Mapinduzi CupNyumbani
Kivumbi nusu fainali Mapinduzi Cup

NUSU fainali ya kwanza ya michuano ya Kombe la Mapinduzi inapigwa leo kati ya APR na Mlandege kwenye uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Katika nusu fainali ya pili Simba itaikabili Singida Fountain Gate Januari 10.
Kutinga nusu fainali APR imeitoa Yanga, Mlandege imeitupa nje KVZ, Simba ikaitoa Jamhuri huku Singida Fountain Gate ikiiondosha Azam.