Burudani
Kolabo ya Kiba, Mondi inakuja

Msanii wa Bongo fleva Naseeb Abdul, ‘Diamond’ amesema hivi karibuni anatarajia kuachia wimbo alioshirikiana na Msanii Abdul Kiba.
Amesema pia anatarajia uwepo wa msanii Abdul Kiba kwenye tamasha la Wasafi festival kwa kuwa wameimba pamoja.
“Katika tamasha la Wasafi festival tunatarajia kuwepo kwa msanii Abdul Kiba lakini pia Alli Kiba kama atakuwa na nafasi ratiba zisipo mbana kwa kuwa ni msanii mkubwa na hapatikani kirahisi akiwa na nafasi tutakuwa nae pamoja na Monde.” Amesema Diamond