tz/mrembo-wa-sudan-aibuka-mwanamitindo-bora-wa-mwaka-2025/) - LOS ANGELES: UMUHIMU wa dunia ya mitindo ulimwenguni umeelekezwa kwa mara nyingine kwa mrembo kutoka Sudan Kusini-Marekani, Anok Yai, baada ya kuteuliwa kuwa Mwanamitindo Bora wa Mwaka 2025 kwenye Tuzo za Fashion zilizofanyika London. Ms Yai alipokea tuzo hiyo katika ukumbi wa Royal Albert Hall wakati wa hafla iliyoandaliwa na Baraza la Mitindo la Uingereza - [Bien aingia kwenye mbio za Ng’ombe](https://spotileo.co.tz/bien-aingia-kwenye-mbio-za-ngombe/) - NAIROBI: MWIMBAJI maarufu wa Kenya, Bien Aimé Baraza, ametoa amefichua kiasi cha pesa ambacho mmliki wa ng'ombe na mshindi hupata baada ya kushinda pambano la mchezo huo. Akizungumza kwenye kipindi cha Mic Cheque, Bien alifichua kuwa amemwita ng'ombe wake jina la bendi maarufu ya Kenya, Sauti Sol. Hata hivyo, ng'ombe huyo hajashiriki mashindano yoyote. Bien - [Mbappe aibeba tena Madrid, yaifumua Bilbao](https://spotileo.co.tz/mbappe-aibeba-tena-madrid-yaamka-yaifumua-bilbao/) - MADRID: MSHAMBULIAJI wa Real Madrid Kylian Mbappé meisaidia klabu hiyo kukomesha mfululizo wa matokeo mabaya baada ya kucheza mechi tatu za ligi bila ushindi baada ya kufunga mabao mawili na kutoa pasi ya goli wakati klabu yake ilipoichapa Athletic Bilbao mabao 3-0 usiku wa Jumatano. Eduardo Camavinga pia aliifungia Madrid, ambayo sasa imerejea kuwa pointi - [Arteta alia na ratiba EPL](https://spotileo.co.tz/arteta-alia-na-ratiba-epl/) - LONDON: KOCHA wa Arsenal, Mikel Arteta, amekosoa ratiba ya Ligi Kuu England baada ya kiungo Declan Rice na beki Cristhian Mosquera kuwa wachezaji wa hivi karibuni kuongezeka kwenye orodha ya majeruhi wa klabu hiyo wakati wa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Brentford Jumatano usiku. Arsenal tayari inakabiliwa na upungufu mkubwa kikosini, ikiwakosa mabeki tegemeo - [RFEF yaufungia uwanja wa Sevilla](https://spotileo.co.tz/rfef-yaufungia-uwanja-wa-sevilla/) - SEVILLE: SHIRIKISHO la Soka la Hispania (RFEF) limetangaza kuwa sehemu ya Uwanja wa Ramón Sánchez-Pizjuán nyumbani kwa klabu ya Sevilla itafungwa kwa mechi tatu zijazo baada ya mashabiki kurusha vitu uwanjani wakati wa kipigo chao cha mabao 2-0 dhidi ya Real Betis kwenye mchezo wa LaLiga Jumapili. Kamati ya nidhamu pia imeitoza Sevilla faini ya - [Slot aendelea kukuna Kichwa Liverpool](https://spotileo.co.tz/slot-aendelea-kukuna-kichwa-liverpool/) - LIVERPOOL: Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya England Liverpool walilazimika kutegemea shuti la ‘deflection’ la Florian Wirtz lililojaa wavuni dakika ya 81 kujiokoa na kipigo na kupata sare ya 1-1 dhidi ya Sunderland kwenye mchezo wa ligi hiyo wa Jumatano usiku, mchezo uliotafsiriwa kama hatua moja nyuma baada ya awali kupata ushindi wa 2-0 walioupata - [‘One Battle After Another’ ya Thomas Anderson kuwania tuzo za National Board of Review](https://spotileo.co.tz/one-battle-after-another-ya-thomas-anderson-kuwania-tuzo-za-national-board-of-review/) - LOS ANGELES: “One Battle After Another” imetajwa movie bora ya mwaka 2025 na National Board Review Awards ambayo pia mwanzo imeweza kupokea tuzo chini ya Director Paul Thomas Anderson. Ni tuzo baada ya tuzo kwa filamu mpya alioigiza Leonardo DiCaprio, ambayo imeng’ara katika tangazo la tuzo za kifahari za National Board of Review (NBR) lililotolewa - [Angelina Jolie aingia katika filamu za kutisha](https://spotileo.co.tz/angelina-jolie-aingia-katika-filamu-za-kutisha/) - NEW YORK: MCHEZA filamu Angelina Jolie, ambaye amecheza katika filamu ya ‘The Maria,’ amekuwa akianza uzalishaji wa filamu mpya yenye maudhui ya kutisha inayoitwa ‘Sunny.’. Filamu hii inamuhusu mwanamke gaidi ambaye anapigana kuwalinda watoto wake dhidi ya mhalifu wa dawa za kulevya, lakini anabaki na muda mchache wa kukimbia baada ya tukio la kushtua. Muongozaji - [Rose Muhando aeleza mateso aliyopitia](https://spotileo.co.tz/rose-muhando-aeleza-mateso-aliyopitia/) - DAR ES SALAAM: MWANAMUZIKI mkongwe wa nyimbo za injili kutoka Tanzania, Rose Muhando, ameeleza ugumu aliopitia katika maishani mwake. Rose amesema aliytokea kumuamini mtu wa karibu yake lakini alifanyiwa njama za udanganyifu hali iliyomsababishia akamatwe uwanja wa ndege alipokuwa kwenye maandalizi ya kwenda Marekani. Katika mahojiano maalum na Askofu Kathy Kiuna, Rose Muhando alieleza changamoto - [Ibenge aonesha kutoridhishwa na matokeo Azam FC](https://spotileo.co.tz/ibenge-aonesha-kutoridhishwa-na-matokeo-azam-fc/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, ameonesha kutoridhishwa na kiwango cha ubora wa umaliziaji wa kikosi chake licha ya timu hiyo kulazimishwa sare tasa dhidi ya Singida Black Stars, mchezo ambao Azam walitengeneza nafasi nyingi za wazi. Akizungumza baada ya mchezo huo wa Ligi Kuu jana, Ibenge alisema kikosi chake kilipaswa - [Esma Khan: Mavazi ya sasa si mapya](https://spotileo.co.tz/esma-khan-mavazi-ya-sasa-si-mapya/) - DAR ES SALAAM: DADA wa Msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Khan, amesema kuwa katika ulimwengu wa mavazi hakuna kitu kipya kwani mitindo mingi ya sasa imeshawahi kuvaliwa tangu enzi za mabibi na mababu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Esma ameandika: “Enzi za mabibi na mababu zetu hakuna hata aliyekuwa na kitambi, - [Mange Kimambi aomba msaada kwa Trump](https://spotileo.co.tz/mange-kimambi-aomba-msaada-kwa-trump/) - WASHINGTON DC: MWANAHARAKATI kutoka Tanzania, Mange Kimambi, amemwandikia barua ya dharura rais wa Marekani, Donald Trump, akilalamika kuhusu kufungiwa kwa akaunti zake za mitandao ya kijamii na kampuni ya Meta. Mange, ambaye amekuwa akiishi Marekani tangu 2012, alidai kuwa kufungiwa kwa akaunti zake kumemnyamazisha mmoja wa njia chache zilizobaki za kuandika na kushuhudia ukiukaji wa - [Niffer aandika ujumbe mzito kwa vijana](https://spotileo.co.tz/niffer-aandika-ujumbe-mzito-kwa-vijana/) - DAR ES SALAAM: BAADA ya kuachiwa kwa msamaha, msanii maarufu wa mitandaoni Jenifer Jovini, 'Niffer', ametoa ujumbe mzito wenye kugusa hisia nyingi kupitia ukurasa wake wa Instagram, akiwashukuru wanaompenda na kuwaasa vijana kujifunza kupitia safari yake. Katika ujumbe mrefu ameuandika, Niffer alianza kujieleza kwa unyenyekevu: “Name: Jenifer .b. Jovin, age: 26 years, season completed: madrasa - [Kasililika kufungua michuano ya Dunia leo](https://spotileo.co.tz/kasililika-kufungua-michuano-ya-dunia-leo/) - DUBAI: MASHINDANO ya Ubingwa wa Dunia ya Chama cha Kimataifa cha Ngumi (IBA) yanaanza rasmi leo jijini Dubai, Falme za Kiarabu ambapo Bondia wa Timu ya Taifa ya Tanzania “Faru Weusi”, Enzi Kasililika, atafungua pazia kwa kwa kupanda ulingoni dhidi ya Joshua Cousin wa Shelisheli. Pambano la Kasililika litakuwa katika uzani wa kilo 75 (Middleweight), - [Emegha asimamishwa kwa ukosefu wa maadili](https://spotileo.co.tz/emegha-asimamishwa-kwa-ukosefu-wa-maadili/) - STRASBOURG: KLABU ya Strasbourg imemsimamisha nahodha na mshambuliaji wake, Emmanuel Emegha mchezo mmoja kutokana na kile ilichokitaja kama ‘kutoheshimu maadili, matarajio na kanuni za klabu.’ Katika tangazo la uamuzi huo lililotolewa leo Jumatano, Strasbourg haikufafanua undani ni tukio lipi hasa lililopelekea uamuzi huo lakini imesema kwamba mchezaji huyo atarejea kwenye kikosi kwa mchezo unaofuata. “Tumechukua - [Olmo nje mwezi mmoja](https://spotileo.co.tz/olmo-afunga-mwaka-barcelona/) - BARCELONA: vinara wa LaLiga FC Barcelona, wamethinitisha kuwa Kiungo wao Dani Olmo, atakosekana kwa takribani mwezi mmoja baada ya kuvunjika bega lake la kushoto. Taarifa ya Barcelona imesema: “Olmo amepata jeraha la kuvunjika bega lake la kushoto wakati wa mchezo dhidi ya Atletico Madrid jana. Baada ya vipimo kufanyika, matibabu yasiyo ya upasuaji yamechaguliwa. Muda - [Mcheza filamu ahukumiwa kujihusisha na propaganda](https://spotileo.co.tz/mcheza-filamu-ahukumiwa-kujihusisha-na-propaganda/) - IRAN: JAFAR Panahi, ambaye ni mkali wa filamu mwenye umri wa miaka 65, amehukumiwa na Iran hukumu ya nje ya mahakama kwa kosa la kujihusisha na shughuli za propaganda dhidi ya nchi hiyo. Jafar Panahi, ambaye alishinda tuzo kuu ya Cannes mwaka huu kwa filamu yake ‘It Was Just an Accident’. Filamu hii inaelezea hadithi - [Miley Cyrus achumbiwa na Maxx Morando](https://spotileo.co.tz/miley-cyrus-achumbiwa-na-maxx-morando/) - LOS ANGELES: BAADA ya kuibua minong’ono na kuvutia maoni mengi, Mwanamuziki Miley Cyrus, ambaye ana umri wa miaka 33, amethibitisha rasmi kuwa anachumbiwa na Maxx Morando, mchezaji wa bendi ya Liily, baada ya miaka minne ya kuwa wapenzi. Habari hii imethibitishwa na tovuti kadhaa maarufu kama Page Six na People za nchini Marekani. Miley na - [‘Avatar: Fire and Ash’ kuachiwa Desemba 19](https://spotileo.co.tz/avatar-fire-and-ash-kuachiwa-desemba-19/) - LOS ANGELES: FILAMU mpya ya James Cameron, ‘Avatar: Fire and Ash’, imezinduliwa rasmi kwenye ukumbi wa Dolby Theatre, Hollywood, kwa ajili ya kuoneshwa kwenye kumbi za sinema ambapo watu maarufu na waandishi wa habari walihudhuria kwa wingi. Uzinduzi huu pia ulihudhuriwa na wakosoaji wa filamu kutoka sehemu mbalimbali za dunia, na baada ya kuangaliwa kwa - [Leverkusen yaiondoa Dortmund DFB Pokal](https://spotileo.co.tz/leverkusen-yaiondoa-dortmund-dfb-pokal/) - DORTMUND: MABINGWA wa zamani wa Bundesliga Bayer Leverkusen wamewatupa nje wababe Borussia Dortmund katika hatua ya 16-bora ya Kombe la Ujerumani baada ya ushindi wa 1-0 ugenini, Jumanne, kwa bao pekee la Ibrahim Maza. Maza alifunga dakika ya 34, akiwaweka mabingwa hao wa Kombe la Ujerumani wa 2024 kwenye njia ya ushindi na kulipa kisasi - [Filamu ya Leonardo DiCaprio 'yaoga' tuzo](https://spotileo.co.tz/filamu-ya-leonardo-dicaprio-yaoga-tuzo/) - LOS ANGELES: FILAMU ya Paul Thomas Anderson, ‘One Battle After Another’, imeshinda tuzo moja pekee na kuibuka mshindi wa jumla kwa kutwaa tuzo ya ‘Best Feature’ licha ya kugombea vipengere sita. Wakati wa kupokea tuzo hiyo, Anderson alikiri kwa unyenyekevu kwamba hakutegemea kupata tuzo hiyo, ambayo muhusika mkuu ni Leonardo DiCaprio, “Sikutarajia hili,”. Tuazo hiyo - [Moyes amkingia kifua Grealish](https://spotileo.co.tz/moyes-amkingia-kifua-grealish/) - BRIGHTON: KOCHA wa Everton, David Moyes, amemtetea winga Jack Grealish akisema hajawa hasara tangu ajiunge na klabu hiyo kwa mkopo kutoka Manchester City, licha ya ukosoaji unaofuatia kupungua kwa kiwango chake siku za hivi karibuni kabla ya kufunga bao lake la pili msimu huu katika ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya Bournemouth, Jumanne. Grealish, mwenye - [Arteta awataka wachezaji, mashabiki kuwa kama ‘wanyama’](https://spotileo.co.tz/arteta-awataka-wachezaji-mashabiki-kuwa-kama-wanyamaarteta-awataka-wachezaji-mashabiki-kuwa-kama-wanyama/) - LONDON: KOCHA wa Arsenal, Mikel Arteta, ametoa wito wa nguvu na msisimko mkubwa kwa wachezaji wake na mashabiki wakati kikosi chake kikijiandaa kuvaana na Brentford leo Jumatano, mchezo muhimu baada ya sare mbili katika mechi tatu za Premier League zilizopunguza kasi yao. Arsenal, wanaoongoza ligi kwa tofauti ya pointi mbili na mchezo mmoja mkononi, wanaendelea - [Maresca ahaha kutafuta mbadala wa Caicedo](https://spotileo.co.tz/maresca-ahaha-kutafuta-mbadala-wa-caicedo/) - LONDON: KOCHA wa Chelsea, Enzo Maresca, anakabiliwa na mtihani mkubwa wa kutafuta mbadala wa kiungo wake muhimu, Moises Caicedo, kuelekea mchezo wa ligi kuu ya England (Premier League) dhidi ya Leeds United usiku wa leo Jumatano. Caicedo, ambaye amecheza mechi 50 kati ya 51 tangu Maresca achukue timu hiyo, alioneshwa kadi nyekundu na kutolewa nje - [Haaland aweka rekodi mpya EPL](https://spotileo.co.tz/haaland-aweka-rekodi-mpya-epl/) - LONDON: MSHAMBULIAJI wa Manchester City, Erling Haaland, ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufikisha mabao 100 ya Premier League kwa haraka zaidi, akifanya hivyo kwa kishindo katika mchezo wake wa 111 walipoibuka na ushindi wa mabao 5-4 dhidi ya Fulham, Jumanne usiku. Haaland, mwenye umri wa miaka 25, alifunga bao hilo dakika ya 17 - [“Paquetá anapitia magumu” – Nuno](https://spotileo.co.tz/paqueta-anapitia-magumu-nuno/) - LONDON: KOCHA Nuno Espírito Santo wa West Ham United, amesema kiungo wa klabu hiyo Lucas Paquetá, anapitia kipindi kigumu na amesikitishwa sana na kutolewa kwake nje kwa kadi nyekundu katika kichapo chao cha mabao 2-0 dhidi ya Liverpool Jumapili. Paquetá mwenye umri wa miaka 28, alipewa kadi mbili za njano kwa kupingana na mwamuzi (dissent) - [Serena Williams akana kurudi kwenye tenisi](https://spotileo.co.tz/serena-williams-akana-kurudi-kwenye-tenisi/) - NEWYORK: WIKI hii, kulizuka tetesi kubwa kuhusu mcheza tenesi maarufu duniani Serena Williams kurejea kwenye ulingo wa tenisi, baada ya jina lake kuonekana kwenye orodha ya wachezaji waliojisajili kwa ajili ya vipimo vya doping na Taasisi ya Uadilifu wa Tenisi (ITIA). Miaka mitatu sasa tangu alipoacha mchezo huo rasmi, baada ya kufanya safari ndefu ambayo - [Jaya Bachchan awatibua wapiga picha](https://spotileo.co.tz/jaya-bachchan-awatibua-wapiga-picha/) - MUMBAI: MMOJA wa waigizaji wakongwe wa Bollywood, Jaya Bachchan amejikuta kwenye ugonvi na wapiga picha maarufu Paparazi baada ya kusema maneno makali kuhusu wao. Alizungumza na mwandishi wa habari, Barkha Dutt, ambapo aliulizwa kuhusu uhusiano wake na paparazzi. Jaya alijibu kwa kusema hana uhusiano wowote na wapiga picha. "Mimi ni sehemu ya vyombo vya habari. - [Matola: Hakuna mechi nyepesi Ligi Kuu](https://spotileo.co.tz/matola-hakuna-mechi-nyepesi-ligi-kuu/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Msaidizi wa Simba, Seleman Matola, amesema kikosi chake kinauchukulia kwa uzito mkubwa mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City, akisisitiza kuwa hakuna mechi rahisi katika ligi hiyo. Simba watacheza mchezo wa Ligi Kuu kesho dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo saa moja jioni. - [Pedro: Yanga haibadilishi falsafa](https://spotileo.co.tz/pedro-yanga-haibadilishi-falsafa/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Pedro Goncalves, amesema licha ya safari ndefu kutoka Algeria, kikosi chake kipo tayari kurejea kwenye ushindani wa Ligi Kuu na kuendeleza kasi ya ushindi ambayo imekuwa utambulisho wa klabu hiyo. Yanga inatarajia kumenyana na Namungo kesho katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara kwenye Uwanja wa KMC - [Mgogoro wa urithi kugombanisha familia za waigizaji India](https://spotileo.co.tz/mgogoro-wa-urithi-kugombanisha-familia-za-waigizaji-india/) - MUMBAI: MAMA wa Sunjay, Rani Kapur, ametangaza madai makubwa kwamba mtoto wake alitenda jambo la kisiasa na kisheria kabla ya kufariki, kwa kumchukua Priya Sachdev kutoka kwenye bodi ya kampuni ya Sona Comstar. Kulingana na madai ya Rani Kapur, Sunjay alifanya uamuzi huo mnamo Machi 2023, akisema kuwa kuna jambo lilihitaji kurejeshwa kabla ya kifo - [Miss Universe Asia ang'ang'ania taji](https://spotileo.co.tz/miss-universe-asia-angangania-taji/) - FILIPINO: MSHINDI wa Miss Universe Filipino 2025 na Miss Universe Asia, Ahtisa Manalo ambaye ameshiriki mashindano ya dunia ya Miss Universe na kushika nafasi ya tatu ametangaza kwa umma kuwa hana nia ya kuachana na taji la Miss Universe Asia, kamamalivyoshinikizwa hapo awali. Ahtisa, mwenye umri wa miaka 28, alichagua kuendelea kushikilia majukumu yake kama - [Gamondi aita 53 Stars mchujo wa awali](https://spotileo.co.tz/gamondi-aita-53-stars-mchujo-wa-awali/) - DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Taifa Stars Miguel Gamondi ametangaza kikosi cha awali cha wachezaji 53 kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya mataifa ya Afrika AFCON 2025 itakayofanyika nchini Morocco kuanzia Desemba 21 mwaka huu hadi Januari 18, mwakani. Kikosi hicho kina wachezaji wakongwe na wazoefu wa michuano hiyo wakiongozwa na Mbwana Samatta - [AFCON kunogeshwa kwa Kiswahili mechi zote 52](https://spotileo.co.tz/afcon-kunogeshwa-kwa-kiswahili-mechi-zote-52/) - DAR ES SALAAM:MICHEZO ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) itatangazwa kwa lugha mbalimbali ikiwemo Kiswahili. Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam na Mkuu wa Masoko wa DStv Tanzania, Ronald Shelukindo, wakati wa uzinduzi wa kampeni iitwayo ‘Wanafamilia Tuna Kikao, Chimbo ni SuperSport’. Amesema DStv itaonesha mechi zote 52 za michuano hiyo kupitia chaneli - [Mkwakwate kuvutana na Mcongo Desemba 26](https://spotileo.co.tz/mkwakwate-kuvutana-na-mcongo-desemba-26/) - DAR ES SALAAM: BONDIA Ramadhan Mkwakwate maarufu kama Sungu Mtata anatarajiwa kupanda ulingoni kuvaana na mpiganaji mwenye nguvu kutoka DR Congo, Regan Pacho, katika pambano la kimataifa litakalopigwa Desemba 26, 2025 Dar es Salaam. Akizungumza wakati wa maandalizi yake Chamanzi, Mkwakwate alisema amejiandaa kikamilifu kuhakikisha ushindi unabaki nyumbani. “Maandalizi ni asilimia mia. Mashabiki waje kuona - [Simba, Azam vita yarudi upya Ligi Kuu](https://spotileo.co.tz/simba-azam-vita-yarudi-upya-ligi-kuu-2/) - DAR ES SALAAM: BAADA ya pilikapilika za mashindano ya kimataifa, vigogo wa soka nchini Simba, Azam FC na Singida Black Stars wanarejea kwenye mwendelezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakitafuta kuondoa machungu ya matokeo mabaya kwenye michuano ya CAF. Simba inatarajiwa kushuka dimbani kesho kutwa kuivaa Mbeya City, ikitokea kwenye kupoteza michezo miwili mfululizo ya - [Wabunifu wa mitindo kuchuana Swahili Fashion Ijumaa](https://spotileo.co.tz/wabunifu-wa-mitindo-kuchuana-swahili-fashion-ijumaa/) - DAR ES SALAAM: TAMASHA la Swahili Fashion Week (SFW) linarejea kwa msimu wake wa 18 likiwa limejikita zaidi katika kuibua vipaji na kuendeleza utambulisho wa mitindo ya Kiafrika duniani. Tamasha hilo linalotajwa kuwa miongoni mwa majukwaa makubwa barani Afrika litafanyika Desemba 5–7 jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa mwandaaji wa tamasha hilo, Mustafa Hassanal, - [Kamwe: Tunajifunza kwa wakubwa ili kuvuka kundi](https://spotileo.co.tz/kamwe-tunajifunza-kwa-wakubwa-ili-kuvuka-kundi/) - DAR ES SALAAM: OFISA Habari wa Yanga, Ally Kamwe, amesema kuwa licha ya timu hiyo kufanikiwa kutimiza lengo lake la awali la kufika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, safari bado haijakamilika kwani wanatamani kufika mbali zaidi. Kamwe amesema Yanga ina alama nne, ambazo bado hazitoshi kuwapa uhakika wa kufuzu hatua ya robo - [Becker ‘fiti’ kuwavaa Forest](https://spotileo.co.tz/becker-fiti-kuwavaa-forest/) - LIVERPOOL: mabingwa watetezi wa Ligi kuu ya England Liverpool wanatarajia kumkaribisha tena kipa wao namba moja Alisson Becker dhidi ya Nottingham Forest Jumamosi, jambo litakalotoa ahueni mpya kwa kikosi cha Arne Slot baada ya kipindi kigumu kabla ya mapumziko ya kimataifa. Mlinda mlango huyo wa Brazil anatarajiwa kuanza kwenye Uwanja wa Anfield baada ya kukosa - [Newcastle yalia na Polisi wa Ufaransa](https://spotileo.co.tz/newcastle-yalia-na-polisi-wa-ufaransa/) - NEWCASTLE: KLABU ya Newcastle United ya Ligi kuu ya England imeibua madai kuwa Mashabiki wake walishambuliwa na kunyanyaswa na polisi wa Ufaransa baada ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wa Jumanne usiku dhidi ya Marseille. Newcastle imesema katika taarifa yake kuwa imetuma malalamiko rasmi kwa shirikisho la soka barani Ulaya UEFA, polisi wa Ufaransa - [Huddah Monroe: Wanawake tuwe makini wakati tunapenda](https://spotileo.co.tz/huddah-monroe-wanawake-tuwe-makini-wakati-tunapenda/) - NAIROBI: VIDEO vixen na mtumiaji maarufu wa mitandao ya kijamii kutoka Kenya, Huddah Monroe, amewahimiza wanawake kuwa makini wanapochanganya mvuto wa kimwili na mapenzi. Katika chapisho lake kwenye Instagram leo Alhamisi, Novemba 27, 2025, Huddah ameeleza kwamba kemikali za asili mwilini zinaweza wakati mwingine kufanya watu waamini kuwa wako katika mapenzi halali, ilhali ni tamaa - [Fermín Lopez nje wiki mbili](https://spotileo.co.tz/fermin-lopez-nje-wiki-mbili/) - BARCELONA: KIUNGO wa mabingwa watetezi wa LaLiga FC Barcelona, Fermín López, atakuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki mbili baada ya kupata jeraha la mguu, klabu hiyo imethibitisha. Iwapo makadirio hayo yatabaki vilevile, Fermín atakosa mechi nne, ikiwemo ya LaLiga dhidi ya Atletico Madrid wiki ijayo na mechi muhimu ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya - [Gamondi hafungwi mara mbili,](https://spotileo.co.tz/gamondi-hafungwi-mara-mbili/) - ZANZIBAR: SINGIDA Black Stars imejipanga upya kuelekea mchezo wake wa marudiano dhidi ya Stellenbosch FC, ikisisitiza kuwa chini ya Kocha Miguel Gamondi hawatarudia makosa yaliyowapotezea alama kwenye mchezo wa kwanza. Timu hiyo ipo Zanzibar ambapo inaendelea na maandalizi ya mwisho kabla ya mchezo huo utakaopigwa Jumapili. Msemaji wa Singida Black Stars, Hussein Masanza, amesema maandalizi - [James Cameron: Sitoendelea na Avatar](https://spotileo.co.tz/james-cameron-sitoendelea-na-avatar/) - NEW YORK: MUONGOZAJI na muandaaji maarufu wa filamu za kisayansi, James Cameron, amedokeza kuwa ana nia ya kumaliza mfululizo wa Avatar ikiwa sinema yake ijayo, ‘Fire and Ash’, haitafikia matokeo mazuri kimataifa. Filamu hiyo inayofuata itakuwa sehemu nyingine ya mfululizo wa mafanikio kwa Cameron, mwenye miaka 71. Akizungumza kwenye kipindi cha The Town na Matt - [Simba yawatuliza mashabiki juu ya Bajaber](https://spotileo.co.tz/simba-yawatuliza-mashabiki-juu-ya-bajaber/) - DAR ES SALAAM: WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamewatuliza mashabiki zake juu ya kutochezeshwa kwa mchezaji Mohamed Bajaber wakiwataka kuwa wavumilivu. Ofisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally, ametaja sababu zilizomfanya kiungo huyo kutoka Kenya, kushindwa kusafiri na kikosi hicho kuelekea nchini Mali ni kwa kuwa bado hajapona vizuri. Simba wameifuata Stade Malien kwa ajili ya - [Simbu aifuata tuzo Ufaransa](https://spotileo.co.tz/simbu-aifuata-tuzo-ufaransa/) - DAR ES SALAAM: MWANARIADHA wa Kimataifa wa Tanzania kutoka timu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Alphonce Simbu, ameenda nchini Ufaransa ambako anatarajiwa kushiriki sherehe za Tuzo za Wanariadha Bora wa Dunia 2025 zinazoandaliwa na Shirikisho la Riadha la Dunia (World Athletics). Hafla hiyo itakayofanyika Novemba 30, 2025 jijini Monaco, itawakutanisha wanariadha 12 bora - [“Slot aiokoe Liverpool mapema” - Gerrard](https://spotileo.co.tz/slot-aiokoe-liverpool-mapema-gerrard/) - LIVERPOOL: ALIYEKUWA nahodha wa Liverpool Steven Gerrard, amesema Kocha Arne Slot, wa klabu hiyo ni lazima atafute mbinu mpya za kusitisha mwendo mbaya wa klabu hiyo huku presha ikizidi kupanda juu ya mustakabali wake klabuni hapo baada ya kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa PSV Eindhoven kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano. Kipigo hicho cha - [Kane ataka utulivu Bayern](https://spotileo.co.tz/kane-ataka-utulivu-bayern/) - LONDON: Mshambuliaji wa Bayern Munich Harry Kane, alikuwa na siku mbaya kazini wakati miamba hiyo ya Ujerumani ikipokea kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Arsenal kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumatano ikiwa ni kipigo chao cha kwanza msimu huu. Nahodha huyo wa England, ambaye tayari amefunga mabao 29 kwenye mashindano yote - [Vitinha afanya kweli PSG ikiifumua Spurs](https://spotileo.co.tz/vitinha-afanya-kweli-psg-ikiifumua-spurs/) - PARIS: MABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya Paris St Germain (PSG) walionesha roho ya kutokata tamaa baada ya kutoka nyuma mara mbili na kuichapa Tottenham Hotspur mabao 5-3 katika Ligi hiyo, ushindi uliowekwa alama na ubora wa kipekee wa Vitinha ambaye alikiongoza kikosi cha Luis Enrique kuzoa pointi zote tatu. PSG walionekana kuyumba, wakiruhusu - [“Dunia bila watu haina radha” - Obby Alpha](https://spotileo.co.tz/dunia-bila-watu-haina-radha-obby-alpha/) - DAR ES SALAAM: MWIMBAJI wa Nyimbo za Injili nchini, Obby Alpha, amesema kuwa hata mtu akiwa na utajiri na mali nyingi, bado dunia inaweza kuonekana chungu endapo ataishi peke yake bila kuwa na watu wengine. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Obby Alpha ameandika ujumbe unaohimiza umuhimu wa watu katika maisha ya kila siku, akieleza kuwa - [Agusta Masaki kukiwasha onesho la mavazi Nigeria](https://spotileo.co.tz/agusta-masaki-kukiwasha-onesho-la-mavazi-nigeria/) - DAR ES SALAAM: MBUNIFU wa mavazi na mwanamitindo Agusta Masaki anatarajiwa kuiwakilisha Tanzania katika onyesho kubwa la mavazi Africana Royal Elegance Collection at Wearnigeria, linalotarajiwa kufanyika nchini Nigeria kuanzia Novemba 28 hadi 302025. Akizungumza na Spoti Leo, Agusta Masaki alisema kuwa fursa hiyo ni hatua muhimu katika safari yake ya ubunifu na pia ni heshima - [Arsenal hawatanii msimu huu](https://spotileo.co.tz/arsenal-hawatanii-msimu-huu/) - LONDON: WASHIKA mitutu wa jiji la London Arsenal wameitandika Bayern Munich 3-1 na kupata ushindi wao wa kwanza dhidi ya miamba hiyo wa Ujerumani katika kipindi cha miaka 10, na kuendeleza rekodi yao ya ushindi wa asilimia 100 kwenye Ligi ya Mabingwa msimu huu, ushindi ambao umewaweka kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo. Jurrien Timber - [Monaco, Pafos ngoma ngumu](https://spotileo.co.tz/monaco-pafos-ngoma-ngumu/) - KOLOSSI: WABABE kutoka Ligue 1 AS Monaco wamebanwa mbavu ugenini dhidi ya Pafos ya Cyprus baada ya kupata sare ya mabao 2-2 katika Ligi ya Mabingwa Jumatano usiku, wenyeji wakipata bahati ya bao la kujifunga dakika za mwisho, wakitoka nyuma mara mbili na kuwanyima Wafaransa hao ushindi wa pili mfululizo ugenini. Monaco, ambao walipata ushindi - [“Bado tuko Imara” - Reijnders](https://spotileo.co.tz/bado-tuko-imara-reijnders/) - MANCHESTER: KIUNGO wa Manchester city Tijjani Reijnders amesema hakuna sababu ya kupoteza kujiamini ndani ya klabu hiyo licha ya kichapo cha kushtua kutoka kwa Bayer Leverkusen kwenye Ligi ya Mabingwa ulaya usiku wa Jumanne. Manchester City ilipoteza kwa mabao 2-0 nyumbani, mchezo ambao kocha Pep Guardiola aliamua kufanya mabadiliko 10 kwenye kikosi chake cha kwanza, - [Ødegaard mguu sawa kuwavaa Bayern](https://spotileo.co.tz/odegaard-mguu-sawa-kuwavaa-bayern/) - LONDON: KOCHA wa vinara wa ligi kuu ya England Arsenal Mikel Arteta amesema nahodha wa timu hiyo, Martin Ødegaard, ana nafasi ya kurejea uwanjani baada ya kupona jeraha kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Bayern Munich leo usiku. Ødegaard amekuwa nje ya kikosi cha washika mitutu hao tangu Oktoba kutokana na - [Chilwell atamani kurudi England](https://spotileo.co.tz/chilwell-atamani-kurudi-england/) - STRASBOURG: BAADA ya kipindi kigumu Chelsea, beki wa England Ben Chilwell anajaribu kurejesha makali yake klabuni Strasbourg huku akilenga kurejea kwenye timu ya taifa kuonesha mashabiki wake na wapenzi wa soka waliomupuuza kuwa hawakuwa sahihi. Mchezaji huyo wa umri wa miaka 28 anakiri kuwa kazi kubwa bado inamsubiri ikiwa atataka kuingia kwenye kikosi cha England - [Dembélé aiwahi Spurs UCL](https://spotileo.co.tz/dembele-aiwahi-spurs-ucl/) - PARIS: MSHAMBULIAJI wa PSG na mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or Ousmane Dembélé anatarajiwa uwanjani hii leo baada ya kujumuishwa kwenye kikosi cha Paris Saint-Germain kitakachokutana na Tottenham kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa ulay kufuatia kupona majeraha ya mguu wa kushoto. Dembélé hajacheza tangu alipotolewa mapema kipindi cha kwanza kwenye kichapo cha 2-1 cha - [Aliyezimia uwanjani aendelea vizuri](https://spotileo.co.tz/aliyezimia-uwanjani-aendelea-vizuri/) - NAPLES: BEKI wa Qarabağ Kevin Medina aliyezimia baada ya kupigwa na shuti kali la mchezaji wa Napoli Scott McTominay katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Jumanne anaendelea vizuri. Medina alianguka chini dakika ya 51 baada ya mpira kumpiga usoni kwa nguvu kutoka karibu, na mcolombia huyo alionekana kutotikisika akiwa hapo chini kwa karibu dakika moja. - [Thomas Frank atamani ‘pointi’ za PSG](https://spotileo.co.tz/thomas-frank-atamani-pointi-za-psg/) - PARIS: KOCHA wa Tottenham Hotspur Thomas Frank ameapa kusimama imara na mpango wake wa ujenzi wa muda mrefu wa kikosi chake licha ya kupokea kipigo Kizito cha mabao 4-1 kutoka kwa Arsenal kwenye Premier League wikiendi iliopita, wakati timu huu yake ikijiandaa kwa mechi ngumu ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Paris St Germain usiku - [Guardiola ajitwisha zigo la lawama Man City](https://spotileo.co.tz/guardiola-ajitwisha-zigo-la-lawama-man-city/) - MANCHESTER: KOCHA mkuu wa Manchester City Pep Guardiola amejitwisha zigo la lawama kwa kipigo cha kushtukisha cha mabao 2-0 dhidi ya Bayer Leverkusen katika Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumanne, akisema uamuzi wake wa kubadili kikosi kizima lilikuwa kosa kubwa. Guardiola alifanya mabadiliko 10 katika kikosi kilichocheza mchezo wa Premier League wa wikiendi iliyopita, - [Estevão amgaragaza Yamal, Maresca amsifu](https://spotileo.co.tz/estevao-amgaragaza-yamal-maresca-amsifu/) - LONDON: ILE vita iliyosubiriwa kwa hamu ya vijana barobaro Estevão na Lamine Yamal pale Stamford Bridge iliamuliwa kwa kishindo, baada ya Estevão wa Chelsea kung’ara na kufunga bao maridadi katika ushindi wa 3-0, huku Lamine Yamal wa Barcelona akiwa kimya sawa na wenzake wengi. Estevão alikimbia kwa kasi akiwapita mabeki wawili kabla ya kupiga shuti - [Newcastle yakwama Marseille](https://spotileo.co.tz/newcastle-yakwama-marseille/) - MARSEILLE: NDOTO ya Newcastle United ya kushinda mechi nne mfululizo kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya imevunjika usiku wa kuamkia leo baada ya kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Olympique de Marseille, shukrani kwa mabao mawili ya mkongwe Pierre-Emerick Aubameyang. Harvey Barnes aliwapa Waingereza hao mwanzo mzuri katika uwanja wa Stade Vélodrome baada ya kufunga dakika - [Leverkusen yavuruga rekodi ya Man City Etihad](https://spotileo.co.tz/leverkusen-yavuruga-rekodi-ya-man-city-etihad/) - MANCHESTER: KLABU ya Bayer Levekusen ya Ujerumani imevuruga rekodi ya Manchester City ya kucheza mechi 23 za nyumbani kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya bila kupoteza baada ya kipigo adimu cha mabao 2-0 jana Jumanne. Kipigo hicho kimeharibu sherehe ya mechi ya 100 ya Pep Guardiola kama kocha wa Man City kwenye - [Octopizzo awasisitiza wanafunzi kujiandikisha kupiga Kura](https://spotileo.co.tz/octopizzo-awasisitiza-wanafunzi-kujiandikisha-kupiga-kura/) - NAIROBI: MSANII wa muziki wa hip hop na mhamasishaji wa vijana, Henry Ohanga maarufu Octopizzo, ametoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, vyuo vya kati na taasisi za TVET kote nchini kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kama wapiga kura, kwa kuwa mustakabali wa nchi ya Kenya uko mikononi mwao. Katika kauli, Octopizzo alisisitiza kwamba mabadiliko ya - [Nyota Ndogo awajibu wakosoaji wa weusi wake](https://spotileo.co.tz/nyota-ndogo-awajibu-wakosoaji-wa-weusi-wake/) - NAIROBI: MWANAMUZIKI Nyota Ndogo ameibuka tena kujibu ukosoaji kuhusu rangi yake ya ngozi, akijitetea kwa uthabiti na kusheherekea weusi wake bila kujutia. Leo mapema msanii huyo alimjibu mtumiaji mmoja wa Instagram aliyemwandikia, “shida yako wewe ni mweusi sana.” Katika majibu yake, aliandika: “Sasa nakujibu. Hii rangi sio ghali. Haipatikani dukani. Kwa hivyo ni rangi special.” - [‘All’s Fair’ yaongezewa msimu wa Pili](https://spotileo.co.tz/alls-fair-yaongezewa-msimu-wa-pili/) - NEW YORK: TAMTHILIA ya kisheria ya Kim Kardashian, ‘All’s Fair’, imeongezewa msimu wa pili baada ya kupata mafanikio makubwa katika siku zake za kwanza sehemu mbalimbali ilipooneshwa. Kampuni ya uandaaji wa filamu ya Disney imeagiza msimu wa pili wa kipindi hicho cha Ryan Murphy ambacho pia kinawashirikisha Naomi Watts, Niecy Nash-Betts, Teyana Taylor, Matthew Noszka, - [Lupita Nyong’o: Niliombwa mno niigize kama mtumwa](https://spotileo.co.tz/lupita-nyongo-niliombwa-mno-niigize-kama-mtumwa/) - NEW YORK: MUIGIZAJI kutoka Mexico mwenye asili ya Kenya, Lupita Nyong’o ameweka wazi kuwa baada ya kushinda tuzo ya Oscar alipokea maombi mengi yakimtaka aigize kama mtumwa, jambo ambalo lilimshangaza na kumuumiza kiakili. Muigizaji huyo mwenye miaka 42 alishinda Tuzo ya Academy ya Muigizaji Bora Msaidizi kwa uchezaji wake mahiri kama Patsey katika filamu ya - [Miss India amshitaki mumewe adai fidia](https://spotileo.co.tz/miss-india-amshitaki-mumewe-adai-fidia/) - MUMBAI: KATIKA tukio jingine, aliyekuwa muigizaji na Miss India, Celina Jaitly, amefungua kesi ya unyanyasaji wa kinyumbani dhidi ya mumewe, Peter Haag, raia wa Austria. Kesi hiyo iliwasilishwa katika Mahakama ya Andheri, Mumbai, chini ya Sheria ya Ukatili wa Kinyumbani. Kwa mujibu wa taarifa, Celina anadai fidia ya randi50 crore pamoja na malipo mengine kufidia - [Nikitin Dheer: Dharmendra alipiga Simu akiwa ICU](https://spotileo.co.tz/nikitin-dheer-dharmendra-alipiga-simu-akiwa-icu/) - MUMBAI: MUIGIZAJI Nikitin Dheer ameonesha hisia nzito baada ya kifo cha gwiji wa Bollywood, Dharmendra, aliyefariki jana akiwa na umri wa miaka 89. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nikitin alisimulia uhusiano wa karibu uliokuwepo kati ya familia yao na marehemu, akifichua tukio la kipekee ambapo Dharmendra alipiga simu kutoka ICU kutoa pole za kifo cha - [Tiwa Savage: Sitamwacha mwanaume kwa usaliti](https://spotileo.co.tz/tiwa-savage-sitamwacha-mwanaume-kwa-usaliti/) - LAGOS: MKALI wa muziki wa Afro Beat kutoka Nigeria, Tiwa Savage, amezua gumzo baada ya kufunguka kuwa hawezi kuachana na mwanaume wake kwa sababu ya usaliti wa kimapenzi, isipokuwa iwapo mwanaume huyo atahusishwa na vitendo vya uhalifu kama wizi au matumizi ya dawa za kulevya. Akimzungumzia msimamo wake kupitia moja ya podcast, Tiwa Savage amesema - [Mwanamuziki wa reggae, Jimmy Cliff afariki dunia](https://spotileo.co.tz/mwanamuziki-wa-reggae-jimmy-cliff-afariki-dunia/) - JAMAICA: MWANAMUZIKI mkongwe wa reggae na ikoni ya utamaduni wa Jamaica, Jimmy Cliff, ambaye sauti yake ya kipekee na mchango wake mkubwa katika tasnia ya filamu ulichangia kufanya muziki wa nchi yake ya Jamaica kuwa sehemu ya utamaduni maarufu duniani, amefariki akiwa na umri wa miaka 81. Taarifa kutoka kwa familia yake ilishirikishwa Jumatatu kwenye - [‘God Design’ yapenya kimataifa kwa streams milioni 5](https://spotileo.co.tz/god-design-yapenya-kimataifa-kwa-streams-milioni-5/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Fleva, Juma Mkambala ‘Jux’, amepokea kwa furaha mafanikio makubwa ya wimbo wake God Design baada ya kutambuliwa rasmi kuvuka streams zaidi ya milioni tano kwenye mtandao wa Spotify. Wimbo huo ambao ameuachia kwa ushirikiano na mkali wa muziki kutoka Nigeria, Phyno, umeandika historia mpya ndani ya miezi sita pekee - [Yanga yatua Algeria kuwafuata JS Kabylie](https://spotileo.co.tz/yanga-yatua-algeria-kuwafuata-js-kabylie/) - ALGIERS: KIKOSI cha Yanga kimewasili Algeria tayari kwa mchezo wao wa pili wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya JS Kabylie, utakaochezwa Ijumaa wiki hii. Msemaji wa Yanga, Ally Kamwe, amesema dhamira iko kwenye kuhakikisha wanapata ushindi katika uwanja wa ugenini licha ya mchezo kutarajiwa kuwa mgumu na wenye presha kubwa. - [Simba haijakata tamaa yajipanga kurejea kwa kasi](https://spotileo.co.tz/simba-haijakata-tamaa-yajipanga-kurejea-kwa-kasi/) - DAR ES SALAAM: SIMBA SC imeweka pembeni machungu ya kupoteza mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Petro Atletico, baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0, na sasa macho yote yameelekezwa kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Stade Malien nchini Mali. Kupitia msemaji wake, Ahmed Ally, Wekundu wa Msimbazi wametoa - [Osama aahidi kumakalisha Mazome](https://spotileo.co.tz/osama-aahidi-kumakalisha-mazome/) - DAR ES SALAAM: BONDIA kutoka Mtwara, Osama Alabi, ambaye ameweka kambi yake ya maandalizi Mazense ametangaza kumkalisha mpinzani wake Ally Mazome wa Morogoro kwa TKO katika pambano la Boxing on Boxing Day litakalofanyika Desemba 26, 2025 katika Ukumbi wa Warehouse, Masaki. Akizungumza m Dar es Salaam , Alabi anayefahamika pia kama Osama Korosho amesema amejipanga - [Azam FC yaapa kuwashangaza Wydad](https://spotileo.co.tz/azam-fc-yaapa-kuwashangaza-wydad/) - DAR ES SALAAM: MSEMAJI wa Azam FC, Hasheem Ibwe, amesema kikosi chao kimejipanga kikamilifu visiwani Zanzibar kwa ajili ya kujiandaa na mchezo muhimu wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Wydad Athletic Club ya Morocco. Akizungumza kuhusu maandalizi ya mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa Ijumaa, Novemba 28, Ibwe amesema Wydad ni moja - [Hasheem Thabit: Haikuwa rahisi](https://spotileo.co.tz/hasheem-thabit-haikuwa-rahisi/) - DAR ES SALAAM: NAHODHA wa Timu ya Basketball ya Dar City, Hasheem Thabit, amesema mashindano waliyoshiriki nchini Kenya yalikuwa na ushindani mkubwa, lakini wanashukuru kwa nafasi waliyoipata na matokeo waliyofikia. Akizungumza na Spoti Leo mara baada ya kurejea nchini, Thabiti amesema mchezo wa basketball una siku zake, na si kila mara matokeo huwa upande mmoja. - [Ruto ashuhudia mtoto wa Gavana akifunga ndoa ya Kimaasai](https://spotileo.co.tz/ruto-ashuhudia-mtoto-wa-gavana-akifunga-ndoa-ya-kimaasai/) - NAIROBI: RAIS wa Kenya, William Ruto ameshuhudia harusi ya furaha iliyozungukwa na rangi nyekundu kila kona, wakati mtoto wa Gavana Patrick Ntutu, Jordan Ntutu, alipofunga ndoa na mchumba wake Abigael Moriaso katika hafla ya kuvutia iliyoandaliwa kwa mtindo wa kitamaduni wa Kimaasai. Hafla hiyo iliashiria muunganiko wa ustaarabu wa kisasa na utamaduni wa jamii hiyo - [Wapenzi wachekeshaji kufanya Onesho lao la kwanza](https://spotileo.co.tz/wapenzi-wachekeshaji-kufanya-onesho-lao-la-kwanza/) - NAIROBI: WAPENZI mashuhuri Andrew Smollo na Boera Bisieri wako mbioni kuandika historia mpya wanapojiandaa kuigiza pamoja kwa mara ya kwanza katika jukwaa la Kenya National Theatre. Hili ndilo onesho lao la kwanza la wawili hao jukwaani tangu waanze safari yao ya sanaa na mapenzi. Onesho hilo, la ‘The Vows’, ni mchanganyiko wa hisia halisi, vicheko, - [Shoo za Burna Boy Marekani zawachanganya mashabiki](https://spotileo.co.tz/shoo-za-burna-boy-marekani-zawachanganya-mashabiki/) - HOUSTON: MWANAMUZIKI nyota wa Afrobeats na mshindi wa Grammy, Burna Boy, amejikuta katikati ya mjadala mikali mtandaoni baada ya video kadhaa kutoka maonesho yake ya hivi karibuni nchini Marekani kuibua sintofahamu kuhusu mahudhurio. Mwisho wa wiki, vipande vya video vilivyosambaa kwa kasi vilionesha sehemu za juu za ukumbi wa tamasha lake la Houston zikiwa na - [Gwiji la filamu za India Dharmendra amefariki dunia](https://spotileo.co.tz/gwiji-la-filamu-za-india-dharmendra-amefariki-dunia/) - MUMBAI: GWIJI wa filamu za Bollywood, KewalKrishan Deol amefariki dunia asubuhi ya leo Jumatatu, Novemba 24 akiwa na umri wa miaka 89. Habari za kifo chake zimelitikisa jiji la Mumbai na ulimwengu mzima wa filamu, hasa ikizingatiwa kuwa wiki moja tu iliyopita alikuwa ameruhusiwa kutoka Hospitali ya Breach Candy baada ya kutibiwa kwa zaidi ya - [Donald Glover afunguka kuhusu afya yake](https://spotileo.co.tz/donald-glover-afunguka-kuhusu-afya-yake/) - LOS ANGELES: MWANAMUZIKI Donald Glover amefunguka ugonjwa mzito kumpata katika maisha yake, na kukiri kuwa na kiharusi tangu mwaka 2024 uliomfanya kumfanya kuhairisha show zake kwa mwaka mzima. Glover ambaye pia ni mwandishi wa filamu, na mchekeshaji kupitia tamasha la Tyler the Creater Camp Flog Gnaw Festival lililofanyika Jumamosi usiku huko Los Angeles alisema nilipitia - [Rammy Galis afichua aliwahi kukaa gerezani kwa kusingiziwa](https://spotileo.co.tz/rammy-galis-afichua-aliwahi-kukaa-gerezani-kwa-kusingiziwa/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa Bongo Movie, Rammy Galis, amefunguka kuhusu tukio zito lililowahi kumpata katika maisha yake, akisema aliwahi kukaa gerezani kwa kipindi cha miezi 10 baada ya kusingiziwa. Rammy ameeleza kuwa wakati huo alikuwa akifanya kazi katika shirika moja la benki, ambako ndipo matatizo hayo yalianzia. “Nilifanya kazi kwenye shirika la benki nitaliweka - [Raphinha, Yamal waamsha mzuka Barca](https://spotileo.co.tz/raphinha-yamal-wakoleza-moto-barca/) - BARCELONA: KOCHA Hansi Flick wa mabingwa watetezi wa LaLiga FC Barcelona amesema winga Lamine Yamal, aliyeikosa Hispania katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia mwezi huu kutokana na majeraha ya nyonga, yupo fiti kuelekea mchezo wa LaLiga dhidi ya Athletic Bilbao utakaochezwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Camp Nou. Yamal, ambaye amekosa mechi tatu msimu huu - [“Tunamhitaji sana Woltemade” – Eddie Howe](https://spotileo.co.tz/tunamhitaji-sana-woltemade-eddie-howe/) - LONDON: MENEJA wa Newcastle United Eddie Howe amesema Newcastle wanahitaji mchango mkubwa zaidi kutoka kwa mchezaji wao ghali zaidi, Nick Woltemade, huku wakijaribu kuamsha msimu wao wa Ligi Kuu England. The Magpies wanarejea uwanjani Jumamosi dhidi ya Manchester City wakiwa nafasi ya 14 kwenye msimamo, tofauti kubwa na kiwango chao kizuri walichoonesha kwenye Ligi ya - [“Tunaanza msimu sasa” - Guardiola](https://spotileo.co.tz/tunaanza-msimu-sasa-guardiola/) - MANCHESTER: KOCHA wa Manchester City, Pep Guardiola, amesisitiza Ijumaa hii kwamba msimu halisi ndo unaanza sasa huku timu yake sasa ikipambanai kupunguza gepu na kuwapita Arsenal kileleni mwa Ligi Kuu ya England (Premier League). City walifanikiwa kupunguza pengo la pointi na vinara Arsenal hadi kufikia nne kabla ya mapumziko ya kimataifa yaliyomalizika. Hii ilitokana na - [Mjane Simone Boseman aleta kitu cha thamani ‘Walk of Fame’](https://spotileo.co.tz/mjane-simone-boseman-aleta-kitu-cha-thamani-walk-of-fame/) - LOS ANGELES: MKE wa aliyekua muigizaji wa Black Panther Chadwick Boseman, Simone Boseman amesema Chadwick alikua na moyo wa ajabu sana kiasi kwamba angeweza kutoa nafsi yake kwa yeyote. Simone ameeleza hayo alivyokua akipokea tuzo ya ‘Walk of Fame’ ambayo ametunukiwa Chadwick Boseman ambaye ni mume wake. “Chadwick alitufundisha wote mambo mengi sana, moyo wake - [AR Rahman: Wazazi walitelekezwa Mtaani, sikuwa sawa](https://spotileo.co.tz/ar-rahman-wazazi-walitelekezwa-mtaani-sikuwa-sawa/) - MUMBAI: MWANAMUZIKI na mtayarishaji maarufu wa muziki, AR Rahman, amesimulia kuhusu maisha yake magumu ya utotoni akisema kuwa wazazi wake waliwahi kutupwa mtaani na ndugu wa baba yake, hali iliyowalazimu kuanza upya katika mazingira magumu. Rahman alisema baba yake alifanya kazi tatu kwa wakati mmoja ili kuipatia familia nyumba na kuwaweka salama, jambo ambalo baadaye - [Palmer kukosa mechi mbili zaidi](https://spotileo.co.tz/palmer-kukosa-mechi-mbili-zaidi/) - LONDON: MSHAMBULIAJI wa Chelsea na timu ya taifa ya England, Cole Palmer, atakosa mechi mbili zaidi za Premier League pamoja na mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Barcelona wiki ijayo baada ya kuvunjika kidole cha mguu, kocha Enzo Maresca amethibitisha. Palmer, mwenye umri wa miaka 23, alikuwa amerejea mazoezini hivi karibuni baada ya - [Serie A kurejea na kishindo cha Milan Derby](https://spotileo.co.tz/serie-a-kurejea-na-kishindo-cha-milan-derby/) - MILAN: JUMAPILI usiku jiji la Milan litakuwa kitovu cha burudani wakati mahasimu wa jiji hilo, Inter Milan na AC Milan, watakapokutana San Siro katika pambano linaloamua kilele cha Serie A, huku Napoli wakijaribu kurejea kwenye reli baada ya mapumziko ya kimataifa. Inter ndio wanaoongoza ligi kwa tofauti ya mabao dhidi ya Roma, na wanarejea katika - [Pogba awaweka Rennes mtegoni](https://spotileo.co.tz/pogba-awaweka-rennes-mtegoni/) - RENNES: KIUNGO wa AS Monaco raia wa Ufaransa Paul Pogba anatarajiwa kurejea uwanjani kwa mara ya kwanza baada ya zaidi ya miaka miwili nje ya soka, wakati klabu yake ya Monaco watakapokuwa ugenini dhidi ya Rennes kesho Jumamosi kwenye Ligue 1. Mshindi huyo wa Kombe la Dunia 2018 amecheza mechi 12 pekee katika misimu mitatu - [Nyota wa Wimbledon, aomba milioni 1.4 kumwokoa Shangazi yake ICU](https://spotileo.co.tz/nyota-wa-wimbledon-aomba-milioni-1-4-kumwokoa-shangazi-yake-icu/) - NAIROBI: MCHEZA tenisi nyota wa Kenya na mshindi wa taji la Wimbledon, Angella Okutoyi, amejitokeza kwa umma akiomba msaada wa milini 1.4 za Kenya ili kugharamia bili ya shangazi yake aliyelazwa katika chumba mahututi katika Hospitali ya Radiant jijini Nairobi. Okutoyi, mwenye umri wa miaka 21, aliandika ujumbe wa kusikitisha akieleza hali ya shangazi yake: - [Mastaa wa Afrika washirikishwa albamu ya Mzimbabwe, ‘The Producer’s Album 2’](https://spotileo.co.tz/mastaa-wa-afrika-washirikishwa-albamu-ya-mzimbabwe-the-producers-album-2/) - HARARE: MIAKA kumi tangu albamu ya kwanza ‘The Producer’s’ itoke ndiypo DJ na mtayarishaji mahiri wa muziki Zimbabwe St. Emmo ameamua kurudi upya na albamu yake mpya aliyopiita ‘The Producer’s Album 2’, ikiwa ni muendelezo wa albamu yake ya kwanza. Ndani ya miaka 10 Dj huyo na mtayarishaji maarufu wa muziki amesema ameamua kuachia albamu - [Chadwick Boseman apewa Nyota ya Hollywood Walk of Fame](https://spotileo.co.tz/chadwick-boseman-apewa-nyota-ya-hollywood-walk-of-fame/) - LOS ANGELES: ALIYEKUWA muigizaji kiongozi wa filamu ya Black Panther, Chadwick Boseman, amepewa heshima kubwa baada ya kutunukiwa nyota ya Hollywood Walk of Fame baada ya miaka kadhaa ya kifo chake. Familia, marafiki na wasanii wenzake walikusanyika kusherehekea kazi zake, utu wake, na urithi aliouacha duniani kupitia filamu, falsafa na uongozi wake kimichezo na kihisia. - [Simba yatoa msaada, Kaduguda akoshwa na umoja](https://spotileo.co.tz/simba-yatoa-msaada-kaduguda-akoshwa-na-umoja/) - DAR ES SALAAM: TAASISI ya Mo Dewji kwa kushirikiana na Simba SC imetembelea na kutoa msaada katika Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha Al-Zam kilichopo Temeke, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza wajibu wao kwa jamii. Simba inafanya tukio hilo kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi dhidi ya Petro - [Miss Universe apingwa mitandaoni](https://spotileo.co.tz/miss-universe-apingwa-mitandaoni/) - THAILAND: Shindano la 74 la Miss Universe 2025 limetamatika nchini Thailand, na mrembo wa Mexico, Fatima Bosch, ametangazwa mshindi wa taji la dunia. Hata hivyo, mtandaoni kumekuwa na hisia mseto, baadhi wakipongeza ushindi wake huku wengine wakipinga matokeo hayo. Wengi waliodhani kuwa mwakilishi wa India Manika Vishwakarma ambaye ni mwanafunzi wa sayansi ya siasa mwenye - [Ngwando: “Mikono Itaongea Siku Ya Boxing Day”](https://spotileo.co.tz/ngwando-mikono-itaongea-siku-ya-boxing-day/) - DAR ES SALAAM: BONDIA Ally Ngwando amesema hana haja ya maneno mengi kuelekea pambano lake na Mussa Makuka litakalopigwa Desemba 26, akisisitiza kuwa Watanzania wanaufahamu uwezo wake ulingoni. Akizungumza na waandishi wa habari, Ngwando alisema muda wa maneno umekwisha na kwamba kazi yake itaonekana siku ya pambano. “Sina maneno mengi kwa sababu Watanzania wanaijua kazi - [Sanjay Leelah kuachia ‘Do Deewane Seher Mein’ mwakani](https://spotileo.co.tz/sanjay-leelah-kuachia-do-deewane-seher-mein-mwakani/) - MUMBAI: MTAYARISHAJI wa filamu Sanjay Leelah Bhansali kufanikiwa kuzindua tarehe ya ujio wa filamu yake ‘Do Deewane Seher Mein’. Muongozaji wa filamu hiyo Ravi Udyawar kupitia Zee studios na Bhansali production alisema filamu hiyo itaachiwa February 20,2026. Waigizaji wakubwa na mashuhuri Siddhant Chaturvedi na Mnural Thakur kuwepo ndani ya filamu hiyo. Watayarishaji waelezea kionjo cha - [“Kundi la Kifo? Tutashindana na Mabingwa” Pedro](https://spotileo.co.tz/kundi-la-kifo-tutashindana-na-mabingwa-pedro/) - ZANZIBAR: KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Pedro Goncalves, amesema kuwa mchezo wa kesho dhidi ya FAR Rabat utakuwa changamoto kubwa, lakini timu yake ipo tayari kuushinda. Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mchezo huo Leo, amesema: “Kesho ni mchezo wetu wa kwanza kwenye hatua ya makundi. Kila mtu anasema ni kundi la kifo - [Barcelona na matumaini lukuki Camp Nou](https://spotileo.co.tz/barcelona-na-matumaini-lukuki-camp-nou/) - BARCELONA: MABINGWA watetezi wa LaLiga FC Barcelona wana kila sababu ya kusherehekea kurejea Camp Nou, lakini kocha wao Hansi Flick anasisitiza furaha yake itakamilika endapo watafungua uwanja wao uliokarabatiwa kwa ushindi watakapokaribisha Athletic Bilbao Jumamosi. Vigogo hao wa Catalonia wanarejea katika makazi yao wakiwa nyuma ya Real Madrid kwa pointi tatu, baada ya mwanzo wa - [Iniesta aimiliki kikamilifu Israel-Premier Tech](https://spotileo.co.tz/iniesta-aimiliki-kikamilifu-israel-premier-tech/) - BARCELONA: TIMU ya baiskeli ya Israel-Premier Tech sasa itajulikana kama NSN Cycling Team baada ya kununuliwa na kampuni ya michezo na burudani, Never Say Never, iliyoanzishwa na nyota wa zamani wa Barcelona na Hispania, Andrés Iniesta. Timu hiyo yenye leseni ya Israel imekuwa ikikumbwa na ukosoaji mkubwa katika mashindano mbalimbali mwaka huu, hatua iliyochangia Premier - [Gattuso hana presha na Kombe la Dunia 2026](https://spotileo.co.tz/gattuso-hana-presha-na-kombe-la-dunia-2026/) - MILAN: KOCHA wa timu ya taifa ya Italia, Gennaro Gattuso, amesema timu yake inatarajia mechi gumu dhidi ya Ireland Kaskazini mwezi Machi kwenye nusu fainali ya Playoff ya kufuzu Kombe la Dunia la mwakani. Italia, mabingwa wa dunia mara nne, wanapigania kurejea katika fainali hizo kwa mara ya kwanza tangu 2014 baada ya kukosa michuano - [MLS kusimama wiki saba](https://spotileo.co.tz/mls-kusimama-wiki-saba/) - FLORIDA: LIGI kuu ya Marekani Major League Soccer (MLS) imetenga mapumziko ya wiki saba katika kalenda ya msimu ujao ili kuruhusu wachezaji kushiriki Kombe la Dunia la 2026 litakalofanyika nchini humo na majirani zao Mexico na Canada. Kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa Alhamisi, ligi hiyo itasimama kuanzia Mei 25 tarehe ya lazima ya kuripoti kwa - [Donnum achunguzwa kwa ubaguzi](https://spotileo.co.tz/donnum-achunguzwa-kwa-ubaguzi/) - PARIS: WINGA wa Toulouse, Aron Donnum, yuko chini ya uchunguzi wa awali kufuatia tuhuma za kuonesha ishara ya kibaguzi, kwa mujibu wa ofisi ya mwendesha mashtaka wa Toulouse, kama alivyoliambia shirika la Reuters Alhamisi, baada ya taarifa za awali kutoka kwenye gazeti la L’Equipe la Ufaransa. Uchunguzi huo unatokana na tukio lililotokea katika mechi ya - [Job: Yanga tuko tayari kuivaa Far Rabat](https://spotileo.co.tz/job-yanga-tuko-tayari-kuivaa-far-rabat/) - ZANZIBAR: NAHODHA wa Yanga SC, Dickson Job, amewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kesho kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar, wakati mabingwa hao wa kihistoria wakipambana na FAR Rabat ya Morocco kwenye mchezo wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Job amesema wachezaji wote wako tayari kupambana na kuhakikisha wanapata matokeo, akisisitiza - [Dar City yanusa fainali za ligi ya kikapu Afrika](https://spotileo.co.tz/dar-city-yanusa-fainali-za-ligi-ya-kikapu-afrika/) - NAIROBI: KLABU ya Dar City imeweka historia mpya baada ya kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya kufuzu Fainali za Ligi ya Afrika, kufuatia rekodi ya ushindi katika michezo yake yote mitatu ya Kundi B. Katika mchezo wa kwanza, Dar City ilianza kwa kishindo baada ya kuichapa Matera Magic kwa pointi 85–78, kabla ya - [“Pilipili ameondoka wakati Taifa linamhitaji” - Steve Nyerere](https://spotileo.co.tz/pilipili-ameondoka-wakati-taifa-linamhitaji-steve-nyerere/) - DODOMA:MWENYEKITI wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steve Mengele maarufu kama Steve Nyerere, amesema kifo cha mchekeshaji MC Pilipili kimetokea katika wakati ambao taifa lilikuwa bado linamhitaji kwa kiasi kikubwa. Akitoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu, Steve Nyerere alisema taifa lote linaomboleza kuondokewa na msanii aliyekuwa na mchango - [Wasanii watakiwa kuongeza viwango vya filamu za Tanzania](https://spotileo.co.tz/wasanii-watakiwa-kuongeza-viwango-vya-filamu-za-tanzania/) - DAR ES SALAAM: WADAU wa filamu nchini wamehimiza utengenezaji wa kazi zenye ubora na viwango vya kimataifa ili kukuza hadhi ya soko la filamu Tanzania na kuinua vipaji vipya. Akizungumza katika uzinduzi huo, Munirah Pendeza, 'Tusa' ndani ya tamthilia hiyo, amesema sekta ya filamu kwa sasa imekuwa na hamasa, morali na motisha kubwa miongoni mwa - [Italia yawekewa ‘vigingi’ WC 2026](https://spotileo.co.tz/italia-yawekewa-vingingi-wc-2026/) - ZURICH: TIMU ya taifa ya Italia itaanzia nyumbani dhidi ya Ireland ya Kaskazini katika michezo ya mchujo ya kufuzu Kombe la Dunia mwezi Machi mwakani, lakini safari yao ya kurejea kwenye fainali hizo baada ya kukosa mara mbili mfululizo inaweza kuhitaji ushindi ugenini. Hii ni baada ya FIFA kuchezesha droo ya michezo ya mechi hizo - [Mwanafa: Kifo cha MC Pilipili kitukumbushe wema](https://spotileo.co.tz/mwanafa-kifo-cha-mc-pilipili-kitukumbushe-wema/) - DODOMA: NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwanafa’, amesema msiba wa msanii wa uchekeshaji Emanuel Mathias ‘MC Pilipili’ umewaunganisha watu kutoka makundi mbalimbali na kuwa ukumbusho wa thamani ya maisha. Akizungumza katika ibada ya kumuaga msanii huyo iliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali, Dodoma leo, Mwanafa alisema kifo cha MC Pilipili kimetumika - [Miriam Mauki amlilia MC Pilipili](https://spotileo.co.tz/miriam-mauki-amlilia-mc-pilipili/) - DAR ES SALAAM: MSANII wa muziki wa Injili, Miriam Mauki, ametoa ushuhuda wake kuhusu marehemu Emanuel “Mc Pilipili”, akimuelezea kama kijana aliyekuwa na kiwango cha juu cha heshima, shukrani na hekima sifa ambazo amesema hazipatikani kwa vijana wengi wa kizazi cha sasa. Akizungumza kuhusu maisha na tabia za mchekeshaji huyo, Miriam amesema kuwa siri kubwa - [Hapatoshi CAFCL wikiendi hii](https://spotileo.co.tz/hapatoshi-cafcl-wikiendi-hii/) - CAIRO: VIGOGO wa Afrika, Al Ahly, Mamelodi Sundowns na Esperance de Tunis, Simba na Yanga wanatarajiwa kulinda heshima ya nyumbani katika mechi zao za ufunguzi wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) msimu wa 2025/26. Bingwa wa kihistoria wa mara 12, Al Ahly ya Misri, wataingia kwenye Derby ya Afrika Kaskazini watakapovaana - [Advocaat atoa neno Curaçao kufuzu WC 2026](https://spotileo.co.tz/advocaat-atoa-neno-curacao-kufuzu-wc-2026/) - AMSTERDAM: KOCHA mkongwe Dick Advocaat amesema kufuzu kwa taifa dogo la Curaçao katika Kombe la Dunia ni “kitu cha ajabu zaidi” kuwahi kutokea katika maisha yake yote ya ukocha. Kisiwa hicho cha Caribbean chenye idadi ya watu wasiozidi laki moja na nusu, ambacho ni sehemu ya Uholanzi kinachojitawala, kiliandika historia Jumanne mjini Kingston baada ya - [‘Kila mchezo kwetu Simba Queens ni fainali’](https://spotileo.co.tz/kila-mchezo-kwetu-simba-queens-ni-fainali/) - DAR ES SALAAM: KOCHA wa Simba Queens Mussa Hassan ‘Mgosi’ amesema soka la wanawake limebadilika siku hizi hakuna timu ya kudharau kila mpinzani wanamuheshimu na kuuchukulia mchezo kama fainali. Kauli yake inakuja baada ya kutoka kushinda mabao 3-0 dhidi ya Bunda Queens katika mchezo wa Ligi Kuu Wanawake uliochezwa jana kwenye Uwanja wa KMC. Mgosi - [Sonam Kapoor atangaza ujauzito wa Pili](https://spotileo.co.tz/sonam-kapoor-atangaza-ujauzito-wa-pili/) - MUMBAI: MUIGIZAJI na ikoni ya mitindo huko Bollywood, Sonam Kapoor Ahuja, ametangaza rasmi kwamba yeye na mumewe Anand Ahuja wanatarajia mtoto wao wa pili. Wawili hao tayari ni wazazi wa mtoto mmoja anayeitwa Vayu. Kwa miezi kadhaa mashabiki walikuwa wakihisi kuwa Sonam ana ujauzito baada ya video na picha za uwanja wa ndege kuzua tetesi. - [Oscars 2026 kuonesha Tuzo zote 24 'Live'](https://spotileo.co.tz/oscars-2026-kuonesha-tuzo-zote-24-live/) - LOS ANGELES: WAANDAAJI wa tuzo za Oscars 2026 wameahidi kutanua wigo wa tuzo hizo na kuongeza ubunifu mbalimbali ikiwemo kuonesha vipengele vyote vya tuzo 24 mubashara. Waandaaji hao wamethibitisha kwamba kipengele kipya cha ubora katika casting kitaonekana kwenye matangazo ya moja kwa moja ya Tuzo za 98 za Academy Awards mwezi Machi. Hatua hii inaifanya - [Ronaldo uso kwa uso na Trump](https://spotileo.co.tz/ronaldo-uso-kwa-uso-na-trump/) - WASHINGTON DC: MWANASOKA maarufu duniani Cristiano Ronaldo ambaye sasa anakipiga katika timu ya Al Naasr ya Saudi Arabia akiwa na mchumba wake Georgina wamekutana na kuzungumza na Raisi wa Marekani Donald Trump mambo kadhaa. Mazungumzo hayo yamefanyika ndani ya ofisi ya Rais Ikulu ya Marekani. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ronaldo amemshukuru Rais Trump na - [Mwakinyo: Mchanja yupo kamili kwa Mfilipino](https://spotileo.co.tz/mwakinyo-mchanja-yupo-kamili-kwa-mfilipino/) - MANILA: KOCHA wa bondia Yohana Mchanja, Khamis Mwakinyo amesema bondia wake yupo tayari kumvaa Mfilipino Regie Suganob Bingwa wa dunia wa WBO Global Jr. Flyweight katika pambano lisilokuwa la ubingwa litakalopigwa Jumamosi nchini Ufilipino. Akizungumza na SpotiLeo Mwakinyo amesema tayari wameshawasili salama Ufilipino wakiwa katika hali nzuri na tayari kumvaa mpinzani. “Tunashukuru Mungu tumefika salama - [Mashabiki wamwagiwa maji Tamasha la Travis Scott](https://spotileo.co.tz/mashabiki-wamwagiwa-maji-tamasha-la-travis-scott/) - MUMBAI: MSANII nyota kutoka Marekani, Travis Scott, akiwa anatumbuiza katika jukwaa la Mahalaxmi Racecourse mjini Mumbai nchini India jana huku joto kali likitanda katika ukumbi huo na kuzua taharuki kwa wahudhuliaji. Baada ya joto kuzidi ukumbini hapo walinzi waliamua kunyunyizia maji mashabiki ili kupunguza joto. Katika klipu inayovuma, kikosi cha ulinzi kinaonekana kikiwa na mabomba - [Vince Gill atunukiwa Tuzo ya Lifetime Achievement Award](https://spotileo.co.tz/vince-gill-atunukiwa-tuzo-ya-lifetime-achievement-award/) - NASHVILLE: MWANAMUZIKI mkongwe wa country, Vince Gill, ameandikisha sura mpya katika safari yake ya zaidi ya nusu karne baada ya kuheshimiwa kwa kupewa tuzo ya Willie Nelson Lifetime Achievement Award katika Tuzo za CMA 2025. Gill alipokea tuzo hiyo jana Jumatano, Novemba 19, kwenye sherehe zilizofanyika Nashville. Kabla ya kupokea heshima hiyo, Brandi Carlile na - [Paula 'amuwekea fensi' Marioo](https://spotileo.co.tz/paula-amuwekea-fensi-marioo/) - DAR ES SALAAM: MSANII nyota wa Bongo Fleva, Omary Mwanga ‘Marioo’, amefichua namna mpenzi wake Paula Kajala anavyomjali katika suala la lishe, akisisitiza kuwa Paula hupenda amuone akiwa kwenye hali bora kiafya na kimwili. Akizungumza hivi karibuni, Marioo amesema Paula ni miongoni mwa wanawake wanaojali afya za wapenzi wao na hawapendi waone wakila vyakula visivyo - [Filamu ya Sinners yashinda tuzo 3 Hollywood](https://spotileo.co.tz/filamu-ya-sinners-yashinda-tuzo-3-hollywood/) - CALIFORNIA: FILAMU ya Sinners imeshinda tuzo tatu kubwa katika tuzo za 16 za Hollywood Music in Media Awards (HMMAs), zilizofanyika Jana Jumatano November 19 katika ukumbi wa The Avalon, Hollywood, California nchini Marekani. Filamu hiyo imepokea tuzo hizo ikiweka rekodi ya kuwa filamu iliyoshinda tuzo nyingi zaidia ya filamu zote zilizoshindanishwa katika tuzo hizo. Mtunzi - [Mboso Khan kuja na Pawa Remix](https://spotileo.co.tz/mboso-khan-kuja-na-pawa-remix/) - DAR ES SALAAM: Msanii mahiri wa Bongo Fleva, Mbwana Kilungi ‘Mboso Khan’, anatarajia kuachia wimbo wake mpya “Pawa Remix” usiku wa leo saa sita kamili (00:00). Hii inakuja baada ya toleo la awali la wimbo “Pawa” kufanya vizuri na kushika chati mbalimbali, jambo lililompa msanii huyo sababu ya kuongeza moto kwenye kiwanda cha muziki wa - [CAF yamtuza Rais Samia kwa mchango katika michezo](https://spotileo.co.tz/caf-yamtuza-rais-samia-kwa-mchango-katika-michezo/) - RABAT: SHIRIKISHO la Soka Barani Afrika (CAF) limemkabidhi tuzo Rais Dk Samia Suluhu Hassan, kutambua mchango wake mkubwa katika kukuza michezo hususan mpira wa miguu nchini. Tuzo hiyo ilipokelewa kwa niaba ya Rais Samia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa, katika hafla - [Davido atoa pole kwa WanaKebbi](https://spotileo.co.tz/davido-atoa-pole-kwa-wanakebbi/) - LAGOS: NYOTA wa muziki wa Nigeria David Adeleke maarufu Davido, ametuma ujumbe wa faraja kwa familia za wasichana waliotekwa katika Jimbo la Kebbi nchini Nigeria. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Davido ameeleza masikitiko yake ya kutekwa kwa wasichana hao wa Kebbi huku akiwaomba Wanigeria wote waungane na kuwa na umoja kuhakikisha watoto ambao hawajatekwa wawe - [Tuzo ya goli bora! Mzize awapa tano mashabiki](https://spotileo.co.tz/tuzo-ya-goli-bora-mzize-awapa-tano-mashabiki/) - DAR ES SALAAM: MSHAMBULIAJI wa Yanga SC, Clement Mzize, ametoa shukrani kwa mashabiki na wote waliomuunga mkono baada ya kutangazwa mshindi wa Tuzo ya Goli Bora Afrika, katika hafla ya utoaji wa tuzo za CAF iliyofanyika jana nchini Morocco. Mzize alishindwa kuhudhuria katika hafla hizo kutokana na majeraha baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti. Kupitia - [MC Pilipili Kuzikwa Leo](https://spotileo.co.tz/mc-pilipili-kuzikwa-leo/) - DODOMA: MSANII wa vichekesho Emmanuel Mathias, maarufu kama Mc Pilipili, ambaye amefariki dunia Novemba 16, 2025 , anatarajiwa kuagwa na kuzikwa leo nyumbani Swaswa, mkoani Dodoma, Ibada Kuu kufanyika Chinangali Kwa mujibu wa taarifa za familia, mwili wa marehemu utatolewa nyumbani kwao Swaswa, kisha kupelekwa Viwanja vya Chinangali ambapo ibada kuu na shughuli ya kuaga - [Picha za ngono zamponza ‘staa’ wa Benfica](https://spotileo.co.tz/picha-za-ngono-zamponza-staa-wa-benfica/) - COPENHAGEN: MAHAKAMA nchini Denmark imemkuta na hatia ya kusambaza video ya ngono inayowahusisha wavulana wawili walio chini ya miaka 18 mchezaji wa timu ya taifa ya Norway Andreas Schjelderup, na ikamhukumu kifungo cha nje cha wiki mbili. Schjelderup, mwenye umri wa miaka 21, ambaye mwaka jana alikuwa akikichezea klabu ya FC Nordsjaelland ya Denmark, aliieleza - [Eder Militao ahofiwa kukosa mechi kadhaa](https://spotileo.co.tz/eder-militao-ahofiwa-kukosa-mechi-kadhaa/) - MADRID: WABABE wa soka la Ulaya Real Madrid wamethibitisha kwamba beki wao raia wa Brazil, Eder Militao, amepata majeraha ya nyonga, ingawa klabu hiyo haijaweka wazi muda atakaokaa nje ya uwanja. Katika taarifa yao ya Jumatano, Madrid imesema vipimo vilivyofanywa na timu ya madaktari vimeonesha kwamba Militao ana jeraha la misuli katika eneo la nyonga, - [Tuzo za CAF: Hakimi mchezaji bora Afrika, Morocco yang’aa](https://spotileo.co.tz/tuzo-za-caf-hakimi-mchezaji-bora-afrika-morocco-yangaa/) - RABAT: NAHODHA wa timu ya taifa ya Morocco, Achraf Hakimi, ameibuka mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika kwa upande wa wanaume katika tuzo za CAF zilizofanyika usiku wa jana Jumatano, akihitimisha msimu ambao alinyanyua taji la UEFA Champions League na klabu yake ya Paris Saint-Germain (PSG). Beki huyo wa kulia mwenye umri wa - [“Haiti imestahili Kufuzu Kombe la Dunia 2026” – kocha Migne](https://spotileo.co.tz/haiti-imestahili-kufuzu-kombe-la-dunia-2026-kocha-migne/) - WILLEMSTAD: KOCHA wa timu ya taifa ya soka ya Haiti, Sebastien Migne, amesema kuwa umoja wa kikosi na ustahimilivu ndiyo ilikuwa siri kuu iliyopelekea taifa hilo kufuzu Kombe la Dunia la mwaka 2026, kufuatia ushindi wao wa magoli 2-0 dhidi ya Nicaragua. Haiti ilishinda vikwazo vikubwa kufuzu kwa mara ya pili katika historia yao ya - [Arsenal yamalizana na Visit Rwanda](https://spotileo.co.tz/arsenal-yamalizana-na-visit-rwanda/) - KIGALI: BODI ya Maendeleo ya Rwanda (Rwanda Development Board - RDB) imetangaza kuwa itasitisha mkataba wake wa ushirikiano na klabu ya Ligi Kuu ya England, Arsenal, mwishoni mwa msimu huu kwa makubaliano ya pande zote mbili. Ushirikiano huo, uliojulikana kama "Visit Rwanda," ulianza miaka nane iliyopita, lakini umezidi kukosolewa kutokana na kuongezeka kwa ghasia mashariki - [CMA Awards 2025 kufanyika leo usiku Nashville](https://spotileo.co.tz/cma-awards-2025-kufanyika-leo-usiku-nashville/) - NASHVILLE: USIKU wa leo, Novemba 19, 2025, tamasha la CMA Awards la mwaka wa 59 litafanyika huko Nashiville. Tamasha hili la kila mwaka linaandaliwa kwa kura za wanachama zaidi ya elfu saba wa Chama cha Muziki (Country Music Association), ambao ni wasanii, waandishi wa nyimbo, waandaaji, na wafanyakazi wa redio wanaoshiriki ndani ya tasnia. Chama - [UEFA yatoa kibali Camp Nou](https://spotileo.co.tz/uefa-yatoa-kibali-camp-nou/) - BARCELONA: MABINGWA watetezi wa LaLiga, FC Barcelona, wamepokea idhini kutoka Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA) kuruhusiwa kutumia uwanja wake wa Camp Nou, ambao unakarabatiwa, kwa ajili ya mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya (Champions League). Hatua hii inajiri baada ya miamba hiyo wa Hispania kukaa zaidi ya miaka miwili ugenini kutokana na changamoto za - [McClaren abwaga manyaga Jamaica](https://spotileo.co.tz/mcclaren-abwaga-manyaga-jamaica/) - KINGSTON: KOCHA wa zamani wa timu ya Taifa ya England, Steve McClaren, amejiuzulu kama kocha wa timu ya Taifa ya Jamaica baada ya “Reggae Boyz” kulazimishwa sare ya 0-0 dhidi ya Curaçao na kushindwa kufuzu moja kwa moja Kombe la Dunia la 2026. Matokeo hayo yalimaanisha Curaçao kuongoza Kundi B kwa CONCACAF na kwenda mashindano - [Dick Advocaat kuweka rekodi WC 2026](https://spotileo.co.tz/dick-advocaat-kuweka-rekodi-wc-2026/) - KINGSTON: KATIKA umri wa miaka 78, Dick Advocaat atakuwa kocha mwenye umri mkubwa zaidi kuongoza timu katika Kombe la Dunia (WC 2026) baada ya timu yake ya Curacao kulazimisha sare ya kusisimua dhidi ya Jamaica na kufuzu kwa mara ya kwanza kwenye fainali za mashindano hayo. Advocaat, ambaye amefundisha timu saba tofauti za taifa, ikiwemo - [Mbadala wa VAR kuanza majaribio Australia](https://spotileo.co.tz/mbadala-wa-var-kuanza-majaribio-australia/) - SYDNEY: SHIRIKISHO la Soka nchini Australia (Football Australia) limesema Ligi ya Championship ya Australia itafanya majaribio mfumo mpya wa usaidizi wa waamuzi wa FIFA wa Football Video Support (FVS), toleo dogo la mfumo wa Video Assistant Referee (VAR), wakati wa michezo ya mtoano ndani ya wiki chache zijazo. FVS imetengenezwa na shirikisho la soka duniani - [Salim na Salma Khan washerehekea miaka 61 ya ndoa yao](https://spotileo.co.tz/salim-na-salma-khan-washerehekea-miaka-61-ya-ndoa-yao/) - MUMBAI: SALIM Khan na mke wake Salma Khan wamefurahia siku yao ya kipekee kwa kusherehekea miaka 61 ya ndoa yao kwa hafla ya faragha iliyoandaliwa nyumbani kwao wakiwa na familia. Sherehe hiyo ilijumuisha marafiki wa karibu na jamaa wa familia, ikiwa ni tukio la kipekee la kuonesha upendo na umoja wa familia hiyo maarufu. Hali - [Ned Nwoko: Sitaki kumuona Regina Daniels nyumbani kwangu](https://spotileo.co.tz/ned-nwoko-sitaki-kumuona-regina-daniels-nyumbani-kwangu/) - DELTA NORTH: MBUNGE anayeiwakilisha jimbo la Delta North, Ned Nwoko amekanusha madai kwamba anataka kurejea na mke wake wa zamani ambaye ni muigizaji wa Nollywood, Regina Daniels. Hii imekuja baada ya Regina kudai kuwa seneta huyo alikuwa amewatuma wanachama wa familia yake kuomba msamaha kwa niaba yake. Muigizaji mwenzake, Doris Ogala, pia aliunga mkono madai - ["Nilikuwa mwizi wa dhahabu" - DJ Kulet](https://spotileo.co.tz/nilikuwa-mwizi-wa-dhahabu-dj-kulet/) - LAGOS: DJ maarufu nchini, Kudirat Gbemisola, anayojulikana sana nchini humo kwa umaarufu wa DJ Kulet, amefichua kuwa alihusika katika wizi wa dhahabu alipokuwa na umri mdogo. Uamuzi huo wa kusema ukweli alifanya wakati wa kipindi kifupi cha mahojiano yake ya hivi karibuni na muigizaji Biola Adebayo kwenye podcast ya ‘Talk to B’. Akifikiria juu ya - [Wanasimba njooni mtusapoti](https://spotileo.co.tz/wanasimba-njooni-mtusapoti/) - DAR ES SALAAM: KLABU ya Simba imeita mashabiki kuisapoti timu kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Petro Atletico ya Angola utakaochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Akizungumza Dar es Salaam leo katika mkutano wa hamasa Msemaji wa Simba Ahmed Ally alisema mchezo huo una umuhimu kwao kuhakikisha wanashinda - [Manara azitakia heri Simba, Yanga kimataifa](https://spotileo.co.tz/manara-azitakia-heri-simba-yanga-kimataifa/) - DAR ES SALAAM: DIWANI wa Kata ya Kariakoo, Haji Manara, amezitakia heri timu zote nne Simba, Yanga, Singida Black Stars na Azam zifanye vizuri katika michuano ya makundi Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika itakayochezwa mwishoni mwa wiki hii. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam Leo, Manara ambaye aliwahi kuwa Msemaji - [Akon amtaka mkewe wamlea binti yao pamoja](https://spotileo.co.tz/akon-amtaka-mkewe-wamlea-binti-yao-pamoja/) - LOS ANGELES: MUIMBAJI wa wimbo wa ‘Lonely’, Akona ameiomba mahakama ihakikishe kuwa yeye na mtalaka wake Tomeka Thaim wanashiriki kwa pamoja majukumu ya malezi ya binti yao. Awali Tomeka, alifungua talaka mwezi Septemba, siku chache kabla ya kumbukumbu yao ya ndoa ya miaka 29, huku akihitaji haki ya kisheria na ya kuwa muangalizi wa binti - [Pluto: Sijamuona mwanangu Zoey mwaka sasa](https://spotileo.co.tz/pluto-sijamuona-mwanangu-zoey-mwaka-sasa/) - NAIROBI: THEE Pluto amesema kwamba amekuwa katika hali ngumu kutokana na kutopata fursa ya kuonana na kuzungumza na mwanawe Zoey kwa karibu mwaka mmoja sasa. Akizungumza kwenye kipindi cha Oga Obinna, Pluto alisema anaimani wataonana tu kwa kuwa hawakuwa na mawasiliano tangu Desemba 17, 2024. Aidha, Pluto amesema suala hilo anajitahidi kulishughulikia kwa utaratibu na - [Robertson: Natamani Jota angekuwepo Marekani](https://spotileo.co.tz/robertson-natamani-jota-angekuwepo-marekani/) - GLASGOW: Beki wa Liverpool na nahodha wa timu ya taifa ya Scotland Andy Robertson amesema alikuwa huzuni kubwa kabla ya Scotland kuibuka na ushindi wa 4-2 dhidi ya Denmark na kufuzu Kombe la Dunia 2026, akifichua kuwa mawazo yake yalikuwa yakirudi mara kwa mara kwa aliyekuwa mchezaji mwenzake wa Liverpool, Diogo Jota, na ndoto yao - ["Japan inaweza kushinda kombe la Dunia” - Honda](https://spotileo.co.tz/japan-inaweza-kushinda-kombe-la-dunia-honda/) - HONG KONG: mmoja wa mastaa wakubwa wa soka nchini Japan Keisuke Honda amesema Timu ya Taifa hilo inao ubora na kiwango cha juu hivyo ina uwezo wa kushinda Kombe la Dunia la mwakani nchini Marekani, Canada na Mexico. Honda ambaye alicheza mechi 90 na timu ya taifa ya Japan na kushiriki Kombe la Dunia mara - [Czech yailima adhabu Timu ya Taifa](https://spotileo.co.tz/czech-yailima-adhabu-timu-ya-taifa/) - PRAGUE: SHIRIKISHO la soka la Jamhuri ya Czech limeipa adhabu timu ya taifa hilo kwa kumvua unahodha Tomáš Souček na kuwanyima wachezaji wenzake posho zao kama adhabu kwa kupuuza mashabiki wao baada ya mchezo wa mwisho wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Gibraltar. Wachezaji wa Czech, ambao tayari walikuwa wamejihakikishia nafasi ya pili katika - [McTominay atupia bao la kideo Scotland ikifuzu WC2026](https://spotileo.co.tz/mctominay-atupia-bao-la-kideo-scotland-ikifuzu-wc2026/) - GLASGOW: KIUNGO wa wababe wa Serie A SSC Napoli Scott McTominay alifunga bao maridadi kwa "bicycle kick" dakika tatu baada ya kuanza kwa mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia (WC2026) wa Scotland dhidi ya Denmark usiku ya Jumanne. Ben Gannon-Doak aliutuma mpira wa krosi ya juu kutoka upande wa kulia na McTominay akaufuata akiwa amegeukia - [Curaçao Kwenda WC na Historia](https://spotileo.co.tz/curacao-kwenda-wc-na-historia/) - KINGSTON: TIMU ya Taifa ya Curaçao imefanikiwa kuwa timu ya taifa dogo zaidi kwa idadi ya watu kuwahi kufuzu Kombe la Dunia baada ya kupata sare ya 0-0 dhidi ya Jamaica jana Jumanne na itaungana na mataifa mengine ya CONCACAF ya Panama na Haiti ambayo pia yamefuzu Curaçao ilimaliza michuano yakufuzu ikiwa timu pekee ambayo - [Khadija Kopa awapasha 'Content Creators'](https://spotileo.co.tz/khadija-kopa-awapasha-content-creators/) - DAR ES SALAAM: MSANII nguli wa muziki wa taarab nchini, Khadija Kopa, amewataka watengeneza maudhui na wanahabari wa mitandaoni kuacha kuangazia tu mabaya ya wasanii na badala yake wawasaidie kwa kuwashauri na kuwaelekeza mambo ya kufanya ili kuboresha maisha yao. Akizungumza na Spoti Leo, Malkia Kopa amesema kuwa jukumu lake katika programu anayoshiriki ni kutoa - [Yakoub Suleman atuma ujumbe wa faraja kwa Camara](https://spotileo.co.tz/yakoub-suleman-atuma-ujumbe-wa-faraja-kwa-camara/) - DAR ES SALAAM: GOLIKIPA wa Simba SC, Yakoub Suleman, ametuma salamu za faraja na pole kwa mlinda mlango mwenzake, Moussa Camara, ambaye amefanyiwa upasuaji wa goti nchini Morocco. Kwa mujibu wa taarifa ya klabu ya Simba, Moussa Camara amefanyiwa upasuaji na umekamilika kwa mafanikio nchini Morocco. Baada ya taarifa hiyo, Yakoub kupitia akaunti yake ya - [‘MC Pilipili’ kuzikwa Dodoma Novemba 20](https://spotileo.co.tz/mc-pilipili-kuzikwa-dodoma-novemba-20/) - DODOMA: Msanii wa vichekesho Emmanuel Mathias, maarufu kama Mc Pilipili, ambaye amefariki dunia jana Novemba 16, 2025 , anatarajiwa kuagwa na kuzikwa Alhamisi, Novemba 20, 2025, nyumbani kwao Swaswa, mkoani Dodoma. Taarifa hizo zimetolewa na rafiki yake wa karibu, Godfrey Lughalabamu ‘Gara B’, ambaye amethibitisha kuwa msiba upo nyumbani kwa familia ya Mc Pilipili eneo - [Steve Nyerere: Daraja la jamii na mwana-Harakati wa maendeleo](https://spotileo.co.tz/steve-nyerere-daraja-la-jamii-na-mwana-harakati-wa-maendeleo/) - DA R ES SALAAM: MWENYEKITI wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steven Waiton Mengele, maarufu kama Steve Nyerere, ni miongoni mwa wadau muhimu wa maendeleo nchini kupitia mchango wake mkubwa katika sanaa za maigizo na uchekeshaji kwa miaka mingi. Kwa muda mrefu, Steve ameendelea kuwa nguzo kwa makundi mbalimbali yenye uhitaji, wasanii na wadau - [Historia ya MC Pilipili (Kuishi kwake hadi umauti ulipomkuta) 1985-2025](https://spotileo.co.tz/historia-ya-mc-pilipili-kuishi-kwake-hadi-umauti-ulipomkuta-1985-2025/) - Maandiko yanasema kuishi ni Kristo kufa ni faida MNAMO tarehe 1 Oktoba 1985, katika ardhi ya Mkoa wa Dodoma, alizaliwa mtoto wa pili wa Mathias na Mariam Matebe, aliyepewa jina Emmanuel Mathias baadaye akaja kufahamika na wananchi wengi kama MC Pilipili, mmoja wa washehereshaji na wacheshi maarufu nchini Tanzania. Kipai na maisha yake ya utotoni - [Regina Daniels: Mume wangu alininyanyasa muda mrefu](https://spotileo.co.tz/regina-daniels-mume-wangu-alininyanyasa-muda-mrefu/) - LAGOS: MUIGIZAJI maarufu wa filamu za Nollywood, Regina Daniels, ametoa tahadhari kali kwa mume wake wa zamani, Ned Nwoko, akidai kuwa amekuwa akimnyanyasa kwa muda mrefu. Katika ujumbe mrefu aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram, Regina amedai kuwa mumewe huyo alimfanya kifungoni tangu akiwa na umri wa miaka 17, kwa sasa anapigana kwa ajili ya - [MwanaYouTube akamatwa kwa dawa za kulevya](https://spotileo.co.tz/mwanayoutube-akamatwa-kwa-dawa-za-kulevya/) - MIAMI: MWANZILISHI wa mtandao wa YouTube, Jack Doherty, amekamatwa kwa mashtaka ya kumiliki dawa za kulevya na mashtaka mengineyo huko Miami. Doherty, ambaye amejulikana kwa kuunda video za kejeli, alikamatwa wakati akirekodi video na kujaribu kuwasiliana na maofisa wa polisi katikati ya barabara, hali iliyozuia msongamano, kulingana na nyaraka za kukamatwa zilizochapishwa na vyombo vya - [Nitafanya kazi hadi nikiwa na miaka 82](https://spotileo.co.tz/nitafanya-kazi-hadi-nikiwa-na-miaka-82/) - NEW YORK: MWANZILISHI maarufu wa familia ya Kardashians, Kris Jenner, ameshiriki malengo yake mapya baada ya kuadhimisha miaka 70. Nyota huyo na watoto wake Kim, Kourtney, Khloe, Rob Kardashian, Kendall na Kylie Jenner, amesema anatarajia kuendelea kufanya kazi kwa miaka mingi ijayo kwa kuwa anajilinda kiafya pamoja na kuwa na uhusiano imara na watu waliomzunguka. - [Ryan Coogler kuja na Black Panther 3](https://spotileo.co.tz/ryan-coogler-kuja-na-black-panther-3/) - NEW YORK: MTENGENEZAJI wa filamu maarufu na mwandishi wa filamu wa Marekani, Ryan Coogler, amethibitisha kuwa filamu ya Black Panther 3 itakuwa kazi yake inayofuata. Katika mahojiano na jopo la filamu la ‘Deadline’s Contenders Film: Los Angeles’, Coogler alielezea kuwa anafanya kazi kwa bidii kukamilisha kazi yake ya Marvel Cinematic Universe (MCU), na kusema wazi - [Sakata la Ronaldo latua FIFA](https://spotileo.co.tz/sakata-la-ronaldo-latua-fifa/) - GENEVA: GWIJI wa soka Duniani Cristiano Ronaldo huenda akasubiri takriban wiki tatu kujua urefu wa adhabu yake ya kufungiwa na FIFA kuelekea Kombe la Dunia 2026. Nyota huyo wa kimataifa Ureno anaweza kufungiwa mechi mbili au tatu kufuatia kadi nyekundu aliyooneshwa Alhamisi baada ya kumpiga kiwiko beki wa Ireland, Dara O’Shea, katika kipigo cha 2-0 - [Uzbekistan Kwenda kujifunza kombe la Dunia 2026](https://spotileo.co.tz/uzbekistan-kwenda-kujifunza-kombe-la-dunia-2026/) - TASHKENT: TIMU ya Taifa ya Uzbekistan itashiriki Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwakani, na viongozi wao wanasema malengo yao ni kujenga timu na kupata uzoefu badala ya kutafuta mafanikio ya haraka. Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Uzbekistan, Ravshan Irmato ambaye aliwahi kuchezesha mechi kwenye Kombe la Dunia mara tatu amesema kufuzu - [Mbappé kuwakosa Azerbaijan Jumapili](https://spotileo.co.tz/mbappe-kuwakosa-azerbaijan-jumapili/) - PARIS: SHIRIKISHO la Soka la Ufaransa (FFF) limetangaza Nahodha wa Timu ya taifa hilo, Kylian Mbappé, atakosa mchezo wao wa mwisho wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Azerbaijan Jumapili kutokana na jeraha la kifundo cha mguu. “Mbappé bado anasumbuliwa na uvimbe kwenye kifundo cha mguu wa kulia unaohitaji uchunguzi zaidi. Atafanyiwa vipimo leo mjini - [Haaland awaka Norway ikiifumua Estonia 4-1](https://spotileo.co.tz/haaland-awaka-norway-ikiifumua-estonia-4-1/) - OSLO: KIUNGO wa Timu ya Taifa ya Norway Morten Thorsby amesema mawaidha ya nahodha wao Erling Haaland wakati wa mapumziko iliamsha ari ya timu na kuisaidia Norway kuifunga Estonia mabao 4-1, ushindi uliowaweka karibu na nafasi ya kufuzu Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1998. Haaland, aliyekuwa na kitambaa cha unahodha kufuatia kukosekana - [Kocha Martinez: Kadi nyekundu ya Ronaldo ni ya kikatili](https://spotileo.co.tz/kocha-martinez-kadi-nyekundu-ya-ronaldo-ni-ya-kikatili/) - DUBLIN: KOCHA wa timu ya Taifa ya Ureno, Roberto Martinez, amesema kadi nyekundu aliyopewa nahodha wake Cristiano Ronaldo ilikuwa ya kikatili na kali mno, baada ya mshambuliaji huyo kutolewa nje kwa mara ya kwanza katika mechi za kimataifa wakati Ureno ikilala mabao 2-0 dhidi ya Ireland kwenye mechi ya kufuzu Kombe la Dunia, Alhamisi usiku - [Camara kufanyiwa upasuaji wa goti kesho](https://spotileo.co.tz/camara-kufanyiwa-upasuaji-wa-goti-kesho/) - DAR ES SALAAM: GOLIKIPA namba moja wa Simba SC, Moussa Camara, anatarajiwa kuondoka nchini kesho kuelekea Morocco kwa ajili ya kufanyiwa matibabu na upasuaji wa goti, ambao umepangwa kufanyika Jumatatu, Novemba 17. Camara alipata majeraha hayo wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United, ambapo alilazimika kutolewa nje baada ya kugongana - [MLS kuiga kalenda ya Ligi Ulaya](https://spotileo.co.tz/mls-kuiga-kalenda-ya-ligi-ulaya/) - FLORIDA: LIGI kuu ya Marekani Major League Soccer (MLS) imepanga kufanya mageuzi makubwa kwenye kalenda yake ya mashindano kuanzia mwaka 2027, ambapo ligi hiyo itahamia ratiba ya majira ya kiangazi hadi masika mfumo unaotumika na ligi kubwa za Ulaya na hatua za mtoano (playoffs) zitafanyika mwezi Mei. Mabadiliko hayo yataanza na msimu wa mpito kuanzia - [Mancini na Esposito waiokoa Italia moldova](https://spotileo.co.tz/mancini-na-esposito-waiokoa-italia-moldova/) - CHISINAU: MABAO ya dakika za lala salama kutoka kwa Gianluca Mancini na Francesco Pio Esposito yaliipa timu ya taifa ya Italia ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Moldova, na kufufua matumaini ya kuendelea kusalia kwenye mbio za kutafuta nafasi ya kufuzu moja kwa moja Kombe la Dunia 2026. Ushindi huu umeifanya Italia kuwa na - [Mbili za Mbappé zaipeleka Ufaransa Kombe la Dunia](https://spotileo.co.tz/mbili-za-mbappe-zaipeleka-ufaransa-kombe-la-dunia/) - PARIS: TIMU ya Taifa ya Ufaransa imeonesha tena ubora wake katika michezo ya kufuzu baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 nyumbani dhidi ya Ukraine, ushindi uliowahakikishia tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia kwa mara ya nane mfululizo. Nahodha wa kikosi hicho Kylian Mbappé aliibeba Les Bleus kwa kufunga mabao mawili kipindi cha pili - [Mwakinyo amuita Okwiri wamalize ubishi](https://spotileo.co.tz/mwakinyo-amuita-okwiri-wamalize-ubishi/) - DAR ES SALAAM: BAADA ya maneno makali ya bondia wa Kenya Rayton Okwiri kwamba Hassan Mwakinyo anamkwepa hataki kupambana naye , Mwakinyo hakuacha jibu lipite. Kupitia ujumbe aliouweka mtandaoni, Mwakinyo amefichua kuwa tayari kulikuwa na mazungumzo ya pambano, na akaonesha ‘screenshot’ za tarehe na mawasiliano kuonesha kuwa hakuwa mkimbiaji kama anavyodaiwa. “Kwa mujibu wa mmoja - [Luvanga azidi kuweka rekodi Saudi Arabia](https://spotileo.co.tz/luvanga-azidi-kuweka-rekodi-saudi-arabia/) - RIYADH: MSHAMBULIAJI wa Al Nassr na Twiga Stars Clara Luvanga, ameendeleza moto wake katika Ligi Kuu ya Wanawake Saudi Arabia baada ya usiku wa jana kufunga hat-trick na kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Neom. Katika mchezo huo uliochezwa mjini Riyadh, Luvanga alionesha ubora wake wa kawaida kwa kutumia kasi, nguvu - [Kelvin: Ni wakati wangu wa kung’ara Stars](https://spotileo.co.tz/kelvin-ni-wakati-wangu-wa-kungara-stars/) - ISMAILIA: MSHAMBULIAJI wa Taifa Stars, Kelvin John, amesema kikosi cha timu ya taifa kipo katika maandalizi mazuri kuelekea mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Kuwait utakaopigwa kesho Ismailia, nchini Misri. Amesema huu ni wakati wake wa kung’ara tena huku akisisitiza kuwa morali ya wachezaji ipo juu na kila mmoja yupo tayari kuonesha kiwango bora. - [Mancini arudi Uarabuni](https://spotileo.co.tz/mancini-arudi-uarabuni/) - DOHA: KLABU ya Al Sadd ya Qatar imemtangaza rasmi Roberto Mancini, aliyewahi kuwa kocha wa Inter Milan na timu ya taifa ya Italia, kuwa meneja wao mpya kwa mkataba wa misimu miwili na nusu. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 60 anarejea kwenye ukocha zaidi ya mwaka mmoja tangu aachane na kazi yake na timu ## Pages - [Home](https://spotileo.co.tz/) - [News](https://spotileo.co.tz/news/) - [td_block_ad_box spot_id="sidebar" spot_title="- Advertisement -" media_size_image_height="938" media_size_image_width="938" - [Matangazo: Maelekezo na Bei](https://spotileo.co.tz/matangazo-maelekezo-na-bei/) - [Kuhusu SpotiLEO](https://spotileo.co.tz/kuhusu-spotileo/) ## Downloads - [BEI ZA KWENYE GAZETI (TSH)](https://spotileo.co.tz/download/bei-za-kwenye-gazeti-tsh/) - [BEI ZA KWENYE GAZETI (USD)](https://spotileo.co.tz/download/bei-za-kwenye-gazeti-usd/) - [BEI ZA KWENYE TOVUTI (TSH)](https://spotileo.co.tz/download/bei-za-kwenye-tovuti-tsh/) ## Categories - [Ligi Daraja La Kwanza](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/ligi-daraja-la-kwanza/) - [Featured](https://spotileo.co.tz/category/featured/) - Featured posts - [Nyumbani](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/) - [Ligi Kuu](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/ligi-kuu/) - [Mapinduzi Cup](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/mapinduzi-cup/) - [FA](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/fa/) - [U20](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/u2o/) - [Tennis](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/tennis/) - [EPL](https://spotileo.co.tz/category/kwingineko/epl/) - [Kikapu](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/kikapu/) - [TV](https://spotileo.co.tz/category/burudani/tv/) - [Ligi Kuu Zanzibar](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/ligi-zanzibar/) - [Ligi Ya Wanawake](https://spotileo.co.tz/category/nyumbani/ligi-wanawake/) - [Kwingineko](https://spotileo.co.tz/category/kwingineko/) - [Serie A](https://spotileo.co.tz/category/kwingineko/serie-a/) - [Bundesliga](https://spotileo.co.tz/category/kwingineko/bundesliga/) - [La Liga](https://spotileo.co.tz/category/kwingineko/la-liga/) - [Europa](https://spotileo.co.tz/category/kwingineko/eurpoa/) - [Africa](https://spotileo.co.tz/category/africa/) - [AFCON](https://spotileo.co.tz/category/africa/afcon/) - [CHAN](https://spotileo.co.tz/category/africa/chan/) - [Afrika Mashariki](https://spotileo.co.tz/category/africa/ea/) - [Afrika Magharibi](https://spotileo.co.tz/category/africa/afrika-magharibi/) - [Afrika Ya Kati](https://spotileo.co.tz/category/africa/africa-kati/) - [Kusini Mwa Afrika](https://spotileo.co.tz/category/africa/kusini-afrika/) - [Afrika Ya Kaskazini](https://spotileo.co.tz/category/africa/afrika-kaskazini/) - [World Cup](https://spotileo.co.tz/category/world-cup/) - [Habari Mpya](https://spotileo.co.tz/category/world-cup/habari-mpya-wc/) - [Burudani](https://spotileo.co.tz/category/burudani/) - [Muziki](https://spotileo.co.tz/category/burudani/muziki/) - [Filamu](https://spotileo.co.tz/category/burudani/filamu/) - [Picha](https://spotileo.co.tz/category/burudani/picha/) - [Michezo Mingine](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/) - [Masumbwi](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/masumbwi/) - [Riadha](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/riadha/) - [Soka La Ufukweni](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/soka-ufukweni/) - [Nyavu](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/nyavu/) - [Pete](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/pete/) - [Golf](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/golf/) - [Kuogelea](https://spotileo.co.tz/category/michezo-mingine/kuogelea/) - [Mitindo](https://spotileo.co.tz/category/mitindo/) - [Mavazi](https://spotileo.co.tz/category/mitindo/mavazi/) - [Jikoni](https://spotileo.co.tz/category/mitindo/jikono/) - [Familia](https://spotileo.co.tz/category/mitindo/familia/) - [Mahusiano](https://spotileo.co.tz/category/mitindo/mahusiano/) - [Mastaa](https://spotileo.co.tz/category/mitindo/mastaa/) - [Tetesi](https://spotileo.co.tz/category/tetesi/) - [Wasifu](https://spotileo.co.tz/category/wasifu/) ## Tags - [World](https://spotileo.co.tz/tag/world/) - [Classic](https://spotileo.co.tz/tag/classic/) - [Color](https://spotileo.co.tz/tag/color/) - [Timeline](https://spotileo.co.tz/tag/timeline/) - [Content](https://spotileo.co.tz/tag/content/) - [Tech](https://spotileo.co.tz/tag/tech/) - [Business](https://spotileo.co.tz/tag/business/) - [Foods](https://spotileo.co.tz/tag/foods/) - [Team](https://spotileo.co.tz/tag/team/) - [Life Style](https://spotileo.co.tz/tag/life-style/) - [About](https://spotileo.co.tz/tag/about/) - [Travel](https://spotileo.co.tz/tag/travel/) - [Games](https://spotileo.co.tz/tag/games/) - [Festo Polea](https://spotileo.co.tz/tag/festo-polea/)