Filamu
Johari awapa neno Wasanii chipukizi

MSANII wa Filamu Bongo, Blandina Chengula ‘Johari’ amewataka wasanii wachanga kujituma kuweza kutimiza ndoto zao.
Akizungumza na SpotiLeo jijini Dar es Salaam, Johari amesema kuwa wao walipita kwenye vikundi wakafundishwa jinsi ya kujituma.
“Nilikaa miaka mingi Kaole nikifanya mazoezi na kurudi nyumbani bila kuonekana kwenye TV lakini wasanii wasasa kufanya mazoezi hawataki wakifanya mwezi mmoja analalamika wakati sisi tulikaa miaka ndo tukaja kuonekana.”amesema Johari